< 耶利米哀歌 3 >

1 在上主盛怒的鞭責下,我成了受盡痛苦的人;
Mimi ndiye mtu aliyeona mateso kwa fimbo ya ghadhabu yake.
2 他引我走入黑暗,不見光明;
Amenifukuzia mbali na kunifanya nitembee gizani wala si katika nuru;
3 且終日再三再四,伸手與我為敵;
hakika, amegeuza mkono wake dhidi yangu tena na tena, mchana kutwa.
4 他使我肌膚枯瘦,折斷我的骨頭;
Amefanya ngozi yangu na nyama yangu kuchakaa na ameivunja mifupa yangu.
5 他在我四周築起圍牆,用毒草和痛苦環繞我,
Amenizingira na kunizunguka kwa uchungu na taabu.
6 讓我居住在黑暗之中,好像久已死去的人。
Amenifanya niishi gizani kama wale waliokufa.
7 他用垣牆圍困我,不能逃脫;並且加重我的桎梏;
Amenizungushia ukuta ili nisiweze kutoroka, amenifunga kwa minyororo mizito.
8 我呼籲求救時,他卻掩耳不聽我的祈禱。
Hata ninapoita au kulia ili kuomba msaada, anakataa kupokea maombi yangu.
9 他用方石堵住了我的去路,阻塞了我的行徑。
Ameizuia njia yangu kwa mapande ya mawe, amepotosha njia zangu.
10 上主之於我,像是一隻潛伏的狗熊,是一頭藏匿的獅子,
Kama dubu aviziaye, kama simba mafichoni,
11 他把我拖到路旁,撲捉撕裂,加以摧殘;
ameniburuta kutoka njia, akanirarua na kuniacha bila msaada.
12 又拉開他的弓,瞄準我,把我當作眾矢之的。
Amevuta upinde wake na kunifanya mimi niwe lengo kwa ajili ya mishale yake.
13 他用箭囊的箭,射殺了我的雙腰;
Alinichoma moyo wangu kwa mishale iliyotoka kwenye podo lake.
14 使我成了萬民的笑柄,終日受他們的嘲笑;
Nimekuwa kichekesho kwa watu wangu wote, wananidhihaki kwa wimbo mchana kutwa.
15 他使我飽食苦菜,醉飲苦酒。
Amenijaza kwa majani machungu na kunishibisha kwa nyongo.
16 他用砂礫破碎我的牙齒,用灰塵給我充饑。
Amevunja meno yangu kwa changarawe, amenikanyagia mavumbini.
17 他除去了我心中的平安,我已經忘記了一切幸福;
Amani yangu imeondolewa, nimesahau kufanikiwa ni nini.
18 於是我說:「我的光榮已經消逝,對上主的希望也已經幻滅。」
Kwa hiyo nasema, “Fahari yangu imeondoka na yale yote niliyokuwa nimetarajia kutoka kwa Bwana.”
19 我回憶著我的困厄和痛苦,盡是茹苦含辛!
Nayakumbuka mateso yangu na kutangatanga kwangu, uchungu na nyongo.
20 我的心越回想,越覺沮喪。
Ninayakumbuka vyema, nayo nafsi yangu imezimia ndani yangu.
21 但是我必要追念這事,以求獲得希望:
Hata hivyo najikumbusha neno hili na kwa hiyo ninalo tumaini.
22 上主的慈愛,永無止境;他的仁慈,無窮無盡。
Kwa sababu ya upendo mkuu wa Bwana, hatuangamii, kwa kuwa huruma zake hazikomi kamwe.
23 你的仁慈,朝朝常新;你的忠信,浩大無垠!
Ni mpya kila asubuhi, uaminifu wako ni mkuu.
24 我心中知道:上主是我的福分;因此,我必信賴他。
Nimeiambia nafsi yangu, “Bwana ni fungu langu, kwa hiyo nitamngojea.”
25 上主對信賴他和尋求他的人,是慈善的。
Bwana ni mwema kwa wale ambao tumaini lao ni kwake, kwa yule ambaye humtafuta;
26 最好是靜待上主的救援,
ni vyema kungojea kwa utulivu kwa ajili ya wokovu wa Bwana.
27 最好是自幼背負上主的重軛,
Ni vyema mtu kuchukua nira bado angali kijana.
28 默然獨坐,因為是上主加於他的軛;
Na akae peke yake awe kimya, kwa maana Bwana ameiweka juu yake.
29 他該把自己的口貼近塵埃,這樣或者還有希望;
Na azike uso wake mavumbini bado panawezekana kuwa na matumaini.
30 向打他的人,送上面頰,飽受凌辱。
Na atoe shavu lake kwa yule ampigaye, na ajazwe na aibu.
31 因為上主決不會永遠把人遺棄;
Kwa kuwa watu hawakatiliwi mbali na Bwana milele.
32 縱使懲罰,他必按照自己豐厚的慈愛,而加以憐憫。
Ingawa huleta huzuni, ataonyesha huruma, kwa kuwa upendo wake usiokoma ni mkuu.
33 因為他苛待和懲罰世人,原不是出於他的心願。
Kwa maana hapendi kuwaletea mateso au huzuni watoto wa wanadamu.
34 將世上所有的俘虜,都踐踏在腳下,
Kuwaponda chini ya nyayo wafungwa wote katika nchi,
35 在至上者前剝奪人的權利,
Kumnyima mtu haki zake mbele za Aliye Juu Sana,
36 與人爭訟時,欺壓他人:難道上主看不見﹖
kumnyima mtu haki: Je, Bwana asione mambo kama haya?
37 若非上主有命,誰能言出即成呢﹖
Nani awezaye kusema nalo likatendeka kama Bwana hajaamuru?
38 吉凶禍福,難道不是出自至上者之口﹖
Je, si ni kwenye kinywa cha Aliye Juu Sana ndiko yatokako maafa na mambo mema?
39 人生在世,為自己的罪受罰,為什麼還叫苦﹖
Mwanadamu yeyote aliye hai aweza kulalamika wakati anapoadhibiwa kwa ajili ya dhambi zake?
40 我們應檢討考察我們的行為,回頭歸向上主!
Tuzichunguze njia zetu na kuzijaribu, na tumrudie Bwana Mungu.
41 應向天上的大主,雙手奉上我們的心!
Tuinue mioyo yetu pamoja na mikono yetu kwa Mungu mbinguni, na tuseme:
42 正因為我們犯罪背命,你纔沒有寬恕。
“Tumetenda dhambi na kuasi nawe hujasamehe.
43 你藏在盛怒之中,追擊我們,殺死我們,毫不留情。
“Umejifunika mwenyewe kwa hasira na kutufuatilia; umetuchinja bila huruma.
44 你隱在濃雲深處,哀禱不能上達。
Unajifunika mwenyewe kwa wingu, ili pasiwe na ombi litakaloweza kupenya.
45 你使我們在萬民中,成了塵垢和廢物。
Umetufanya takataka na uchafu miongoni mwa mataifa.
46 我們所有的仇人,都向我們大張其口。
“Adui zetu wote wamefumbua vinywa vyao wazi dhidi yetu.
47 為我們只有恐怖和陷阱,破壞和滅亡。
Tumeteseka kwa hofu kuu na shida ya ghafula, uharibifu na maangamizi.”
48 為了我女兒──人民的滅亡,我的眼淚湧流如江河。
Vijito vya machozi vinatiririka kutoka machoni mwangu, kwa sababu watu wangu wameangamizwa.
49 我的眼淚湧流不止,始終不停,
Macho yangu yatatiririka machozi bila kukoma, bila kupata nafuu,
50 直到上主從天垂顧憐視,
hadi Bwana atazame chini kutoka mbinguni na kuona.
51 因我城中的一切女兒,使我觸目傷心。
Lile ninaloliona huniletea huzuni nafsini kwa sababu ya wanawake wote wa mji wangu.
52 我的仇人無故追捕我,像獵取飛鳥一樣;
Wale waliokuwa adui zangu bila sababu wameniwinda kama ndege.
53 他們將我投入坑穴之中,把石塊擲在我身上;
Walijaribu kukomesha maisha yangu ndani ya shimo na kunitupia mawe;
54 水淹沒了我的頭頂,我想:「我要死了! 」
maji yalifunika juu ya kichwa changu, nami nikafikiri nilikuwa karibu kukatiliwa mbali.
55 上主,我從坑穴深處,呼號你的聖名;
Nililiitia jina lako, Ee Bwana, kutoka vina vya shimo.
56 你曾俯聽過我的呼聲,對我的哀禱,不要掩耳不聞。
Ulisikia ombi langu: “Usikizibie masikio yako kilio changu nikuombapo msaada.”
57 在我呼號你的那一天,願你走近而對我說:「不要害怕! 」
Ulikuja karibu nilipokuita, nawe ukasema, “Usiogope.”
58 上主,你辯護了我的案件,贖回我的性命。
Ee Bwana, ulichukua shauri langu, ukaukomboa uhai wangu.
59 上主,你見我遭受冤屈,你替我伸了冤,
Umeona, Ee Bwana, ubaya niliotendewa. Tetea shauri langu!
60 你看見了他們對我的種種仇恨和陰謀。
Umeona kina cha kisasi chao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu.
61 上主,你聽見了他們加於我的種種侮辱和陰謀,
Ee Bwana, umesikia matukano yao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu:
62 你也聽見了反對我者的誹謗,和他們終日對我的企圖。
kile adui zangu wanachonongʼona na kunungʼunikia dhidi yangu mchana kutwa.
63 你看! 他們或坐或立,我始終是他們嘲笑的對象。
Watazame! Wakiwa wameketi au wamesimama, wananidhihaki katika nyimbo zao.
64 上主,求你按照他們雙手的作為,報復他們;
Uwalipe kile wanachostahili, Ee Bwana, kwa yale ambayo mikono yao imetenda.
65 求你使他們的心思頑固,並詛咒他們。
Weka pazia juu ya mioyo yao, laana yako na iwe juu yao!
66 上主,求你憤怒地追擊他們,將他們由普天之下除掉。
Wafuatilie katika hasira na uwaangamize kutoka chini ya mbingu za Bwana.

< 耶利米哀歌 3 >