< Semtilbu 40 >
1 Hicheng thilsoh kichai nung chun Pharaoh lengpa natong ju vaihompa le an vai hompan apupa Egypt lengpa doumah abol lhon in achonse lhontai.
Baada ya muda, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri, wakamkosea bwana wao, mfalme wa Misri.
2 Hiche lamkai teni chunga hi Pharaoh nasatah in alunghang tan ahi.
Farao akawakasirikia hawa maafisa wake wawili, mnyweshaji mkuu na mwokaji mkuu,
3 Chuin Pharaoh in amani chu Joseph umna lengpa songkul natong ho umna ah akoiyin ahi.
akawaweka chini ya ulinzi katika nyumba ya mkuu wa kikosi cha ulinzi katika gereza lile lile alimofungwa Yosefu.
4 Songkul ngahpan amani chu Joseph thanei na noiya a umsah in Joseph in jong amani chu vetkolna anei jing in ahi.
Mkuu wa kikosi cha ulinzi akawakabidhi kwa Yosefu, naye akawahudumia. Walipokuwa wamekaa chini ya ulinzi kwa muda,
5 Jan khat chun songkul insunga kihen teni Egypt lengpa juvaihompa le an vaihompa chun mang khat cheh, amang ledohna toh kilhon cheh-in anei lhon in ahi.
kila mmoja wa hao wawili waliokuwa wamewekwa gerezani, yaani mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri, waliota ndoto usiku mmoja, na kila ndoto ilikuwa na maana yake tofauti.
6 Hichun Joseph in amani chu jingkah lama amailhon lunglhai lou chu ahedohtan Joseph in amani chu adongin, ibola nang teni namai lhon kipah lou ham ati.
Yosefu alipowajia asubuhi yake, akawaona kwamba walikuwa na huzuni.
7 Joseph in adong in, “Sopi teni ibola namai lhon lhailou ham,” ati.
Ndipo Yosefu akawauliza maafisa hao wa Farao waliokuwa chini ya ulinzi pamoja naye nyumbani mwa bwana wake, akasema, “Mbona nyuso zenu zimejaa huzuni leo?”
8 Amanin adon but lhon in, “Janlhah in keinin mang kanei gel lhon in amavang koi machan kamang ipi kisei na ahi aledoh thei aumpoi ati lhon e, ahin Joseph in adonbut in,” mang in ipi ahetsah dichu Pathen kin ahi. Chule namang lhon chu neisei peh lhon in ati.
Wakamjibu, “Sisi sote tuliota ndoto, lakini hapakuwa na mtu yeyote wa kuzifasiri.” Ndipo Yosefu akawaambia, “Je, kufasiri ndoto si kazi ya Mungu? Niambieni ndoto zenu.”
9 Hichun khon dom le a pang lamkai pa chun Joseph chu amang ho chu asei peh tai. Ka manga lengpi bah ka masanga ka mun.
Basi mkuu wa wanyweshaji akamweleza Yosefu ndoto yake. Akamwambia, “Katika ndoto yangu niliona mzabibu mbele yangu,
10 Hiche lengpi phunga chun abah thum ajam kamun, gang tah in ahung mum in chu in apah lha tai, hiche aga hochu lengpithei ga ahung hitai.
nao mzabibu ulikuwa na matawi matatu. Mara tu ulipoanza kuchipua, maua yalichanua na vishada vyake vikawa zabibu zilizoiva.
11 Pharaoh chakhon chu ka khut chunga ana um'in, hichun keiman lengpi ga chu ka sujot in atwi chu Pharaoh khona ka sun peh e.
Kikombe cha Farao kilikuwa mkononi mwangu, nikazitwaa zabibu, nikazikamua katika kikombe cha Farao, na nikaweka kikombe mkononi mwake.”
12 Joseph in hitin aseiye, “Lengpi bah thum hochu nithum tina ahi.
Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Matawi matatu ni siku tatu.
13 Nithum sunga hi Pharaoh in nithum jou teng nadom sang intin, chule masanga nana toh na a nanung koi kit ding ahi.
Katika siku hizi tatu, Farao atakutoa gerezani na kukuweka tena kwenye nafasi yako, nawe utaweka kikombe cha Farao mikononi mwake, kama vile ulivyokuwa unafanya ulipokuwa mnyweshaji wake.
14 Chule nangma koma katao ahi, chanvou pha nahung chan teng neihin sumil hih beh in Pharaoh koma hitobang kathil bol hohi eina seipeh in, ajeh chu songkul'a kona eilha doh thei na ding in,” ati.
Lakini wakati mambo yatakapokuwia mazuri, unikumbuke, unifanyie wema, useme mema juu yangu kwa Farao ili niondoke huku gerezani.
15 Ajeh chu Hebrew gam a ka in apat a eikiman doh tua hiche songkul'a kaum hi mona neilou bolkhel ka neipoi.
Kwa maana nilichukuliwa kwa nguvu kutoka nchi ya Waebrania, na hata hapa nilipo sikufanya lolote linalostahili niwekwe gerezani.”
16 Hichun changlhah hom'a lamkai pachu Joseph in amang hoitah a ale chu amu le ama jong atha anom lheh in; Joseph jah ah hitin aseiye, “Keiman jong jan mang kaneiye, ka manga chun paipeh thum changlhah dimset kalu chunga kapoi.
Yule mwokaji mkuu alipoona kuwa Yosefu amefasiri ikiwa na maana nzuri, akamwambia Yosefu, “Mimi pia niliota ndoto: Kichwani mwangu kulikuwepo vikapu vitatu vya mikate.
17 Paipeh achuna pa sunga chun changlhah ajat lhingsel in aum in, Pharaoh a ding ahi, ahin vacha ho ahung leng un ka luchunga changlhah ho chu ane doh tauve.”
Katika kikapu cha juu kulikuwa na aina zote za vyakula vilivyookwa kwa ajili ya Farao, lakini ndege walikuwa wakivila kutoka kwenye kikapu nilichokuwa nimebeba kichwani.”
18 Joseph in amang chu ale pehtan, “Paipeh thum chun nithum ma avetsah ahin,
Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Vikapu vitatu ni siku tatu.
19 Nithum sunga hi Pharaoh in nalu adopsang ding thing phunga nakhai sang a, vachaten naphe anehchai ding'u ahi.”
Katika siku hizi tatu, Farao atakata kichwa chako na kukutundika juu ya mti. Nao ndege watakula nyama ya mwili wako.”
20 Pharaoh in nithum jou in ama penni kipapina in anoiya a semang pachonga pang jouse akou khom in hiche a pang dinga chu juvai hom lamkai pa le an vaihom lamkaipa chu alhadoh gel in,
Mnamo siku ya tatu, ilikuwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Farao, naye akawaandalia maafisa wake wote karamu. Akawatoa gerezani mnyweshaji mkuu na mwokaji mkuu, akawaweka mbele ya maafisa wake:
21 Ju vaihom pachu aju vaihom na ma man apansah kit'in, aman jong jukhon chu Pharaoh khut a agapetai.
Ndipo akamrudisha mnyweshaji mkuu kwenye nafasi yake, ili aweke kikombe mikononi mwa Farao tena,
22 Ahin an vaihom lamkaipa vang chu Joseph in amani henga mang alepeh bang chun akhai lih tan ahi.
lakini akamwangika yule mwokaji mkuu, sawasawa na jinsi Yosefu alivyowaambia katika tafsiri yake.
23 Hichun ju vaihom lamkaipan Joseph chu ageldoh tapon asumil deltai.
Pamoja na hayo, mnyweshaji mkuu hakumkumbuka Yosefu, bali alimsahau.