< 2 Setouknae 18 >

1 Jehoshaphat teh ka tangreng poung e lah ao teh, barinae a tawn. Ahab hoi a kâkuet roi.
Basi, Yehoshafati alikuwa na mali nyingi sana na heshima. Naye akafanya urafiki na Ahabu kwa mwanawe kumwoa binti wa Ahabu.
2 Kum moikasaw aloum hnukkhu Samaria e Ahab koe a cei. Ahab ni Jehoshaphat hoi a taminaw hanlah maitotan hoi tunaw moikapap a thei pouh. Hahoi Gilead ram Ramoth kho tuk hanelah a coun.
Baada ya miaka kadhaa akashuka kumtembelea Ahabu huko Samaria. Ahabu akachinja ngʼombe na kondoo wengi kwa ajili yake na watu aliokuwa amefuatana nao. Kisha Ahabu akamshawishi Yehoshafati kukwea pamoja naye ili kuishambulia Ramoth-Gileadi.
3 Isarel siangpahrang Ahab ni Judah siangpahrang Jehoshaphat koe, kai koe Gilead ram Ramoth kho na tho han maw, telah a pacei. Ahni ni, kai hoi nang, ka taminaw hoi na taminaw teh cungtalah doeh. Hatdawkvah taran rei tuk awh sei atipouh.
Ahabu mfalme wa Israeli akamuuliza Yehoshafati mfalme wa Yuda, “Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Ramoth-Gileadi?” Yehoshafati akamjibu mfalme wa Israeli, “Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako. Tutakuwa pamoja nawe vitani.”
4 Jehoshaphat ni Isarel siangpahrang koevah, BAWIPA e lawk na ring mahoeh maw, telah a pacei.
Lakini Yehoshafati pia akamwambia mfalme wa Israeli, “Kwanza tafuta shauri la Bwana.”
5 Hatnavah Isarel siangpahrang ni, profet 400 touh a kaw teh, ahnimouh koevah, Gilead ram Ramoth kho tuk hanelah ka cei han maw, ka cet mahoeh maw, telah atipouh. Ahnimouh ni cet yawkaw Cathut ni siangpahrang kut dawk na poe han, telah atipouh awh.
Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawaleta pamoja manabii wanaume wapatao mia nne, akawauliza, “Je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi, au niache?” Wakajibu, “Naam, nenda kwa kuwa Mungu ataiweka Ramoth-Gileadi mkononi mwa mfalme.”
6 Hatei, Jehoshaphat ni BAWIPA e profet buet touh boehai awm hoeh maw atipouh.
Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa ambaye tunaweza kumuuliza?”
7 Isarel siangpahrang ni Jehoshaphat koe, BAWIPA koe ka pacei pouh hane buet touh ngoun teh ao. Hatei, ahni teh ka hmuhma e doeh. Bangkongtetpawiteh, ahawinae dei boihoeh. Ahni teh Imlah capa Mikah doeh atipouh. Jehoshaphat ni, siangpahrang ni hottelah dei hanh naseh atipouh.
Mfalme wa Israeli akamjibu Yehoshafati, “Bado yupo mtu mmoja ambaye kupitia yeye twaweza kumuuliza shauri la Bwana, lakini namchukia kwa sababu huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu mimi, lakini kila mara hunitabiria mabaya tu. Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.” Yehoshafati akajibu, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
8 Hat torei teh, Isarel siangpahrang ni kahrawikung buet touh a kaw teh, karanglah Imlah capa Mikah hrawi haw, atipouh.
Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwita mmoja wa maafisa wake na kusema, “Mlete Mikaya mwana wa Imla mara moja.”
9 Isarel siangpahrang hoi Judah siangpahrang teh Samaria longkha hmalah, siangpahrang e khohna a khohna roi teh, bawitungkhung dawk rei a tahung roi. Hahoi profetnaw pueng ni profet lawk a dei pouh awh.
Wakiwa wamevalia majoho yao ya kifalme, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi juu ya viti vyao vya kifalme katika sakafu ya kupuria, kwenye ingilio la lango la Samaria, pamoja na manabii wote wakiwa wakitabiri mbele yao.
10 Kenan capa Zedekiah ni sumki a sak teh, BAWIPA ni hettelah a dei, hete kinaw ni Sirianaw koung raphoe ditouh na deng han, telah atipouh.
Wakati huu Sedekia mwana wa Kenaana alikuwa ametengeneza pembe za chuma, akatangaza, “Hivi ndivyo Bwana asemavyo, ‘Kwa hizi pembe utawapiga na kuwarudisha Waaramu nyuma mpaka wameangamizwa.’”
11 Hottelah profet alouknaw nihai, Gilead ram Ramoth kho dawk takhang nateh tuk leih, BAWIPA ni siangpahrang kut dawk a hnawng han doeh, telah ati awh.
Manabii wengine wote walikuwa wanatabiri kitu hicho hicho, wakisema, “Ishambulie Ramoth-Gileadi na uwe mshindi. Kwa kuwa Bwana ataitia mkononi mwa mfalme.”
12 Mikah kaw hanelah patoune ni, khenhaw! profetnaw ni lawk rip kânging lah siangpahrang koe lawk kahawi a dei awh. Hatdawkvah nang ni hai lawk kahawi dei pouh, telah atipouh.
Mjumbe aliyekuwa amekwenda kumwita Mikaya akamwambia, “Tazama, manabii wote kama mtu mmoja wanatabiri ushindi kwa mfalme. Neno lako na likubaliane na lao, nawe unene mema kuhusu mfalme.”
13 Mikah ni, BAWIPA a hring e patetlah ka Cathut ni a dei e patetlah ka dei han atipouh.
Lakini Mikaya akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, nitamwambia kile tu Bwana atakachoniambia.”
14 Siangpahrang koe a pha toteh, siangpahrang ni ahni koe, Mikah Gilead ram Ramoth kho tuk hanelah ka cei han maw, ka cet mahoeh maw, telah a pacei. Ahni ni tuk awh na ta awh yawkaw han doeh, na kut dawk a hnawng han doeh, telah atipouh.
Alipofika, mfalme akamuuliza, “Mikaya, je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi au niache?” Akamjibu, “Shambulia na ushinde, kwa kuwa watatiwa mkononi mwako.”
15 Siangpahrang ni ahni koe, lawkkatang hoeh laipalah teh kai koe BAWIPA min lahoi dei hoeh hanelah vai nâyittouh maw lawk na kam sak han, telah atipouh.
Mfalme akamwambia, “Je, ni mara ngapi nitakuapisha ili usiniambie kitu chochote ila kweli tu kwa jina la Bwana?”
16 Ahni ni, khoumkung ka tawn hoeh e tu patetlah Isarelnaw pueng teh mon dawk pareng kâkapek e ka hmu. Hahoi BAWIPA ni hetnaw teh kahrawikung tawn awh hoeh dawkvah, ma im lengkaleng ban awh lawiseh, ati telah atipouh.
Ndipo Mikaya akajibu, “Niliona Israeli wote wametawanyika vilimani kama kondoo wasio na mchungaji, naye Bwana akasema, ‘Watu hawa hawana bwana. Mwache kila mmoja aende nyumbani kwa amani.’”
17 Isarel siangpahrang ni Jehoshaphat koevah, kaie kong a thoenae hoeh laipalah teh ahawinae dei boi mahoeh telah ka ti toung nahoehmaw, telah atipouh.
Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu bali mabaya tu?”
18 Mikah ni, hatdawkvah BAWIPA e lawk thai awh haw, Bawipa teh a bawitungkhung dawk a tahung teh, kalvantaminaw pueng avoilah aranglah a tahung e ka hmu.
Mikaya akaendelea, “Kwa hiyo lisikie neno la Bwana: Nilimwona Bwana ameketi juu ya kiti chake cha enzi pamoja na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama upande wa kulia na wa kushoto.
19 BAWIPA ni Isarel siangpahrang Ahab teh Gilead ram Ramoth khovah a cei vaiteh, due hanelah apinimaw a tacuek han telah ati. Hahoi buet touh ni hettelah doeh, alouke ni hottelah doeh atipouh.
Naye Bwana akasema, ‘Ni nani atakayemshawishi Ahabu, mfalme wa Israeli, ili aishambulie Ramoth-Gileadi na kukiendea kifo chake huko?’ “Mmoja akapendekeza hili na mwingine lile.
20 Hahoi muitha buet touh a tho teh, BAWIPA hmalah a kangdue teh, kai ni ka dum han telah ati navah, BAWIPA ni ahni koevah, nâ lah maw atipouh.
Mwishoni, roho akajitokeza, akasimama mbele za Bwana na kusema, ‘Nitamshawishi.’ “Bwana akauliza, ‘Kwa njia gani?’
21 Ahni ni ka cei vaiteh a profetnaw pueng e pahni dawk laithoe ka dei e muitha lah ka coung han, atipouh. Ahni ni dum haw, na dum thai han doeh. Hatdawkvah, cet nateh hottelah sak loe atipouh.
“Akasema, ‘Nitakwenda na kuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.’ “Bwana akasema, ‘Utafanikiwa katika kumshawishi. Nenda ukafanye hivyo.’
22 Hatdawkvah, khenhaw! BAWIPA ni hete profetnaw e a pahni dawkvah laithoe muitha a hruek toe. Hahoi BAWIPA ni nang na rawk nahane yo a dei toe telah atipouh.
“Kwa hiyo sasa Bwana ameweka roho ya kudanganya ndani ya vinywa vya hawa manabii wako wote. Bwana ameamuru maafa kwa ajili yako.”
23 Kenan capa Zedekiah ni rek a hnai teh Mikah e hmaibei dawk a tambei teh, nang koe lawk dei hanelah BAWIPA e Muitha teh nâ lahoi maw kai koehoi a tâco, telah atipouh.
Kisha Sedekia mwana wa Kenaana akatoka na kumpiga Mikaya kofi usoni. Akauliza, “Huyo Roho kutoka kwa Bwana alipita njia gani alipotoka kwangu ili kusema nawe?”
24 Mikah ni, khenhaw! kâhro hanelah imthungkhu na kâen hnin vah na panue han atipouh.
Mikaya akajibu, “Utagundua siku hiyo utakapokwenda kujificha kwenye chumba cha ndani.”
25 Isarel siangpahrang ni, Mikah heh khobawi Ammon hoi siangpahrang capa Joash koevah cetkhai awh.
Kisha mfalme wa Israeli akaagiza, “Mchukueni na mkamrudishe kwa Amoni mtawala wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.
26 Hahoi siangpahrang ni hettelah a dei, hete tami heh thongim pabawt awh. Roumnae hoi ka ban hoehroukrak reknae bu hoi tui poe awh, telah atipouh.
Mkaseme, ‘Hivi ndivyo asemavyo mfalme: Mwekeni mtu huyu gerezani na asipewe chochote ila mkate na maji mpaka nitakaporudi salama.’”
27 Mikah ni roumnae hoi bout na ban pawiteh, BAWIPA ni kai dawk hoi lawk a dei hoeh e han doeh, atipouh. Hahoi ahni ni nangmouh pueng ni hai thai awh, atipouh.
Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, basi Bwana hajanena kupitia kwangu.” Kisha akaongeza kusema, “Zingatieni maneno yangu, enyi watu wote!”
28 Hatdawkvah, Isarel siangpahrang hoi Judah siangpahrang Jehoshaphat teh Gilead ram. Ramoth khovah a takhang roi.
Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakaenda Ramoth-Gileadi.
29 Isarel siangpahrang ni Jehoshaphat koevah, nang teh tarankâtuknae koe vah, siangpahrang puengcang kâmahrawk loe, kai tet tami rumram e patetlah ka khohna han atipouh. Hottelah Isarel siangpahrang teh tami rumram patetlah hoi tarankâtuknae koe a cei.
Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Nitaingia vitani nikiwa nimejibadilisha, lakini wewe uvae majoho yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadilisha na kwenda vitani.
30 Siria siangpahrang ni rangleng kauknaw koe, Isarel siangpahrang hoeh laipalah teh, tamikathoung kalen apihai tuk awh hanh telah kâ a poe.
Wakati huu, mfalme wa Aramu alikuwa amewaagiza majemadari thelathini na wawili wa magari ya vita, “Msipigane na yeyote, mdogo au mkubwa, isipokuwa mfalme wa Israeli.”
31 Hahoi rangleng kaukkungnaw ni Jehoshaphat a hmu navah, Isarel siangpahrang nahoehmaw ati awh. Ahni tuk hanelah a kalup awh navah Jehoshaphat teh thouk a hram. BAWIPA ni a kabawp teh Cathut ni koung a ban sak.
Wakati wale majemadari wa magari ya vita walipomwona Yehoshafati, wakafikiri, “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo wakageuka ili wamshambulie, lakini Yehoshafati akapiga kelele, naye Bwana akamsaidia. Mungu akawaondoa kwake,
32 Rangleng kaukkungnaw ni Isarel siangpahrang nahoeh tie a panue toteh, pâlei laipalah a ban takhai awh.
wale majemadari wakaona kwamba hakuwa mfalme wa Israeli nao wakaacha kumfuatilia.
33 Hahoi, tami buet touh ni noe laipalah pala hoi a ka teh, Isarel siangpahrang e saiphei rahak a ka dawkvah, rangleng ka mawng koevah, kai na tâcawtkhai leih, hmâ ka ca e a patawpoung telah ati.
Lakini mtu fulani akavuta upinde pasipo lengo na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya kiungio cha mavazi yake ya chuma, mfalme akamwambia mwendesha gari lake, “Geuza gari na uniondoe mimi katika mapigano, nimejeruhiwa.”
34 Hat hnin vah, puenghoi a kâtuk awh. Hahoi Isarel siangpahrang teh tangmin lah totouh rangleng dawk a tahung laihoi, Sirianaw koelah kangvawi lahoi tami dawk a kamngawi teh kanî khup tawmlei vah a due.
Vita vikaendelea mchana kutwa, naye mfalme wa Israeli akajitegemeza ndani ya gari lake kuwaelekea Waaramu hadi jioni. Basi jioni yake akafa.

< 2 Setouknae 18 >