< 創世記 7 >
1 上主對諾厄說:「你和你全家進入方舟,因為在這一世代,我看只有你在我面前正義。
Ndipo Bwana akamwambia Noa, “Ingia katika safina wewe na jamaa yako yote, kwa sababu katika kizazi hiki nimeona ya kuwa wewe ni mwenye haki.
2 由一切潔淨牲畜中,各取公母七對;由那些不潔淨的牲畜中,各取公母一對;
Uchukue wanyama saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, na wanyama wawili wawili wa kila aina walio najisi wa kiume na wa kike.
3 由天空的飛鳥中,也各取公母七對;好在全地面上傳種。
Pia uchukue ndege saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, ili kuhifadhi aina zao mbalimbali katika dunia yote.
4 因為還有七天,我要在地上降雨四十天四十夜,消滅我在地面上所造的一切生物。」
Siku saba kuanzia sasa nitaleta mvua juu ya nchi kwa siku arobaini usiku na mchana, nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kiumbe hai nilichokiumba.”
Noa akafanya yote kama Bwana alivyomwamuru.
Noa alikuwa na miaka 600 gharika ilipokuja juu ya dunia.
7 諾厄和他的兒子,他的妻子和他的兒媳,同他進了方舟,為躲避洪水。
Noa na mkewe na wanawe na wake zao wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika.
8 潔淨的牲畜和不潔淨的牲畜,飛鳥和各種在地上爬行的動物,
Jozi ya wanyama walio safi na walio najisi, ndege na viumbe vitambaavyo,
9 一對一對地同諾厄進了方舟;都是一公一母,照天主對他所吩咐的。
wa kiume na wa kike, walikuja kwa Noa wakaingia katika safina kama Mungu alivyomwamuru Noa.
Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya dunia.
11 諾厄六百歲那一年,二月十七日那天,所有深淵的泉水都冒出,天上的水閘都開放了;
Katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili mwaka wa 600 wa kuishi kwake Noa, siku hiyo ndipo chemchemi zote hata zilizo chini sana ya ardhi zilibubujika kwa nguvu, na malango ya mafuriko ya mbinguni yakafunguliwa.
Mvua ikanyesha juu ya nchi siku arobaini usiku na mchana.
13 正在這一天,諾厄和他的兒子閃、含、耶斐特,他的妻子和他的三個兒媳,一同進了方舟。
Siku hiyo Noa, na mkewe, na wanawe Shemu, Hamu na Yafethi pamoja na wake zao wakaingia katika ile safina.
14 他們八口和所有的野獸、各種牲畜、各種在地上爬行的爬蟲、各種飛禽,
Nao walikuwa pamoja na kila mnyama wa mwituni kufuatana na aina yake, wanyama wote wafugwao kufuatana na aina zao, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi kwa aina yake, na kila ndege kufuatana na aina yake, naam kila kiumbe chenye mabawa.
15 一切有生氣有血肉的,都一對一對地同諾厄進了方舟。
Viumbe vyote vyenye pumzi ya uhai ndani yake vikaja kwa Noa viwili viwili, vikaingia katika safina.
16 凡有血肉的,都是一公一母地進了方舟,如天主對諾厄所吩咐的。隨後上主關了門。
Wanyama walioingia katika safina walikuwa wa kiume na wa kike, wa kila kiumbe chenye uhai kama Mungu alivyomwamuru Noa, ndipo Bwana akamfungia ndani.
17 洪水在地上氾濫了四十天;水不斷增漲,浮起了方舟,方舟遂由地面上升起。
Kwa siku arobaini mafuriko yaliendelea kujaa duniani na maji yalivyozidi kuongezeka, yaliinua safina juu sana kutoka kwenye uso wa nchi.
Maji yakajaa na kuongezeka sana juu ya nchi, na safina ikaelea juu ya uso wa maji.
19 洪水在地上一再猛漲,天下所有的高山也都沒了頂;
Maji yakazidi kujaa juu ya nchi, yakaifunika milima yote mirefu chini ya mbingu yote.
Maji yakaendelea kujaa yakaifunika milima kwa kina cha zaidi ya dhiraa kumi na tano.
21 凡地上行動而有血肉的生物:飛禽、牲畜、野獸,在地上爬行的爬蟲,以及所有的人全滅亡了;
Kila kiumbe hai kitambaacho juu ya nchi kikaangamia: Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama pori, viumbe vyote juu ya nchi na wanadamu wote.
Kila kiumbe juu ya nchi kavu chenye pumzi ya uhai kikafa.
23 這樣,天主消滅了在地面上的一切生物,由人以至於牲畜、爬蟲以及天空中的飛鳥,這一切都由地上消滅了,只剩下諾厄和同他在方舟內的人物。
Kila kitu chenye uhai juu ya uso wa nchi kilifutiliwa mbali, watu, wanyama, viumbe vitambaavyo na ndege warukao angani wakafutiliwa mbali toka duniani. Waliobaki ni Noa peke yake na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya safina.
Maji yakaifunika dunia kwa siku 150.