< 傳道書 1 >
Maneno ya Mhubiri, mwana wa Daudi, mfalme huko Yerusalemu:
“Ubatili mtupu! Ubatili mtupu!” Mhubiri anasema. “Ubatili mtupu! Kila kitu ni ubatili.”
Mwanadamu anafaidi nini kutokana na kazi yake yote anayotaabikia chini ya jua?
Vizazi huja na vizazi hupita, lakini dunia inadumu milele.
Jua huchomoza na jua huzama, nalo huharakisha kurudi mawioni.
Upepo huvuma kuelekea kusini na kugeukia kaskazini, hurudia mzunguko huo huo, daima ukirudia njia yake.
7 江河流入大海,大海總不滿溢;江河仍向所往之處,川流不息。
Mito yote hutiririka baharini, hata hivyo bahari kamwe haijai. Mahali mito inapotoka, huko hurudi tena.
8 萬事皆辛勞,無人能盡言:眼看,看不夠;耳聽,聽不飽。
Vitu vyote vinachosha, zaidi kuliko mtu anavyoweza kusema. Jicho kamwe halitosheki kutazama, wala sikio halishibi kusikia.
9 往昔所有的,將來會再有;昔日所行的,將來會再行;太陽之下決無新事。
Kile kilichokuwepo kitakuwepo tena, kile kilichofanyika kitafanyika tena, hakuna kilicho kipya chini ya jua.
10 若有人指著某事說:「看,這是新事。」豈不知在我們以前早就有過。
Kuna kitu chochote ambacho mtu anaweza kusema, “Tazama! Kitu hiki ni kipya”? Kilikuwepo tangu zamani za kale, kilikuwepo kabla ya wakati wetu.
11 只是對往者,沒有人去追憶;同樣,對來者,也不會為後輩所記念。
Hakuna kumbukumbu ya watu wa zamani, hata na wale ambao hawajaja bado hawatakumbukwa na wale watakaofuata baadaye.
Mimi, Mhubiri, nilikuwa mfalme wa Israeli katika Yerusalemu.
13 我曾專心用智慧考查研究過天下所發生的一切;--這實在是天主賜與人類的一項艱辛的工作。
Nilitumia muda wangu wote kujifunza na kuvumbua kwa hekima yote yanayofanyika chini ya mbingu. Jinsi gani Mungu ameweka mzigo mzito juu ya wanadamu!
14 我觀察了在太陽下所發生的一切:看,都是空虛,都是追風。
Nimeshaona mambo yote yanayotendeka chini ya jua, hayo yote ni ubatili, hii ni kukimbiza upepo.
15 彎曲的,不能使之正直,虧缺的,實在不可勝數。
Kilichopindika hakiwezi kunyooshwa, kile ambacho hakipo haiwezekani kukihesabu.
16 我心裏自語說:「看,我獲得了又大又多的智慧,勝過了所有在我以前住在耶路撒冷的人,我的心獲得了許多智慧和學問。」
Niliwaza mwenyewe, “Tazama, nimekua na kuongezeka katika hekima kuliko yeyote aliyewahi kutawala Yerusalemu kabla yangu. Nimekuwa na uzoefu mkubwa wa hekima na maarifa.”
17 我再專心研究智慧和學問,愚昧和狂妄,我纔發覺:連這項工作也是追風。
Ndipo nilipojitahidi kufahamu kutofautisha hekima, wazimu na upumbavu, lakini nikatambua hata hili nalo ni kukimbiza upepo.
18 因為,智慧愈多,煩惱愈多;學問越廣,憂慮越深。
Kwa kuwa hekima nyingi huleta huzuni kubwa; maarifa yanapoongezeka, masikitiko yanaongezeka.