< Kamtawngnae 48 >

1 Hathnukkhu, Joseph koe, Thai haw, na pa a pataw, telah atipouh awh. A capa Manasseh hoi Ephraim hah a hrawi teh a ceikhai.
Baada ya muda Yosefu akaambiwa kwamba, “Baba yako ni mgonjwa.” Kwa hiyo akawachukua wanawe wawili Manase na Efraimu, pamoja naye.
2 Jakop koevah, khenhaw! na capa Joseph nang koe a tho, telah atipouh awh. Hatdawkvah, Jakop teh tha a kâsangue teh ikhun dawk a tahung.
Yakobo alipoambiwa, “Mwanao Yosefu amekujia kukuona,” Israeli akakusanya nguvu zake, akaketi kitandani.
3 Jakop ni Joseph koevah, Cathut Athakasaipounge teh Kanaan ram, Luz kho dawk kai koevah a kamnue teh yawhawinae na poe.
Yakobo akamwambia Yosefu, “Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu katika nchi ya Kanaani, huko akanibariki,
4 Kai koevah, ca catounnaw moikapap na poe han, na pungdaw sak han, tamihupui lah na sak han, hahoi hete ram heh ka tho hane na ca catounnaw koe râw lah na poe awh han, telah na ti pouh.
naye akaniambia, ‘Nitakufanya ustawi na kuongezeka hesabu yako, nitakufanya kuwa jamii ya mataifa, nami nitakupa nchi hii uimiliki milele wewe na wazao wako baada yako.’
5 Na ca roi Izip ram, nang koe ka tho hoehnahlan na khe e haiyah kaie doeh. Manasseh hoi Ephraim heh, Reuben hoi Simeon patetlah kaie lah ao han.
“Sasa basi, wanao wawili waliozaliwa kwako huku Misri kabla sijaja hapa kwako watahesabiwa kuwa ni wangu; Efraimu na Manase watakuwa wangu, kama vile Reubeni na Simeoni walivyo wangu.
6 Atu hoi bout na khe e teh namae lah ao han. A coe awh han e râw dawk a hmau roi e min hah a hmawng awh han.
Lakini watoto utakaowazaa baada yao watakuwa wako. Katika nchi watakayoirithi, watatambuliwa kwa jina la ndugu zao.
7 Hatei, kaie kong dawk, Paddanaram ram hoi ka tho navah, Rachel teh Kanaan ram e lampui dawk, Ephrath kho hoi lam bet ahlanae koe kai teng vah a due teh hawvah Ephrath lam dawk ka pakawp. (Hot teh Bethlehem doeh).
Nilipokuwa ninarudi kutoka Padani, katika huzuni yangu Raheli alifariki katika nchi ya Kanaani tulipokuwa tungali tukisafiri, tukiwa karibu kufika Efrathi. Kwa hiyo nilimzika huko, kando ya njia iendayo Efrathi” (yaani Bethlehemu).
8 Hahoi, Isarel ni Joseph e capa roi a khet teh, hetnaw heh apinaw maw telah ati.
Wakati Israeli alipowaona wana wa Yosefu, akauliza, “Hawa ni nani?”
9 Joseph ni a na pa koevah, ahnimouh roi teh ka capa roi doeh, Cathut ni hi vah na poe e roi doeh, telah atipouh. Ahni ni pahren lahoi kai koe thokhai haw, yawhawinae ka poe han, telah ati.
Yosefu akamjibu baba yake, “Hawa ni wana ambao Mungu amenipa nikiwa huku.” Ndipo Israeli akasema, “Walete kwangu ili niwabariki.”
10 Isarel teh a matawng toung dawkvah a mit hah kacailah hmawt thai hoeh toe. Hahoi teh, hnai sak haw, ahni ni a tapam teh a paco.
Basi macho ya Israeli yalikuwa hayaoni vizuri kwa sababu ya uzee, naye aliona kwa shida. Kwa hiyo Yosefu akawaleta wanawe karibu na baba yake, Israeli akawabusu na akawakumbatia.
11 Isarel ni Joseph koevah, Na mei hmu hane boehai ka ngaihawi hoeh ei, Cathut ni na ca catounnaw e mei totouh na hmu sak, telah ati.
Israeli akamwambia Yosefu, “Kamwe sikutazamia kuuona uso wako tena, lakini sasa Mungu ameniruhusu kuwaona watoto wako pia.”
12 Joseph ni ahnimouh teh a na pa e phai rahak hoi a la teh a hmalah a tabo sak.
Ndipo Yosefu akawaondoa wanawe magotini mwa Israeli naye akasujudu hadi nchi.
13 Hahoi, Joseph ni kahni touh hoi a ceikhai teh Ephraim aranglae kut hoi Isarel e avoilae kut koe lah a ceikhai. Manasseh hah avoilae kut hoi Isarel e aranglae kut koe lah a ceikhai.
Yosefu akachukua wale wana wawili, Efraimu kwenye mkono wake wa kuume akimwelekeza kwenye mkono wa kushoto wa Israeli, na Manase katika mkono wake wa kushoto akimwelekeza kwenye mkono wa kuume wa Israeli, akawaleta karibu na babu yao.
14 Hahoi, Isarel ni a kut a khingkhai teh aranglae kut hah kanaw e Ephraim e a lû dawk a toung teh avoilae kut hah Manasseh e lû van vah a toung. Bangkongtetpawiteh, ahni teh camin lah ao.
Lakini Israeli akaupeleka mkono wake wa kuume, akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, ingawa alikuwa ndiye mdogo, na mkono wake wa kushoto akaukatisha, akauweka juu ya kichwa cha Manase, ingawa Manase alikuwa ndiye mzaliwa wa kwanza.
15 Hottelah yawhawinae a poe teh kakhekung Abraham hoi Isak hmalah ouk kaawm pouh e Cathut, sahnin totouh ka hringyung thung pueng na kakawkkung Cathut.
Ndipo akambariki Yosefu akisema, “Mungu ambaye baba zangu Abrahamu na Isaki walimtii, Mungu ambaye amekuwa mchungaji wa maisha yangu yote mpaka leo hii,
16 Hawihoehnae pueng thung hoi na karatangkung kalvantaminaw ni hete camo roi yawhawinae poe naseh, Abraham hoi Isak min teh ahnimouh roi ni sin naseh. Hahoi, talai lungui vah tami moikapap lah pungdaw awh naseh telah ati.
Malaika ambaye aliniokoa kutoka madhara yote, yeye na awabariki vijana hawa. Na waitwe kwa jina langu na kwa majina ya baba zangu Abrahamu na Isaki, wao na waongezeke kwa wingi katika dunia.”
17 A na pa ni aranglae kut Ephraim e lû dawk a toung e Joseph ni a hmu navah, a lungkuep hoeh dawkvah a na pa e kut Ephraim lû dawk a toung e hah Manasseh e a lû dawk puen hanelah a tawm.
Yosefu alipoona baba yake akiweka mkono wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu, hakupendezwa, kwa hiyo akauchukua mkono wa baba yake kutoka kichwa cha Efraimu na kuuweka juu ya kichwa cha Manase.
18 Joseph ni a na pa koevah, Apa hettelah mahoeh. Bangkongtetpawiteh, het nahoehmaw a camin. Aranglae na kut a lû dawk na toung hane vaw, telah atipouh.
Yosefu akamwambia, “Hapana, baba yangu, huyu ndiye mzaliwa wa kwanza; uweke mkono wako wa kuume juu ya kichwa chake.”
19 Hatei, a na pa ni a ngai hoeh dawk, ka panue ka ca, ka panue. Ahni haiyah miphun telah kaw han e kamcu lah ao vaiteh a lentoe van han. Hatei, a nawngha heh ahni hlakvah hoe a lentoe vaiteh a ca catounnaw haiyah miphun moikapap lah ao awh han, telah ati.
Lakini baba yake akakataa, akasema, “Ninajua, mwanangu, ninajua. Yeye pia atakuwa taifa, naye pia atakuwa mkuu. Hata hivyo, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye, nao wazao wake watakuwa kundi la mataifa.”
20 Hatdawkvah, hote hnin dawk yawhawinae a poe teh, nang pawlawk dawk Cathut ni Isarel teh yawhawinae poe naseh, nang teh Ephraim hoi Manasseh patetlah na tat naseh telah atipouh teh, Manasseh hmalah Ephraim ao sak.
Akawabarikia siku ile na kusema, “Kwa jina lenu Israeli watatamka baraka hii: ‘Mungu na awafanye kama Efraimu na Manase.’” Kwa hiyo akamtanguliza Efraimu mbele ya Manase.
21 Hottelah, Isarel ni Joseph koevah, khenhaw! meimei ka due toe, hat eiteh Cathut teh nang koevah ao vaiteh mintoenaw e ram dawk na hrawi awh han.
Ndipo Israeli akamwambia Yosefu, “Mimi ninakaribia kufa, lakini Mungu atakuwa pamoja nanyi, na atawarudisha katika nchi ya baba zenu.
22 Hothloilah, na hmaunawnghanaw hane thung hoi ham buet touh, tahloi hoi licung, Amor taminaw e kut dawk ka la e hah na thap pouh, telah ati.
Kwako wewe, kama aliye juu ya ndugu zako, ninakupa sehemu moja zaidi ya ndugu zako, lile eneo nililoteka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”

< Kamtawngnae 48 >