< 使徒行传 12 >
Wakati huo mfalme Herode akanyosha mkono wake kwa baadhi ya wale wanaotoka kwenye kusanyiko ili kuwatesa.
Akamwuua Yakobo nduguye Yohana kwa upanga.
3 由于此举受到了犹太人的支持,于是他又在除酵节期间捉拿彼得。
Baada ya kuona kuwa inawapendeza Wayahudi, akamkamata na Petro tena. Hii ilikuwa wakati wa mikate isiyochachwa.
4 他们逮捕了彼得后将其投入监牢,由四班士兵看守,每班四个人。君王希律打算逾越节过后,就对他进行公审。
Alipomkamata, akamweka gerezani na akaweka vikosi vinne vya askari ili kumlinda, alikuwa akitarajia kumpeleka kwa watu baada ya Pasaka.
Petro akawekwa gerezani, lakini maombi yakafanywa kwa bidii na kusanyiko kwa ajili yake kwa Mungu.
6 就在希律打算将他公审的前一夜,彼得被安排睡在两名士兵中间,手腕上的两条锁链分别与两人栓在一起,还有卫兵守在门前。
Siku kabla Herode hajaenda kumtoa, Usiku huo Petro alikuwa amelala katikati ya maaskari wawili, akiwa amefungwa na minyororo miwili, na walinzi mbele ya mlango walikuwa wakilinda gereza.
7 忽然,一名天使出现,光芒照亮了牢房。天使将彼得唤醒,说:“快点!起来吧!”于是彼得手上的锁链就脱落了。
Tazama, malaika wa Bwana ghafla akamtokea na nuru ikang'aa ndani. Akampiga Petro ubavuni na kumwamsha akisema, “Amka haraka.”ndipo minyororo aliyokuwa amefungwa ikafunguka kutoka mikononi mwake.
8 天使对他说:“穿上衣服和鞋!”彼得照做了。天使又对他说:“披上外衣,跟我走!”
Malaika akamwambia, “Vaa nguo zako na vaa viatu vyako.” Petro akafanya hivyo. Malaika akamwambia, “Vaa vazi lako na unifuate.”
9 于是彼得就跟着天使走出去,但他只是以为看到了异象,没有意识到天使所做的一切都在真实发生。
Hivyo Petro akamfuata Malaika na akatoka nje. Hakuamini kilichofanywa na malaika kama ni cha kweli. Alidhani anaona maono.
10 他们经过第一队和第二队守卫,来到通往城内的铁门,门便自动给他们打开。他们出来后沿着街道行走,天使忽然就离开了。
Baada ya kupita lindo la kwanza na la pili, wakafika kwenye geti la chuma la kuingilia kwenda mjini, likafunguka lenyewe kwa ajili yao. Wakatoka nje wakashuka kwenye mtaa, mara Malaika akamwacha.
11 彼得这时候才明白,说:“现在我知道怎么回事了!主派天使将我从希律的权势中拯救出来,让我躲过犹太人的阴谋。”
Petro alipojitambua, akasema, “Sasa nimeamini kuwa Bwana alimtuma Malaika wake ili kunitoa katika mikono ya Herode, na kwa matarajio ya watu wote wa uyahudi.”
12 明白这一切,他就到约翰(又名马可)的母亲玛利亚家中,很多信徒聚在那里祷告。
Baada ya kujua haya, akaja kwenye nyumba ya Mariamu mama yake Yohana ambaye ni Marko; Wakristo wengi walikusanyika wakiomba.
13 彼得敲了敲大门,一位名叫罗大的侍女出来准备开门。
Alipobisha kwenye mlango wa kizuizi, mtumishi mmoja msichana anayeitwa Roda akaja kufungua.
14 但认出是彼得的声音后,她兴奋的顾不上开门就跑进屋,大声喊:“彼得就在门外!。”
Alipotambua ni sauti ya Petro, kwa furaha akashindwa kuufungua mlango; badala yake, akakimbia ndani ya chumba; na kuwajulisha kuwa Petro amesimama mbele ya Mlango.
15 大家说:“你疯了!”她却坚持地说这是真的。他们说:“那一定是他的天使!”
Hivyo, Wakasema kwake, “Wewe ni mwendawazimu” lakini alikazia kuwa ni kweli ni yeye. Wakasema “Huyo ni malaika wake.”
16 彼得继续敲门,他们最终打开了门,一见是他,非常惊讶。
Lakini Petro aliendelea kubisha, na walipofungua mlango, wakamwona na wakashangaa sana. Petro akawanyamazisha kwa mkono kimya kimya na akawaambia jinsi Bwana alivyomtoa kutoka Gerezani. akasema,
17 彼得向他们举起手示意安静,然后对他们解释主如何带他走出监牢。他又说:“把这事告诉雅各和众兄弟。”然后就离开去往别处了。
“Wajulishe haya mambo Yakobo na ndugu zake.” Kisha akaondoka akaenda sehemu nyingine.
18 天亮的时候,士兵们惊慌不已,不知彼得去了哪里。
Kulipokuwa mchana, kukawa na huzuni kubwa kati ya askari, kuhusiana na kilichotokea kwa Petro.
19 希律开始四处搜索他,但始终没有找到。于是就审问卫兵,然后下令把他们处死。随后希律便离开犹太去往该撒利亚,在那里住下。
Baada ya Herode kumtafuta na hakumwona akawauliza walinzi na akaamuru wauawe. Akaenda kutoka uyahudi mpaka Kaisaria na kukaa huko.
20 此刻的希律对推罗和西顿人充满了愤怒。这两个地方的人派了一个联合代表团来见他,设法拉拢了国王的个人助理伯拉斯。这个代表团希望向希律求和,因为这两地在粮食供应商都依赖希律的国家。
Herode alikuwa na hasira juu ya watu wa Tiro na Sidoni. Wakaenda kwa pamoja kwake. Wakawa na urafiki na Blasto msaidizi wa mfalme, ili awasaidie. Kisha wakaomba amani, kwa sababu nchi yao ilipokea chakula kutoka katika nchi ya mfalme.
21 到了约定见面的日期,希律穿上国王的长袍,坐在王座上,向众人讲话。
Siku iliyokusudiwa Herode alivaa mavazi ya kifalme na kukaa kwenye kiti chake cha kifalme, na akawahutubia.
22 人群中有人大声说:“这是上帝的声音,不是人的声音!”
Watu wakapiga kelele, “Hii ni sauti ya mungu wala si sauti ya mwanadamu!”
23 但由于他没有将荣耀归于上帝,主的使者将他击倒。 他被虫吃掉了,死了。
Mara ghafla malaika akampiga, kwa sababu alikuwa hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango na akafa
Lakini neno la Mungu likakua na kusambaa.
25 巴拿巴和扫罗完成了送捐款的任务,就带着约翰(马克)从耶路撒冷返回。
Baada ya Barnaba na Sauli kukamilisha huduma yao wakatoka pale wakarejea Yerusalemu, wakamchukua na Yohana ambaye jina la kuzaliwa ni Marko.