< Kamtawngnae 39 >
1 Joseph teh Ishmael taminaw koe Izip ram a thokhai awh teh, Izip siangpahrang Faro kut rahim imkaringkung lah kaawm e Potiphar ni a ran.
Wakati huu Yosefu alikuwa amechukuliwa mpaka Misri. Mmisri aliyeitwa Potifa aliyekuwa mmojawapo wa maafisa wa Farao, mkuu wa ulinzi, akamnunua Yosefu kutoka kwa Waishmaeli waliomleta Misri.
2 BAWIPA teh Joseph koe ao teh, ahni teh a lam ka cawn e tami lah ao teh Izip tami a bawipa im vah ao.
Bwana alikuwa pamoja na Yosefu, naye akastawi, Yosefu akaishi nyumbani kwa bwana wake Mmisri.
3 A bawipa ni BAWIPA teh ahni koe a o, a hnosak tangkuem dawk a lamcawn tie hah a panue.
Potifa alipoona kuwa Bwana alikuwa pamoja na Yosefu na kwamba Bwana alimfanikisha kwa kila kitu alichokifanya,
4 Joseph teh a bawipa e a lungyouk lah thaw ouk a tawk. A bawipa ni a imkaringkung kacue lah a ta teh, a tawn e hnonaw pueng ahnie kâtawnnae rahim koung a ta pouh.
Yosefu alipata kibali machoni pa Potifa, akamfanya mhudumu wake. Potifa akamweka kuwa msimamizi wa nyumba yake, naye akamkabidhi kuwa mwangalizi wa kila kitu alichokuwa nacho.
5 Hahoi, imkaringkung lah a ta hnukkhu, BAWIPA ni Joseph pawlawk hoi Izip imthungkhu hah yawhawi a poe.
Kuanzia wakati huo Potifa alipomweka Yosefu kuwa msimamizi wa nyumba na mali zake zote alizokuwa nazo, Bwana aliibariki nyumba ya Mmisri huyo kwa sababu ya Yosefu. Baraka ya Bwana ilikuwa juu ya kila kitu alichokuwa nacho Potifa, nyumbani na shambani.
6 A tawn e pueng hah Joseph kut dawk be a ta pouh teh, a ca e vaiyei hloilah teh ahni koe kaawm e hnonaw pueng hah be a poe. Joseph teh a tungtang kahawi e lah ao teh a mei hai a hawi.
Kwa hiyo Potifa akamwachia Yosefu uangalizi wa kila kitu alichokuwa nacho, Yosefu alipokuwa katika uongozi, Potifa hakuwa na sababu ya kujishughulisha na kitu chochote isipokuwa chakula alichokula. Yosefu alikuwa mwenye umbo zuri na sura ya kuvutia;
7 Hathnukkhu, a bawipa e yu ni Joseph hah a noe teh, na ipkhai leih ti hoi pou a pasawt.
baada ya kitambo mke wa Potifa akamtamani Yosefu, akamwambia, “Njoo, ukutane nami kimwili!”
8 Hatei ngai pouh hoeh. A bawipa e yu koevah, khenhaw! ka bawipa ni hete im dawkvah, bang hno maw kaawm tie panuek hoeh, a tawn e naw pueng ka kut dawk koung a ta.
Lakini Yosefu akakataa. Akamwambia yule mwanamke, “Mimi nikiwa katika uongozi, bwana wangu hahusiki na kitu chochote katika nyumba hii, kila kitu alicho nacho amenikabidhi.
9 Hete im dawk kai hlak ka len e apihai awm hoeh. A yu na tho patetlah nang hloilah kai hane a pasoung hoeh e banghai awm hoeh. Hatdawkvah, hethloilah kalen e thoenae hoi yonnae heh Cathut taranlahoi bangtelamaw khuet ka sak han vaw, telah ati.
Hapa nyumbani hakuna aliye mkuu kuliko mimi. Bwana wangu hakunizuilia kitu chochote isipokuwa wewe, kwa kuwa wewe ni mke wake. Nitawezaje basi kufanya uovu huu na kutenda dhambi dhidi ya Mungu?”
10 Hahoi, hnin touh hnukkhu hnin touh, Joseph hah a pasawt nakunghai a ikhai hane teh ngai pouh hoeh.
Ingawa yule mwanamke aliendelea kumshawishi Yosefu siku baada ya siku, Yosefu alikataa kukutana naye kimwili wala kukaa karibu naye.
11 Hatei, a hnin hnin touh teh, Joseph imthungkhu thaw tawk hanelah a kâen teh, hatnae tueng dawk imthungkhu tami buet touh hai la awm hoeh.
Siku moja Yosefu akaingia ndani ya nyumba kufanya kazi zake, wala hapakuwepo na mfanyakazi yeyote ndani ya nyumba.
12 Hahoi teh, napui ni na ipkhai leih telah a angki dawk a kuet pouh teh, a kut dawk angki pak rading teh alawilah a yawng takhai.
Mke wa Potifa akashika vazi Yosefu alilokuwa amevaa, akamwambia, “Njoo tukutane kimwili!” Lakini Yosefu akaacha vazi lake mkononi mwa huyo mwanamke, akatoka nje ya nyumba akikimbia.
13 Hahoi teh, a angki a kut dawk pak a rading teh a yawng takhai tie a panue toteh,
Yule mwanamke alipoona kwamba Yosefu amemwachia vazi lake mkononi na kukimbilia nje ya nyumba,
14 a im kaawmnaw hah a kaw teh, khenhaw! kai na kaya sak hanelah hete Hebru tami ni kai na yonkhai hanelah imthungkhu na kâen sin teh thayung hoi ka hram pouh.
akawaita watumishi wake wa nyumbani, akawaambia, “Tazameni! Huyu Mwebrania ameletwa hapa kutudhihaki! Aliingia hapa ndani ili akutane nami kimwili, lakini nikapiga kelele.
15 Hahoi, ka lawk hoi thayung hoi ka hram toteh, kama koe a angki pak a rading teh a yawng takhai telah ati.
Aliposikia kelele za kuomba msaada, akaacha vazi lake kando yangu akakimbilia nje.”
16 A bawipa a tho hoehroukrak a hnicu teh ama koevah pou a hruek.
Yule mwanamke akaliweka lile vazi karibu naye mpaka Potifa aliporudi nyumbani.
17 Hahoi teh a vâ koe telah a dei pouh. Hete Hebru tami san kai koe na thokhai e heh, yeiraipo sak hanelah hoi kai koe na kâen sin.
Ndipo akamweleza kisa hiki, akisema: “Yule mtumwa wa Kiebrania uliyetuletea alinijia ili kunidhihaki.
18 Hahoi, lawk hoi tha hoi ka hram tahma vah, a khohna a yawng takhai telah ati.
Lakini mara nilipopiga kelele kuomba msaada, akaliacha vazi lake kando yangu akakimbia nje ya nyumba.”
19 Hahoi, a bawipa koe na san ni hettelah na sak tie a yu ni a dei e lawk hah a thai toteh a lungkhuek.
Potifa aliposikia kisa hiki mkewe alichomweleza, akisema, “Hivi ndivyo mtumwa wako alivyonitenda.” Hasira ya Potifa ikawaka.
20 Hottelah a bawipa ni Joseph a ceikhai teh thongim siangpahrang ni tami khik katek hoi ouk tanae thongim thung a paung awh.
Potifa akamchukua Yosefu na kumweka gerezani, mahali ambapo wahalifu wa mfalme walikuwa wamefungwa. Lakini wakati Yosefu alipokuwa huko gerezani,
21 Hateiteh, BAWIPA teh Joseph koe ao teh, a lathueng vah lungmanae a tawn teh thongim ka ring e hmalah minhmai kahawi a hmu sak.
Bwana alikuwa pamoja naye, akamhurumia na kumpa kibali mbele ya msimamizi wa gereza.
22 Hahoi teh, thongim karingkung ni thongkabawtnaw pueng hah Joseph kut dawk koung a ta teh, haw e sak e naw teh Joseph e tawk sak e lah koung a coung.
Kwa hiyo msimamizi wa gereza akamweka Yosefu awe mkuu wa wafungwa pamoja na kusimamia yote ambayo yalitendeka mle gerezani.
23 BAWIPA teh ahni koe ao teh, a lamcawn sak dawkvah, thongim karingkung ni Joseph e kâtawnnae rahim kaawmnaw pueng hah banghai khen awh hoeh toe.
Msimamizi wa gereza hakujishughulisha tena na kitu chochote kilichokuwa chini ya uangalizi wa Yosefu, kwa sababu Bwana alikuwa pamoja na Yosefu akimfanikisha kwa kila alichofanya.