< 1 Siangpahrang 21 >
1 Hathnukkhu vah, hettelah ao. Jezreel tami Naboth ni misur takha a tawn. Hot teh, Jezreel e Samaria siangpahrang Ahab e im teng vah ao.
Baada ya hayo, Nabothi, Myezreeli, alikuwa na shamba la mizabibu jirani na jumba la kifalme la Ahabu mfalme wa Samaria.
2 Ahab ni Naboth koe na misur takha heh ka im teng ao dawkvah, saring khoum nahanlah na poe lawih. A yueng lah takha ka hawihnawn e na poe han. Nahoeh pawiteh, tangka lah na ngai pawiteh tangka lah na poe han telah atipouh.
Ahabu akamwambia Nabothi, “Nipe shamba lako la mizabibu nilitumie kwa bustani ya mboga, kwa kuwa liko karibu na jumba langu la kifalme. Badala yake, nitakupa shamba jingine la mizabibu zuri zaidi au, kama utapenda, nitakulipa kiasi chochote unachoona ni thamani yake.”
3 Hateiteh, Naboth ni Ahab koevah, ka mintoenaw e râw nang poe hane teh BAWIPA ni na ngang naseh telah ati.
Lakini Nabothi akamjibu, “Bwana na apishe mbali kukupa wewe urithi wa baba zangu.”
4 Jezreel tami Naboth ni ka mintoenaw e râw teh nang koe na poe mahoeh telah a dei dawkvah, Ahab teh minhmai mathoe hoi lungphuen laihoi a im dawk a kâen. A ikhun dawk a yan teh avangvanglah a kamlang teh rawca cat ngai hoeh.
Basi Ahabu akaenda nyumbani, mwenye huzuni na hasira kwa sababu ya yale ambayo Nabothi, Myezreeli, alikuwa amesema, “Sitakupa urithi wa baba zangu.” Akajinyoosha juu ya kitanda akisononeka, na akakataa kula.
5 Hateiteh, a yu Jezebel ni ahni koe a cei teh, bangkongmaw na muitha lungmathoe laihoi ao teh, rawca ca hanelah na ngai hoeh telah atipouh.
Yezebeli mke wake akaingia na akamuuliza, “Kwa nini unahuzunika hivi? Kwa nini huli chakula?”
6 Ahni ni Jezebel koevah, Jezreel tami Naboth koevah, na misur takha hah na ran sak, nahoeh pawiteh, na ngaihnawn e awm pawiteh misur takha alouke na poe han telah ka ti pouh. Ahni ni, ka misur takha na poe mahoeh telah na pathung dawkvah, telah atipouh.
Akamjibu, “Kwa sababu nilimwambia Nabothi, Myezreeli, ‘Niuzie shamba lako la mizabibu, au kama ukipenda, nitakupa shamba jingine la mizabibu badala yake.’ Lakini akasema, ‘Sitakupa shamba langu la mizabibu.’”
7 A yu Jezebel ni ahni koevah, nang ni Isarel uknaeram hah kâtawnnae na tawn hoeh na maw. Thaw nateh lunghawicalah rawca cat leih. Jezreel tami Naboth e misur teh kai ni na poe han telah ati.
Yezebeli mke wake akasema, “Hivi ndivyo unavyofanya, nawe ni mfalme katika Israeli yote? Inuka na ule! Changamka. Nitakupatia shamba la mizabibu la Nabothi, Myezreeli.”
8 Hatdawkvah, Ahab e min lahoi ca a thut teh, kuthrawt hoi a dei teh, ca hah Naboth a onae kho dawk ahni hoi rei kaawm e kacuenaw hoi bawinaw koe a patawn.
Kwa hiyo akaandika barua kwa jina la Ahabu akaweka muhuri wake juu ya hizo barua, akazipeleka kwa wazee na kwa watu wenye cheo walioishi katika mji pamoja na Nabothi.
9 Rawcahainae kong oung nateh, Naboth hah tami pueng e hmalah barinae hmuen koe tahung naseh.
Katika barua hizo aliandika: “Tangazeni siku ya watu kufunga na mkamketishe Nabothi mahali pa wazi miongoni mwa watu.
10 Tamikayon kahni touh ahmalah tahung sak vaiteh, Cathut hoi siangpahrang na pahnawt telah yon kapenkung lah sak awh, telah atipouh.
Lakini waketisheni watu wawili wabaya kabisa mkabala naye, nao washuhudie kuwa yeye amemlaani Mungu na mfalme. Kisha mtoeni nje na kumpiga kwa mawe hadi afe.”
11 A onae khocanaw, a onae kho dawk e kaawm e kacuenaw hoi bawinaw ni Jezebel ni a thut e ca patetlah a sak awh.
Hivyo wazee na watu wenye cheo walioishi katika mji wa Nabothi wakafanya kama Yezebeli alivyoelekeza katika barua aliyowaandikia.
12 Rawcahainae kong hah a pathang awh teh, tamipueng thung dawk hoi Naboth teh hmalah a tahung sak awh.
Wakatangaza mfungo na kumketisha Nabothi mahali pa wazi miongoni mwa watu.
13 Tamikayon kahni touh a hmalah a tahung teh, tamikayon roi ni tami pueng e hmalah, Naboth ni Cathut hoi siangpahrang a pahnawt telah Naboth hah yon a pen roi. Hottelah, kho thung hoi a sin awh e talung hoi kadout lah a dêi awh.
Kisha watu wawili wabaya kabisa wakaja wakaketi mkabala naye, nao wakaleta mashtaka dhidi ya Nabothi mbele ya watu, wakisema, “Nabothi amemlaani Mungu na mfalme.” Kwa hiyo wakamtoa nje na kumpiga kwa mawe hadi akafa.
14 Hatdawkvah, Naboth teh talung hoi kadout lah a dêi awh teh a due toe telah Jezebel koe kamthang a thaisak awh.
Kisha wakatuma ujumbe kwa Yezebeli, kusema, “Nabothi amepigwa mawe na amekufa.”
15 Jezebel ni Naboth teh talung hoi kadout lah a dêi awh toe tie a panue toteh, Ahab koevah, hettelah atipouh. Thaw nateh, Jezreel tami Naboth e misur takha, tangka lah yo hane a pasoung hoeh e hah lat leih. Bangkongtetpawiteh, Naboth teh hring hoeh toe, a due toe telah atipouh.
Mara tu Yezebeli aliposikia kwamba Nabothi amepigwa mawe na amekufa, akamwambia Ahabu, “Amka na uchukue lile shamba la mizabibu la Nabothi, Myezreeli, ambalo alikataa kukuuzia. Hayuko hai tena, bali amekufa.”
16 Ahab ni Naboth a due toe tie a thai navah, Jezreel tami Naboth e misur takha dawk cei vaiteh, la hanelah Ahab teh a kamthaw.
Ahabu aliposikia Nabothi amekufa, akainuka na kushuka ili kulichukua shamba la mizabibu la Nabothi.
17 Hahoi, BAWIPA e lawk hah Tishbit tami Elijah koevah a pha.
Kisha neno la Bwana likamjia Eliya, Mtishbi:
18 Thaw nateh, Samaria kho kaawm e Isarel siangpahrang Ahab kâhmo hanelah cet. Ahni teh Naboth e misur takha la hanelah a cei teh haw vah ao.
“Shuka ukakutane na Ahabu mfalme wa Israeli, anayetawala Samaria. Sasa yuko katika shamba la mizabibu la Nabothi, ambapo amekwenda alimiliki.
19 Ahni koevah, BAWIPA ni hettelah a dei. Uinaw ni Naboth e thi a palemnae hmuen dawk nange thi hai uinaw ni a palem van han telah na ti pouh han telah ati.
Umwambie, ‘Hivi ndivyo Bwana asemavyo: Je, hujamuua mtu na kuitwaa mali yake?’ Kisha umwambie, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Mahali ambapo mbwa waliramba damu ya Nabothi, mbwa watairamba damu yako, naam, yako wewe!’”
20 Ahab ni Elijah koevah, kâhmo roi toe khe, ka taran telah atipouh. Ahni ni Oe kâhmo roi toe. Bangkongtetpawiteh, BAWIPA e hmaitung vah hawihoehnae sak hanlah namahoima na kâyo hah te telah atipouh.
Ahabu akamwambia Eliya, “Kwa hiyo umenipata, wewe adui yangu!” Akajibu, “Ndiyo, nimekupata. Kwa sababu umejiuza mwenyewe kufanya uovu mbele ya macho ya Bwana.
21 Khenhaw! nange lathueng vah, rawknae ka pha sak han. Koung na raphoe awh han. Ahab totouh hoi na ca catounnaw pueng, Isarel ram dawk tami ka hlout thoseh, ka hlout hoeh thoseh, koung ka pâmit han.
‘Nitaleta maafa juu yako. Nitaangamiza uzao wako na kukatilia mbali kutoka kwa Ahabu kila mzaliwa wa mwisho wa kiume katika Israeli, wa mtumwa au wa mtu huru.
22 Nang ni ka lungkhueknae na pahrue teh, Isarelnaw yonnae na sak sak dawkvah, Nebat capa Jeroboam imthungkhu hoi Ahijah capa Baasha imthungkhu patetlah na imthungkhunaw hai ka o sak han telah ati.
Nitaifanya nyumba yako kama ile ya Yeroboamu mwana wa Nebati na ile ya Baasha mwana wa Ahiya, kwa sababu umenighadhibisha kwa kuwa umesababisha Israeli kutenda dhambi.’
23 BAWIPA ni Jezebel e kong hai a dei toe. Jezreel kalupnae koe uinaw ni Jezebel heh a ca han.
“Pia kwa habari ya Yezebeli Bwana anasema, ‘Mbwa watamla Yezebeli karibu na ukuta wa Yezreeli.’
24 Ahab imthungkhu dawk hoi khopui dawk kadout e hah uinaw ni a ca vaiteh, kahrawng kadout e pueng teh kalvan e tava ni a ca han telah ati.
“Mbwa watawala wale wa nyumba ya Ahabu watakaofia mjini, nao wale watakaofia mashambani wataliwa na ndege wa angani.”
25 A yu Jezebel ni a tacuek teh BAWIPA e mithmu vah, hawihoehnae sak hanlah, ka kâyawt e Ahab patet e tami apihai awm hoeh.
(Hapajapata kamwe kuwa na mtu kama Ahabu, aliyejiuza mwenyewe kutenda uovu machoni mwa Bwana, akiwa anachochewa na Yezebeli mkewe.
26 BAWIPA ni Isarelnaw koehoi a pâlei e Amor taminaw e sak e patetlah. meikaphawk hah bawk hoi panuettho e hnonaw hah ouk a sak awh.
Alitenda kwa uovu sana katika kuabudu sanamu, kama wale Waamori ambao Bwana aliowafukuza mbele ya Israeli.)
27 Ahab ni hote lawk a thai toteh, a hni a phi teh, burihni hah a kâkhu, rawca a hai teh rawca burihni kâkhu hoi a i teh paiyaica hoi a kâroe.
Ahabu aliposikia maneno haya, akararua nguo zake, akavaa nguo za gunia na kufunga. Akalala na kujifunika nguo za gunia na kwenda kwa unyenyekevu.
28 Hahoi, BAWIPA e lawk teh Tishbit tami Elijah koevah a pha.
Ndipo neno la Bwana lilipomjia Eliya Mtishbi kusema,
29 Ka hmalah Ahab a kârahnoumnae hah na hmu maw. Ka hmalah a kârahnoum dawkvah, ahnie se nateh hawihoehnae ka phat sak mahoeh. A capa se nah a imthungkhu dawk hawihoehnae ka pha sak han telah ati.
“Umeona jinsi Ahabu alivyojinyenyekeza mbele zangu? Kwa kuwa amejishusha mwenyewe, sitaleta maafa haya wakati akiwa hai, lakini nitayaleta juu ya nyumba yake katika siku za mwanawe.”