< 1 Samuel 12 >
1 Samuel ni Isarelnaw pueng koe, khenhaw! kai koe na dei awh e pueng hah ka tarawi teh nangmouh siangpahrang na poe awh.
Samweli akawaambia Israeli wote, “Nimesikiliza kila kitu mlichoniambia nami nimewawekea mfalme juu yenu.
2 Atu khenhaw! siangpahrang ni na hrawi awh toe. Kai hateh kamatong toe. Ka sam hai a po toe. Khenhaw! ka capanaw teh nangmouh koe ao awh teh, a nawca hoi sahnin totouh na hrawi awh toe.
Sasa mnaye mfalme kama kiongozi wenu. Lakini kwa habari yangu mimi ni mzee na nina mvi, nao wanangu wapo hapa pamoja nanyi. Nimekuwa kiongozi wenu tangu ujana wangu mpaka siku hii ya leo.
3 Hivah ka o, BAWIPA hmalah hoi satui a awi e hmalah ka o. Dei awh haw. Apie maito maw ouk ka lawp. Apie la maw ouk ka lawp. Apimaw ouk ka hmuhma. Apimaw ouk ka pacekpahlek. Ka mit dawn sak hanlah api kut dawk e tadawngnae maw ouk ka ca. Koung na patho awh han telah atipouh.
Mimi ninasimama hapa. Shuhudieni juu yangu mbele za Bwana na mpakwa mafuta wake. Nimechukua maksai wa nani? Nimechukua punda wa nani? Ni nani nimepata kumdanganya? Ni nani nimepata kumwonea? Ni kutoka kwenye mkono wa nani nimepokea rushwa ili kunifanya nifumbe macho yangu? Kama nimefanya chochote katika hivi, mimi nitawarudishia.”
4 Ahnimouh ni na dum boi awh hoeh. Na pacekpahlek boi awh hoeh. Apie kut dawk e hno hai na lat boihoeh atipouh awh.
Wakajibu, “Hujatudanganya wala kutuonea. Hujapokea chochote kutoka kwenye mkono wa mtu awaye yote.”
5 Samuel ni hai kaie kut dawk buetbuet touh hai nangmouh ni na hmu awh hoeh e hah BAWIPA teh nangmouh koe lah kapanuekkhaikung lah ao. Satui awi lah kaawm e hai kapanuekkhaikung lah ao telah ati. Ahnimouh ni hai ahni teh kapanuekkhaikung lah ao telah ati awh.
Samweli akawaambia, “Bwana ni shahidi juu yenu, pia mpakwa mafuta wake ni shahidi siku hii ya leo, kwamba hamkukuta chochote mkononi mwangu.” Wakasema, “Yeye ni shahidi.”
6 Samuel ni taminaw koe, Mosi hoi Aron thaw ka poe niteh, Izip ram hoi na mintoenaw ka tâcawtkhai e hai BAWIPA doeh.
Kisha Samweli akawaambia watu, “Bwana ndiye alimchagua Mose na Aroni, na kuwaleta baba zenu akiwapandisha kutoka Misri.
7 Hatdawkvah, na mintoenaw koe hno kalan a saknae hah BAWIPA e hmalah pouk pouh thai nahanlah, atu sairasuepcalah kangdout awh.
Sasa basi, simameni hapa, kwa sababu nitakabiliana nanyi kwa ushahidi mbele za Bwana wa matendo yote ya haki yaliyofanywa na Bwana kwenu na kwa baba zenu.
8 Jakop ni Izip ram a pha hnukkhu nangmae mintoenaw ni BAWIPA koe a hram awh navah, Mosi hoi Aron hah Cathut ni a patoun teh, ahnimouh ni nangmae mintoenaw hah Izip ram hoi a tâcokhai hnukkhu, ahnimanaw teh hete ram dawk ao sak awh.
“Baada ya Yakobo kuingia Misri, walimlilia Bwana kwa ajili ya msaada, naye Bwana akawatuma Mose na Aroni, ambao waliwatoa baba zenu kutoka Misri na kuwakalisha mahali hapa.
9 BAWIPA Cathut hah a pahnim awh navah Hazar ransabawi Sisera kut dawk thoseh, Filistinnaw e kut dawk thoseh, Moab siangpahrang kut dawk thoseh, a yo teh ahnimanaw ni, ahnimanaw ni ahnimouh a tuk awh.
“Lakini wakamsahau Bwana Mungu wao, hivyo Mungu akawauza katika mkono wa Sisera, jemadari wa jeshi la Hazori na katika mikono ya Wafilisti na mfalme wa Moabu, ambaye alipigana dhidi yao.
10 BAWIPA koevah a hram awh teh, BAWIPA a pahnawt awh. Baal hoi Ashtaroth e thaw tawk awh kecu dawkvah, yon awh toe. Hatei sahnin tarannaw e kut dawk hoi na rungngang nateh na thaw ka tawk awh han telah a ti.
Wakamlilia Bwana na kusema, ‘Tumetenda dhambi; tumemwacha Bwana na kutumikia Mabaali na Maashtorethi. Lakini sasa tuokoe kutoka mikono ya adui zetu, nasi tutakutumikia.’
11 BAWIPA ni Jerubbaal, Bendan, Jephthah, hoi Samuel tinaw a patoun teh, nangmanaw na tengpam e taran kut dawk hoi na rungngang awh teh, nangmanaw runae awm laipalah lungmawng lah na o awh.
Ndipo Bwana akawatuma Yerub-Baali, Baraka, Yefta na Samweli, naye akawaokoa kutoka mikononi mwa adui zenu kila upande, ili ninyi mpate kukaa salama.
12 Ammon miphunnaw e siangpahrang Nahash ni nangmouh na tuk awh hane hah, nangmouh ni na hmu awh navah nangmae Cathut teh nangmae siangpahrang nahlangva, telah nahoeh. Siangpahrang ni ma kaimouh na uk seh telah na ti awh.
“Lakini mlipomwona yule Nahashi mfalme wa Waamoni anakuja dhidi yenu, mliniambia, ‘Hapana, tunataka mfalme atutawale,’ hata ingawa Bwana Mungu wenu alikuwa mfalme wenu.
13 Atu na hei e nangmouh ni na rawi e siangpahrang khenhaw! khenhaw! BAWIPA ni nangmae lathueng siangpahrang a rawi toe.
Sasa huyu hapa ndiye mfalme mliyemchagua, yule mliyeomba; tazameni, Bwana amemweka mfalme juu yenu.
14 Nangmouh ni BAWIPA na taki awh teh, BAWIPA e thaw na tawk awh pawiteh, BAWIPA e lawk na tarawi na ngâi awh pawiteh, nangmouh hoi nangmouh koe lawkcengkung siangpahrang hoi BAWIPA Cathut e hnuk na dawn awh pawiteh ahawi.
Kama mkimcha Bwana na kumtumikia na kumtii nanyi msipoasi dhidi ya amri zake, ninyi pamoja na mfalme anayetawala juu yenu mkimfuata Bwana, Mungu wenu, mambo yatakuwa mema kwenu!
15 Hatei Cathut e lawk na tarawi awh hoeh lah kâlawk na tapoe awh pawiteh, BAWIPA e a kut teh na mintoenaw e lathueng, runae a pha sak e patetlah nangmouh koehai a pha han.
Lakini kama hamkumtii Bwana, nanyi kama mkiasi dhidi ya amri zake, mkono wake utakuwa dhidi yenu, kama ulivyokuwa dhidi ya baba zenu.
16 BAWIPA ni nangmae na mithmu hno ka lentoe poung a sak hane hah, duem awm awh nateh khenhaw.
“Sasa basi, simameni kimya mkaone jambo hili kubwa ambalo Bwana anakwenda kulifanya mbele ya macho yenu!
17 Sahnin catun anae tueng nahoehmaw. Kho rak sak hane hoi khoparit sak hanelah, kai ni Cathut ka kaw han. Hatnavah, siangpahrang na heinae kong dawk, BAWIPA mithmu vah yonnae kalenpoung na sak awh e na kâpanue awh vaiteh na hmu awh han telah a ti.
Je, sasa si mavuno ya ngano? Nitamwomba Bwana ili alete ngurumo na mvua. Nanyi mtatambua jambo hili lilivyo baya mlilolifanya mbele za macho ya Bwana mlipoomba mfalme.”
18 Samuel ni BAWIPA a kaw teh, BAWIPA ni hote hnin dawk, kho a parit sak teh, kho a rak sak. Hat torei teh taminaw ni BAWIPA hoi Samuel hah a taki poung awh.
Kisha Samweli akamwomba Bwana, na siku ile ile Bwana akatuma ngurumo na mvua. Hivyo watu wote wakamwogopa sana Bwana na Samweli.
19 Tamihunaw ni Samuel koevah, due awh hoeh nahan, BAWIPA na Cathut koe sannaw hanelah na ratoum pouh haw. Hettelah e Siangpahrang ka hei awh e heh, ka payonae kâthap sin e lah ao telah ati awh.
Watu wote wakamwambia Samweli, “Mwombe Bwana Mungu wako kwa ajili ya watumishi wako, ili tusije tukafa, kwa kuwa tumeongeza uovu juu ya dhambi zetu nyingine kwa kuomba mfalme.”
20 Samuel ni taminaw koevah, taket awh hanh. Kahawi hoeh e heh na sak awh katang doeh. Hatei BAWIPA e hnuk na kabang awh e phen laipalah, BAWIPA e thaw na lungthin katang hoi tawk awh.
Samweli akajibu, “Msiogope, mmefanya uovu huu wote; hata hivyo msimwache Bwana, bali mtumikieni Bwana kwa moyo wenu wote.
21 Banglahai ka cungkeihoehe hnukkâbang e lahoi phen awh hanh. Hawinae na poe mahoeh na rungngang thai mahoeh. Hotnaw teh a yawmyin doeh.
Msigeukie sanamu zisizofaa. Haziwezi kuwatendea jema, wala haziwezi kuwaokoa kwa sababu hazina maana.
22 Bangkongtetpawiteh, ka lentoe e min kecu dawk BAWIPA ni a taminaw cettakhai mahoeh. Bangkongtetpawiteh, a tami lah coung sak e hah BAWIPA a lunghawinae doeh.
Kwa ajili ya jina lake kuu Bwana hatawakataa watu wake, kwa sababu ilimpendeza Bwana kuwafanya kuwa wake mwenyewe.
23 Kai hateh, nangmouh han ratoumnae kâhatnae lahoi BAWIPA koe ka yonnae hoi kâhlat naseh. Kai ni nangmouh hah kahawi ni teh ka lamkahawi hoi lamkatang na pâtue awh han.
Kwa habari yangu, iwe mbali nami kutenda dhambi dhidi ya Bwana kwa kushindwa kuwaombea. Mimi nitawafundisha njia iliyo njema na ya kunyooka.
24 Nangmouh ni BAWIPA dueng mah taket awh haw, lungthin abuemlahoi yuemkamcu lah amae thaw tawk awh haw. Bangkongtetpawiteh, nangmouh hanelah, a sak e hno kalenpoung hah pouk awh haw.
Lakini hakikisheni mnamcha Bwana na kumtumikia kwa uaminifu kwa moyo wenu wote; tafakarini mambo makubwa aliyoyatenda kwa ajili yenu.
25 Nangmouh ni thoenae na sak awh rah pawiteh, nangmouh hoi nangmae siangpahrang khuehoi koung pâmit lah na o awh han telah atipouh.
Hata hivyo mkiendelea kufanya uovu, ninyi na mfalme wenu mtafutiliwa mbali!”