< 耶利米哀歌 3 >
Mimi ndiye mtu aliyeona mateso kwa fimbo ya ghadhabu yake.
Amenifukuzia mbali na kunifanya nitembee gizani wala si katika nuru;
hakika, amegeuza mkono wake dhidi yangu tena na tena, mchana kutwa.
Amefanya ngozi yangu na nyama yangu kuchakaa na ameivunja mifupa yangu.
Amenizingira na kunizunguka kwa uchungu na taabu.
Amenifanya niishi gizani kama wale waliokufa.
Amenizungushia ukuta ili nisiweze kutoroka, amenifunga kwa minyororo mizito.
Hata ninapoita au kulia ili kuomba msaada, anakataa kupokea maombi yangu.
Ameizuia njia yangu kwa mapande ya mawe, amepotosha njia zangu.
10 上主之於我,像是一隻潛伏的狗熊,是一頭藏匿的獅子,
Kama dubu aviziaye, kama simba mafichoni,
ameniburuta kutoka njia, akanirarua na kuniacha bila msaada.
Amevuta upinde wake na kunifanya mimi niwe lengo kwa ajili ya mishale yake.
Alinichoma moyo wangu kwa mishale iliyotoka kwenye podo lake.
Nimekuwa kichekesho kwa watu wangu wote, wananidhihaki kwa wimbo mchana kutwa.
Amenijaza kwa majani machungu na kunishibisha kwa nyongo.
Amevunja meno yangu kwa changarawe, amenikanyagia mavumbini.
17 他除去了我心中的平安,我已經忘記了一切幸福;
Amani yangu imeondolewa, nimesahau kufanikiwa ni nini.
18 於是我說:「我的光榮已經消逝,對上主的希望也已經幻滅。」
Kwa hiyo nasema, “Fahari yangu imeondoka na yale yote niliyokuwa nimetarajia kutoka kwa Bwana.”
Nayakumbuka mateso yangu na kutangatanga kwangu, uchungu na nyongo.
Ninayakumbuka vyema, nayo nafsi yangu imezimia ndani yangu.
Hata hivyo najikumbusha neno hili na kwa hiyo ninalo tumaini.
Kwa sababu ya upendo mkuu wa Bwana, hatuangamii, kwa kuwa huruma zake hazikomi kamwe.
Ni mpya kila asubuhi, uaminifu wako ni mkuu.
24 我心中知道:上主是我的福分;因此,我必信賴他。
Nimeiambia nafsi yangu, “Bwana ni fungu langu, kwa hiyo nitamngojea.”
Bwana ni mwema kwa wale ambao tumaini lao ni kwake, kwa yule ambaye humtafuta;
ni vyema kungojea kwa utulivu kwa ajili ya wokovu wa Bwana.
Ni vyema mtu kuchukua nira bado angali kijana.
Na akae peke yake awe kimya, kwa maana Bwana ameiweka juu yake.
Na azike uso wake mavumbini bado panawezekana kuwa na matumaini.
Na atoe shavu lake kwa yule ampigaye, na ajazwe na aibu.
Kwa kuwa watu hawakatiliwi mbali na Bwana milele.
32 縱使懲罰,他必按照自己豐厚的慈愛,而加以憐憫。
Ingawa huleta huzuni, ataonyesha huruma, kwa kuwa upendo wake usiokoma ni mkuu.
Kwa maana hapendi kuwaletea mateso au huzuni watoto wa wanadamu.
Kuwaponda chini ya nyayo wafungwa wote katika nchi,
Kumnyima mtu haki zake mbele za Aliye Juu Sana,
kumnyima mtu haki: Je, Bwana asione mambo kama haya?
Nani awezaye kusema nalo likatendeka kama Bwana hajaamuru?
Je, si ni kwenye kinywa cha Aliye Juu Sana ndiko yatokako maafa na mambo mema?
Mwanadamu yeyote aliye hai aweza kulalamika wakati anapoadhibiwa kwa ajili ya dhambi zake?
Tuzichunguze njia zetu na kuzijaribu, na tumrudie Bwana Mungu.
Tuinue mioyo yetu pamoja na mikono yetu kwa Mungu mbinguni, na tuseme:
“Tumetenda dhambi na kuasi nawe hujasamehe.
43 你藏在盛怒之中,追擊我們,殺死我們,毫不留情。
“Umejifunika mwenyewe kwa hasira na kutufuatilia; umetuchinja bila huruma.
Unajifunika mwenyewe kwa wingu, ili pasiwe na ombi litakaloweza kupenya.
Umetufanya takataka na uchafu miongoni mwa mataifa.
“Adui zetu wote wamefumbua vinywa vyao wazi dhidi yetu.
Tumeteseka kwa hofu kuu na shida ya ghafula, uharibifu na maangamizi.”
48 為了我女兒──人民的滅亡,我的眼淚湧流如江河。
Vijito vya machozi vinatiririka kutoka machoni mwangu, kwa sababu watu wangu wameangamizwa.
Macho yangu yatatiririka machozi bila kukoma, bila kupata nafuu,
hadi Bwana atazame chini kutoka mbinguni na kuona.
Lile ninaloliona huniletea huzuni nafsini kwa sababu ya wanawake wote wa mji wangu.
Wale waliokuwa adui zangu bila sababu wameniwinda kama ndege.
Walijaribu kukomesha maisha yangu ndani ya shimo na kunitupia mawe;
maji yalifunika juu ya kichwa changu, nami nikafikiri nilikuwa karibu kukatiliwa mbali.
Nililiitia jina lako, Ee Bwana, kutoka vina vya shimo.
56 你曾俯聽過我的呼聲,對我的哀禱,不要掩耳不聞。
Ulisikia ombi langu: “Usikizibie masikio yako kilio changu nikuombapo msaada.”
57 在我呼號你的那一天,願你走近而對我說:「不要害怕! 」
Ulikuja karibu nilipokuita, nawe ukasema, “Usiogope.”
Ee Bwana, ulichukua shauri langu, ukaukomboa uhai wangu.
Umeona, Ee Bwana, ubaya niliotendewa. Tetea shauri langu!
Umeona kina cha kisasi chao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu.
Ee Bwana, umesikia matukano yao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu:
62 你也聽見了反對我者的誹謗,和他們終日對我的企圖。
kile adui zangu wanachonongʼona na kunungʼunikia dhidi yangu mchana kutwa.
63 你看! 他們或坐或立,我始終是他們嘲笑的對象。
Watazame! Wakiwa wameketi au wamesimama, wananidhihaki katika nyimbo zao.
Uwalipe kile wanachostahili, Ee Bwana, kwa yale ambayo mikono yao imetenda.
Weka pazia juu ya mioyo yao, laana yako na iwe juu yao!
66 上主,求你憤怒地追擊他們,將他們由普天之下除掉。
Wafuatilie katika hasira na uwaangamize kutoka chini ya mbingu za Bwana.