< 詩篇 119 >

1 品行完美遵行上主法律的,這樣的人才算是真有福的,
Heri wale walio waadilifu katika njia zao, wanaoenenda katika sheria ya Bwana.
2 遵守上主誡命全心尋求祂的,這樣的人才算是真有福的。
Heri wale wanaozishika shuhuda zake, wamtafutao kwa moyo wao wote.
3 他們總不為非作惡,只按祂的道路生活。
Wasiofanya lolote lililo baya, wanaoenenda katika njia zake.
4 您頒發了您的命令,叫他們嚴格去遵行。
Umetoa maagizo yako ili tuyatii kwa ukamilifu.
5 願我的行徑堅定,為遵守您的章程!
Laiti mwenendo wangu ungekuwa imara katika kuyatii maagizo yako!
6 我若重視您的每條誡律,我就絕對不會蒙羞受辱。
Hivyo mimi sitaaibishwa ninapozingatia amri zako zote.
7 我一學習您正義的判詞,就以至誠的心靈頌謝您。
Nitakusifu kwa moyo mnyofu ninapojifunza sheria zako za haki.
8 我要遵守您的規矩,不要將我完全棄去!
Nitayatii maagizo yako; usiniache kabisa.
9 青年怎樣才能守身如玉?那就只有遵從您的言語。
Kijana aifanye njia yake kuwa safi jinsi gani? Ni kwa kutii, akilifuata neno lako.
10 我要用我整個心尋覓您,不要讓我錯行您的諭旨!
Ninakutafuta kwa moyo wangu wote, usiniache niende mbali na amri zako.
11 我將您的話藏在我心裏,免得我犯罪而獲罪於您。
Nimelificha neno lako moyoni mwangu ili nisikutende dhambi.
12 上主,您理應受讚頌,教訓我遵守您的誡命。
Sifa ni zako, Ee Bwana, nifundishe maagizo yako.
13 您所傳授的一切法度,我要以我的脣舌敘述。
Kwa midomo yangu nitasimulia sheria zote zinazotoka katika kinywa chako.
14 我喜愛您約法的道路,就如喜愛一切的財富。
Ninafurahia kufuata sheria zako kama mtu afurahiaye mali nyingi.
15 我要默想上主的法度,要沉思您一切的道路。
Ninatafakari maagizo yako na kuziangalia njia zako.
16 我喜歡您一切的章程,我永遠不忘您的聖言。
Ninafurahia maagizo yako, wala sitalipuuza neno lako.
17 請恩待您的僕人我得以生存,這樣使我能夠服從您的綸音。
Mtendee mema mtumishi wako, nami nitaishi; nitalitii neno lako.
18 求您開明我的眼睛,透視您法律的奇能。
Yafungue macho yangu nipate kuona mambo ya ajabu katika sheria yako.
19 我原是寄居塵世的旅客,不要向我隱瞞您的規則。
Mimi ni mgeni duniani, usinifiche amri zako.
20 我因常常渴慕您的諭令,我的靈魂便為此而成病。
Nafsi yangu inataabika kwa shauku kubwa juu ya sheria zako wakati wote.
21 您已經怒責了驕矜橫蠻的人,背棄您誡命的,是可咒詛的人。
Unawakemea wenye majivuno, waliolaaniwa waendao mbali na amri zako.
22 請除去我所受的淩辱與輕謾,因為我已經遵守了您的規範。
Niondolee dharau na dhihaka, kwa kuwa ninazishika sheria zako.
23 判官雖然反對我而開庭,您僕人仍然默思您的章程。
Ingawa watawala huketi pamoja na kunisingizia, mtumishi wako atatafakari juu ya maagizo yako.
24 因為您的誡命是我的喜樂,您的典章是我的謀士。
Sheria zako ni furaha yangu, nazo ni washauri wangu.
25 我的靈魂雖已輾轉於灰塵,求你照你的諾言使我生存。
Nimelazwa chini mavumbini, yahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako.
26 我陳明我的行徑,您便垂聽了我;
Nilikueleza njia zangu ukanijibu, nifundishe sheria zako.
27 請指給我您約法的路徑,我要沉思您的奇妙工程。
Nijulishe mafundisho ya mausia yako, nami nitatafakari maajabu yako.
28 我的靈魂因憂傷而滴滴流淚,請照您的諾言使我奮昂興起。
Nafsi yangu imechakazwa kwa huzuni, uniimarishe sawasawa na neno lako.
29 求您不要使我走錯誤的道路,求您賜我常遵守您的法度。
Niepushe na njia za udanganyifu, kwa neema unifundishe sheria zako.
30 我揀定真理的途徑,我矢志服從您的諭令。
Nimechagua njia ya kweli, nimekaza moyo wangu katika sheria zako.
31 我時常依戀著您的法度,上主不要叫我蒙受羞辱。
Nimengʼangʼania sheria zako, Ee Bwana, usiniache niaibishwe.
32 我必奔赴您誡命的路程,因為您舒展了我的心靈。
Nakimbilia katika njia ya maagizo yako, kwa kuwa umeuweka moyo wangu huru.
33 上主,給我指出您章程的道路,我要一直到死仔細遵守。
Ee Bwana, nifundishe kuyafuata maagizo yako, nami nitayashika mpaka mwisho.
34 求您教訓我遵守您的法律,我要以整個心靈持守不逾。
Nipe ufahamu, nami nitaishika sheria yako na kuitii kwa moyo wangu wote.
35 求您引導我走您誡命的捷徑,因為這捷徑使我非常高興。
Niongoze kwenye njia ya amri zako, kwa kuwa huko napata furaha.
36 使我的心傾慕您的律例,不要讓我的心貪財好利。
Ugeuze moyo wangu kuelekea sheria zako, na siyo kwenye mambo ya ubinafsi.
37 求您轉回我的眼目免看虛榮,求您按照您的道路賜我生命。
Geuza macho yangu kutoka kwenye mambo yasiyofaa, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako.
38 求您向您的僕人實踐您的許諾,即您向敬愛您的人所許的恩賜。
Mtimizie mtumishi wako ahadi yako, ili upate kuogopwa.
39 求您除去我所怕的羞恥,因為您的約法是我的甘飴。
Niondolee aibu ninayoiogopa, kwa kuwa sheria zako ni njema.
40 我如何渴慕您的規約,按照您的正義賜我生活。
Tazama jinsi ninavyoonea shauku mausia yako! Hifadhi maisha yangu katika haki yako.
41 上主,願您的仁慈和救恩,照您的諾言臨於我身!
Ee Bwana, upendo wako usiokoma unijie, wokovu wako sawasawa na ahadi yako,
42 對凌辱我的人,我有所答辯,因為我全寄望於你的聖言。
ndipo nitakapomjibu anayenidhihaki, kwa kuwa ninalitumainia neno lako.
43 不要由我口撤去真理的訓言,因我一心一意渴望你的判斷。
Usilinyakue neno la kweli kutoka kinywani mwangu, kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika amri zako.
44 我要常常遵守你的法典,時時不斷,一直要到永遠。
Nitaitii amri yako daima, naam, milele na milele.
45 我要行走平坦寬闊的途徑,因為我常常追求你的誡命。
Nitatembea nikiwa huru, kwa kuwa nimejifunza mausia yako.
46 我要傳述您的規律,在列王前也不畏懼。
Nitasema sheria zako mbele za wafalme wala sitaaibishwa,
47 我非常喜悅您的規誡,因為我對此有所鍾愛。
kwa kuwa ninazifurahia amri zako kwa sababu ninazipenda.
48 我向您的誡命舉起我的手,對您的一切章程沉思不休。
Ninaziinulia amri zako ambazo ninazipenda mikono yangu, nami ninatafakari juu ya maagizo yako.
49 求您莫把您給您的僕人的諾言遺忘,因為您在這諾言裏賜給我希望。
Kumbuka neno lako kwa mtumishi wako, kwa sababu umenipa tumaini.
50 在我的憂苦中,這是我的安慰,因為您的聖言,賜給了我生氣。
Faraja yangu katika mateso yangu ni hii: Ahadi yako inahifadhi maisha yangu.
51 驕傲人雖加給我極度的侮辱,但我卻沒有偏離過您的法律。
Wenye majivuno wamenisimanga bila kuchoka, hata hivyo sitaiacha sheria yako.
52 我一思到您永怚的斷定;上主,我是多麼安慰而高興。
Ee Bwana, ninazikumbuka sheria zako za zamani, nazo zinanifariji.
53 為了背棄您法律的罪人,我不知不覺地恕火焚心。
Nimeshikwa sana na ghadhabu kwa ajili ya waovu, ambao wameacha sheria yako.
54 在我這客居不定的寓所,您的法令成了我的詩歌。
Maagizo yako ni kiini cha nyimbo zangu popote ninapoishi.
55 上主,夜間我想起您的聖名,我就決意遵守您的法令。
Ee Bwana, wakati wa usiku ninalikumbuka jina lako, nami nitatii sheria yako.
56 我之所以如此這般,因我遵守您的規範。
Hili limekuwa zoezi langu: nami ninayatii mausia yako.
57 上主,我說:我的福分,就是遵守您的教訓。
Ee Bwana, wewe ni fungu langu, nimeahidi kuyatii maneno yako.
58 我全心仰膽著您的容貌,求您按您的諾言憐憫我。
Nimetafuta uso wako kwa moyo wangu wote, nihurumie sawasawa na ahadi yako.
59 我一默想到我所走的道路,就把我的腳轉您的法度。
Nimezifikiri njia zangu na nimeelekeza hatua zangu katika mausia yako.
60 爽爽快快,毫不躊躇,我常遵守您的法度。
Nitafanya haraka bila kuchelewa kuzitii amri zako.
61 惡人的繩索雖將我纏起,我郤未將您的法律忘記。
Hata waovu wanifunge kwa kamba, sitasahau sheria yako.
62 為了您正義的判語,我半夜起身讚美您。
Usiku wa manane ninaamka kukushukuru kwa sababu ya sheria zako za haki.
63 我常向敬愛您的人為友,與遵守您誡命的人為侶。
Mimi ni rafiki kwa wale wote wakuchao, kwa wote wanaofuata mausia yako.
64 上主,您的慈愛充滿大地,求您教我遵守您的律例。
Ee Bwana, dunia imejaa upendo wako, nifundishe maagizo yako.
65 上主,您依照您的言詞,善待了您的僕役。
Mtendee wema mtumishi wako Ee Bwana, sawasawa na neno lako.
66 您以知識和聰慧教訓我,我要一心信賴您的誡條。
Nifundishe maarifa na uamuzi mzuri, kwa kuwa ninaamini amri zako.
67 我在受苦以前徘徊岐途,但我現今順從您的訓語。
Kabla sijapata shida nilipotea njia, lakini sasa ninalitii neno lako.
68 您是慈善的,好施仁惠,求您給我教授您的規矩。
Wewe ni mwema, unalotenda ni jema, nifundishe maagizo yako.
69 驕傲人捏造謊言陷害我,我要全心遵守您的規約。
Ingawa wenye majivuno wamenisingizia uongo, nitafuata mausia yako kwa moyo wangu wote.
70 他們的心遲純如蒙脂肪,然而我卻喜歡您的典章。
Mioyo yao ni katili na migumu, bali mimi napendezwa na sheria yako.
71 為叫我能學習您的法度,受若遭難於我確有好處。
Ilikuwa vyema mimi kupata shida ili nipate kujifunza maagizo yako.
72 您頒的法律對我的利益,連千萬的金銀也不能比。
Sheria inayotoka kinywani mwako ina thamani kubwa kwangu kuliko maelfu ya vipande vya fedha na dhahabu.
73 您的雙手創造了我,形成了我;求您賜我智力,為學您的誡條。
Mikono yako ilinifanya na kuniumba, nipe ufahamu niweze kujifunza amri zako.
74 敬愛您的人,見我就喜歡;因為我常仰望您的聖言。
Wakuchao wafurahie wanaponiona, kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika neno lako.
75 上主,我知道您的審判是公正無私的,您叫我遭受磨難是理所當然的。
Ee Bwana, ninajua kwamba sheria zako ni za haki, katika uaminifu wako umeniadhibu.
76 照您給您僕人的許諾,按您的仁慈來安慰我。
Upendo wako usiokoma uwe faraja yangu, sawasawa na ahadi yako kwa mtumishi wako.
77 願您的仁愛臨於我,使我生活,因為您的法律就是我的喜樂。
Huruma yako na inijie ili nipate kuishi, kwa kuwa naifurahia sheria yako.
78 願無端難為我的驕傲人蒙羞!但是我要默想沉思您的法律。
Wenye majivuno na waaibishwe kwa kunikosea mimi bila sababu, lakini mimi nitatafakari juu ya mausia yako.
79 願那些敬愛您的人歸向我,願關心您的人依附我!
Wale wakuchao na wanigeukie mimi, hao ambao wanazielewa sheria zako.
80 願我全心遵守您的法典,這樣我便不致自覺羞赧。
Moyo wangu usiwe na lawama katika kutii maagizo yako, ili nisiaibishwe.
81 我靈渴慕您的救援而衰弱,我熱切地盻望著您的許諾。
Nafsi yangu inazimia kwa kutamani wokovu wako, lakini nimeweka tumaini langu katika neno lako.
82 我對您的諾言望眼欲穿,究竟您何時才賜我慰安?
Macho yangu yamefifia, nikingoja ahadi yako; ninasema, “Utanifajiri lini?”
83 我雖然相似煙熏的皮囊,我仍然不忘卻您的典章。
Ingawa nimekuwa kama kiriba kwenye moshi, bado sijasahau maagizo yako.
84 您僕人的歲月還能有多久?您何時處罰迫害我的惡徒?
Mtumishi wako itampasa angoje mpaka lini? Ni lini utawaadhibu washtaki wangu?
85 不按您法律生活的驕傲人,暗中給我挖掘了陷阱深坑。
Wenye majivuno wananichimbia mashimo, kinyume na sheria yako.
86 您所有的一切誡命全是真道;他們無理迫害我,求您協助我。
Amri zako zote ni za kuaminika; unisaidie, kwa sababu watu wananishtaki bila sababu.
87 我們幾乎將我由地上滅絕,但我卻沒有背棄您的規誡。
Walikaribia kabisa kunifuta kutoka uso wa dunia, lakini sijaacha mausia yako.
88 您按照您的仁慈使我生活,這樣我必遵守您口中的條約。
Yahifadhi maisha yangu sawasawa na upendo wako, nami nitatii sheria za kinywa chako.
89 上主您的聖言,永遠存留,它堅固而不移,好似蒼天。
Ee Bwana, neno lako ni la milele, linasimama imara mbinguni.
90 您所有的忠誠,代代流傳,您所造的大地,屹立不變。
Uaminifu wako unaendelea kwa vizazi vyote, umeiumba dunia, nayo inadumu.
91 天地時常遵守您的旨意,因為萬物都是您的僕役。
Sheria zako zinadumu hadi leo, kwa kuwa vitu vyote vinakutumikia.
92 我如果不喜愛您的法令,我早已在我苦患中喪命。
Kama nisingefurahia sheria yako, ningeangamia katika taabu zangu.
93 我永遠不忘卻您的法令,因為您藉此賜給我生命。
Sitasahau mausia yako kamwe, kwa maana kwayo umehifadhi maisha yangu.
94 我全屬於您,求您救拔我,因為我尋求了您的法約。
Uniokoe, kwa maana mimi ni wako, kwa kuwa nimetafuta mausia yako.
95 惡人窺視我,忌把我殺害,然而我仍細想您的規誡。
Waovu wanangojea kuniangamiza, bali mimi ninatafakari sheria zako.
96 我看任何齊全的都有界限,唯您的誡命卻廣闊無邊。
Katika ukamilifu wote ninaona mna kikomo, lakini amri zako hazina mpaka.
97 上主,我是多麼愛慕您的法律,它是我終日對默想的題目。
Aha! Tazama, sheria yako naipenda mno ajabu. Ninaitafakari mchana kutwa.
98 您的誡命永遠存在於我心,它使我比我的仇敵聰明。
Amri zako zimenipa hekima zaidi kuliko adui zangu, kwa kuwa nimezishika daima.
99 我比我所有的教師更聰明,因為我常默想您的法令。
Nina akili zaidi kuliko walimu wangu wote, kwa kuwa ninatafakari juu ya sheria zako.
100 我比老年的人更有智慧,因為我恪守您的律例。
Nina ufahamu zaidi kuliko wazee, kwa kuwa ninayatii mausia yako.
101 我使我的腳迴避一切惡路,為叫我能夠遵守您的言語。
Nimezuia miguu yangu isiende kwenye kila njia mbaya, ili niweze kutii neno lako.
102 我不偏離您的約法,因為是您教訓了我。
Sijaziacha sheria zako, kwa kuwa umenifundisha wewe mwenyewe.
103 您的教言對我上顎多麼甘美!在我的口中比蜂蜜更要甘美!
Tazama jinsi maneno yako yalivyo matamu kwangu, matamu kuliko asali katika kinywa changu!
104 由您的誡命,我獲得了聰明,因我憎惡一切欺詐的途徑。
Ninapata ufahamu kutoka mausia yako, kwa hiyo ninachukia kila njia ya upotovu.
105 上主,您的言語是我腳步的明燈,是我路途上的光明。
Neno lako ni taa ya miguu yangu na mwanga katika njia yangu.
106 我今起誓,我要定志,堅守您正義的諭令。
Nimeapa na nimethibitisha, kwamba nitafuata sheria zako za haki.
107 上主,我已經受苦很重,照您的諾言,保我生命。
Nimeteseka sana, uhifadhi maisha yangu, Ee Bwana, sawasawa na neno lako.
108 上主,請悅納我口中的祭獻,請教訓我明白您的審斷。
Ee Bwana, pokea sifa za hiari za kinywa changu, nifundishe sheria zako.
109 我的生命常處於危險中,但我仍不忘記您的法典。
Ingawa maisha yangu yako hatarini siku zote, sitasahau sheria yako.
110 惡人雖然給我設下陷阱,我仍然不偏離您的章程。
Waovu wamenitegea mtego, lakini sijayakiuka maagizo yako.
111 您的誡命永做我的家產,因為這是我心中的喜歡。
Sheria zako ni urithi wangu milele, naam ni furaha ya moyo wangu.
112 我要傾心遵守您的法典,千秋萬世,一直到永遠。
Nimekusudia moyoni mwangu kuyafuata maagizo yako mpaka mwisho.
113 我惱恨心懷二意的人,對您的法律,我喜愛萬分。
Ninachukia watu wa nia mbili, lakini ninapenda sheria yako.
114 您是我的庇護我的盾牌,因此我唯您的聖言是賴。
Wewe ni kimbilio langu na ngao yangu, nimeweka tumaini langu katika neno lako.
115 作惡的人,您們應離我遠去!因為我要遵守天主的法度。
Ondokeni kwangu, ninyi mtendao mabaya, ili niweze kushika amri za Mungu wangu!
116 照您的諾言,扶持我的生命,不要讓我的希望成成為泡影。
Nihifadhi sawasawa na ahadi yako, nami nitaishi; usiache matumaini yangu yakavunjwa.
117 求您扶持我得蒙拯救,能時常留意您的制度。
Nitegemeze, nami nitaokolewa, nami daima nitayaheshimu maagizo yako.
118 凡背棄您法令的,您都鄙棄,因為他們的思念全是詐欺。
Unawakataa wote wanaoyaasi maagizo yako, kwa maana udanganyifu wao ni bure.
119 地上的惡人您都看作渣滓,因此我非常喜愛您的法制。
Waovu wa nchi unawatupa kama takataka, kwa hivyo nazipenda sheria zako.
120 我的肉身因敬愛您而戢戰憟,對您的諭令失也知所敬愛。
Mwili wangu unatetemeka kwa kukuogopa wewe, ninaziogopa sheria zako.
121 我行正義及合法律的事情,別把我交於壓迫我的壞人。
Nimetenda yaliyo haki na sawa, usiniache mikononi mwa watesi wangu.
122 求您保證您僕人的安全,沒有驕傲心將我磨難。
Mhakikishie mtumishi wako usalama, usiache wenye kiburi wanionee.
123 對您的救助和正義的諾言,我熱切渴盻已經望眼欲穿。
Macho yangu yamefifia, yakitazamia wokovu wako, na kuitazamia ahadi yako ya kweli.
124 求您照您的仁慈恩待您的僕人,也求您教訓我能明白您的章程。
Mfanyie mtumishi wako kulingana na upendo wako na unifundishe maagizo yako.
125 我是您的僕人,求賜我明達,為使我能夠通曉您的約法。
Mimi ni mtumishi wako; nipe ufahamu ili niweze kuelewa sheria zako.
126 現今是上主行動的時候,因他們違反了您的法度。
Ee Bwana, wakati wako wa kutenda umewadia, kwa kuwa sheria yako inavunjwa.
127 所以我愛慕您的誡律,遠勝各種黃金和寶玉。
Kwa sababu nazipenda amri zako zaidi ya dhahabu, naam, zaidi ya dhahabu safi,
128 我尊重您的一切誡命,憎惡所有的欺詐途徑。
na kwa sababu naona maagizo yako yote ni adili, nachukia kila njia potovu.
129 您的約法誠然是美妙神奇,因此我的靈魂要遵守不離。
Sheria zako ni za ajabu, hivyo ninazitii.
130 您的言語經過解釋必會發亮光照,連知識淺薄的人也可以通達知曉。
Kuingia kwa maneno yako kunaleta nuru, kunampa mjinga ufahamu.
131 我張開我的口嗟嘆唏嚧,因為我極渴慕您的誡律。
Nimefungua kinywa changu na kuhema, nikitamani amri zako.
132 求您回身向我,垂憐我,如素常對待愛您名者然。
Nigeukie na unihurumie, kama uwafanyiavyo siku zote wale wanaolipenda jina lako.
133 引導我的腳步履行您的訓誥,不要允許任何邪惡來主宰我。
Ongoza hatua zangu kulingana na neno lako, usiache dhambi yoyote initawale.
134 求您救我擺挩人的欺壓,為使我能遵守您的律法。
Niokoe na uonevu wa wanadamu, ili niweze kutii mausia yako.
135 求您給您的僕人顯示您的慈顏,同時也您們給我教導您的規範。
Mwangazie mtumishi wako uso wako na unifundishe amri zako.
136 我的眼淚滴滴下流有如溪水,因為他們全不遵守您的法規。
Chemchemi za machozi zinatiririka kutoka machoni yangu, kwa kuwa sheria yako haifuatwi.
137 上主,您原是公義的,您的判決是正直的。
Ee Bwana, wewe ni mwenye haki, sheria zako ni sahihi.
138 您以正義和至誠,立定了您的誡命。
Sheria ulizoziweka ni za haki, ni za kuaminika kikamilifu.
139 我的熱火快要將我消耗殆盡,因為我的敵人忘了您的聖訓。
Jitihada yangu imenidhoofisha, kwa kuwa adui zangu wanayapuuza maneno yako.
140 您的教言經過千捶百鍊,您的僕人對它愛不知倦。
Ahadi zako zimejaribiwa kikamilifu, mtumishi wako anazipenda.
141 我雖然年記幼小,被人輕看,可是我總不忘卻您的法範。
Ingawa ni mdogo na ninadharauliwa, sisahau mausia yako.
142 您的正義永遠公正,您的法律永遠堅定。
Haki yako ni ya milele, na sheria yako ni kweli.
143 困苦和壓迫雖然來臨我身,但您的誡命仍是我的歡欣。
Shida na dhiki zimenipata, lakini amri zako ni furaha yangu.
144 您的約法永遠公允,賜我智慧,使我生存。
Sheria zako ni sahihi milele, hunipa ufahamu ili nipate kuishi.
145 我全心呼號,並求您俯聽,上主,我要遵守您的法令。
Ee Bwana, ninakuita kwa moyo wangu wote, nami nitayatii maagizo yako.
146 我呼號您,求您救護,我必遵守您的法度。
Ninakuita; niokoe nami nitazishika sheria zako.
147 天還未亮,我就起來求助,熱切期待您的訓語,
Ninaamka asubuhi na mapema na kukuomba msaada; nimeweka tumaini langu katika neno lako.
148 夜裏每更,我都睜開眼睛,全是為了您的聖訓。
Sikufumba macho yangu usiku kucha, ili niweze kutafakari juu ya ahadi zako.
149 上主,請照您的仁慈俯聽我的呼聲,上主,請照您的正義使我得以重生。
Usikie sauti yangu sawasawa na upendo wako, Ee Bwana, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na sheria zako.
150 非法迫害我的人已經臨近,他們都遠離了您的法令。
Wale wanaopanga mipango miovu wako karibu nami, lakini wako mbali na sheria yako.
151 上主,願您時常與我親近,您一切的誡命全屬忠信。
Ee Bwana, hata hivyo wewe u karibu, na amri zako zote ni za kweli.
152 我早就已由您的約法得知,那都是您從永遠所立定。
Tangu zamani nimejifunza kutoka shuhuda zako kwamba umezithibitisha ili zidumu milele.
153 求您垂視我的苦難而救拔我、因為我媲沒有忘記您的約法。
Yaangalie mateso yangu, uniokoe, kwa kuwa sijasahau sheria yako.
154 求您辯護我的案件而拯救我,並請依照您的諾言,使我生活。
Nitetee katika hali hii yangu na unikomboe, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na ahadi yako.
155 恨不得救恩達達離開惡徒,因為他們不理睬您的法度。
Wokovu uko mbali na waovu, kwa kuwa hawatafuti maagizo yako.
156 上主,您的仁愛何其廣闊,按照您的諭旨,賜我生命。
Ee Bwana, huruma zako ni kuu, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na sheria zako.
157 迫害與磨難我的人確實眾多,然而我卻不曾偏離您的法約。
Adui wanaonitesa ni wengi, lakini mimi sitaziacha sheria zako.
158 奸黨惡輩我一看見就會生厭,因為他們都不遵守您的規範。
Ninawatazama wasioamini kwa chuki, kwa kuwa hawalitii neno lako.
159 上主,請您看我如何愛您的訓令,上主,照您的仁慈保全我的生命。
Tazama jinsi ninavyopenda mausia yako; Ee Bwana, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na upendo wako.
160 您聖言的總綱確是真實無欺,您正義的一切判斷永遠不移。
Maneno yako yote ni kweli, sheria zako zote za haki ni za milele.
161 王侯雖然無緣無故加我苦難,我的心靈仍舊敬愛您的教言。
Watawala wamenitesa bila sababu, lakini moyo wangu unatetemeka kwa neno lako.
162 我對您的諾言實在歡喜若狂,像得到許多勝利品的人一像。
Nafurahia ahadi zako kama mtu aliyepata mateka mengi.
163 奸詐邪惡是我所恨所愛的,您的法令是我所喜所愛的。
Ninachukia na kuchukizwa sana na uongo, lakini napenda sheria yako.
164 為了您那正義的判詞,我一要讚美您七次。
Ninakusifu mara saba kwa siku, kwa ajili ya sheria zako za haki.
165 愛慕您法律的必飽享平安,沒有一點失足跌倒的危險。
Wanaopenda sheria yako wana amani tele, wala hakuna kitu kinachoweza kuwakwaza.
166 上主,我期待您的助佑,上主,我遵守您的法度。
Ee Bwana, ninangojea wokovu wako, nami ninafuata amri zako,
167 我的靈魂恪守您的規誡,因為我對規誡十分喜愛。
Ninazitii sheria zako, kwa sababu ninazipenda mno.
168 我必要遵守您的規誡和勸言,因我的一切道路在您的面前。
Nimetii mausia yako na sheria zako, kwa kuwa njia zangu zote zinajulikana kwako.
169 上主,願我呼聲上達於您,求您照您的約言使我明理。
Ee Bwana, kilio changu na kifike mbele zako, nipe ufahamu sawasawa na neno lako.
170 願我的祈求到達您的面前,求您照您的諾言救我脫險。
Maombi yangu na yafike mbele zako, niokoe sawasawa na ahadi yako.
171 願我的雙脣湧溢讚美歌曲!因為您給我教授您的法律。
Midomo yangu na ibubujike sifa, kwa kuwa unanifundisha maagizo yako.
172 願我的舌頭歌詠您的訓令!因您的一切誡命盡屬公正。
Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako, kwa kuwa amri zako zote ni za haki.
173 願您伸出您的手救助我!因為我揀選您的法約。
Mkono wako uwe tayari kunisaidia, kwa kuwa nimechagua mausia yako.
174 上主,我渴望您的救援,您的法律是我的喜樂。
Ee Bwana, ninatamani wokovu wako, na sheria yako ni furaha yangu.
175 願我的靈魂活著讚美您,願您的斷語來支持我!
Nijalie kuishi ili nipate kukusifu, na sheria zako zinitegemeze.
176 我像迷路的亡羊,請尋回您的僕人,因為我總沒有忘記您任何的誡命。
Nimetangatanga kama kondoo aliyepotea. Mtafute mtumishi wako, kwa kuwa sijasahau amri zako.

< 詩篇 119 >