< Matthew 27 >

1 Jingpi matah in thempu pipui holeh miho lah'a upa ho atoukhom kit un, Yeshua thana ding angaito tauve.
Asubuhi na mapema, viongozi wa makuhani wote na wazee wa watu wakafanya shauri pamoja dhidi ya Yesu ili kumuua.
2 Chujouvin amaho chun Ama akan un, apui mang un, chuin Rome gamvaipo Pilate henga apui tauve.
Wakamfunga, wakampeleka na kumkabidhi kwa Pilato, ambaye alikuwa mtawala wa Kirumi.
3 Ama pedoh'a pangpa Judas chun Yeshua chu thi chan geiya dinga themo achan'u chu ahen, alunga akisih lheh jeng tai. Hiti chun aman dangka somthum chu alan, thempu pipui holeh upa ho koma achoiyin,
Yuda, ambaye alikuwa amemsaliti Yesu, alipoona kuwa Yesu amehukumiwa, akajuta na akarudisha vile vipande thelathini vya fedha alivyopewa na viongozi wa makuhani na wazee wa watu.
4 aman aphongdoh in, “Ka chonse tai, ajeh chu keiman themmona neilou chu kapedoh tai” ati. Ama hon adonbut'un, “Keihon ija kageldeh uvem, hichu nangma boina hibouva chu,” atiuve.
Akasema, “Nimetenda dhambi, kwa maana nimeisaliti damu isiyo na hatia.” Wakamjibu, “Hilo latuhusu nini sisi? Ni shauri yako.”
5 Chujouvin Judas chun dangka sum nong chu Hou'in sunga aleh lhan chule apotdoh in ama le ama akikhai lihtai.
Basi Yuda akavitupa vile vipande vya fedha ndani ya Hekalu akaondoka akaenda kujinyonga.
6 Thempu pipui ho chun sum nong chu aloh khom un, aseiyun, “Hiche sum hi Hou'in a sumkoina a koikhom nom ponte, ajeh chu mithana dinga ki pedohsa ahi,” atiuve.
Wale viongozi wa makuhani wakazichukua zile fedha wakasema, “Si halali kuchanganya fedha hizi na sadaka kwa sababu hizi ni fedha zenye damu.”
7 Aki houtoh jouvun, ajonan amahon bel dengpa honlei chohna ding in agellha tauve. Chule hichu gam pam mi kivuina ding in asem tauve.
Kwa hiyo baada ya kushauriana, waliamua kuzitumia kununulia shamba la mfinyanzi, liwe mahali pa kuzikia wageni.
8 Hijeh'a chu leimun min chu Thisan Man kitia ahi.
Hii ndiyo sababu lile shamba likaitwa Shamba la Damu hadi leo.
9 Hiche hi Jeremiah themgao thusei aguilhun nan “Amahon dangka som thum nong chu alauvin, Israel miten aman dinga agel-uva aphasah nau man chu ahi.
Ndipo likatimia lile lililonenwa na nabii Yeremia, kwamba, “Walichukua vile vipande thelathini vya fedha, thamani aliyopangiwa na watu wa Israeli,
10 Chuin amahon bel dengpa honlei chu, Pakaiyin ahilna bangtah in acho tauve.”
wakanunulia shamba la mfinyanzi, kama vile Bwana alivyoniagiza.”
11 Chupet'a chu Rome gamvaipo Pilate ang-a Yeshua ding ahin, Gamvaipo chun “Nangma Judah te Lengpa nahim?” tin adonge. Yeshuan adonbut in, “Nasei khai” ati!
Wakati huo Yesu akiwa amesimama mbele ya mtawala, mtawala akamuuliza, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?” Yesu akasema, “Wewe wasema hivyo.”
12 Hinlah Thempu pipui holeh upa hon ama douna thu aseiyun, Yeshua athipbeh in ahi.
Lakini viongozi wa makuhani na wazee walipomshtaki, hakujibu neno.
13 “Amahon nangma douna thu hijatpi aseiyu hi na jahlou ham?” tin Pilate in adong in ahi.
Ndipo Pilato akamuuliza, “Je, husikii ni mambo mangapi wanayokushtaki nayo?”
14 Chuin Yeshuan athemmosah naho'uva imacha adonbutlou jeh chun Gamvaipo chun adatmo lheh e.
Lakini Yesu hakumjibu hata kwa shtaka moja, kiasi kwamba mtawala alishangaa sana.
15 Kalchuh Kut kumseh le kiman jina'a chu mi honpin adeiyu khat gamvaipo chun sohchang khat alhadoh jiu ahi.
Basi ilikuwa ni desturi ya mtawala kumfungua mfungwa mmoja aliyechaguliwa na umati wa watu wakati wa sikukuu.
16 Hiche kum'a hi sohchang giloutah khat Barabbas atiu ana um'ah ahi.
Wakati huo alikuwepo mfungwa mmoja mwenye sifa mbaya, aliyeitwa Baraba.
17 Mihonpi chu Pilate in'a akikhop pet un, hiche jingkah chun, aman amaho chu adong in, “Nangho dinga koijoh ham kalha dohpeh diu? Barabbas ham ahilouleh Yeshua kiti Messiah hi kalha dohpeh diu ham?” ati.
Hivyo umati wa watu walipokusanyika, Pilato akawauliza, “Mnataka niwafungulie nani, Baraba au Yesu yeye aitwaye Kristo?”
18 (Amahin houlamkai hon Yeshua chu thangthip man'a amat'u ahi, ti ahe chen lheh in ahi).
Kwa kuwa alitambua Yesu alikuwa amekabidhiwa kwake kwa ajili ya wivu.
19 Pilate thutanna'a atoupet tah in ajinu chun hiche thuhi athot in: “Hiche themmona beipa hi limsah hih in. Ama jeh hin tujan ka-ihmutna'a chun kathoh gimlheh jenge,” ati.
Pilato akiwa ameketi kwenye kiti cha hukumu, mkewe akampelekea ujumbe huu: “Usiwe na jambo lolote juu ya mtu huyu asiye na hatia, kwa kuwa leo nimeteseka sana katika ndoto kwa sababu yake.”
20 Hichepet chun thempu pipui holeh upa ho chun mi honpi chu atem un, Barabbas chu lhadoh'a auma chule Yeshua chu thisah ding in atil tauvin ahi.
Lakini viongozi wa makuhani na wazee wakaushawishi ule umati wa watu kwamba waombe Baraba afunguliwe, naye Yesu auawe.
21 Hiti chun Gamvaipopa chun adong kit in, “Koijoh hi lhadohpeh leuveng nalung uham?” ati. Mi honpi chun, Barabbas atiuve.
Mtawala akawauliza tena, “Ni yupi kati ya hawa wawili mnayetaka niwafungulie?” Wakajibu, “Baraba.”
22 Pilate in adonbut in, “Messiah kiti Yeshua hila ikalo ding ham?” ati. Amahon, “Thingpel'a khenbeh in,” atiuve.
Pilato akawaambia, “Basi nifanye nini na huyu Yesu aitwaye Kristo?” Wakajibu wote, “Msulubishe!”
23 Pilate in “Ipi jeh inem? Ipi suhkhel len anei ham?” ati. Hinlah mi honpi chun aha sap cheh uvin, “Thingpel'a khenbeh in,” atiuve.
Pilato akauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa gani?” Lakini wao wakazidi kupiga kelele, wakisema, “Msulubishe!”
24 Plate chun imacha phatchomna aum-louva chusanga boina asocheh ding chu amu phat in, aman cha-konga twi athum in chule mi honpi masanga chun akhut akisop in aseitai, hichepa thisan kisona'a hin themmona kaneipoi: Nanghon kimopoh tauvin'ati.
Pilato alipoona kwamba hawezi kufanya lolote, lakini badala yake ghasia zilikuwa zinaanza, akachukua maji, akanawa mikono yake mbele ya ule umati wa watu, akasema, “Sina hatia juu ya damu ya mtu huyu, hili ni jukumu lenu!”
25 Chuin miho jouse chun, Ama thina chunga keiho le ka chateu geiyin mo kipoh naveh tangu tin ale donbut un ahi.
Watu wote wakajibu, “Damu yake na iwe juu yetu na juu ya watoto wetu!”
26 Chuin aman Barabbas chu alhadoh peh in, Yeshua vang chu sakol jepna thih lingneiya jep ding in Rome sepai ho thu apen chule amahon thingpel'a akhetbeh diuvin apedoh tai.
Basi akawafungulia Baraba. Lakini baada ya kuamuru Yesu achapwe mijeledi, akamtoa ili asulubishwe.
27 Gamvaipopa sepai ho chun Yeshua chu atol-piu thutanna mun'a apuiyun chule sepai ho chu akou doh un ahi.
Kisha askari wa mtawala wakampeleka Yesu kwenye Praitorio na wakakusanya kikosi kizima cha askari kumzunguka.
28 Amahon apon chu ahoh lhauvin, chule ponsandup asilpeh uvin ahi.
Wakamvua nguo zake na kumvika vazi la rangi nyekundu, kisha
29 Amahon ling bah ho chu lukhuh in asem un chule alu chunga akoiyun, chuin akhut jetlam'a peng tengol akichoisah un leng-tengolin aneisah uve. Chujouvin totnan a-anga adilsu-uvin chuin dainopnan, Kajabol'ui, Judah te Lengpa atiuve.
wakasokota taji ya miiba, wakaiweka kichwani pake. Wakamwekea fimbo katika mkono wake wa kuume, na wakapiga magoti mbele zake na kumdhihaki, wakisema, “Salamu, mfalme wa Wayahudi!”
30 Chujongleh chil aset khum un chuin atenggol chu alahpeh un chule hichea chun aluchang avohpeh un ahi.
Wakamtemea mate, wakachukua ile fimbo wakampiga kichwani tena na tena.
31 Achaina keiya totnopna'a anei nung-uvin, amahon ponsan chu alahpeh uvin chuin amapon asilpeh kit tauve. Chujouvin amahon thingpel'a khetbeh ding in apui tauvin ahi.
Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile joho, wakamvika tena nguo zake. Kisha wakampeleka ili wakamsulubishe.
32 Lampia chun mikhat Simon, Cyrene a kona hung ahin, chuin sepai ho chun ada adoiyin Yeshua thingpel chu aputsah tauve.
Walipokuwa wakienda, wakakutana na mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, nao wakamlazimisha kuubeba ule msalaba.
33 Chuin amaho Golgotha atiu (Hichu lugumun kitina) mun chu alhung tauve.
Wakafika mahali palipoitwa Golgotha (maana yake ni Mahali pa Fuvu la Kichwa).
34 Sepai ho chun juthuh le gilkha kihal apeuvin, hinlah aman ate jouvin, adon nom-tapoi.
Hapo wakampa Yesu divai iliyochanganywa na nyongo ili anywe; lakini alipoionja, akakataa kuinywa.
35 Amahon Thingpel chunga akhetbeh jouvun, sepaiho chun aponsil chu avangpha pha chang hen tin vang asang tauve.
Walipokwisha kumsulubisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura. [Hili lilifanyika ili litimie lile neno lililonenwa na nabii, “Waligawa nguo zangu miongoni mwao na vazi langu wakalipigia kura.”]
36 Chujouvin amaho akimvela atouvun chule ama kikhai pet in angah un ahi.
Kisha wakaketi, wakamchunga.
37 Yeshua luchunga chun melchihna khat atah un, ama douna a aheh setnau phondohnan, “Hiche hi Yeshua Judah te lengpa,” tin akijih in ahi.
Juu ya kichwa chake, kwenye msalaba, wakaandika shtaka lake hivi: Huyu ni Yesu, Mfalme wa Wayahudi.
38 Gamsung kivaipoh kikhelsah goa mini chu khat ajet lama chule khat aveilama Amatoh akhetbeh thauvin ahi.
Wanyangʼanyi wawili walisulubiwa pamoja naye, mmoja upande wake wa kuume na mwingine upande wa kushoto.
39 Chule ahin hopa ho chun isahlou tah in akhasuh khum uvin,
Watu waliokuwa wakipita njiani wakamtukana huku wakitikisa vichwa vyao
40 amahon asam un, “Kiven tun, nangman Hou'in chu nasuh chima chule ni thum sunga natundoh ding in naseiye. Chutia nangma Pathen Chapa nahileh nangma kihuhhing'in lang chule thingpel'a kon'in hungkum lhan,” atiuve.
na kusema, “Wewe ambaye utalivunja Hekalu na kulijenga kwa siku tatu, jiokoe mwenyewe basi! Kama wewe ni Mwana wa Mungu, shuka kutoka msalabani.”
41 Thempu pipui ho, houdan thuhil ho chule upa ho jong chun totnopnan Yeshua chu ahouvun,
Vivyo hivyo, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria pamoja na wazee wakamdhihaki wakisema,
42 ataitom un, “Aman midang ahuhhing theiyin, hinlah ama akihuhhing theipoi” atiuve. Hitia hi ama Israel te lengpa hiya ham? Tutah hin ama thingpel a kon'in hung kumlha hen, chutileh katahsan diu ahi.
“Aliwaokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe! Yeye ni Mfalme wa Israeli! Ashuke sasa kutoka msalabani, nasi tutamwamini.
43 Aman Pathen atahsan in, hijeh chun Pathen in ama adeiya ahileh huhhing hen. Ajeh chu aman aseiyin, “Keima Pathen Chapa kahi, ati” atiuve.
Anamwamini Mungu, basi Mungu na amwokoe sasa kama anamtaka, kwa maana alisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu.’”
44 Gamsung kivaipoh kikhelsah goteni jong chun hitima chun ahouse lhon in ahi.
Hata wale wanyangʼanyi waliosulubiwa pamoja naye wakamtukana vivyo hivyo.
45 Sunkim'a pat nilhangkai nidan thum geiyin gamsung pumpia mu athim in ahi.
Tangu saa sita hadi saa tisa giza liliifunika nchi yote.
46 Nilhangkai nidan thum don in, Yeshuan aw sangtah in asam in, “Eli, Eli, lema sabach thani?” hichu “Ka Pathen, ka Pathen, ipi dinga neidon lou hitam?” ti kiseina ahi.
Ilipofika saa tisa, Yesu akapaza sauti akalia, “Eloi, Eloi, lama sabakthani?” (maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?”)
47 Akimvela dingho phabep chun ahekhel-uvin, chuti chun themgao Elijah akouvin agel uve.
Baadhi ya watu waliokuwa wamesimama pale waliposikia hayo, wakasema, “Anamwita Eliya.”
48 Amaho lah'a khat chu alhai jelin chuin twichop phonna juthuh chu agadelhop in, pumpeng leh'a chun adontheina ding in atah sang in ahi.
Ghafula mmoja wao akaenda mbio na kuleta sifongo, akaichovya kwenye siki, akaiweka kwenye mwanzi na akampa Yesu ili anywe.
49 Hinlah midangho chun, “Khongaiyin, Elijah ahuhhing dinga hungnam, veuhite,” atiuve.
Wengine wakasema, “Basi mwacheni. Hebu tuone kama Eliya atakuja kumwokoa.”
50 Chujouvin Yeshuan ahinsam kit in, chuin a-Lhagao alhadoh tai.
Yesu alipolia tena kwa sauti kuu, akaitoa roho yake.
51 Hichepet chun Hou'in munthenga pondal chu anah a pat ato geiyin keh ni akiso tai. Leiset akithing in chule songpi ho jong akehlha jeng e.
Wakati huo huo pazia la Hekalu likachanika vipande viwili, kuanzia juu hadi chini. Dunia ikatetemeka na miamba ikapasuka.
52 Chuin lhankot ho akihong in, Pathen ngaisah athisa ho tahsa chu kaithouvin aumkit un ahi.
Makaburi yakafunguka na miili ya watakatifu waliokuwa wamekufa ikafufuliwa.
53 Yeshua thokit jouvin amahon lhankhuh chu adalha uvin, Jerusalem khopia alut un, chule mitamtah henga aga kimusah uvin ahi.
Wakatoka makaburini, na baada ya Yesu kufufuka, waliingia kwenye Mji Mtakatifu na kuwatokea watu wengi.
54 Rome sepai ja lamkai pa le sepai dang ho akikhetbehna mun'a umho chun ling akihoa hiti ho thusoh chun atijatsah lheh uvin ahi. Amahon aseiyun, “Hiche hi Pathen Chapa tahbeh ahiye,” atiuve.
Basi yule jemadari na wale waliokuwa pamoja naye wakimlinda Yesu walipoona lile tetemeko na yale yote yaliyokuwa yametukia, waliogopa, wakasema, “Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
55 Chule numei tampi Yeshua toh Galilee akon'a ahin lhonpi ama gelkhoh ho chun gamlatah a kon in aveu vin ahi.
Walikuwako wanawake huko wakiangalia kwa mbali. Hawa walikuwa wamemfuata Yesu tangu Galilaya ili kushughulikia mahitaji yake.
56 Amaho lah'a Mary Magdalene, James le Joseph nu Mary, chule James le John (Zebedee chapateni) ahiuve:
Miongoni mwao walikuwepo Maria Magdalene, na Maria mama yao Yakobo na Yosefu, na mama yao wana wa Zebedayo.
57 Nilhah ahung hi phat in, Joseph Arimathea khoa mihaopa, amahin Yeshua nung anajui ahin,
Ilipofika jioni, alifika mtu mmoja tajiri kutoka Arimathaya aitwaye Yosefu, ambaye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
58 Pilate henga aga chen chule Yeshua tahsa chu athum in ahi. Chule Pilate chun ama pehdoh ding in phalna apetai.
Akamwendea Pilato ili kumwomba mwili wa Yesu. Pilato akaamuru apewe.
59 Joseph hin atahsa chu alan tupat ponnem thengsel'in atom in ahi.
Yosefu akauchukua mwili wa Yesu, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi,
60 Aman ama lhan thah, songpia kon'a kigeihom sunga chun akoiyin ahi. Chujouvin aman alutna mun'a chun songlentah khat atahlut jouvin achemangtai.
na kuuweka katika kaburi lake mwenyewe jipya, alilokuwa amelichonga kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa katika ingilio la kaburi, akaenda zake.
61 Mary le Magdalene chule Mary chomnu lhan'a atou un chule angah un ahi.
Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwepo mahali pale, wakiwa wameketi mkabala na kaburi.
62 Ajingin, Sabbath nikhon thempu pipuho le Pharisee ho Pilate kimupidin aga-cheuvin ahi.
Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya Maandalizi ya Sabato, viongozi wa makuhani na Mafarisayo wakamwendea Pilato
63 Amahon ajah a, “Pu, hiche milhem lhapa chun ahinlaiya khatvei anasei chu kageldoh uve. Aman ni thum joule thina'a kon'a kathodoh kit ding ahi.
na kusema, “Bwana, tumekumbuka kwamba yule mdanganyifu wakati alikuwa bado hai alisema, ‘Baada ya siku tatu nitafufuka.’
64 Hijeh'a hi lhan chu ni thum lhinkah'a ding in mohor nam in. Hiche hin aseijuite ahung uva chule atahsa guhmangna chule mijouse koma ama athilah'a kon in athoudohtai atina diu umta ponte. Hiti chu hileh amasa suhkhel sang'a phajo hiding ahi,” ati.
Kwa hiyo uamuru kaburi lilindwe kwa uthabiti mpaka baada ya siku tatu. La sivyo, wanafunzi wake wanaweza kuja kuuiba mwili wake na kuwaambia watu kwamba amefufuliwa kutoka kwa wafu. Udanganyifu huu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa kwanza.”
65 Pilate in adonbut in, “Hou'in ngah ho chu puiyun lang chule nahonbit thei chan un hongbit un,” ati.
Pilato akawaambia, “Ninyi mnao askari walinzi. Nendeni, liwekeeni ulinzi kadri mwezavyo.”
66 Hiti chun amahon lhan chu mohor anam'un chule avetup ding'in angah akoi tauve.
Kwa hiyo wakaenda na walinzi ili kulilinda kaburi kwa uthabiti, wakatia muhuri kwenye lile jiwe na kuweka ulinzi.

< Matthew 27 >