< 彌迦書 3 >

1 我曾經說過:「雅各伯的首領,以色列家的官吏,請你們傾聽! 認識正義,豈不是你們分內的事﹖」
Kisha nikasema, “Sikilizeni enyi viongozi wa Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli. Je, hampaswi kujua hukumu,
2 然而他們惡善好惡,從平民身上剝下他們的皮,從骨頭上剔下他們的肉。
ninyi mnaochukia mema na kupenda maovu; ninyi mnaowachuna watu wangu ngozi na kuondoa nyama kwenye mifupa yao;
3 他們吞食我百姓的肉,剝去他們的皮,折斷他們的骨頭,將他們切成碎塊,如釜中的肉,如鼎中的肉。
ninyi mnaokula nyama ya watu wangu, mnaowachuna ngozi na kuvunja mifupa yao vipande vipande; mnaowakatakata kama nyama ya kuwekwa kwenye sufuria na kama nyama ya kuwekwa kwenye chungu?”
4 當他們呼求上主時,上主決不俯聽他們;反要掩面不理他們,因為他們行了窮凶極惡的事。
Kisha watamlilia Bwana, lakini hatawajibu. Wakati huo atawaficha uso wake kwa sababu ya uovu waliotenda.
5 論及迷我百姓的先知,上主這樣說:當他們的牙齒有咀嚼的東西時,他們便呼喊:「和平。」但凡不將食物送到他們口上的,他們便宣佈「戰爭。」
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kuhusu manabii wanaowapotosha watu wangu, mtu akiwalisha, wanatangaza ‘amani’; kama hakufanya hivyo, wanaandaa kupigana vita dhidi yake.
6 因此,為你們只有黑夜而沒有神視,只有黑暗而沒有神諭;太陽必為先知而沒落,白畫必為他們而變為黑暗。
Kwa hiyo usiku utawajieni, msiweze kuwa na maono, na giza, msiweze kubashiri. Jua litawachwea manabii hao, nao mchana utakuwa giza kwao.
7 先知必將抱愧,巫士必將蒙羞,他們都要掩住自己的鬍鬚,因為沒有天主的答覆。
Waonaji wataaibika na waaguzi watafedheheka. Wote watafunika nyuso zao kwa sababu hakuna jibu litokalo kwa Mungu.”
8 至於我,我因上主的神而充滿 力量、正義和勇氣,向雅各伯指出她的邪惡,向以色列說明她的罪過。
Lakini kuhusu mimi, nimejazwa nguvu, nimejazwa Roho wa Bwana, haki na uweza, kumtangazia Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake.
9 雅各伯家的領袖,以色列家的官吏,請你們傾聽這事! 你們憎惡正義,曲解一切正理;
Sikieni hili, enyi viongozi wa nyumba ya Yakobo, enyi watawala wa nyumba ya Israeli, mnaodharau haki na kupotosha kila lililo sawa;
10 你們以血債建設耶路撒冷。
mnaojenga Sayuni kwa kumwaga damu na Yerusalemu kwa uovu.
11 她火首領為賄賂而審判,司祭為薪俸而設教,先知為銀錢而占卜,尚依賴上主說:「上主不是在我們中間嗎﹖災禍決不會臨在我們身上! 」
Viongozi wake wanahukumu kwa rushwa, na makuhani wake wanafundisha kwa malipo, nao manabii wake wanatabiri kwa fedha. Hata hivyo wanamwegemea Bwana na kusema, “Je, Bwana si yumo miongoni mwetu? Hakuna maafa yatakayotupata.”
12 因此,為了你的緣故,熙雍必被耕耘有如一塊地.耶路撒冷必成為一堆廢墟,聖殿山必成為叢林中的一個丘陵。
Kwa hiyo kwa sababu yenu, Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa lundo la kokoto, na kilima cha Hekalu kitakuwa kichuguu kilichofunikwa na vichaka.

< 彌迦書 3 >