< 腓利門書 1 >

1 基督耶穌的被囚者保祿,和弟茂德弟兄,致書給我們可愛的合作者費1肋孟,
Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, pamoja na Timotheo ndugu yetu: Kwa Filemoni rafiki yetu mpendwa na mtendakazi mwenzetu,
2 並給姊妺阿丕雅和我們的戰友阿爾希頗,以及在妳家中的教會。
kwa dada yetu mpendwa Afia, kwa Arkipo askari mwenzetu na kwa kanisa lile likutanalo nyumbani mwako:
3 願恩寵與平安,由天主我們的父及主耶穌基督賜與你們。
Neema iwe nanyi na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
4 在我的祈禱記念你時,我常感謝我的天主,
Siku zote ninamshukuru Mungu ninapokukumbuka katika maombi yangu,
5 因為聽說你對主耶穌,和對眾聖徒所表現的愛德與信德。
kwa sababu ninasikia juu ya imani yako katika Bwana Yesu na upendo wako kwa watakatifu wote.
6 我祈求天主,為使你因信德而懷有的慷慨發生功效,使你認清我們所能行的一切善事,都是為基督而行的。
Naomba utiwe nguvu katika kuishuhudia imani yako, ili upate kuwa na ufahamu mkamilifu juu ya kila kitu chema tulicho nacho ndani ya Kristo.
7 弟兄,我由於你的愛德,確實獲得了極大的喜樂和安慰,因為與著你,聖徒的心都舒暢了。
Upendo wako umenifurahisha mno na kunitia moyo, kwa sababu wewe ndugu, umeiburudisha mioyo ya watakatifu.
8 為此,我雖然在基督內,能放心大膽地命你去作這件該作的事,
Hata hivyo, ingawa katika Kristo ningeweza kuwa na ujasiri na kukuagiza yale yakupasayo kutenda,
9 可是,我這年老的保祿,如今且為基督耶穌作囚犯的,寧願因著愛德求你,
lakini ninakuomba kwa upendo, mimi Paulo, mzee na pia sasa nikiwa mfungwa wa Kristo Yesu,
10 就是為失在鎖鏈中所生的兒子敖乃息摩來求你。
nakuomba kwa ajili ya mwanangu Onesimo, aliyefanyika mwanangu nilipokuwa kwenye minyororo.
11 他曾一度為你是無用的,可是,如今為你我都有用了;
Mwanzoni alikuwa hakufai, lakini sasa anakufaa sana wewe na mimi pia.
12 我現今把他給打發回去,[你收下]他,他是我的心肝。
Namtuma kwako, yeye aliye moyo wangu hasa.
13 我本來願意將他留在我這裏,叫他替你服侍我這為福音而被囚 的人,
Ningependa nikae naye ili ashike nafasi yako ya kunisaidia wakati huu nikiwa kifungoni kwa ajili ya Injili.
14 可是沒有你的同意,我什麼也不願意做,好叫你所行的善不是出於勉強,而是出於甘心。
Lakini sikutaka kufanya lolote bila idhini yako, ili wema wowote uufanyao usiwe wa lazima, bali wa hiari.
15 也許他暫時離開了你,是為叫你永遠收下他, (aiōnios g166)
Huenda sababu ya yeye kutengwa nawe kwa kitambo kidogo ni ili uwe naye daima. (aiōnios g166)
16 不再當一個奴隸,而是超過奴隸,作可愛的弟兄:他為我特別可愛,但為你不拘是論肉身方面,或是論主方面,更加可愛。
Si kama mtumwa, bali bora kuliko mtumwa, kama ndugu mpendwa. Yeye ni mpendwa sana kwangu na hata kwako zaidi, yeye kama mwanadamu na kama ndugu katika Bwana.
17 所以,若你以我為同志,就嫉留他當作收留我罷!
Hivyo kama unanihesabu mimi kuwa mshirika wako, mkaribishe kama vile ungenikaribisha mimi mwenyewe.
18 他若虧負了你或欠下你什麼,就算在我的賬上罷!
Kama amekukosea lolote au kama unamdai chochote, nidai mimi.
19 我中親手簽字:「我必要償還。」至於你,你所欠於我的,竟是你本身:這我就不必對你說了!
Ni mimi Paulo, ninayeandika waraka huu kwa mkono wangu mwenyewe. Nitakulipa. Sitaji kwamba nakudai hata nafsi yako.
20 弟兄,望你使我在主內得此恩惠,並在基督內使我心舒暢!
Ndugu yangu, natamani nipate faida kwako katika Bwana, uuburudishe moyo wangu katika Kristo.
21 我自信你必聽從,才給你寫了這信,我知道就是超過我所的,你也必 作。
Nikiwa na hakika ya utii wako, nakuandikia, nikijua kwamba utafanya hata zaidi ya yale ninayokuomba.
22 同時也請你給準備一個住處,因為我希望因 的祈禱,主必要把我賜給你們。
Jambo moja zaidi: Niandalie chumba cha wageni, kwa kuwa nataraji kurudishwa kwenu kama jibu la maombi yenu.
23 為基督耶穌與我一同被囚的厄帕夫辣、
Epafra, aliye mfungwa mwenzangu katika Kristo Yesu, anakusalimu.
24 我的合作者馬爾谷、阿黎斯塔苛、德瑪斯、路加都問攸候你。
Vivyo hivyo Marko, Aristarko, Dema na Luka, watendakazi wenzangu wanakusalimu.
25 願主基督的恩寵,與你們的心靈同在! 阿們。
Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho zenu. Amen.

< 腓利門書 1 >