< 撒母耳記上 12 >

1 撒慕爾對全以色列人說:「看,我全聽從了你們向我所說的話,立了一位君王管理你們。
Samweli akawaambia Israeli wote, “Nimesikiliza kila kitu mlichoniambia nami nimewawekea mfalme juu yenu.
2 從此以後,有君王領導你們。至於我,我已老了,頭髮也白了;不過我的兒子還同你們在一起。我從小直到今天,常在你們面往來。
Sasa mnaye mfalme kama kiongozi wenu. Lakini kwa habari yangu mimi ni mzee na nina mvi, nao wanangu wapo hapa pamoja nanyi. Nimekuwa kiongozi wenu tangu ujana wangu mpaka siku hii ya leo.
3 看,我在這裏,請你們在上主面前,在他受傅者面前答覆我:我奪過誰的牛,或奪過誰的驢﹖我壓迫過誰,或虐待過誰﹖從誰手裏接受過掩人耳目的賄賂﹖若有,我必歸還你們。」
Mimi ninasimama hapa. Shuhudieni juu yangu mbele za Bwana na mpakwa mafuta wake. Nimechukua maksai wa nani? Nimechukua punda wa nani? Ni nani nimepata kumdanganya? Ni nani nimepata kumwonea? Ni kutoka kwenye mkono wa nani nimepokea rushwa ili kunifanya nifumbe macho yangu? Kama nimefanya chochote katika hivi, mimi nitawarudishia.”
4 他們答說:「你總沒有壓迫或虐待過我們,也沒有從任何人手裏接受過什麼。」
Wakajibu, “Hujatudanganya wala kutuonea. Hujapokea chochote kutoka kwenye mkono wa mtu awaye yote.”
5 他又對他們說:「上主給你們作證,受傅者今日也作證:你們在我手中沒有找出什麼。」他們答說:「可以作證。」
Samweli akawaambia, “Bwana ni shahidi juu yenu, pia mpakwa mafuta wake ni shahidi siku hii ya leo, kwamba hamkukuta chochote mkononi mwangu.” Wakasema, “Yeye ni shahidi.”
6 撒慕爾又對百姓說:「作見證的,是興起梅瑟和亞郎,並領你們祖先從埃及地上來的上主。
Kisha Samweli akawaambia watu, “Bwana ndiye alimchagua Mose na Aroni, na kuwaleta baba zenu akiwapandisha kutoka Misri.
7 現今你們要前來,我要在上主面前使你們認清,上主向你們和你們祖先所施行的一切恩惠:
Sasa basi, simameni hapa, kwa sababu nitakabiliana nanyi kwa ushahidi mbele za Bwana wa matendo yote ya haki yaliyofanywa na Bwana kwenu na kwa baba zenu.
8 當雅各伯和他的兒子來到埃及時,埃及人壓迫他們,你們的祖先就向上主哀號,上主遂派遺梅瑟和亞郎領你們的祖先離開了埃及,使他們住在這個地方。
“Baada ya Yakobo kuingia Misri, walimlilia Bwana kwa ajili ya msaada, naye Bwana akawatuma Mose na Aroni, ambao waliwatoa baba zenu kutoka Misri na kuwakalisha mahali hapa.
9 但他們忘卻了上主他們的天主,他就將他們交在哈祚爾的元帥息色辣手中、培肋舍特人手中和摩阿布王手中,使這些人攻打他們。
“Lakini wakamsahau Bwana Mungu wao, hivyo Mungu akawauza katika mkono wa Sisera, jemadari wa jeshi la Hazori na katika mikono ya Wafilisti na mfalme wa Moabu, ambaye alipigana dhidi yao.
10 他們就呼求上主說:我們犯了罪,離棄了上主,事奉了巴耳和阿市托勒特諸神;如今求你救我們脫離我們敵人的手,我們願事奉你。
Wakamlilia Bwana na kusema, ‘Tumetenda dhambi; tumemwacha Bwana na kutumikia Mabaali na Maashtorethi. Lakini sasa tuokoe kutoka mikono ya adui zetu, nasi tutakutumikia.’
11 上主就派耶魯巴耳、巴辣克、依弗大和三松,從你們四圍敵人的手中拯救了你們,你們纔得安居。
Ndipo Bwana akawatuma Yerub-Baali, Baraka, Yefta na Samweli, naye akawaokoa kutoka mikononi mwa adui zenu kila upande, ili ninyi mpate kukaa salama.
12 當你們看見阿孟子民的君王納哈王來攻打你們時,曾對我說:不,我們要有一位君王來管理我們,──雖然上主你們的天主原是你們的君王。
“Lakini mlipomwona yule Nahashi mfalme wa Waamoni anakuja dhidi yenu, mliniambia, ‘Hapana, tunataka mfalme atutawale,’ hata ingawa Bwana Mungu wenu alikuwa mfalme wenu.
13 現今,看,你們所揀選,所要求的君王;看,上主立了一位君王管理你們。
Sasa huyu hapa ndiye mfalme mliyemchagua, yule mliyeomba; tazameni, Bwana amemweka mfalme juu yenu.
14 若是你們敬畏上主,事奉上主,聽從他的話,不背叛上主的命令;若是你們和管理你們的君王,隨從上主你們的天主,便可生存。
Kama mkimcha Bwana na kumtumikia na kumtii nanyi msipoasi dhidi ya amri zake, ninyi pamoja na mfalme anayetawala juu yenu mkimfuata Bwana, Mungu wenu, mambo yatakuwa mema kwenu!
15 倘若你們不聽從上主的話,背叛上主的命令,上主的手必要與你們和你們的君王作對。
Lakini kama hamkumtii Bwana, nanyi kama mkiasi dhidi ya amri zake, mkono wake utakuwa dhidi yenu, kama ulivyokuwa dhidi ya baba zenu.
16 現今你們前來,看上主在你們眼前要作的這偉大的奇事。
“Sasa basi, simameni kimya mkaone jambo hili kubwa ambalo Bwana anakwenda kulifanya mbele ya macho yenu!
17 現今不是收割麥子的季節嗎﹖但是我要呼求上主打雷下雨,使你們明白,也看出:你們要求一位君王,是行了上主眼中多麼可惡的事。」
Je, sasa si mavuno ya ngano? Nitamwomba Bwana ili alete ngurumo na mvua. Nanyi mtatambua jambo hili lilivyo baya mlilolifanya mbele za macho ya Bwana mlipoomba mfalme.”
18 撒慕爾呼籲了上主,上主就在那天打雷下雨;全民眾對上主和撒慕爾很是害怕,
Kisha Samweli akamwomba Bwana, na siku ile ile Bwana akatuma ngurumo na mvua. Hivyo watu wote wakamwogopa sana Bwana na Samweli.
19 都對撒慕爾說:「你為你的僕人們轉求上主你的天主,別使我們死了,因為在我們一切罪惡之上,又加了一個為我們要求君王的罪過。」
Watu wote wakamwambia Samweli, “Mwombe Bwana Mungu wako kwa ajili ya watumishi wako, ili tusije tukafa, kwa kuwa tumeongeza uovu juu ya dhambi zetu nyingine kwa kuomba mfalme.”
20 撒慕爾對民眾說:「你們不必害怕;你們固然犯了這一切罪過,但決不要遠離上主,反而要全心事奉上主。
Samweli akajibu, “Msiogope, mmefanya uovu huu wote; hata hivyo msimwache Bwana, bali mtumikieni Bwana kwa moyo wenu wote.
21 你們不要追求不能援助,也不能施救的虛無邪神,因為他們只是「虛無」而已。
Msigeukie sanamu zisizofaa. Haziwezi kuwatendea jema, wala haziwezi kuwaokoa kwa sababu hazina maana.
22 上主為了自己的大名,決不拋棄自己的百姓,因為上主喜歡你們作他的百姓。
Kwa ajili ya jina lake kuu Bwana hatawakataa watu wake, kwa sababu ilimpendeza Bwana kuwafanya kuwa wake mwenyewe.
23 我也決不願得罪上主,停止為你們祈禱,或停止教訓你們行善道,走正路。
Kwa habari yangu, iwe mbali nami kutenda dhambi dhidi ya Bwana kwa kushindwa kuwaombea. Mimi nitawafundisha njia iliyo njema na ya kunyooka.
24 你們只該敬畏上主,全心忠誠事奉上主,因為你們看見了,他為你們作的,是何等偉大的事。
Lakini hakikisheni mnamcha Bwana na kumtumikia kwa uaminifu kwa moyo wenu wote; tafakarini mambo makubwa aliyoyatenda kwa ajili yenu.
25 假使你們仍固執於惡,你們和你們的君王都必要喪亡。」
Hata hivyo mkiendelea kufanya uovu, ninyi na mfalme wenu mtafutiliwa mbali!”

< 撒母耳記上 12 >