< 哥林多前書 16 >
1 於為聖徒捐款的事,我怎樣給迦拉達各教會規定了,你們也該照樣做。
Sasa, yahusu ule mchango kwa ajili ya watu wa Mungu: fanyeni kama nilivyoyaagiza makanisa ya Galatia.
2 每週的第一日,你們每中要照自己的能力積畜一點,各自存放著,免得我來到時再現湊。
Kila Jumapili kila mmoja wenu atenge kiasi cha fedha kadiri ya mapato yake, ili kusiwe na haja ya kufanya mchango wakati nitakapokuja.
3 幾時我一來到,就派你們所認可的人,帶著信,把你們的恩賜送到耶路撒冷去;
Wakati nitakapokuja kwenu, nitawatuma wale mtakaowachagua miongoni mwenu wapeleke barua na zawadi zenu Yerusalemu.
Kama itafaa nami niende, basi, watakwenda pamoja nami.
5 我巡行了馬其頓以後,就往你們那裏去,因為我只願巡行馬其頓,
Nitakuja kwenu, baada ya kupitia Makedonia—maana nataraji kupitia Makedonia.
6 但在你們那裏,可能我要住下,甚至過冬,以後我無論哪裡去,你們可以給我送行,
Labda nitakaa kwenu kwa muda fulani, au huenda nitakaa pamoja nanyi wakati wote wa baridi, ili mpate kunisaidia niendelee na safari yangu kokote nitakakokwenda.
7 因為這次我不願只路過時見見你們;主若准許,我就希望在你們那裏多住一些時候;
Sipendi kupita kwenu harakaharaka na kuendelea na safari. Natumaini kukaa kwenu kwa kitambo fulani, Bwana akiniruhusu.
Lakini nitabaki hapa Efeso mpaka siku ya Pentekoste.
9 因為有成效的大門已給我坦誠了,但也有許多敵對的人。
Mlango uko wazi kabisa kwa ajili ya kazi yangu muhimu hapa, ingawa wapinzani nao ni wengi.
10 若是弟茂德到了,你們要留意,叫他在你們那裏無恐無懼,因為他是辨理主的工作,如同我一樣,
Timotheo akija, angalieni asiwe na hofu yoyote wakati yupo kati yenu, kwani anafanya kazi ya Bwana kama mimi.
11 所以誰也不可輕視他。以後,你們當送他平安起程,回到我這裏,因為我與弟兄們等候著他。
Kwa hiyo mtu yeyote asimdharau, ila msaidieni aendelee na safari yake kwa amani ili aweze kurudi kwangu, maana mimi namngojea pamoja na ndugu zetu.
12 關於阿頗羅弟兄,我多次懇他,要他同弟兄們一起到你們那裏去,但他決沒有意思如今去;一有好機會,他一定會去。
Kuhusu ndugu Apolo, nimemsihi sana aje kwenu pamoja na ndugu wengine, lakini hapendelei kabisa kuja sasa ila atakuja mara itakapowezekana.
13 你們應該儆醒,應屹立在信德上,應有大丈夫氣概,應剛強有力。
Kesheni, simameni imara katika imani, muwe hodari na wenye nguvu.
Kila mfanyacho kifanyike kwa upendo.
15 弟兄們,我還要勸告你們:你們知道斯特法納一家原是阿哈雅的初果,且自願委身服事聖徒;
Ndugu, mnaifahamu jamaa ya Stefana; wao ni watu wa kwanza kabisa kuipokea imani ya Kikristo katika Akaya, na wamejitolea kuwatumikia watu wa Mungu. Ninawasihi ninyi ndugu zangu,
16 對這樣的人,和一個勞苦的人,你們應該表示服從。
muufuate uongozi wa watu kama hao, na uongozi wa kila mtu afanyaye kazi na kutumikia pamoja nao.
17 斯特法納和福突納托及阿哈依科來了,我很喜歡,因為他們填補了你們的空缺;
Nafurahi sana kwamba Stefana, Fortunato na Akaiko wamefika; wamelijaza pengo lililokuwako kwa kutokuwako kwenu.
18 他們使我和你們的心神都感到了快慰。對他們這樣的人,你們應該敬重。
Wameiburudisha roho yangu na yenu pia. Kwa hiyo inafaa kuwakumbuka watu wa namna hii.
19 亞細亞各教會問候你們;阿桂拉和普黎史拉以及他們家內的教會,在主內問候你們。
Makanisa yote ya Asia yanawasalimuni. Akula na Priskila pamoja na watu wote wa Mungu walio nyumbani mwao wanawasalimuni sana katika Bwana.
20 所有的弟兄都問候你們;你們也該以聖吻彼此問候。
Ndugu wote wanawasalimuni. Nanyi salimianeni kwa ishara ya mapendo ya Mungu.
Mimi Paulo nawasalimuni, nikiandika kwa mkono wangu mwenyewe.
Yeyote asiyempenda Bwana, na alaaniwe. MARANA THA—BWANA, njoo!
Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
Mapendo yangu yawe kwenu katika kuungana na Kristo Yesu.