< 詩篇 107 >
1 請您們向上主讚頌,因為祂是美善寬仁,祂的仁慈永遠常存。
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
2 歌詠此曲的人們是:上主親身所救贖的,由敵人手中救出的,
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 他們在曠野和沙漠中漂流,找不到安居之城的道路。
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6 他們於急難中一哀救上主,上主即拯救他們脫離困苦,
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
9 因為祂使饑渴的人得到飽飫,祂使肚餓人享盡美物。
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
10 他們坐在黑暗與死影裏,盡為痛苦與鐵鍊所縛繫,
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
11 因為背棄了天主的命令,又輕視了至高者的叮嚀。
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
12 因此,祂以苦難折磨了他們的心神,他們跌倒了,卻沒有人來扶持他們。
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
13 他們在急難中哀求上主,上主即救他們脫離困苦,
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
14 領他們擺脫死影與黑暗,把他們的銬鐐完全弄斷。
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
15 願他們感謝上主的仁慈,稱頌祂給人子顯的奇蹟。
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
19 他們於急難中一哀求主,上主即拯救他們脫離困苦。
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
20 主發一言就將他們病除,且拯救他們脫離了陰府。
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
21 願他們感謝上主[的仁慈,稱頌祂給人子顯的奇蹟。
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
22 願他們獻上感恩的祭獻,將祂的工程歡樂地宣傳。
Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
24 他們看見過上主的奇異作為,遇到過祂行於汪洋中的奇跡:
Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
26 時而忽躍沖天,時而忽墜棎淵;此危急之中,他們膽戰心寒,
Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
28 他們於急難中一哀求上主,上主即拯救他們脫離困苦。
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
30 祂使風平浪靜,大家個個歡忭,祂領他們登上了渴薶的海岸。
Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
36 把饑餓的人徒置在那地,使他們與興建者安居的城邑;
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
37 耕田種地,開懇了葡萄園,因此收穫果實,豐富出產。
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
38 上主祝福了他們人口繁衍,賞賜他們的牲畜有增無減。
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
40 但上主卻使權貴遭受恥辱,任他們徘徊歧途無路可走。
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
41 但拯救貧窮人脫離災難,使他們家屬多如羊群一般。
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
42 正直的人見到必然歡忭,但邪惡的人卻啞口無言。
Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.