< 使徒行传 9 >

1 与此同时,扫罗仍在暴力威胁着主的使徒,想要杀死他们。他到大祭司那里,
Wakati ule ule, Sauli alikuwa bado anazidisha vitisho vya kuua wanafunzi wa Bwana, akamwendea kuhani mkuu,
2 要大祭司提供授权函,扫罗想要送到大马士革的各会堂,在发现奉行此道之人后,无论男女,都准许扫罗将其缉拿,带回耶路撒冷。
naye akamwomba kuhani mkuu ampe barua za kwenda kwenye masinagogi huko Dameski, ili akimkuta mtu yeyote wa Njia Ile, akiwa mwanaume au mwanamke, aweze kuwafunga na kuwaleta Yerusalemu.
3 快到大马士革的时候,他周围忽然被来自天堂的光照亮。
Basi akiwa katika safari yake, alipokaribia Dameski, ghafula nuru kutoka mbinguni ikamwangaza kotekote.
4 他伏倒在地,听见有声音对他说:“扫罗啊,扫罗!你为什么迫害我?”
Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, “Sauli, Sauli, mbona unanitesa?”
5 他说:“主啊,你是谁?” 主说:“我就是你所迫害的耶稣。
Sauli akajibu, “U nani wewe, Bwana?” Ile sauti ikajibu, “Mimi ni Yesu unayemtesa.
6 起来吧,到城里去,会有人告诉你应当做什么。”
Sasa inuka uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda.”
7 与扫罗同行的人听见了声音,却看不见人影,于是站在那里说不出话来。
Watu waliokuwa wakisafiri pamoja na Sauli wakasimama bila kuwa na la kusema, kwa sababu walisikia sauti lakini hawakumwona aliyekuwa akizungumza.
8 扫罗从地上爬起来,睁开眼睛后却什么也看不见。随行的人牵着他的手,领他进入大马士革。
Sauli akainuka kutoka pale chini na alipojaribu kufungua macho yake hakuweza kuona kitu chochote. Basi wakamshika mkono wakamwongoza mpaka Dameski.
9 随后三天,他什么也看不到,不吃不喝。
Naye kwa muda wa siku tatu alikuwa kipofu naye hakula wala kunywa chochote.
10 大马士革有一名叫亚拿尼亚的使徒,主在异像中唤他:“亚拿尼亚!” 他说:“主啊,我在这里。”
Huko Dameski alikuwepo mwanafunzi mmoja jina lake Anania. Bwana alimwita katika maono, “Anania!” Akajibu, “Mimi hapa Bwana.”
11 主说:“起来到直街去,在犹大家里找一位来自大数的人。他叫扫罗,现在正在祷告,
Bwana akamwambia, “Ondoka uende katika barabara iitwayo Nyofu ukaulize katika nyumba ya Yuda mtu kutoka Tarso, jina lake Sauli, kwa maana wakati huu anaomba,
12 他在异象中看见一位名叫亚拿尼亚的人,过去为他按手,让他可以再次看得见。”
katika maono amemwona mtu aitwaye Anania akija na kuweka mikono juu yake ili apate kuona tena.”
13 但亚拿尼亚回答:“主啊,很多人都说起过这个人,他在耶路撒冷做了许多迫害你信徒的事,
Anania akajibu, “Bwana, nimesikia kutoka kwa watu wengi habari nyingi kuhusu mtu huyu na madhara yote aliyowatendea watakatifu wako huko Yerusalemu.
14 祭司长还给了他权力,逮捕所有膜拜和追随你的人。”
Naye amekuja hapa Dameski akiwa na mamlaka kutoka kwa viongozi wa makuhani ili awakamate wote wanaotaja jina lako.”
15 但主对他说:“去吧,我已选中此人,把我的名传给异教徒、君王和以色列人。
Lakini Bwana akamwambia Anania, “Nenda! Mtu huyu ni chombo changu kiteule nilichokichagua, apate kulichukua Jina langu kwa watu wa Mataifa na wafalme wao na mbele ya watu wa Israeli.
16 我会向他显示,为了我之名,他不得不受苦。”
Nami nitamwonyesha jinsi impasavyo kuteseka kwa ajili ya Jina langu.”
17 于是亚拿尼亚出发去了那栋房子,为扫罗按手,说:“扫罗兄弟,主耶稣在你来的路上已向你显现,他派我来让你可以重见光明,可以被圣灵充满。”
Kisha Anania akaenda kwenye ile nyumba, akaingia ndani. Akaweka mikono yake juu ya Sauli akasema, “Ndugu Sauli, Bwana Yesu aliyekutokea njiani amenituma kwako ili upate kuona tena na ujazwe Roho Mtakatifu.”
18 话音刚落,扫罗的眼里立刻掉下来鳞片一样的东西,然后他就恢复了视力,然后起身接受施洗。
Ghafula vitu kama magamba vikaanguka chini, kutoka machoni mwa Sauli, akapata kuona tena. Akasimama, akabatizwa.
19 他还吃了些东西,感觉有些力气了,之后他和大马士革的使徒同住了几天。
Baada ya kula chakula, akapata nguvu tena. Sauli akakaa siku kadhaa pamoja na wanafunzi huko Dameski.
20 然后,他立刻在各会堂宣讲耶稣,说“耶稣是上帝之子。”
Papo hapo akaanza kuhubiri kwenye masinagogi kwamba “Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu”
21 众人听此都感到很惊讶,说:“他不是在耶路撒冷迫害那些相信耶稣的人吗?他来这里,不是为了捉拿信徒,然后交给祭司长吗?”
Watu wote waliomsikia Sauli walishangaa na kuuliza, “Huyu si yule mtu aliyesababisha maangamizi makuu huko Yerusalemu miongoni mwa watu waliolitaja jina hili? Naye si amekuja hapa kwa kusudi la kuwakamata na kuwapeleka wakiwa wafungwa mbele ya viongozi wa makuhani?”
22 但扫罗变得越来越有信心,以强有力的方式证明耶稣就是基督,住在大马士革的犹太人完全无法与他辩论。
Sauli akazidi kuwa hodari na kuwashangaza Wayahudi walioishi Dameski kwa kuthibitisha kuwa Yesu ndiye Kristo.
23 过了一段时间后,犹太人商议要杀掉他。
Baada ya siku nyingi kupita, Wayahudi wakafanya shauri kumuua Sauli.
24 但扫罗知晓了他们的阴谋。犹太人在各城门处日夜把守,打算除掉他。
Lakini shauri lao likajulikana kwa Sauli. Wayahudi wakawa wanalinda malango yote ya mji, usiku na mchana ili wapate kumuua.
25 于是在一天晚上,他的门徒从城墙的一个开口处,用大篮子把他顺了下去。
Lakini wafuasi wake wakamchukua usiku wakamshusha akiwa ndani ya kapu kupitia mahali penye nafasi ukutani.
26 扫罗来到耶路撒冷后想要见其他门徒,但大家都怕他,不相信他也是个门徒。
Sauli alipofika Yerusalemu akajaribu kujiunga na wanafunzi lakini wote walimwogopa, kwa maana hawakuamini kwamba kweli naye alikuwa mwanafunzi.
27 但巴拿巴带着他去见其他门徒,还帮他解释了如何在路上看见主、主如何与他说话,以及扫罗如何在大马士革以耶稣之名传道。
Lakini Barnaba akamchukua, akampeleka kwa wale mitume. Akawaeleza jinsi Sauli akiwa njiani alivyomwona Bwana, jinsi Bwana alivyosema naye na jinsi alivyohubiri kwa ujasiri kwa jina la Yesu huko Dameski.
28 于是扫罗与其他门徒待在一起,与他们走遍耶路撒冷,
Kwa hiyo Sauli akakaa nao akitembea kwa uhuru kila mahali huko Yerusalemu, akihubiri kwa ujasiri katika jina la Bwana.
29 以主之名勇敢讲道。他与说希腊语的犹太人讲述辩论,那些人却想杀了他。
Alinena na kuhojiana na Wayahudi wenye asili ya Kiyunani lakini wao walijaribu kumuua.
30 他的兄弟们得知这件事,就把他带到该撒利亚,派他往大数去。
Wale ndugu walipopata habari wakampeleka hadi Kaisaria, wakamsafirisha kwenda Tarso.
31 当时位于犹太、加利利、撒玛利亚各处的教会都太平无事。这些教会越来越强大,人数也越来越多,因为信徒们在圣灵的鼓励下,为主过着虔诚的生活。
Ndipo kanisa katika Uyahudi wote, Galilaya na Samaria likafurahia wakati wa amani. Likatiwa nguvu, na kwa faraja ya Roho Mtakatifu, idadi yake ikazidi kuongezeka, na likaendelea kudumu katika kumcha Bwana.
32 彼得周游各地过程中,去造访吕大的信徒。
Petro alipokuwa akisafiri sehemu mbalimbali, alikwenda kuwatembelea watakatifu walioishi huko Lida.
33 在那里他遇见了以尼雅,此人瘫痪在床已经整整八年。
Huko alimkuta mtu mmoja aitwaye Ainea, ambaye alikuwa amepooza na kwa muda wa miaka minane alikuwa hajaondoka kitandani.
34 彼得对他说:“以尼雅,耶稣基督让你痊愈了!起来,拿好你的垫子!”以尼雅立刻站起来。
Petro akamwambia, “Ainea, Yesu Kristo anakuponya, inuka utandike kitanda chako.” Mara Ainea akainuka.
35 吕大和沙仑的所有居民看见以尼雅,于是就成为了主的信徒。
Watu wote wa Lida na Sharoni walipomwona Ainea akitembea wakamgeukia Bwana.
36 在约帕有一个名叫戴比莎(希腊语为多加)的女信徒,为人一向乐善好施。
Huko Yafa palikuwa na mwanafunzi jina lake Tabitha (ambalo kwa Kiyunani ni Dorkasi). Huyu alikuwa mkarimu sana, akitenda mema na kuwasaidia maskini.
37 但在那时候她因病去世,人们把她洗净后安置在楼上。
Wakati huo akaugua, akafa na wakiisha kuuosha mwili wake wakauweka katika chumba cha ghorofani.
38 吕大与约帕距离不远,门徒们听说彼得在那边,就派两个人去求他,说:“请立刻到我们这边来。”
Kwa kuwa Yafa hapakuwa mbali sana na Lida, wanafunzi waliposikia kwamba Petro yuko huko waliwatuma watu wawili kwake ili kumwomba, “Tafadhali njoo huku pasipo kukawia.”
39 于是彼得动身跟他们前去。来到这里后,他们把他带上楼。所有寡妇都在那里哭泣,把多加在世时给她们做的衣服拿给彼得看。
Kwa hiyo Petro akainuka akaenda nao, naye alipowasili, wakampeleka hadi kwenye chumba cha ghorofani alipokuwa amelazwa. Wajane wengi walisimama karibu naye wakilia na kuonyesha majoho na nguo nyingine ambazo Dorkasi alikuwa amewashonea alipokuwa pamoja nao.
40 彼得让大家都出去,然后跪下来祷告,接着转过身对那具尸体说:“戴比莎,起来吧!”她睁开眼睛,看见彼得后就坐了起来。
Petro akawatoa wote nje ya kile chumba, kisha akapiga magoti akaomba, akaugeukia ule mwili akasema, “Tabitha, inuka.” Akafumbua macho yake na alipomwona Petro, akaketi.
41 彼得伸手扶她起来,然后叫来信徒和寡妇,活生生的多加就出现在他们面前。
Petro akamshika mkono akamwinua, ndipo akawaita wale watakatifu na wajane akamkabidhi kwao akiwa hai.
42 这事传遍了约帕,很多人便信了主。
Habari hizi zikajulikana sehemu zote za Yafa na watu wengi wakamwamini Bwana.
43 彼得在约帕的制皮匠西门家里住了很久。
Petro akakaa Yafa kwa siku nyingi akiishi na Simoni mtengenezaji ngozi.

< 使徒行传 9 >