< 耶利米書 11 >
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
2 「你們應聽這盟約上的話,將這些話宣讀給猶大人和耶路撒冷的居民聽。
“Sikia maneno ya agano hili, nawe uwaambie watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu.
3 你應對他們說:「上主,以色列的天主這樣說:凡不聽從這盟約上的話的人,是可咒罵的!
Waambie kwamba hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Amelaaniwa mtu ambaye hatayatii maneno ya agano hili,
4 這些話是我在領你們的祖先由鐵爐,即由埃及地出來的那天,對他們吩咐的。我對他們說:你們應聽從我的聲音,應依照我命令你們的一切去做,你們就必做我的人民,我也必做你們的天主,
maneno niliyowaamuru baba zenu nilipowatoa katika nchi ya Misri, kutoka tanuru la kuyeyushia vyuma.’ Nilisema, ‘Nitiini mimi na mfanye kila kitu ninachowaamuru, nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.
5 好我能實踐對你們祖先所起的誓,賜給他們流奶流蜜的土地,有如今日。我即答說:「是,上主! 」
Kisha nitatimiza kiapo nilichowaapia baba zenu, kuwapa nchi itiririkayo maziwa na asali,’ nchi ambayo mnaimiliki leo.” Nikajibu, “Amen, Bwana.”
6 上主對我說:「你應在猶大城邑和耶路撒冷的街上宣佈這些話說:你們應聽從這盟約上的話,依照遵行,
Bwana akaniambia, “Tangaza maneno haya yote katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu: ‘Sikilizeni maneno ya agano hili na kuyafuata.
7 因為在我領你們的祖先由埃及上來的那一天,我就鄭重警告過他們,直到今日仍不斷勸告他們說:你們應我的聲音!
Tangu wakati ule niliwapandisha baba zenu kutoka Misri mpaka leo, niliwaonya tena na tena, nikisema “Nitiini mimi.”
8 他們不但不聽從,氶而各隨自己頑固的惡心生活,為此,我對他們執行了我命他們遵行,而他們沒有遵行的這盟約上的一切話。」
Lakini hawakusikiliza wala kujali. Badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Hivyo nikaleta juu yao laana zote za agano nililokuwa nimewaamuru wao kulifuata, lakini wao hawakulishika.’”
9 上主又對我說:「猶大和耶路撒冷間存有叛逆的陰謀,
Kisha Bwana akaniambia, “Kuna shauri baya linaloendelea miongoni mwa watu wa Yuda na wale wanaoishi Yerusalemu.
10 他們再陷於他們那不願聽從我話的祖先的罪惡中,追隨事奉其他的神祗;以色列家和猶大家都違反了我與他們祖先締結的盟約。
Wamerudia dhambi za baba zao, waliokataa kusikiliza maneno yangu. Wameifuata miungu mingine kuitumikia. Nyumba zote mbili za Israeli na Yuda zimelivunja agano nililofanya na baba zao.
11 為此,上主這樣說:看,我必給他們召來不可逃避的災禍;既使他們向我呼號,我也不俯聽。
Kwa hivyo, hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitaleta juu yao maafa ambayo hawawezi kuyakimbia. Hata kama wakinililia, sitawasikiliza.
12 猶大城邑和耶路撒冷的居民,必去呼號他們獻香敬拜的神祗,佰這些神祗在他們遭難時,決不能拯救他們。
Miji ya Yuda na watu wa Yerusalemu watakwenda kuililia miungu ambayo wameifukizia uvumba, lakini haitawasaidia kamwe wakati maafa yatakapowapiga.
13 的確,猶大! 你神祗的號竟等於你城邑的數目;耶路撒冷有多少街道,你們也給可恥之物設立了多少祭壇,向巴爾獻香的祭壇。
Mnayo miungu mingi kama miji mliyo nayo, ee Yuda, nazo madhabahu mlizozijenga za kufukizia uvumba huyo mungu wa aibu Baali ni nyingi kama barabara za Yerusalemu.’
14 至於你,你不必為這人民祈禱,不必為他們呼號祈求,因為他們在遭難時,才向我呼求,我必不俯聽。
“Wewe usiwaombee watu hawa wala kufanya maombezi yoyote au kunisihi kwa ajili yao, kwa sababu sitawasikiliza watakaponiita wakati wa taabu yao.
15 我心愛的人! 你既為作歹,還在我家做什麼﹖難道許願和祝聖的肉能使你免禍,叫你作惡而能倖免﹖
“Mpenzi wangu anafanya nini hekaluni mwangu, anapofanya mashauri yake maovu na wengi? Je, nyama iliyowekwa wakfu yaweza kuondolea mbali adhabu yako? Unapojiingiza katika ubaya wako, ndipo unashangilia.”
16 上主曾給你起外叫:「青綠茂盛而滿結佳果的橄欖樹」;但現在衪在雷電霹靂聲音中,給綠葉燃起了火,燒毀了枝條。
Bwana alikuita mti wa mzeituni uliostawi ulio na matunda mazuri kwa sura. Lakini kwa ngurumo ya mawimbi makuu atautia moto, nayo matawi yake yatavunjika.
17 那位培埴你的萬軍的上主,命災禍來懲罰你,全是為了以色列家和猶大家自作自受的罪惡,因為他們向巴爾獻香,獨犯了我。
Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliyekupanda, ametamka maafa kwa ajili yako, kwa sababu nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda mmefanya maovu na kunikasirisha kwa kumfukizia Baali uvumba.
18 上主叫我知道, 才知道;那時我看透了他們的作為:
Kwa sababu Bwana alinifunulia hila zao mbaya, nilizifahamu, kwa kuwa wakati ule alinionyesha yale waliyokuwa wanayafanya.
19 我好像一隻馴服被牽去宰殺的羔羊,竟不知他們對我畜意謀害:「讓我毀壞這株生氣蓬勃的樹,將他由活人的地上拔除,使他的名字不再受人記念。」
Nilikuwa kama mwana-kondoo mpole aliyeongozwa machinjoni; mimi sikutambua kwamba walikuwa wamefanya shauri baya dhidi yangu, wakisema, “Sisi na tuuangamize mti na matunda yake; nasi tumkatilie mbali kutoka nchi ya walio hai, ili jina lake lisikumbukwe tena.”
20 公平審判和洞察肺腑的上主! 願我見到你對他們的報復,因為我已向他們提出我的控訴。
Lakini, Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, wewe uhukumuye kwa haki, nawe uchunguzaye moyo na akili, wacha nione ukiwalipiza wao kisasi, kwa maana kwako nimeweka shauri langu.
21 為此,關於那些謀害我的性命,對我說:「你不要事奉上主的名講預言,免得你死在我們手裏」的阿納托特人,上主這樣說,
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana asemalo kuhusu watu wa Anathothi wale wanaotafuta uhai wako wakisema, ‘Usitoe unabii kwa jina la Bwana, la sivyo utakufa kwa mikono yetu’:
22 萬軍的上主這樣說:「看,我必懲罰他們:青年必死在刀下,子女必死於饑荒,
kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nitawaadhibu. Vijana wao waume watakufa kwa upanga, wana wao na binti zao kwa njaa.
23 使他們沒有子嗣,因為在懲罰他們的那年,我必給阿納托人招來災禍。」
Hawatasaziwa hata mabaki kwao, kwa sababu nitaleta maafa kwa watu wa Anathothi katika mwaka wa adhabu yao.’”