< Isaiah 26 >
1 Hiche nikho teng leh Judah gamsung cheng mijousen hiche la hi asah diu ahi: Ka khopiu hi dettah ahi! Pathen mi huhhingna banghon eium kim velun ahi.
Katika siku ile, wimbo huu utaimbwa katika nchi ya Yuda: Tuna mji ulio na nguvu, Mungu huufanya wokovu kuwa kuta zake na maboma yake.
2 Michonpha hodin kotpi hon peh un; tahsan umtah ho chu lut sah un.
Fungua malango ili taifa lenye haki lipate kuingia, taifa lile lidumishalo imani.
3 Nangma tahsan ho jouse, lungmong sel'a nakoiding ahin, alunggel jouse nachunga koidet ho chu.
Utamlinda katika amani kamilifu yeye ambaye moyo wake ni thabiti kwa sababu anakutumaini wewe.
4 Pakai chu tahsan jing jengun, ajehchu Pakai Pathen chu tonsot songpi ahi.
Mtumaini Bwana milele, kwa kuwa Bwana, Bwana, ni Mwamba wa milele.
5 Mi kiletsah ho chu asunem jin, khopi kiletsah chu asu lhujin, leivui asojin ahi.
Huwashusha wale wajikwezao, huushusha chini mji wenye kiburi, huushusha hadi ardhini na kuutupa chini mavumbini.
6 Mivaicha leh suh genthei a umhon akengtou vin achot phaovin, genthei vaichaho achunga avah leu vin ahi.
Miguu huukanyaga chini, miguu ya hao walioonewa, hatua za hao maskini.
7 Ahin, michonpha hodin lampi chu aken pon, ajot hahpoije. Thildih jengbol Pathen chu nahin, amalam u lampi nam pet in nalhai.
Mapito ya wenye haki yamenyooka. Ewe uliye Mwenye Haki, waisawazisha njia ya mtu mnyofu.
8 Pakai, na danthu ho kanit uhin katahsan nao aphongdoh in, namin loupi ding hi kalung ngaichat pennu ahi.
Naam, Bwana, tukienenda katika sheria zako, twakungojea wewe, jina lako na sifa zako ndizo shauku za mioyo yetu.
9 Jan khovah in nangma kaholjin; jingkah teng gunchu tah in Pathen kahol ji. Ajehchu leiset thutanna nahung teng lebou, miten adih chu ahet diu ahi.
Nafsi yangu yakutamani wakati wa usiku, wakati wa asubuhi roho yangu yakuonea shauku. Wakati hukumu zako zinapokuja juu ya dunia, watu wa ulimwengu hujifunza haki.
10 Migiloute nangai lut nan thilpha aboldoh deh pouve. Midangin thilpha abol vang'in, migilouten thildih lou abol jingu vin, Pakai loupina chu hetphah in aneipouve.
Ingawa neema yaonyeshwa kwa waovu, hawajifunzi haki, hata katika nchi ya unyofu huendelea kutenda mabaya wala hawazingatii utukufu wa Bwana.
11 Aw Pakai na khuttum dopsang eman agel pou ve. Na mite na huhdoh nomdan chu musah in, chuteng amaho chu jachatna dimdiu ahitai. Na meikong chun nagalmi ho sumang jeng hen
Ee Bwana, mkono wako umeinuliwa juu, lakini hawauoni. Wao na waone wivu wako kwa ajili ya watu wako tena waaibishwe, moto uliowekwa akiba kwa ajili ya adui zako na uwateketeze.
12 Pakai chamna neipeh diu ahi; kabol ka suh bulhit jouseu hi nang jal'a bou ahi.
Bwana, unaamuru amani kwa ajili yetu, yale yote tuliyoweza kuyakamilisha ni wewe uliyetenda kwa ajili yetu.
13 Aw Pakai ka Pathen u, midang hon kachung uva vai ahin hom uve, ahin nangma bou nahi keima hon ka hou uchu.
Ee Bwana, Mungu wetu, mabwana wengine zaidi ya wewe wametutawala, lakini jina lako pekee ndilo tunaloliheshimu.
14 Kana jen leuho chu athiuvin, aum gam tapouve. A lhagao dalhah hou hung kile talou hel ding ahi! Nangman nasat nin, na sumang gamtai. Amaho chu sottahpi gelphah louvin aumtauve.
Wao sasa wamekufa, wala hawako tena hai, roho za waliokufa hazitarudi tena. Uliwaadhibu na kuwaangamiza, umefuta kumbukumbu lao lote.
15 Aw Pakai, kanam u nei semlet peh taove; lentah nei so tao vin ahi. Ka gamgi hou jong nei kehlet peh un, loupina nangma kahin peuvin ahi!
Umeliongeza hilo taifa, Ee Bwana, umeliongeza hilo taifa. Umejipatia utukufu kwa ajili yako mwenyewe, umepanua mipaka yote ya nchi.
16 Pakai, lung genthei in nangma kana hol ui. Na thunun pohgihna nanoija kahungtao uve.
Bwana, walikujia katika taabu yao, wewe ulipowarudi, waliweza kuomba kwa kunongʼona tu.
17 Numei naovop in nao anei na'a na asah a, apenchoi choi banga, Pakai, na umna'a kaum tenguleh kachuti jiu ve.
Kama mwanamke mwenye mimba aliyekaribia kuzaa anavyogaagaa na kulia kwa ajili ya maumivu yake, ndivyo tulivyokuwa mbele zako, Ee Bwana.
18 Keiho jong lungna in kijel chot chot in ka umun, ahin kagenthei thoh ujong mohseh ahi. Leiset adin huhhingna kape thei pouve, hinna jong vannoi a kapolut thei pouvin ahi.
Tulikuwa na mimba, tuligaagaa kwa maumivu, lakini tulizaa upepo. Hatukuleta wokovu duniani, hatujazaa watu katika ulimwengu huu.
19 Ahin Pakai a thiho chu hung hing diu, atahsau hung thoudoh kit ding ahi! Leiset a imu hochu hungthoudoh diu chuleh kipa jal'a la asah diu ahi. Ajeh chu na hinna-vah kipa chu jingkah daitwi alhah banga namite thi umna munna hunglha ding ahi.
Lakini wafu wenu wataishi, nayo miili yao itafufuka. Ninyi mnaokaa katika mavumbi, amkeni mkapige kelele kwa furaha. Umande wenu ni kama umande wa asubuhi, dunia itawazaa wafu wake.
20 In na cheuvin, kamite, na kot hou kam tup un! Chomkhat adin kisel mangun, Pakai lunghanna akichai masang sen.
Nendeni, watu wangu, ingieni vyumbani mwenu na mfunge milango nyuma yenu, jificheni kwa kitambo kidogo mpaka ghadhabu yake ipite.
21 Ven! Leiset mite a chonset jeh un, gotna pedin Pakai chu van'a konin ahungin ahi. Leiset in akithat ho asel jou tah lou ding, mijouse mudinga hung kipuidoh diu ahi.
Tazama, Bwana anakuja kutoka makao yake ili kuwaadhibu watu wa dunia kwa ajili ya dhambi zao. Dunia itadhihirisha umwagaji damu juu yake, wala haitaendelea kuwaficha watu wake waliouawa.