< 2 Setouknae 12 >

1 Rehoboam uknaeram a cak teh ama roeroe a tha a sai torei teh, ahni koe kambawng e Isarelnaw abuemlahoi BAWIPA e kâlawk a pahnawt awh.
Baada ya nafasi ya Rehoboamu kuimarika na kuwa na nguvu, yeye na Israeli yote waliiacha sheria ya Bwana Mungu.
2 Rehoboam siangpahrang a tawknae kum 5 navah, Izip siangpahrang Shishak ni Jerusalem tuk hanelah a luen takhang. Bangkongtetpawiteh, BAWIPA a taran awh teh, kâ a tapoe awh.
Kwa sababu hawakuwa waaminifu kwa Bwana, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu.
3 Izip lahoi kathonaw teh, rangleng 12,000, marangransanaw 6,000, hahoi touklek thai hoeh e taminaw, Lubimnaw, Sukkiimnaw hoi Ethiopia taminaw doeh.
Akiwa na magari ya vita 1,200 na wapanda farasi 60,000 na idadi isiyohesabika ya majeshi ya Walibia, Wasukii na Wakushi yaliyokuja pamoja naye kutoka Misri.
4 Judah ram dawk e rapan ka tawn e khonaw a la awh teh, Jerusalem kho dawk a pha awh.
Akateka miji ya Yuda yenye ngome akaendelea mpaka Yerusalemu.
5 Rehoboam hoi Judah kahrawikungnaw, Shishak taki kecu dawk Jerusalem kamkhuengnaw koe profet Shemaiah a tho teh, ahnimouh koevah, BAWIPA ni telah a dei, kai na pahnawt awh dawkvah kai ni Shishak kut dawk na hnawng van awh, telah atipouh.
Ndipo nabii Shemaya akaja kwa Rehoboamu na kwa viongozi wa Yuda waliokuwa wamekusanyika huko Yerusalemu kwa ajili ya hofu ya Shishaki naye akawaambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, ‘Ninyi mmeniacha mimi, kwa hiyo, mimi nami sasa ninawaacha ninyi mkononi mwa Shishaki.’”
6 Hat torei teh, Isarel kahrawikungnaw hoi siangpahrang rahim lah a kârahnoum awh teh, BAWIPA teh a lan, telah ati awh.
Viongozi wa Israeli na mfalme wakajinyenyekeza na kusema, “Bwana Mungu ni mwenye haki.”
7 BAWIPA ni a kârahnoum awh e a hmu torei teh, BAWIPA e lawk Shemaiah koe bout ka tho e teh, a kârahnoum awh dawkvah, ka raphoe mahoeh. Hatei, a tangawn teh ka rungngang vaiteh, Shishak kut dawk e ka lungkhueknae teh Jerusalem lathueng ka rabawk mahoeh.
Bwana Mungu alipoona kwamba wamejinyenyekeza, neno hili la Bwana likamjia Shemaya: “Maadamu wamejinyenyekeza, sitawaangamiza bali hivi karibuni nitawapatia wokovu. Ghadhabu yangu haitamwagwa juu ya Yerusalemu kwa kupitia Shishaki.
8 Hatei, ka thawtawknae hoi miphun alouke uknaeram koe thawtawknae a panue vaiteh, kapek thai nahanelah ahnimouh koe san a toung awh han.
Hata hivyo, watamtumikia Shishaki ili wapate kujifunza tofauti kati ya kunitumikia mimi na kuwatumikia wafalme wa nchi nyingine.”
9 Izip siangpahrang Shishak ni Jerusalem tuk hanelah a takhang teh, BAWIPA e im dawk e hnopai, siangpahrang e im dawk e hnopai hoi alouke hnopainaw pueng hai koung a la. Solomon ni a sak e suibahlingnaw hai koung a la.
Shishaki mfalme wa Misri alipoishambulia Yerusalemu, alichukua hazina za Hekalu la Bwana na hazina za jumba la kifalme. Akachukua kila kitu, pamoja na zile ngao za dhahabu ambazo Solomoni alikuwa amezitengeneza.
10 Siangpahrang Rehoboam ni a yueng lah rahum bahling lah a sak teh siangpahrang im takhang karingkungnaw hoi ransanaw koe a ring sak awh.
Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba badala ya zile za dhahabu na kuzikabidhi kwa majemadari wa ulinzi wa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme.
11 Siangpahrang teh BAWIPA e im dawk a kâen tangkuem karingkungnaw ni a sin awh teh, hathnukkhu ama onae koe bout a hruek awh.
Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu la Bwana walinzi walikwenda pamoja naye wakiwa wamebeba hizo ngao na baadaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.
12 Hottelah a kârahnoum torei teh, koung raphoe hoeh hanelah BAWIPA ni a lungkhueknae bout a roum sak teh, Judah ram teh kanawmcalah kho bout a sak awh.
Kwa sababu Rehoboamu alijinyenyekeza, hasira ya Bwana ikageukia mbali naye, hakuangamizwa kabisa. Kukawa na hali nzuri katika Yuda.
13 Hahoi siangpahrang Rehoboam teh Jerusalem lah a cei teh bout a uk. Rehoboam siangpahrang a tawknae teh kum 41 touh a pha teh, BAWIPA ni a min o thai nahanelah Isarel ram thung dawk a rawi e Jerusalem kho dawk kum 17 touh a uk. A manu e min teh Ammon tami Naamah doeh.
Mfalme Rehoboamu akajiweka imara katika Yerusalemu na akaendelea kuwa mfalme. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na saba, mji ambao Bwana alikuwa ameuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli ili aliweke Jina lake humo. Mama yake aliitwa Naama, alikuwa Mwamoni.
14 BAWIPA tawngngainae lungthin a tawn hoeh dawkvah, kathout hno a sak.
Rehoboamu akatenda maovu kwa sababu hakuuelekeza moyo wake katika kumtafuta Bwana Mungu.
15 Rehoboam thawtawknae a kamtawng hoi apout totouh e teh profet Shemaiah e cauk hoi profet Iddo ni thut e setouknae cauk dawk thut lah awm hoeh na maw. Rehoboam hoi Jeroboam teh a hring nathung pou a kâtuk roi.
Kwa habari ya matukio katika utawala wa Rehoboamu, tangu mwanzo mpaka mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Shemaya na mwonaji Ido zinazohusiana na vizazi? Kulikuwako na vita mara kwa mara kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
16 Hahoi, Rehoboam teh mintoenaw koe a i teh Devit khopui dawk a pakawp awh. Ahnie yueng lah a capa Abijah ni siangpahrang let a tawk.
Rehoboamu akalala na baba zake, akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Abiya mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Setouknae 12 >