< 希伯來書 12 >

1 以,我們既有如此眾多如雲的證人,圍繞著我們,就該下卸下所有的累贅和糾纏人的罪過,以堅忍的心,跑那擺在我們眼前的賽程,
Kwahiyo, kwa kuwa tumezungukwa na wingu kubwa la mashaidi, na tutupe kila kitu kinacho tulemea pamoja na dhambi ambayo inatuzingira kwa urahisi. Tupige mbio kwa saburi katika mashindano yaliyowekwa mbele yetu.
2 雙目注視著信德的創始者耶穌:衪為那擺在衪面前的歡樂,輕淩辱,忍受了十字架,而今坐在天主寶座的右邊。
Tuyaelekeze macho yetu kwa Yesu, aliye mwanzilishi na mwenye kutimiliza imani yetu, ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake alistahmili msalaba, akiidharau aibu yake, na akakaa chini mkono wa kulia wa kiti cha enzi cha Mungu.
3 你們常要想,衪所以忍受罪人對衪這樣的叛逆,是怕你們灰心喪志。
Maana mtafakarini yeye aliye stahimili maneno ya chuki kutoka kwa wenye dhambi, dhidi yake mwenyewe ili kwamba msije mkachoka au kuzimia mioyo yenu.
4 你們與罪惡爭鬥,還沒有抵抗到流血的地步。
Hamjataabika au kuteseka mkishindana na dhambi kiasi cha kuishiwa damu.
5 你們竟全忘了天主勸你們,好像勸子女的話說:『我兒,不要輕視上主的懲戒,也不要厭惡衪的譴責,
Tena mmesahau kule kutiwa moyo ambako kunawaelekeza kama watoto wa kiume: “Mwanangu, usiyachukuwe kwa wepesi marudia ya Bwana, wala usikate tamaa unapo rekebishwa na yeye.”
6 因為上主懲戒衪所愛的,鞭打衪所接管的每個兒子。』
Kwa kuwa Bwana humrudi yeyote ambaye anampenda, na humwadhibu kila mwana ambaye humpokea.
7 為接受懲戒,應該堅忍,因為天主對待你們,就如對待子女;那有兒子,做父親的不懲戒他呢﹖
Stahimili majaribu kama kurudiwa. Mungu hushughulika nanyi kama anavyoshughulika na watoto, maana ni mtoto yupi ambaye baba yake hawezi kumrudi?
8 如果你們缺少眾人所共受的懲戒,你們就是私生子,而不是兒子。
Lakini kama hakuna kurudiwa, ambako sisi sote tunashiriki, basi ninyi ni haramu na si watoto wake.
9 再者,我們肉身的父親懲戒我們時,我們尚且表示敬畏;何況靈性的父親,我們不是更該服從,以得生活嗎﹖
Zaidi ya yote, tulikuwa na baba zetu kidunia wa kuturudi, na tuliwaheshimu. Je haitupasi hata zaidi kumtii Baba wa kiroho na kuishi?
10 其實肉身的父親只是在短暫的時日內,照他們的心意來施行懲戒,但是天主卻是為了我們的好處,為叫我們分沾衪的聖善。
Kwa hakika baba zetu walituadhibu kwa miaka michache kama ilivyoonekana sawa kwao, lakini Mungu hutuadhibu kwa faida yetu ili tushiriki utakatifu wake.
11 固然各種懲戒,在當時似乎不是樂事,而是苦事;可是以後卻給那些受訓練的人,結出義德的和平果實。
Hakuna adhabu inayofurahisha kwa wakati huo. Huwa na maumivu. Hata hivyo, baadaye huzaa tunda la amani ya utauwa kwa wale waliofundishwa nayo.
12 為此,你們應該伸直痿弱的手和麻木的膝;
Kwa hiyo inueni mikono yenu iliyolegea na kufanya magoti yenu yaliyo dhaifu kuwa yenye nguvu tena;
13 你們的腳應履行正直的路,叫瘸子不要偏離正道,反叫他能得痊愈。
nyosheni mapito ya nyayo zenu, ili kwamba yeyote aliye mlemavu hataongozwa upotevuni lakini apate kuponywa.
14 你們應設法與眾人和平相處,盡力追求聖德,若無聖德,誰也見不到主;
Tafuteni amani na watu wote, na pia utakatifu ambao bila huo hakuna atakayemwona Bwana.
15 又應該慬慎,免得有人疏忽天主的恩寵免得苦根子長出來,而累及你們,使許多人因此蒙受玷污。
Muwe waangalifu ili kwamba asiwepo atakayetengwa mbali na neema ya Mungu, na kwamba lisije shina la uchungu litakalochipuka na kusababisha shida na kukengeusha wengi.
16 誰也不要成為淫亂和褻聖者,如同厄撒烏一樣,他為了一餐飯,竟出賣了自己長氶的身份。
Angalieni kuwa hakuna zinaa au mtu asiye mtauwa kama vile Esau, ambaye kwa sababu ya mlo mmoja aliuza haki yake ya kuzaliwa.
17 你們知道,後來他縱然願意承受祝福,也遭到了拒絕;雖流淚苦求,但沒有得到翻悔的餘地。
Kwa kuwa mnajua kwamba baadaye, alipotamani kurithi baraka, alikataliwa, kwa sababu hakupata fursa ya kutubu pamoja na baba yake, hata ingawa alitafuta sana kwa machozi.
18 你們原來並不是走近了那可觸摸的山,那裏有烈火、濃雲、黑暗、暴風、
Kwa kuwa hamkuja katika mlima ambao unaweza kuguswa, Mlima unaowaka moto, giza, kukatisha tamaa na dhoruba.
19 號垌的響聲以及說話的聲音,當時那些聽見的人,都懇求天主不要再給他們說話,
Hamkuja kwa sauti za tarumbeta, au kwa maneno yatokanayo na sauti ambayo ilisababisha kila wasikiao wasiombe neno lolote kusemwa kwao.
20 因為他們承擔不起所吩咐的事:『即使是一隻走獸觸摸了這山,也應用石頭砸死;』
Kwa kuwa hawakuweza kuvumilia kile kilichoamuliwa: “Ikiwa hata mnyama agusaye mlima, lazima apigwe kwa mawe.”
21 並且所顯現的是這麼可怕,連梅瑟也說:『我很是恐慌戰憟。』
Ya kutisha zaidi aliyoyaona Musa alisema, “Nimeogopa sana kiasi cha kutetemeka”.
22 然而你們卻接近了熙雍山的永生天主的城,天上的耶路撒冷,接近了千萬天使的盛會,
Badala yake, mmekuja mlima Sayuni na katika mji wa Mungu aliye hai, Yerualem ya mbinguni, na kwa malaika elfu kumi wanaosherehekea.
23 和那些已被登錄在天上的首生者的集會,接近了審判眾人的天主,接近了已獲得成全的義人的靈魂,
Mmekuja katika kusanyiko la wazaliwa wa kwanza wote waliosajiliwa mbinguni, kwa Mungu hakimu wa wote, na kwa roho za watakatifu ambao wamekamilishwa.
24 接近了新約的中保耶穌,以及衪所灑的血:這血比亞伯爾的血說說的更好。
Mmekuja kwa Yesu mpatanishi wa agano jipya, na kwa damu iliyonyunyizwa ambayo hunena mema zaidi kuliko damu ya Habili.
25 你們要慬慎,不要拒絕說話的那位,如果從前那些拒絕聽衪在地上宣佈啟示的人,不能逃避懲罰,何況我們這些背棄由天上說話的那位呢﹖
Angalia kuwa usije ukamkataa mmoja ambaye anenaye. Kwa kuwa kama hawakuepuka walipomkataa mmoja aliye waonya duniani, kwa hakika hatutaepuka ikiwa tutageuka mbali kutoka kwa yule atuonyaye kutoka mbinguni.
26 從前衪的聲音搖動了下地,如今衪卻應許說:『還有一次,我不但動搖下地,而且也動搖下天。』
Kwa wakati huo sauti yake ilitikisa dunia. Lakini sasa ameahidi na kunena, “Bado mara nyingine tena sitatikisa dunia pekee, bali mbingu pia.”
27 這『還有一次』一句,是指明那些被動搖的事物,因為受造的,必起變化,好叫那些不可動搖的事物得以常存。
Maneno haya, “Mara moja tena,” inaonesha kutoweshwa kwa vitu vile vitetemeshwavyo, hivi ni, vitu vile ambavyo vimeumbwa, ili kwamba vile vitu visivyotetemeshwa vibakie.
28 為此,我們既然蒙受一個不可動搖的國度,就應該感恩,藉此懷著虔忱和敬畏之情,事奉天主,叫衪喜悅,
Kwa hiyo, tupokee ufalme ambao hautetemeshwi, tufurahi katika hali ya kumwabudu Mungu kwa kukubali pamoja na kunyenyekea katika kicho,
29 因為我們的天主實是吞滅的烈火。
kwa maana Mungu wetu ni moto ulao.

< 希伯來書 12 >