< 1 Setouknae 26 >

1 Longkha karingkungnaw thaw kâreinae teh, Korah koehoi Asaph casaknaw Kore capa Meshelemiah.
Hii ndiyo migawanyo ya mabawabu: Kutoka kwa wana wa Kora alikuwa: Meshelemia mwana wa Kore, mmoja wa wana wa Asafu.
2 Meshelemiah casak koehoi Zekhariah teh a ca camin, apâhni e teh Jediael, apâthum e teh Zebadiah, apali e teh Jathniel,
Meshelemia alikuwa na wana wafuatao: Zekaria mzaliwa wa kwanza, Yediaeli wa pili, Zebadia wa tatu, Yathnieli wa nne,
3 apanga e teh Elam, ataruk e teh Jehohanan, asari e teh Elioenai,
Elamu wa tano Yehohanani wa sita na Eliehoenai wa saba.
4 Obededom casaknaw teh a camin Shemaiah, apâhni e teh Jehozabad, apâthum e teh Joah, apali e teh Sakar, apanga e teh Nethanel,
Obed-Edomu naye alikuwa na wana wafuatao: Shemaya mzaliwa wa kwanza, Yehozabadi wa pili, Yoa wa tatu, Sakari wa nne, Nethaneli wa tano,
5 ataruk e teh Ammiel, asari e teh Issakhar, ataroe e teh Peulthai, ahni teh Cathut ni yawhawi a poe.
Amieli wa sita, Isakari wa saba, na Peulethai wa nane. (Kwa kuwa Mungu alikuwa amembariki Obed-Edomu.)
6 Shemaiah casaknaw thung hoi hai imthung kahrawinaw ao van. Bangkongtetpawiteh, tarankahawi ni teh athakaawme taminaw lah ao awh.
Shemaya mwanawe pia alikuwa na wana, waliokuwa viongozi katika jamaa ya baba yao kwa sababu walikuwa watu wenye uwezo mkubwa.
7 Shemaiah capanaw teh Othni, Rephael, Obed, a hmaunawngha Elzabad, hno katetthai capa Elihu hoi Semakiah.
Wana wa Shemaya ni: Othni, Refaeli, Obedi na Elizabadi; jamaa zake Elihu na Semakia walikuwa pia watu wenye uwezo.
8 Hetnaw teh Obededom casaknaw doeh. A capanaw hoi a hmaunawnghanaw teh thaw ka tawk thai poung e lah ao. Obed-edomnaw teh 62 touh a pha awh.
Hawa wote walikuwa wazao wa Obed-Edomu; wao na wana wao na jamaa zao walikuwa watu wenye uwezo pamoja na nguvu za kufanya kazi. Wazao wa Obed-Edomu jumla yao walikuwa sitini na wawili.
9 Meshelemiah casaknaw hoi a hmaunawngha a thakaawm capa 18 touh ao awh.
Meshelemia alikuwa na wana na jamaa zake, waliokuwa watu wenye uwezo: jumla yao watu kumi na wanane.
10 Merari casak koehoi Hosah ni hai capanaw a tawn. Shimri te camin la ao hoeh nakunghai a na pa ni kacuepoung lah a ta.
Hosa, Mmerari, alikuwa na wana wafuatao: Shimri alikuwa mkuu wao (baba yake alikuwa amemweka yeye kuwa mkuu ijapokuwa hakuwa mzaliwa wa kwanza),
11 Apâhni e teh Hilkiah, apâthum e teh Tabaliah, apali e teh Zekhariah. Hosah casak hoi a hmaunawnghanaw abuemlah 13 touh a pha.
Hilkia wa pili, Tabalia wa tatu na Zekaria wa nne. Wana na jamaa za Hosa jumla yao walikuwa watu kumi na watatu.
12 Hetnaw teh a hmaunawnghanaw patetlah BAWIPA e im dawk thaw ka tawk e longkha ka ring hanelah ao awh.
Hii migawanyo ya mabawabu, kupitia wakuu wao, walikuwa na zamu za kuhudumu hekaluni mwa Bwana kama jamaa zao walivyokuwa nazo.
13 Kacue kanaw a imthungnaw lahoi longkha tangkuem ring hanelah cungpam a rayu awh.
Kura zilipigwa kwa kila lango, kufuatana na jamaa zao, wakubwa kwa wadogo.
14 Kanîtholae cungpam teh Shelemiah a bo. A lungkaang poung e lawkcengkung capa Zekhariah hanelah cungpam a rayu awh teh tung lae hah a coe.
Kura ya Lango la Mashariki ilimwangukia Shelemia. Kisha wakapiga kura kwa Zekaria mwanawe, aliyekuwa mshauri mwenye hekima, nayo kura ya Lango la Kaskazini ikamwangukia.
15 Akalae Obededom a coe dawk hnopai tanae im teh a capanaw ni coe e lah ao.
Kura ya Lango la Kusini ikamwangukia Obed-Edomu, nayo kura ya maghala ikawaangukia wanawe.
16 Shuppim hoi Hosah ni coe e teh kanîloumlae takhangnae Shalleketh longkha hoi thongim a voivang lae hah doeh.
Kura za Lango la Magharibi na Lango la Shalekethi kwenye barabara ya juu zikawaangukia Shupimu na Hosa. Zamu za walinzi ziligawanywa kwa usawa:
17 Kanîtholae Levihnaw 6 touh ao awh teh, hnin touh dawk atunglah 4, akalah 4, hahoi hnoim dawk 2, reirei ao.
Kulikuwa na Walawi sita kila siku upande wa mashariki, wanne upande wa kaskazini, wanne upande wa kusini, na wawili wawili kwa mara moja kwenye ghala.
18 Kanîloumlae hoi rapan thung kâen nahanelah 4 touh, kalupnae thung 2 touh.
Kuhusu ukumbi kuelekea magharibi, kulikuwa na wanne barabarani na wawili kwenye ukumbi wenyewe.
19 Hetnaw teh Korah e capanaw hoi Merari e capanaw, longkha ka ring hanelah a kapek e naw doeh.
Hii ndiyo iliyokuwa migawanyo ya mabawabu waliokuwa wazao wa Kora na wa Merari.
20 Levihnaw thung hoi Ahijah teh Cathut im dawk hnopai poe e karingkung lah ao.
Katika Walawi, Ahiya alikuwa mwangalizi wa hazina za nyumba ya Mungu na mwangalizi wa hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.
21 Ladan e catounnaw teh Ladan koehoi Gershonnaw lah kaawm e lah ao. Gershonnaw ni Ladan imthung dawk kahrawikung lah ao awh. Hotnaw teh
Wazao wa Ladani, waliokuwa Wagershoni kupitia Ladani na waliokuwa viongozi wa jamaa za Ladani Mgershoni, walikuwa Yehieli,
22 Jehieli casak koehoi Zetham hoi a nawngha Joel teh BAWIPA im dawk e hnopai karingkung lah ao.
wana wa Yehieli, wana wa Zethamu na wa nduguye Yoeli. Wao walikuwa waangalizi wa hazina za Hekalu la Bwana.
23 Amram koehoi hai, Izhar koehoi hai, Hebron koehoi hai, Uzziel koehoi hai ao awh.
Kutoka kwa wana wa Amramu, wana wa Ishari, wana wa Hebroni na wana wa Uzieli:
24 Mosi capa Gershom casak Shubael hai hnopai karingkungnaw dawk kacue lah ao.
Shebueli, mzao wa Gershomu mwana wa Mose, alikuwa afisa mwangalizi wa hazina.
25 Eliezer dawk hoi a hmaunawnghanaw teh Eliezer capa Rehabiah, a capa Isaiah, a capa Joram, a capa Zikhri, a capa Shelmoth.
Jamaa zake kutoka kwa Eliezeri, wanawe walikuwa: Rehabia, Yeshaya, Yoramu, Zikri na Shelomithi.
26 Shelomoth hoi a hmaunawnghanaw hai siangpahrang Devit hoi a imthung kahrawikung ransa 1000 kaukkung bawi, 100 touh kaukkung bawi lah ao awh. Ransabawinaw ni a poe e hnopai karingkung lah ao awh.
Shelomithi na jamaa zake walikuwa waangalizi wa hazina zote za vitu vile vilivyowekwa wakfu na Mfalme Daudi, kwa viongozi wa jamaa waliokuwa majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, na kwa maafisa wengine wa jeshi.
27 Taran a tuknae koe e lawphno a sin awh e teh, BAWIPA e im pathoup nahanelah a poe awh.
Baadhi ya nyara zilizotekwa vitani waliziweka wakfu kwa ajili ya ukarabati wa Hekalu la Bwana.
28 Kahmawtkung Samuel hoi Kish capa Sawl, Ner capa Abner, Zeruiah capa Joab tinaw ni a poe tangcoung e naw hoi poe hanelah kaawm e hnonaw teh Shelomoth hoi a hmaunawnghanaw e kut dawk a kuem awh.
Kila kitu kilichokuwa kimewekwa wakfu na Samweli mwonaji, na Sauli mwana wa Kishi, Abneri mwana wa Neri, na Yoabu mwana wa Seruya, pamoja na vitu vingine vyote vilivyokuwa vimewekwa wakfu, vyote vilikuwa chini ya uangalizi wa Shelomithi na jamaa zake.
29 Izharnaw dawk hoi Kenaniah hoi a capanaw teh Jerusalem rapan alawilae Isarelnaw dawk kahrawikungnaw hoi lawkcengkungnaw lah ao awh.
Kutoka kwa wana wa Ishari: Kenania na wanawe walipewa kazi nje ya Hekalu kama maafisa na waamuzi juu ya Israeli.
30 Hebronnaw dawk hoi Hashabiah hoi a hmaunawnghanaw teh hno katetthai e tami 17000 touh teh Jordan namran kanîloumlah BAWIPA e thawnaw hoi siangpahrang e thawnaw dawk Isarel ram karingkungnaw lah ao awh.
Kutoka kwa wana wa Hebroni: Hashabia na jamaa zake, watu 1,700 wenye uwezo, waliwajibika katika Israeli magharibi ya Yordani kwa ajili ya kazi zote za Bwana na utumishi wa mfalme.
31 Hebronnaw koehoi Jerijah teh Hebronnaw e a na pa a tâconae patetlah kahrawikung lah ao. Devit a bawinae kum 40 touh a pha navah, Gilead ram e Jazer vah ahnimouh thung dawk e athakaawme hoi tarankahawi e moikapap a hmu awh.
Kuhusu wana wa Hebroni, Yeria alikuwa mkuu wao kufuatana na orodha ya jamaa yao. Katika mwaka wa arobaini wa utawala wa Daudi uchunguzi ulifanyika katika kumbukumbu, nao watu wenye uwezo miongoni mwa wana wa Hebroni wakapatikana huko Yazeri katika Gileadi.
32 Cathut hane hoi siangpahrang e thaw dawkvah, Reuben, Gad, Manasseh casaknaw tangawn lathueng kahrawikungnaw hah Devit ni a ta. Imthungnaw ka hrawi hane dawk hoi hno katetthai e a hmaunawnghanaw teh 2, 700 touh a pha. awh.
Yeria alikuwa na jamaa ya watu 2,700 waliokuwa watu wenye uwezo na viongozi wa jamaa, naye Mfalme Daudi akawaweka kuangalia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila Manase kuhusu kila jambo lililomhusu Mungu na shughuli za mfalme.

< 1 Setouknae 26 >