< 約書亞記 2 >
1 農的兒子若蘇厄由史廷暗中派出兩個人作偵探說:「你們去察看那地和耶利哥! 」他們就去了,來到一個名叫辣哈布的妓女家中,就住在那裏。
Kisha Yoshua mwana wa Nuni kwa siri akawatuma wapelelezi wawili kutoka Shitimu, akawaambia, “Nendeni mkaikague hiyo nchi, hasa Yeriko.” Kwa hiyo wakaenda na kuingia kwenye nyumba ya kahaba mmoja jina lake Rahabu na kukaa humo.
2 有人報告耶里哥王說:「夜間有兩個以色列人到了這裡,偵探這地方。」
Mfalme wa Yeriko akaambiwa, “Tazama! Baadhi ya Waisraeli wamekuja huku usiku huu kuipeleleza nchi.”
3 耶里哥王遂派人到辣哈布那裡說:「將那來到你家中的兩個人交出來,因為他們是來偵探這地方的。」
Hivyo mfalme wa Yeriko akatuma huu ujumbe kwa Rahabu: “Watoe wale watu waliokujia na kuingia nyumbani mwako, kwa sababu wamekuja kuipeleleza nchi yote.”
4 但是那女人預先將那兩個人藏起來,就這樣回答說:「那兩個人的確來過我這裡,但他們是從那裡來的,我卻不知道。
Lakini huyo mwanamke alikuwa amewachukua hao watu wawili na kuwaficha. Akasema, “Naam, watu hao walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka.
5 天黑快關城門時,他們兩人出去了;往那裡去了,我也不知道。你們快去追趕,也許還可趕上他們。」
Kulipoingia giza, wakati wa kufunga lango la mji, watu hao waliondoka. Sijui njia waliyoiendea. Wafuatilieni haraka. Huenda mkawapata.”
6 原來她叫那兩個人上了屋頂,藏在她屋頂上堆積的麻秸內。
(Lakini alikuwa amewapandisha darini akawafunika kwa mabua ya kitani aliyokuwa ameyatandika darini.)
7 來問的人便沿著約但河,直向渡口去追趕;追趕的人一出去,城門就關了。
Basi hao watu wakaondoka kuwafuatilia hao wapelelezi katika njia ile inayoelekea vivuko vya Yordani, mara tu wafuatiliaji walipotoka nje, lango likafungwa.
Kabla wale wapelelezi hawajalala, Rahabu akawaendea huko juu darini,
9 對他們二人說:「我知道上主已將這地方交給了你們;你們真叫我們害怕,此地所有的居民,對你們都恐懼不已。
akawaambia, “Ninajua kuwa Bwana amewapa nchi hii na hofu kuu imetuangukia kwa sababu yenu, kiasi kwamba wote waishio katika nchi hii wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yenu.
10 因為我們聽說,你們出埃及時,上主怎樣使紅海在你們面前乾涸;你們又怎樣對待了約但河東岸的兩個阿摩黎王,即息紅和敖格,將他們完全消滅。
Tumesikia jinsi Bwana alivyokausha maji ya Bahari ya Shamu kwa ajili yenu mlipotoka Misri, pia lile mlilowatendea Sihoni na Ogu, wafalme wawili wa Waamori mashariki mwa Yordani, ambao mliwaangamiza kabisa.
11 我們聽了,心都冷了,沒有一人再有勇氣來對抗你們,因為上主你們的天主,就是上天下地的天主。
Tuliposikia juu ya hili, mioyo yetu iliyeyuka na kila mmoja alikosa ujasiri kwa sababu yenu, kwa maana Bwana Mungu wenu ni Mungu juu mbinguni na duniani chini.
12 現在請你們指著上主對我起誓,我既然恩待了你們,你們也要恩待我的父家,請給我一個安全的保證,
Sasa basi, tafadhali niapieni kwa Bwana, kwamba mtaitendea hisani jamaa ya baba yangu, kwa kuwa mimi nimewatendea hisani. Nipeni ishara ya uaminifu
13 使我的父母、兄弟、姊妹和他們所有的一切人,都能生存,救我們的性命免於死亡。」
kwamba mtayahifadhi maisha ya baba yangu na mama yangu, ndugu zangu wa kiume na wa kike, pamoja na wale wote walio wa kwao na kwamba mtatuokoa na kifo.”
14 他們二人回答她說:「如果你不洩漏我們的約定,我們願拿性命為你們擔保;當上主將這地方交給我們時,我們必慈善忠厚地對待你。」
Wale watu wakamhakikishia Rahabu, “Uhai wetu kwa uhai wenu! Ikiwa hutatoa habari ya nini tunachofanya, wakati Bwana atakapotupa nchi hii, tutawatendea kwa hisani na kwa uaminifu.”
15 那女人於是用繩子將他們二人由窗戶縋下去,因為她的房屋是在城牆上,她也住在城牆上。
Kisha akawateremsha dirishani kwa kamba, kwa kuwa nyumba yake aliyokuwa anaishi ilikuwa sehemu ya ukuta wa mji.
16 她又對他們說:「你們要往山中去,免得追趕的人遇見你們。你們在那裡躲藏三天,等追趕的人回來,然後再上道。」
Alikuwa amewaambia, “Nendeni vilimani ili wale wafuatiliaji wasiwapate. Jificheni huko kwa siku tatu mpaka watakaporudi, hatimaye mwende zenu.”
17 他們二人對她說:「如果你不這樣作,你叫我們所起的誓,我們將不負責:
Wale watu wakamwambia, “Hiki kiapo ulichotuapisha hakitatufunga,
18 就是當我們再到這地方時,你應將這根朱紅線繫在你縋下我們的窗戶上,並且叫你的父母、兄弟和你父親全家人口,都聚集在你這屋內。
isipokuwa, hapo tutakapoingia katika nchi hii, utakuwa umefunga hii kamba nyekundu dirishani pale ulipotuteremshia na kama utakuwa umewaleta baba yako na mama yako, ndugu zako na jamaa yako yote ndani ya nyumba yako.
19 誰若走出你的屋門,他的血應由他自己承當,我們不負責任;但凡同你在屋內的,如有人下手加害他,他的血將由我們承當。
Ikiwa mtu yeyote atatoka nje ya nyumba yako akaenda mtaani, damu yake itakuwa juu ya kichwa chake mwenyewe, hatutawajibika. Lakini yule ambaye atakuwa ndani pamoja nawe, kama mkono wa mtu yeyote ukiwa juu yake damu yake itakuwa juu ya vichwa vyetu.
20 但是你若洩漏了我們的約定,那麼,你叫我們所起的誓,我們便不負責。」
Lakini ikiwa utatoa habari ya shughuli yetu tunayofanya, tutakuwa tumefunguliwa kutoka kwenye kiapo hiki ulichotufanya tuape.”
21 她回答說:「就照你們說的做罷!」於是打發他們二人走了。他們走後,她遂把那根朱紅線繫在她的窗戶上。
Naye akajibu, “Nimekubali. Na iwe kama mnavyosema.” Kwa hiyo akaagana nao, nao wakaondoka. Yeye akaifunga ile kamba nyekundu dirishani.
22 他們出去,到了山上,在那裡住了三天,直到追趕的人回去。追趕的人一路尋找他們,結果沒有找到。
Walipoondoka, wakaelekea vilimani na kukaa huko siku tatu, hadi wale waliokuwa wakiwafuatilia wakawa wamewatafuta njia nzima na kurudi pasipo kuwapata.
23 他們二人轉身,由山上下來,渡過了約但河,回到農的兒子若蘇厄那裡,將他們所遇見的事,一一報告給他。
Ndipo wale watu wawili wakaanza kurudi. Wakashuka kutoka kule vilimani, wakavuka mto na kuja kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kumweleza kila kitu kilichowapata.
24 他們對若蘇厄說:「上主實在已將那整個地域交在我們手中,因為那地方的居民對我們都十分恐懼。」
Wakamwambia Yoshua, “Hakika Bwana ametupa nchi yote mikononi mwetu; watu wote wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yetu.”