< 傳道書 12 >
1 在你年輕的時日,在災禍的日子來到之前,即在你說的那些「沒有歡樂」的日子來到之前,你應記念你的造主;
Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, kabla hazijaja siku za taabu, wala haijakaribia miaka utakaposema, “Mimi sifurahii hiyo”:
2 不要等到太陽、光體、月亮、星辰失光,雨後雲彩再來;
kabla jua na nuru, nao mwezi na nyota havijatiwa giza, kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;
3 因為那時,看門者戰慄,大力士屈伏,推磨的婦女因為少而停工,眺望窗外的女人面目昏黑,
siku ile walinzi wa nyumba watakapotetemeka, nao watu wenye nguvu watakapojiinamisha, wakati wasagao watakapokoma kwa sababu ya uchache, nao wachunguliao madirishani kutiwa giza;
4 兩扇街門將要關閉,磨聲低微,雀鳥息聲,歌女低吟,
wakati milango ya kuingia barabarani itakapofungwa na sauti ya kusaga kufifia; wakati watu wataamshwa kwa sauti ya ndege, lakini nyimbo zao zote zikififia;
5 怕上高處,行路危險,杏子被棄,蚱蜢被嫌,續隨子失去效力,因為人要回永久的家鄉,哀悼的人徘徊街頭;
wakati watu watakapoogopa kilichoinuka juu na hatari zitakazokuwepo barabarani; wakati mlozi utakapochanua maua na panzi kujikokota nawe usiwe na shauku ya kitu chochote. Ndipo mwanadamu aiendea nyumba yake ya milele nao waombolezaji wakizunguka barabarani.
6 那時銀鏈將斷,金燈將碎,水罐將破於泉旁,輪子將爛於井邊,
Mkumbuke Muumba wako: kabla haijakatika kamba ya fedha, au bakuli la dhahabu halijavunjika; kabla mtungi kuvunjika kwenye chemchemi, au gurudumu kuvunjika kisimani,
7 灰塵將歸於原來的土中,生氣將歸於天主,因為原是天主之所賜。
nayo mavumbi kurudi ardhini yalikotoka, na roho kurudi kwa Mungu aliyeitoa.
Mhubiri asema, “Ubatili! Ubatili! Kila kitu ni ubatili!”
9 訓道者不但是智者,並且教人獲得知識,在沉思推究之後,編撰了許多格言。
Mhubiri hakuwa tu na hekima, bali aliwagawia watu maarifa pia. Alitafakari na kutafiti na akaweka katika utaratibu mithali nyingi.
10 訓道者費神尋找適當的語句,忠誠地寫下了真理之言。
Mhubiri alitafiti ili kupata maneno sahihi na kila alichoandika kilikuwa sawa na kweli.
11 智者的話好似錐子,收集起的言論集,好像釘牢的釘子:二者都是一位牧者所賜。
Maneno ya wenye hekima ni kama mchokoro, mithali zao zilizokusanywa pamoja ni kama misumari iliyogongomewa ikawa imara, yaliyotolewa na Mchungaji mmoja.
12 除此之外,我兒,不必再找別的書籍,書不論寫多少,總沒有止境;用功過度,必使身體疲倦。
Tena zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo, hakuna mwisho wa kutunga vitabu vingi, nako kusoma sana huuchosha mwili.
13 總而言之:「你應敬畏天主,遵守他的誡命,因為這是眾人的義務。」
Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa: Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.
14 因為天主對一切行為,連最隱秘的,不論好壞,都要一一審判。
Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au baya.