< 耶利米書 2 >
Neno la Bwana lilinijia kusema,
2 「你去! 向耶路撒冷大聲疾呼說:上主這樣說:我憶起你年青時的熱情,你訂婚時的戀愛;那你在曠野裏,在未耕種的地上追隨了我。
“Nenda ukahubiri masikioni mwa watu wa Yerusalemu: “‘Nakumbuka moyo wako wa uchaji katika ujana wako, jinsi ulivyonipenda kama bibi arusi na kunifuata katika jangwa lile lote, katika nchi isiyopandwa mbegu.
3 以色列成了上主的聖民,成了衪收穫的初果,凡舌食她的都要有罪,災禍必要降在他們身上──上主的斷語。
Israeli alikuwa mtakatifu kwa Bwana, kama malimbuko ya kwanza ya mavuno yake; wote waliowaangamiza walihesabiwa kuwa na hatia, nayo maafa yaliwakumba,’” asema Bwana.
4 雅各伯家和以色列家的一切家族! 你們聽上主的話,
Sikia neno la Bwana, ee nyumba ya Yakobo, nanyi nyote jamaa za nyumba ya Israeli.
5 上主這樣說:你們的祖先在我身上發現了什麼不義竟遠離我而去追隨「虛無」,自成為虛無呢﹖
Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “Je, baba zenu waliona kosa gani kwangu, hata wakatangatanga mbali nami hivyo? Walifuata sanamu zisizofaa, nao wenyewe wakawa hawafai.
6 他們也不問一問:那曾引我們由埃及地上來,那經過曠野、荒原和崎嶇之地,乾旱和黑暗之地,沒人遊歷無人居住之地,引領我們的上主現在在哪裏呢﹖
Hawakuuliza, ‘Yuko wapi Bwana, aliyetupandisha kutoka Misri na kutuongoza kupitia nyika kame, kupitia nchi ya majangwa na mabonde, nchi ya ukame na giza, nchi ambayo hakuna mtu asafiriye ndani yake wala hakuna mtu aishiye humo?’
7 我引領你們進入了肥沃的土地,吃其中的出產和美物;但你們一進來,就玷污了我的土地,使我的產業成了可憎之物。
Niliwaleta katika nchi yenye wingi wa vitu ili mpate kula matunda yake na utajiri wa mazao yake. Lakini mkaja na kuinajisi nchi yangu, na kuufanya urithi wangu chukizo.
8 司祭們也不問一問:「上主在哪裏﹖」那些管理法律的,不認識我了;那些為人牧的,叛離了我;先知們也奉巴耳講預言,追隨無能的神袛。
Makuhani hawakuuliza, ‘Yuko wapi Bwana?’ Wale wanaoshughulikia sheria hawakunijua mimi; viongozi waliasi dhidi yangu. Manabii walitabiri kwa jina la Baali, wakifuata sanamu zisizofaa.
9 為此,我要控訴你們──上主的斷語,也要控訴你們的子孫
“Kwa hiyo naleta tena mashtaka dhidi yako,” asema Bwana. “Nami nitaleta mashtaka dhidi ya watoto wa watoto wako.
10 好吧! 你們往基廷島嶼去觀察一下,派人到刻達爾去詳細調察,看看巾沒有與此相類似的事:
Vuka, nenda ngʼambo mpaka pwani ya Kitimu nawe uangalie, tuma watu waende Kedari, wachunguze kwa makini, uone kama kumekuwepo kitu kama hiki.
11 難道有一個民族更換了自己的神袛﹖──雖然他們並非真神;但是我的人民竟以自己的光榮換取了一個「無能的東西。」
Je, taifa limebadili miungu yake wakati wowote? (Hata ingawa hao si miungu kamwe.) Lakini watu wangu wamebadili Utukufu wao kwa sanamu zisizofaa kitu.
12 諸天! 你們對此應驚駭戰慄,大為驚異──上主的斷語,
Shangaeni katika hili, ee mbingu, nanyi tetemekeni kwa hofu kuu,” asema Bwana.
13 因為我的人民犯了雙重的罪惡:他們離棄了我這活水的泉源,卻給自己掘了蓄水池,不能蓄水的漏水池。
“Watu wangu wametenda dhambi mbili: Wameniacha mimi, niliye chemchemi ya maji yaliyo hai, nao wamejichimbia visima vyao wenyewe, visima vilivyobomoka, visivyoweza kuhifadhi maji.
14 以色列豈是 奴隸,或是家生的奴隸﹖為什麼竟成了人的掠奪物﹖
Je, Israeli ni mtumishi, yaani mtumwa kwa kuzaliwa? Kwa nini basi amekuwa mateka?
15 獅子向她咆哮,高聲吼叫:牠們使她的地域變成了荒野,使她的城市化為灰燼,無人居住。
Simba wamenguruma; wamemngurumia. Wameifanya nchi yake kuwa ukiwa; miji yake imeteketezwa, nayo imeachwa haina watu.
Pia watu wa Memfisi na Tahpanhesi wamevunja taji ya kichwa chako.
17 你這不是自作自受嗎﹖因為上主你的天主在路上引導你的時候,你竟離棄了衪。
Je, hukujiletea hili wewe mwenyewe kwa kumwacha Bwana, Mungu wako alipowaongoza njiani?
18 現在你又為什麼路到埃及去喝尼羅河的水,跑到亞述去喝幼發拉的河水﹖
Sasa kwa nini uende Misri kunywa maji ya Shihori? Nawe kwa nini kwenda Ashuru kunywa maji ya Mto Frati?
19 是你的罪惡懲罰你,是你的不忠責斥你,那麼你應該明白覺察:離棄上主你的天主,對我沒有敬畏,是如何邪惡和痛苦的事──吾主萬軍上主的斷語。
Uovu wako utakuadhibu; kurudi nyuma kwako kutakukemea. Basi kumbuka, utambue jinsi lilivyo ovu na chungu kwako unapomwacha Bwana Mungu wako na kutokuwa na hofu yangu,” asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote.
20 的確,從古以來,你就折斷了你的軛,掙斷了你的繩索說:我不願服從;反在一切高丘上,和一切綠樹下,偃臥行淫。
“Zamani nilivunja nira yako na kukatilia mbali vifungo vyako; ukasema, ‘Sitakutumikia!’ Naam kweli, kwenye kila kilima kirefu na chini ya kila mti uliotanda matawi yake ulijilaza kama kahaba.
21 我種植你時,原是精選的葡萄,純粹的真種子;你是怎麼竟給我變成了壞樹,成了野葡萄﹖
Nilikupanda ukiwa mzabibu ulio bora sana, mkamilifu na wa mbegu nzuri. Ilikuwaje basi ukawa kinyume nami, ukaharibika na kuwa mzabibu mwitu?
22 現在既使你用鹼洗濯,多加滷汁,你的罪污仍留在我面前──吾主上主的斷語──
Hata ujisafishe kwa magadi na kutumia sabuni nyingi, bado doa la hatia yako liko mbele zangu,” asema Bwana Mwenyezi.
23 你怎能說:我沒有玷污我自己,我沒有追隨過巴耳﹖觀察你在谷中的行動,便知你的行動,無異一隻到處遊蕩,敏捷的母駱駝;
“Wawezaje kusema, ‘Mimi si najisi, sijawafuata Mabaali’? Kumbuka jinsi ulivyotenda kule bondeni; fikiri uliyoyafanya. Wewe ni ngamia jike mwenye mbio ukikimbia hapa na pale,
24 又像一頭習慣在荒野,急欲求配,呼氣喘息的母野驢;誰能抑制牠的性慾﹖凡尋找牠的,不必費辛苦,在她春情發動的月分,就可找著。
punda-mwitu aliyezoea jangwa, anayenusa upepo katika tamaa yake kubwa: katika wakati wake wa kuhitaji mbegu ni nani awezaye kumzuia? Madume yoyote yanayomfuatilia hayana haja ya kujichosha; wakati wa kupandwa kwake watampata tu.
25 留心! 不要使你的腳赤裸,不要使你的喉嚨乾渴! 但是你卻說:不會,不可能! 我既愛異邦神袛,我要跟隨他們。
Usikimbie hadi miguu yako iwe haina viatu, na koo lako liwe limekauka. Lakini ulisema, ‘Haina maana! Ninaipenda miungu ya kigeni, nami lazima niifuatie.’
26 就如小偷被人發現時,感到羞愧;以色列家:他們,他們的君王和首領,他們的司祭和先知,都要同樣蒙受羞辱。
“Kama vile mwizi aaibikavyo wakati amekamatwa, hivyo ndivyo nyumba ya Israeli inavyoaibishwa: wao wenyewe, wafalme wao na maafisa wao, makuhani wao na manabii wao.
27 他們對木偶說:你是我的父親;對石碣說:是你生了我。的確,他們不但向我轉過臉去,而且也以褙向著我;但是,在他們遭難的時候,卻喊說:起來,拯救我們!
Wanaiambia miti, ‘Wewe ndiwe baba yangu,’ nalo jiwe, ‘Wewe ndiwe uliyenizaa.’ Wamenipa visogo vyao wala hawakunigeuzia nyuso zao; lakini wakiwa katika taabu, wanasema, ‘Njoo utuokoe!’
28 你自己製造的神祗在哪裏﹖在你遭難的時候,他們若能救你,就讓他們起來! 因為猶大! 你祗的數目竟等於你域邑的數目,巴耳的香壇與耶路撒冷的街道一般多。
Iko wapi basi ile miungu mliyojitengenezea? Yenyewe na ije kama inaweza kuwaokoa wakati mko katika taabu! Kwa maana mna miungu mingi kama mlivyo na miji, ee Yuda.
29 你們竟背叛了我,為什麼又向我提出抗議──上主的斷語──
“Kwa nini mnaleta mashtaka dhidi yangu? Ninyi nyote mmeniasi,” asema Bwana.
30 我打擊了你們的子孫,竟是徒然,你們沒有受到教訓;你們的刀劍如同一隻兇殘的獅子吞滅了眾先知。
“Nimeadhibu watu wako bure tu, hawakujirekebisha. Upanga wako umewala manabii wako kama simba mwenye njaa.
31 你們這一代人,體會上主的話吧! 難道我對以色列像一個荒野,或像一個黑暗地方﹖為什麼我的人民說:我們獲得了自由,我們不再來找你﹖
“Enyi wa kizazi hiki, tafakarini neno la Bwana: “Je, nimekuwa jangwa kwa Israeli au nchi ya giza kuu? Kwa nini watu wangu wanasema, ‘Sisi tuko huru kuzurura, hatutarudi kwako tena’?
32 一個處女豈能忘了自己的珍飾﹖一位新娘豈能忘了自己的彩帶﹖我的人民卻忘了我,時日已久長無法計算。
Je, mwanamwali husahau vito vyake, au bibi arusi mapambo yake ya arusi? Lakini watu wangu wamenisahau mimi, tena kwa siku zisizo na hesabu.
33 你怎麼會如此想盡好方法去求愛﹖你也將你的方法教給了邪惡的女人;
Je, wewe una ustadi kiasi gani katika kufuatia mapenzi! Hata wale wanawake wabaya kuliko wote wanaweza kujifunza kutokana na njia zako.
34 連在你的衣邊上也發現無辜窮人的血漬:並不是在挖洞穴時,你捉住他們,而是在橡樹邊。
Katika nguo zako watu huona damu ya uhai ya maskini wasio na hatia, ingawa hukuwakamata wakivunja nyumba. Lakini katika haya yote
35 但你還說:我是無罪的,他的憤怒已離我遠去。看! 我要審判你,因你說:我沒有犯罪。
unasema, ‘Sina hatia; Mungu hajanikasirikia.’ Lakini nitakuhukumu kwa sababu unasema, ‘Mimi sijatenda dhambi.’
36 為什麼這樣輕易改變你的道路﹖你必要因埃及而蒙羞,猶如曾因亞述而蒙羞一樣。
Kwa nini unatangatanga sana, kubadili njia zako? Utakatishwa tamaa na Misri kama ulivyokatishwa na Ashuru.
37 你畢竟要從那裏抱頭出走,因為上主擯棄了你所仗恃的,使你不能靠他們獲得成功。
Pia utaondoka mahali hapo ukiwa umeweka mikono kichwani, kwa kuwa Bwana amewakataa wale unaowatumainia; hutasaidiwa nao.