< 2 Thusimbu 9 >

1 Sheba lengnun Solomon minthan naho thu ajahdoh phat chun, apatep mong mong dingin thudoh hahsa tampi dong dingin Jerusalem a ahungtan ahi. Amanu chu akilhonpi tamtah toh gimnamtui, sana le songmantam tampi sangong sao ahinpoh sah in, thupitah in Solomon kom ahunglhung tan ahi.
Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni, huyo malkia akaja Yerusalemu kumjaribu kwa maswali magumu. Alifika akiwa na msafara mkubwa sana, pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani, alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
2 Solomon chun amanu thudoh jouse abonchan adonbut in, chule bailam tah in ahilchenin ahi.
Solomoni akamjibu maswali yake yote, wala hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwake asiweze kumwelezea.
3 Sheba lengnun Solomon chihna ho, chule a leng inpi sah,
Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
4 Adokhang chunga an le twi ho, amilen milal ho touna, ajen lea pang ho kivonna, akhon doma pangho kivonna le Pakai Houin a pumgo thilto abolho amudoh chun kidang asavallin athia abang jengin ahi.
chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika Hekalu la Bwana alipatwa na mshangao.
5 Chuin Sheba lengnun lengpa komma aseiyin, “Keima gamsunga kana jah na chih na le na natoh thilbol hohi atah mong ahi.
Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
6 Ahinlah kamit tah’a kana musanga chun miho thusei chu atah hidingin kana gelpon ahi. Tahbeh a seidingin nathupi naho hi akehkhat bepbou eina kiseipeh ahibouve, hiche ei kiseipeh kajah ho sangin gam chengin nakho khellin ahi,” ati.
Lakini sikuamini yaliyosemwa hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana kuliko ile taarifa niliyoisikia.
7 Namite iti pan akipah ta diuvem! Namilen-milalte ho, na angsunga adin jinguva nachih na thu ajah jengu hi iti pan akipah tadiu vem! Na Pakai, Pathen chu vahchoiyin umtahen, Amachu nachunga lunglhai tangei unte chule,
Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
8 Pakai na Pathen in vaihom dinga laltouna natousah’a Lenga napansah ahitai. Ijeh-inem itileh na Pathen chun amite Israelte alungsetna atonsotna adop sang nom jeh chule thutahle thudih’a ama ho chunga vai nahop theina dinga Lenga napansah ahitai.
Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe, na akakuweka juu ya kiti chake cha ufalme utawale kwa niaba ya Bwana Mungu wako. Kwa sababu ya upendo wa Mungu wako kwa Israeli na shauku yake ya kuwadhibitisha milele, amekufanya wewe mfalme juu yao, ili kudumisha haki na uadilifu.”
9 Chuin Sheba Lengnu chun Solomon Lengpa chu sana talent jakhat le somni chule gimnamtui le songmantam tamtah apen ahi. Amanun Solomon Lengpa apeh tobang gimnamtui chu tumasangin ana um kha hih laijin ahi.
Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa vikolezi vizuri kama vile Malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
10 Hiram Lengpa soh hole Solomon Lengpa soh ho chun Ophir akonin Sana ahinpouvin, chule algumthing le Songmantam jong ahinpouve.
(Watumishi wa Hiramu na wa Solomoni wakaleta dhahabu kutoka Ofiri, tena wakaleta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
11 Lengpa chun Algum thingho chu Pakai Houin le Leng inpi kalbi ho semnan amangin chule lasathem ho dingin selangdah le pehkhong semnan amangin ahi. Hiti ho tobang hi tumasangin Judah gamsunga ana kimukha hih laijin ahi.
Mfalme akatumia hiyo miti ya msandali kuwa ngazi kwa ajili ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa Yuda tangu siku ile.)
12 Solomon Lengpa chun Sheba Lengnu angaichat le athum jouse chu apen, aman ahinpoh sanga tamjo chu ale peh kitnin ahi. Chuin amilal ho tochun agamlanguva akinungle kit tauvin ahi.
Mfalme Solomoni akampa Malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, zaidi ya vile alivyokuwa amemletea mfalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
13 Kumseh’a Solomon in sana amujat chu talent jaguple somgup le gup aphan,
Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
14 Hiche lah’a hi thilcho-thil joh hole kivei mihon anpeh-u pangloulai ahi. Chujongleh Arabia gam'a Lengho le gamvaipo honjong Solomon chu sana le dangka ahin pohpeh un ahi.
mbali na mapato yaliyoletwa na wafanyabiashara na wachuuzi. Wafalme wote wa Arabuni na watawala wa nchi wakamletea Solomoni dhahabu na fedha.
15 Solomon Lengpa chun sana’a kikheng kidalna pho asemin, kidalna pho khat chun sana shekel som gup alutnin ahi.
Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa. Kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
16 Aman sana’a kikheng kidalna pho aneo jathum jong asemin, kidalna pho khatna chun sana shekhel jathum cheh alut nin ahi. hiche ho sese chu lengpan Lebanon’a gammang inpia chun akoitai.
Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
17 Chuin Lengpan Saiha’a laltouna khat asemin sana thengsellin atomjollin ahi.
Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
18 Laltouna chun kalbi gup aneiyin chule sana touna keng ngapna toh akibuto in ahi. Touna teni jetle veiya chun Sakei bahkai lim ni adingin ahi.
Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na mahali pa kuwekea miguu vyote vya dhahabu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
19 Kalbi mong teni achung chu Sakei bahkai lim Som le ni aumin, kalbi dan gup ma aning cheh a chun sakei bahkai lim khat cheh akikoijin ahi,
Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
20 Solomon twi don'a khon ho jouse chu sana lhanga kisem ahin chule Lebanon’a gammang sana thengsella kisem ngen ahi. Thilho jouse chu dangka kisem khatcha aumpoi, ijen-inem itileh Solomon khang lai chun dangka chu manlhom jepdanin anaki hen ahi.
Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo wakati wa Solomoni.
21 Lengpa chun kiveina kong innei tampi jong aneiyin ahi, kumthum lhunseh leh kong innei ho chun khatvei sana dangka le saiha chule guldute le vahong ho ahin pojiuvin ahi.
Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizoendeshwa na watu wa Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
22 Lengpa Solomon chu leng dang ho jouse sangin haona le chih nan achungnung jon ahi.
Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
23 Nam jousea Leng ho chu Pathen in apeh achihna ho thu ngainom leh, houlim pi dingin ahung jiuvin ahi.
Wafalme wote wa dunia wakatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
24 Akum kumin ama hungvil jouse chun sana le dangka sangkholchol, gimnamtui galmanchah sakol le sangan ho kipa thilpeh adin ahinpoh peh jiuvin ahi.
Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja, alileta zawadi, vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
25 Solomon chun sakolbuh le sakol kangtalai koina indan sangli aneiyin chule sakol jong sang som le ni aneiyin ahi. Hiche ho chu sakol kangtalai koina khopiho le Jersusalema ama kom naiyah akoi in ahi.
Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 kwa ajili ya farasi na magari ya vita, farasi 12,000 ambao aliwaweka katika miji ya magari ya vita na katika Yerusalemu pamoja naye.
26 Solomon chun sahlama Euphrate vadung apat Philestine te gam chan chule lhanglama Egypt gamgi sunga lengho chunga vai ana homin ahi.
Solomoni akatawala juu ya wafalme wote kuanzia Mto Frati mpaka kwenye nchi ya Wafilisti na kuendelea hadi mpaka wa Misri.
27 Lengpa chun Jerusalem khopi sunga dangka nengjeng jungin abolllin song lheo lah abahsah jinge, chule thing mantam jong Judah phaichamma theipi thingkeh ning lhing tah a muntinna akimu jeng thei bangin abollin ahi.
Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
28 Solomon sakol ho chu Egypt gam le gam chom chomma konna hung kipolut ahiuve.
Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka nchi nyingine zote.
29 Solomon vaipoh abulla kipan achaina changei’a thilsoh adangho chu, themgao Nathan Lekhabu chule Sheloh a um, Ahijah gaothuseina chule Nebat chapa Jerobaom chung changa muneipa Iddo Mitva neipa gaomu thusimma akijih lut soh keijin ahi.
Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Nathani, katika unabii wa Ahiya Mshiloni na katika maono ya Ido mwonaji kuhusu Yeroboamu mwana wa Nebati?
30 Solomon chun Jerusalem a Israel pumpi chunga, kum somli vai ana pon ahi.
Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
31 Ama athi chun apa David khopia chun akivuitai. Chuin achapa Rehoboam chu ama banin lengin ahungpang tan ahi.
Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Thusimbu 9 >