< 傳道書 1 >

1 達味之子耶路撒冷的君王「訓道者」的語錄:
Maneno ya Mhubiri, mwana wa Daudi, mfalme huko Yerusalemu:
2 虛而又虛,訓道者說:虛而又虛,萬事皆虛。
“Ubatili mtupu! Ubatili mtupu!” Mhubiri anasema. “Ubatili mtupu! Kila kitu ni ubatili.”
3 人在太陽下辛勤勞作,為人究有何益﹖
Mwanadamu anafaidi nini kutokana na kazi yake yote anayotaabikia chini ya jua?
4 一代過去,一代又來,大地仍然常在。
Vizazi huja na vizazi hupita, lakini dunia inadumu milele.
5 太陽升起,太陽落下,匆匆趕回原處,從新再升。
Jua huchomoza na jua huzama, nalo huharakisha kurudi mawioni.
6 風吹向南,又轉向北,旋轉不息,循環周行。
Upepo huvuma kuelekea kusini na kugeukia kaskazini, hurudia mzunguko huo huo, daima ukirudia njia yake.
7 江河流入大海,大海總不滿溢;江河仍向所往之處,川流不息。
Mito yote hutiririka baharini, hata hivyo bahari kamwe haijai. Mahali mito inapotoka, huko hurudi tena.
8 萬事皆辛勞,無人能盡言:眼看,看不夠;耳聽,聽不飽。
Vitu vyote vinachosha, zaidi kuliko mtu anavyoweza kusema. Jicho kamwe halitosheki kutazama, wala sikio halishibi kusikia.
9 往昔所有的,將來會再有;昔日所行的,將來會再行;太陽之下決無新事。
Kile kilichokuwepo kitakuwepo tena, kile kilichofanyika kitafanyika tena, hakuna kilicho kipya chini ya jua.
10 若有人指著某事說:「看,這是新事。」豈不知在我們以前早就有過。
Kuna kitu chochote ambacho mtu anaweza kusema, “Tazama! Kitu hiki ni kipya”? Kilikuwepo tangu zamani za kale, kilikuwepo kabla ya wakati wetu.
11 只是對往者,沒有人去追憶;同樣,對來者,也不會為後輩所記念。
Hakuna kumbukumbu ya watu wa zamani, hata na wale ambao hawajaja bado hawatakumbukwa na wale watakaofuata baadaye.
12 我訓道者,曾在耶路撒冷作過以色列的君王。
Mimi, Mhubiri, nilikuwa mfalme wa Israeli katika Yerusalemu.
13 我曾專心用智慧考查研究過天下所發生的一切;--這實在是天主賜與人類的一項艱辛的工作。
Nilitumia muda wangu wote kujifunza na kuvumbua kwa hekima yote yanayofanyika chini ya mbingu. Jinsi gani Mungu ameweka mzigo mzito juu ya wanadamu!
14 我觀察了在太陽下所發生的一切:看,都是空虛,都是追風。
Nimeshaona mambo yote yanayotendeka chini ya jua, hayo yote ni ubatili, hii ni kukimbiza upepo.
15 彎曲的,不能使之正直,虧缺的,實在不可勝數。
Kilichopindika hakiwezi kunyooshwa, kile ambacho hakipo haiwezekani kukihesabu.
16 我心裏自語說:「看,我獲得了又大又多的智慧,勝過了所有在我以前住在耶路撒冷的人,我的心獲得了許多智慧和學問。」
Niliwaza mwenyewe, “Tazama, nimekua na kuongezeka katika hekima kuliko yeyote aliyewahi kutawala Yerusalemu kabla yangu. Nimekuwa na uzoefu mkubwa wa hekima na maarifa.”
17 我再專心研究智慧和學問,愚昧和狂妄,我纔發覺:連這項工作也是追風。
Ndipo nilipojitahidi kufahamu kutofautisha hekima, wazimu na upumbavu, lakini nikatambua hata hili nalo ni kukimbiza upepo.
18 因為,智慧愈多,煩惱愈多;學問越廣,憂慮越深。
Kwa kuwa hekima nyingi huleta huzuni kubwa; maarifa yanapoongezeka, masikitiko yanaongezeka.

< 傳道書 1 >