< 士師記 3 >
1 上主保留的民族 這是上主為考驗那些不曉得客納罕一切戰事的以色列人,所留下來的民族,
Sasa Bwana aliyaacha mataifa haya yaijaribu Israeli, yaani kila mtu katika Israeli ambaye hakushiriki vita yoyote huko Kanaani.
2 叫以色列子民的後代,至少那些以前不曉得這些戰事的人,知道和學習作戰。
(Alifanya hivyo ili kuwafundisha vita kizazi kipya cha Waisraeli ambao hawakujua kabla).
3 這些民族就是培勒舍特人的五個酋長,一切客納罕人、漆冬人和住在黎巴嫩山上,即從巴耳赫爾孟山直到哈瑪特關口的希威人。
Haya ndio mataifa: wafalme watano kutoka kwa Wafilisti, Wakanaani wote, Wasidoni, na Wahivi waliokaa milima ya Lebanoni, kutoka Mlima Baali Hermoni hadi Hamathi.
4 他們留在那裏是為考驗以色列人,看他們是否聽從上主藉梅瑟吩咐他們祖先的那些誡命。
Mataifa haya yaliachwa kama njia ambayo Bwana angeijaribu Israeli, kuthibitisha kama watazitii amri alizowapa babu zao kupitia Musa.
5 以色列子民就住在客納罕人、赫特人、阿摩黎人、培黎齊人、希威人和耶步斯人中間,
Basi wana wa Israeli wakakaa kati ya Wakanaani, na Wahiti, na Waamori, na Waperizi, na Wahivi, na Wayebusi.
6 竟然娶了他們的女子為妻,也把自己的女兒嫁給他們的兒子,事奉了他們的神。敖特尼耳民長
Waliwachukua binti zao kuwa wake zao, nao wakawapa wana wao binti zao, nao wakaitumikia miungu yao.
7 以色列子民行了上主視為惡的事,忘卻了上主他們的天主,而事奉了巴耳諸神和阿舍辣諸女神;
Wana wa Israeli walifanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, wakamsahau Bwana, Mungu wao. Waliabudu Baali na Asherah.
8 因此上主對以色列大發忿怒,將他們交在厄東王雇商黎沙塔殷手中,以色列子民遂服事了雇商黎沙塔殷八年。
Basi, hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawauza mkononi mwa Kushan-rishathaimu mfalme wa Aram Naharaimu. Watu wa Israeli walitumikia Kushan Rishathaimu kwa miaka nane.
9 當以色列子民向上主呼籲時,上主給以色列子民興起了一個拯救他們的救星,即加肋布的弟弟刻納次的兒子敖特尼耳。
Watu wa Israeli walipomwomba Bwana, Bwana akamuinua mtu atakayewasaidia wana wa Israeli, na mtu atakayewaokoa: Othnieli mwana wa Kenazi (ndugu mdogo wa Kalebu).
10 上主的神降在他身上,他作了以色列的民長,出去作戰;上主把厄東王雇商黎沙塔殷交在他手中,他的`能力勝過了雇商黎沙塔殷。
Roho wa Bwana akamtia nguvu, naye akahukumu Israeli na akatoka kwenda vitani. Bwana akampa kuishinda Kush-rishataimu mfalme wa Aramu. Mkono wa Othnieli alishinda Kushan Rishathaimu.
11 於是四境平安了四十年。厄胡得民長刻納次的兒子敖特尼耳去世後,
Nchi ilikuwa na amani kwa miaka arobaini. Ndipo Otinieli mwana wa Kenazi akafa.
12 以色列子民又行了上主視為惡的事,上主就強化摩阿布王厄革隆去打以色列,因為他們行了上主視為惡的事。
Baada ya hayo, Waisraeli wakafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana; Bwana akampa Egloni mfalme wa Moabu nguvu, kuwashinda Waisraeli.
13 他聯合了阿孟子民和阿瑪肋克人,前來擊敗以色列,佔據了棕樹城;
Eglon alijiunga na wana wa Amoni na Waamaleki wakaenda na kuwashinda Israeli, na walichukua mji wa Mitende.
Watu wa Israeli walimtumikia Eglon mfalme wa Moabu kwa miaka kumi na nane.
15 當以色列子民向上主呼籲時,上主給他們興起了一位拯救者,就是本雅明人革辣的兒子厄胡得,他是左右手能兼用的人;以色列子民便派他給摩阿布王厄革隆獻貢物。
Wana wa Israeli walipomwomba Bwana, Bwana akamwinua mtu aliyewasaidia, Ehudi mwana wa Gera, Mbenjamini, mtu shoto. Wana wa Israeli wakamtuma kwa Egloni, mfalme wa Moabu, kwa malipo yao ya kodi.
16 厄胡得預備了一把一肘長的雙刃刀,插在右腿衣服底下,
Ehudi akajifanyia upanga uliokuwa na makali kuwili, urefu wa dhiraa moja; aliufunga chini ya nguo zake juu ya mguu wake wa kulia.
17 來到摩阿布王厄革隆前獻貢物─厄革隆原是極肥胖的人。
Akampa Egloni Mfalme wa Moabu malipo ya kodi. (Egloni alikuwa mtu mnene sana.)
Baada ya Ehudi kulipa malipo ya kodi, aliondoka na wale waliokuwa wameibeba.
19 自己卻由基耳加耳柱像那裏退回,說:「王呀! 我有機密事要對你說。」王說:「退下! 」於是侍立左右的人都退去。
Hata hivyo Ehudi mwenyewe, alipofikia mahali ambapo sanamu za kuchonga zilitengenezwa karibu na Gilgali, akageuka na kurudi, akasema, 'Nina ujumbe wa siri kwako, mfalme wangu.' Eglon akasema, 'Nyamazeni kimya!' Kwa hiyo wote waliomtumikia wakatoka kwenye chumba.
20 厄胡得來到他跟前,他正獨自坐在涼台上的房子裏;厄胡得說:「我有神諭告訴你! 」王就從自己的座位上起立;
Ehudi akaja kwake. Mfalme alikuwa amekaa peke yake, peke yake katika chumba cha juu cha baridi. Ehudi akasema, 'Nina ujumbe kutoka kwa Mungu kwa ajili yeko.' Mfalme akasimama kutoka katika kiti chake.
21 厄胡得遂伸左手從右腿上拔出刀來,刺入他的腹部,
Ehudi akanyoosha mkono wake wa kushoto na akachukua upanga kutoka mguu wake wa kulia, na akautia ndani ya mwili wa mfalme.
22 柄和刀都刺了進去,脂肪遂包住了刀子,他沒有從肚子裏把刀抽出來;
Na kipini cha upanga kikaingia ndani yake baada ya upanga, nao ukatokea nyuma yake, na mafuta yakashikamana juu ya upanga, kwa kuwa Ehudi hakuutoa upanga nje ya mwili wake.
23 厄胡得出來到了走廊,把涼台上的門關上,上了鎖。
Kisha Ehudi akatoka kwenye ukumbi na akafunga milango ya chumba cha juu nyuma yake na akawafungia.
24 他出去之後,王臣前來,看見涼台的房門關著,就說:「他一定在涼台上的內室裏便溺。」
Baada ya Ehudi kuondoka, watumishi wa mfalme wakaja; wakaona milango ya chumba cha juu imefungwa, kwa hiyo wakafikiri, 'Hakika atakuwa anajitoa mwenyewe katika hali ya baridi ya chumba cha juu.'
25 待他們等煩了,看見沒有人來開涼台上的門,他們就拿鑰匙把門開了,見他們的主子躺在地上死了。
Walizidi kuwa na wasiwasi hata walipoanza kuhisi kuwa walikuwa wakipuuza wajibu wao wakati mfalme bado hakufungua milango ya chumba cha juu. Kwa hiyo walichukua ufunguo wakawafungua, tazama bwana wao, ameanguka chini, amekufa.
26 在他們猶豫的時候,厄胡得已經逃走,繞過柱像,而逃往色依辣。
Wakati watumishi wakisubiri, wakijiuliza nini wanapaswa kufanya, Ehudi alikimbia na kupita mahali ambako kulikuwa na sanamu za kuchonga, na hivyo akakimbia kwenda Seira.
27 他到了那裏,就在厄弗辣因山地吹號角,以色列子民就同他由山地下來,他在他們前面,
Alipofika, alipiga tarumbeta katika nchi ya mlima wa Efraimu. Kisha wana wa Israeli wakashuka pamoja naye kutoka milimani, naye akawaongoza.
28 對他們說:「你們緊跟著我,因為上主把你們的仇敵摩阿布人已交於你們手中! 」他們遂跟他下去,佔據了摩阿布對面的約但河渡口,不許一人渡過。
Akawaambia, Nifuate, kwa kuwa Bwana atawashinda adui zenu, Wamoabu. Wakamfuata, wakakamata vivuko vya Bonde la Yordani, toka kwa Wamoabi, wala hawakuruhusu mtu yeyote kuvuka mto.
29 就在那個時候,他們擊殺了摩阿布人約有一萬,都是壯丁和兵士,沒有一個人逃脫。
Wakati huo waliwaua watu elfu kumi wa Moabu, na wote walikuwa watu wenye nguvu na wenye uwezo. Hakuna aliyekimbia.
30 從那天起,摩阿布驅服於以色列手下;境內平安了十八年。沙默加爾民長
Kwa hiyo siku hiyo Moabu ilishindwa na nguvu ya Israeli. Na nchi ilikuwa na amani kwa miaka thelathini.
31 在他以後,有阿納特的兒子沙默加爾,他意趕牛棒擊殺了六百培肋舍人,拯救了以色列。
Baada ya Ehudi, mwamuzi aliyefuata alikuwa Shamgari mwana wa Anathi ambaye aliwaua Wafilisti 600 kwa konzo la ng'ombe. Pia aliwaokoa Israeli kutoka kwenye hatari.