< 約伯記 41 >

1 你豈能以魚鉤鉤上鱷魚﹖以繩索縛住牠的舌頭﹖
“Je, waweza kumvua Lewiathani kwa ndoano ya samaki, au kufunga ulimi wake kwa kamba?
2 你豈能以鼻圈穿過牠的鼻子,以鉤子刺透牠的腮骨﹖
Waweza kupitisha kamba puani mwake, au kutoboa taya lake kwa kulabu?
3 牠豈能再三向你哀求,向你說甜言蜜語﹖
Je, ataendelea kukuomba umhurumie? Atasema nawe maneno ya upole?
4 牠豈能同你訂立盟約,使自己常作你的奴隸﹖
Je, atafanya agano nawe ili umtwae awe mtumishi wako maisha yake yote?
5 你豈能玩弄牠像玩弄小鳥,將牠縛著作你女兒的玩物﹖
Je, utamfuga na kumfanya rafiki kama ndege, au kumfunga kamba kwa ajili ya wasichana wako?
6 結夥的漁人不是想在牠身上謀利,將牠售與商人﹖
Je, wafanyabiashara watabadilishana bidhaa kwa ajili yake? Watamgawanya miongoni mwa wafanyao biashara?
7 你豈能以長矛穿透牠的皮,以魚叉刺透牠的頭顱﹖
Je, waweza kuijaza ngozi yake kwa vyuma vyenye ncha kali, au kichwa chake kwa mkuki wa kuvulia samaki?
8 將你的掌撫在牠身上罷! 若你想到惡鬥,決不敢再撫。
Kama ukiweka mkono wako juu yake, utavikumbuka hivyo vita na kamwe hutarudia tena!
9 看,人的希望落了空,並且一見牠就嚇壞了。
Tumaini lolote la kumtiisha ni kujidanganya; kule kumwona tu kunamwangusha mtu chini.
10 沒有一個勇敢的人敢觸犯牠,有誰還敢站立在牠前面呢﹖
Hakuna yeyote aliye mkali athubutuye kumchokoza. Ni nani basi awezaye kusimama dhidi yangu?
11 誰攻擊牠,而能安全無恙﹖普天之下沒有一人!
Ni nani mwenye madai dhidi yangu ili nipate kumlipa? Kila kitu kilicho chini ya mbingu ni mali yangu.
12 論牠的四體百肢,我不能緘默;論牠的力量,我要說:沒有可與牠相比的。
“Sitashindwa kunena juu ya maungo yake, nguvu zake na umbo lake zuri.
13 誰能揭開牠的外衣,誰能穿透牠雙層的鱗甲﹖
Ni nani awezaye kumvua gamba lake la nje? Ni nani awezaye kumsogelea na lijamu?
14 誰敢啟開牠的口﹖牠四周的牙齒,令人戰慄。
Nani athubutuye kuufungua mlango wa kinywa chake, kilichozungukwa na meno yake ya kutisha pande zote?
15 牠的脊背有如盾甲,好像為石印所密封。
Mgongo wake una safu za ngao zilizoshikamanishwa imara pamoja;
16 鱗甲片片相連,氣也透不進去:
kila moja iko karibu sana na mwenzake, wala hakuna hewa iwezayo kupita kati yake.
17 互相聯結,黏在一起不可分離。
Zimeunganishwa imara kila moja na nyingine; zimengʼangʼaniana pamoja wala haziwezi kutenganishwa.
18 牠的噴嚏發出白光,眼睛像旭日閃動。
Akipiga chafya mwanga humetameta; macho yake ni kama mionzi ya mapambazuko.
19 火把從牠口中噴出,火花四射。
Mienge iwakayo humiminika kutoka kinywani mwake; cheche za moto huruka nje.
20 煙從牠鼻孔冒出,宛如燃燒沸騰的鍋鑪。
Moshi hufuka kutoka puani mwake, kama kutoka kwenye chungu kinachotokota kwa moto wa matete.
21 牠的氣息可點燃煤炭,火燄由牠口中射出。
Pumzi yake huwasha makaa ya mawe, nayo miali ya moto huruka kutoka kinywani mwake.
22 牠的力量集中在牠的頸上,在牠面前,沒有不恐怖的。
Nguvu hukaa katika shingo yake; utisho hutangulia mbele yake.
23 牠的肌肉互相連結,緊貼牠身,堅不可動。
Mikunjo ya nyama yake imeshikamana imara pamoja; iko imara na haiwezi kuondolewa.
24 牠的心堅如石塊,堅硬有如磨磐。
Kifua chake ni kigumu kama mwamba, kigumu kama jiwe la chini la kusagia.
25 牠一起立,壯士戰慄,驚慌失措。
Ainukapo, mashujaa wanaogopa; hurudi nyuma mbele yake anapokwenda kwa kishindo.
26 人若想捕捉牠,刀、槍、箭、戟都是徒然。
Upanga unaomfikia haumdhuru, wala mkuki au mshale wala fumo.
27 牠視鐵如草芥,視銅若朽木。
Chuma hukiona kama unyasi, na shaba kama mti uliooza.
28 弓矢不能使牠遁逃;機石打在牠身上好似碎湝。
Mishale haimfanyi yeye akimbie; mawe ya kombeo kwake ni kama makapi.
29 牠視棍棒像麥湝,對射來的箭矢冷笑。
Rungu kwake huwa kama kipande cha jani kavu; hucheka sauti za kugongana kwa mkuki.
30 牠腹下似尖瓦,牠行過之地,有如打禾機碾過。
Sehemu zake za chini kwenye tumbo zina menomeno na mapengo kama vigae vya chungu, zikiacha mburuzo kwenye matope kama chombo chenye meno cha kupuria.
31 牠使深淵沸騰有如沸鼎,使海洋沸騰有如油鍋。
Huvisukasuka vilindi kama sufuria kubwa ichemkayo, na kukoroga bahari kama chungu cha marhamu.
32 牠游過之路發出銀光,令人以為海洋飄揚白髮。
Anapopita nyuma yake huacha mkondo unaometameta; mtu angedhani vilindi vilikuwa na mvi.
33 世上沒有可與牠相比的,牠一無所懼。
Hakuna chochote duniani kinacholingana naye: yeye ni kiumbe kisicho na woga.
34 牠卑視所有的巨獸,牠在猛獸中稱王。
Yeye huwatazama chini wale wote wenye kujivuna; yeye ni mfalme juu ya wote wenye kiburi.”

< 約伯記 41 >