< 約翰福音 17 >

1 穌講完了這些話,便舉目向天說:「父啊!時辰來到了,求你光榮你的子,好叫子也光榮你:
Yesu aliyasema mambo haya; kisha akainua macho yake kuelelea mbinguni na akasema, “Baba, saa imewadia; mtukuze mwanao ili na mwana naye akutukuze wewe -
2 因為你賜給了他權柄掌管凡有血肉的人,是為叫他將永生賜給一切你所賜給他的人。 (aiōnios g166)
kama vile ulivyompatia mamlaka juu ya vyote vyenye mwili ili awape uzima wa milele wale wote uliompatia. (aiōnios g166)
3 永生就是:認識你,唯一的真天主,和你所派遣來的耶穌基督。 (aiōnios g166)
Huu ndio uzima wa milele: kwamba wakujue wewe, Mungu wa kweli na wa pekee, na yeye uliyemtuma, Yesu Kristo. (aiōnios g166)
4 我在地上,已光榮了你,完成了你所委託我所作的工作。
Nilikutukuza hapa duniani, na kuikamilisha kazi uliyonipa niifanye.
5 父啊! 現在,在你面前光榮我罷!賜給我在世界未有以前,我在你前所有的光榮罷!」
Sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja na wewe mwenyewe kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja na wewe kabla ya ulimwengu kuumbwa.
6 「我已將你的名,顯示給那些你由世界中所賜給我的人。他們原屬於你,你把他們托給了我,他們也遵守了你的話。
Nililifunua jina lako kwa watu ulionipa hapa duniani. Walikuwa watu wako; lakini ulinikabidhi mimi. nao wamelishika neno lako.
7 現在他們已知道:凡你賜給我的,都是由你而來的,
Sasa wanajua kuwa kila kitu ulichonipa mimi kinatoka kwako,
8 因為你所授給我的話,我都傳給了他們;他們也接受了,也確實知道我是出於你,並且信是你派遣了我。
kwa maneno yale uliyonipatia mimi— Nimekwisha wapatia wao maneno hayo. Waliyapokea na kweli wakajua ya kuwa mimi nimetoka kwako, na wakaamini kuwa wewe ndiye uliyenituma.
9 我為他們祈求,不為世界祈求,只為你賜給我的人祈求,因為他們原是屬於你的。
Ninawaombea wao. Siuombei ulimwaengu bali wale ulionipa kwa kuwa wao ni wako.
10 我的一切都是你的,你的一切都是我的: 因他們已受到了光榮。
Vitu vyote ambavyo ni vyangu ni vyako, na vile ulivyonavyo wewe ni vyangu; nami ninatukuzwa katika hivyo.
11 從今以後,我不在世界上了,但他們仍在世界上,我卻到你那裏去。聖父啊! 求你因你的名,保全那些你所賜給我的人,使他們合而為一,正如我們一樣。
Mimi simo tena ulimwenguni, bali wao wamo ulimwenguni, nami sasa naja kwako. Baba Mtakatifu, watunze kwa jina lako lile ulilonipa sisi ili wao nao wawe na umoja, kama vile mimi na wewe tulivyo na umoja.
12 當我和他們同在時,我因你的名,保全了你所賜給我的人,護衛了他們,其中除了那喪亡之子,沒有喪亡一個,這是應驗經上的話。
Nilipokuwa nao, niliwalinda kwa jina ulilonipa; Niliwalinda, na hakuna hata mmoja wao aliyepotea isipokuwa mwana wa upotevu, ili kwamba maandiko yatimie.
13 但如今我到你那裏去,我在世上講這話,是為叫他們的心充滿我的喜樂。
Sasa ninakuja kwako; lakini ninasema haya ulimwenguni ili kwamba furaha yangu ikamilishwe ndani yao wenyewe.
14 我己將你的話授給了他們,世界卻憎恨他們,因為他們不屬於世界,就如我不屬於世界一樣。
Nimewapa neno lako; ulimwengu imewachukia kwa sababu wao si wa ulimwengu, kama vile mimi nisivyokuwa wa ulimwengu
15 我不求你將世界上撤去,只求你保護他們脫免邪惡。
Siwaombei kwamba uwatoe ulimwenguni bali uwalinde na yule mwovu.
16 他們不屬於世界,就如我不屬於世界一樣。
Wao si wa dunia kama vile mimi nisivyokuwa wa ulimwenguni.
17 求你以真理祝聖他們,你的話就是真理。
Uwaweke wakfu kwako mwenyewe katika Kweli; neno lako ndiyo kweli.
18 就如你派遣我到世界上來,照樣我也派遣他們到世界上去。
Ulinituma ulimwenguni, nami nimewatuma ulimwenguni.
19 我為他們祝聖我自己,為叫他們也因真理而被祝聖。」「
Kwa ajili yao mimi mwenyewe ninajitoa kwako ili kwamba na wao wajitoe kwako kwa ile kweli.
20 我不但為他們祈求,而且也為那些因他們的話而信從我的人祈求。
Si hawa tu ninaowaombea, bali na wale watakaoamini kupitia neno lao
21 願眾人都合而為一! 父啊! 願他們在我們內合而為一,就如內你在我內,我在你內,為叫世界相信是你派遣了我。
ili kwamba wao nao wawe na umoja, kama vila wewe Baba, ulivyo ndani yangu nami ndani yako. Nawaombea ili kwamba wao pia waweze kuwa ndani yetu ili ulimwengu uweze kuamini kuwa wewe ndiye uliyenituma.
22 我將你賜給我的光榮賜給了他們,為叫他們合而為一,就如我們原為一體一樣。
Utukufu ule ulionipa mimi - nimewapa wao, ili kwamba waweze kuwa na umoja, kama vile sisi tulivyo umoja -
23 我在他們內,你在我內,使他們完全合而為一,為叫世界知道是你派遣了我,並且你愛了他們,如愛了我一樣。
Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili waweze kukamilishwa katika umoja; ili ulimwengu ujue kuwa hakika wewe ndiye uliyenituma, na kuwapenda, kama vile wewe ulivyonipenda, mimi.
24 父啊! 你所賜給我的人,我願我在那裏,他們也同我在一起,使他們享見你所賜給我的光榮,因為你在創世之前,就愛了我。
Baba, kile ulichonipa mimi - Natamani kwamba wao pia waweze kuwa pamoja nami mahali nilipo ili waweze kuona utukufu wangu, ule ulionipa: kwa kuwa wewe ulinipenda mimi kabla ya kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu.
25 公義的父啊! 世界沒有認識你,我卻認識了你,這些人也知道是你派遣了我。
Baba mwenye haki, ulimwengu haukukujua wewe, lakini mimi nakujua wewe; na wanajua kwamba ulinituma.
26 我已將你的名宣示給他們了,我還要宣示,好使你愛我的愛,在他們內,內我也在他們內。」
Nililifanya jina lako lijulikane kwao, na nitalifanya lijulikane ili kwamba lile pendo ambalo kwalo ulinipenda mimi liweze kuwa ndani yao, na mimi niweze kuwa ndani yao.”

< 約翰福音 17 >