< 2 Thusimbu 33 >
1 Manasseh leng ahung chanchun kum 12 bep anahin aman Jerusalem mah kum 55 geijin vai ana hommin ahi
Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka hamsini na mitano.
2 Amahin Pakaiyin Israel chate masanga anano doh namdangho chonna kidah umtah ho chonna chu anache pi in Pakai mitmun thilse ngen abollin ahi
Akafanya maovu machoni pa Bwana, akafuata desturi za machukizo za mataifa ambayo Bwana aliyafukuza mbele ya Waisraeli.
3 Amahin apa Hezekiah in ana vohlhuh munsang hochu anasapha kitnin, Baal doihouna anatung doh kitnin pathen lim semthu Asherah doi hochu ana tungdoh kitnin ahi
Akajenga upya mahali pa juu pa kuabudia miungu ambapo Hezekia baba yake, alikuwa amepabomoa, pia akasimamisha madhabahu za Mabaali na nguzo za Maashera. Akalisujudia jeshi lote la angani na kuliabudu.
4 Aman Pakai houinmai leh amiten ama ahin houna ding mun atiova chun semthu pathen houna maicham atungdoh kitnin ahi
Akajenga madhabahu katika Hekalu la Bwana ambamo Bwana alikuwa amesema, “Jina langu litadumu Yerusalemu milele.”
5 Pakai houin na hongcha teni a chun ahsi ho houna maicham anatung doh in ahi
Katika nyua zote mbili za Hekalu la Bwana akajenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la angani.
6 Hinnom phaicham mah achate pumgo thilto in anakatdoh in ahi. Themka pou anadongin, ailhimjong jong, phunsan jong anachepin, thillha gaochang mijong ana tahsannin mitphel doithem hojong anamangin. Hiti hin Pakai mitmun thet um tahtah anabol doh in Pathen ana phin lung hangin ahi
Akawatoa wanawe kuwa kafara kwa kuwapitisha katika moto katika Bonde la Ben-Hinomu, akafanya ulozi, uaguzi na uchawi, akataka ushauri kwa wenye pepo wa utambuzi na wenye kuwasiliana na mizimu. Akafanya maovu mengi machoni pa Bwana, akaichochea hasira yake.
7 Hiti in Manasseh hin milim doihou najong Pathen houin sungah anatungdoh in ahi hiche houin chung changa Pathennin David le achapa Solomon jah a anasei, “Hiche houin sung le keiman Israel phung hijat laha kalhen dohsa Jerusalem khopi sunga hi a itihchan na jong keima eiki houjing nading munna kalhen doh ahi
Akachukua ile sanamu aliyoichonga na kuiweka katika Hekalu la Mungu ambalo Mungu alikuwa amemwambia Daudi na mwanawe Solomoni, “Katika Hekalu hili na katika Yerusalemu niliouchagua kutoka kabila zote za Israeli, nitaliweka Jina langu milele.
8 “Chuleh Israel mipiten kathupeh hi ajuijuva chuleh kalhacha pa Mosen anapeh u daanchu anit uva ahileh apu apateo kanapeh gam ma konna koima kakaidoh sah louhelding ahi”
Sitaifanya tena miguu ya Waisraeli iondoke tena katika nchi niliyowapa baba zenu, ikiwa watakuwa waangalifu kufanya kila kitu nilichowaamuru kuhusu sheria zote, maagizo na amri zilizotolewa kwa mkono wa Mose.”
9 Manasseh in Judah mipi te achonset sah hi keiman kamite ahung kitolluva kana nodoh peh namdang ho chonset sangin agimnei jon ahi.
Lakini Manase akawaongoza Yuda na watu wa Yerusalemu katika upotovu, kiasi kwamba walifanya maovu mengi kuliko mataifa ambayo Bwana aliwaangamiza mbele ya Waisraeli.
10 Pakaiyin Manasseh leh amipi te anagih vang'in amahon ana nahsah pouvin ahi
Bwana akasema na Manase pamoja na watu wake, lakini hawakumjali.
11 Hijeh chun Pakaiyin Assyria sepaite atildoh in Judahte chungah gal abolsah in, amahon Manasseh chu aman nun thihkol toh abutaovin thih khaovin akan nun Babylon nah akailut nun ahi
Hivyo Bwana akaleta juu yao majemadari wa jeshi la mfalme wa Ashuru, ambao walimchukua Manase kwenda kifungoni, wakaweka ndoana katika pua yake, wakamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli.
12 Ahahsat phatnin ahung kineosah in a Pakai a Pathen nah ahung kiheilut nin kithopi athummin ahi
Katika dhiki yake akamsihi Bwana Mungu wake na kujinyenyekeza sana mbele za Mungu wa baba zake.
13 Pathen nin Manasseh taona asangin Jerusalemma ale sollin avaihom sahkitnin ahi. Hiche phat chun Manasseh in Pakai chu Pathen tahbeh ahi ahechen taan ahi
Naye alipomwomba, Bwana akaguswa na kule kusihi kwake na akasikiliza kilio chake, kwa hiyo akamrudisha Yerusalemu na kwenye ufalme wake. Ndipo Manase akatambua kwamba Bwana ndiye Mungu.
14 Hiche jouhin Manasseh chun David khopi solang panga chun polang pal chu asesangin, nga kelkot sahleng Gihon twiphul kom phaicham ma kon in Ophel kiti khopi kom geijin pal chu asesangin ahi. Kul kiget khum Judah khopi ho khatcheh a chun sepai aloi loijin lamkai khatnoija akoiyin ahi
Baadaye akajenga ukuta wa nje wa Mji wa Daudi, magharibi mwa chemchemi ya Gihoni katika bonde, hadi kufikia ingilio la Lango la Samaki na akakizunguka kilima cha Ofeli, pia akaufanya kuwa mrefu zaidi. Akawaweka majemadari katika miji yote ya Yuda iliyokuwa imejengewa ngome.
15 Houin na konchun gamdang pathen holeh milim semthu aman anakoi holeh, namdang maicham thinglhanga atundoh nao ahouin houleh Jerusalem mundang danga umho chu aladoh sohkeijin aga paimang jengin ahi
Akaondolea mbali miungu ya kigeni na kuondoa sanamu kutoka Hekalu la Bwana pamoja na madhabahu zote alizozijenga katika kile kilima kilichojengwa Hekalu na katika Yerusalemu, akazitupa nje ya mji.
16 Aman Pakai ahounao maicham jongchu asemphan ahi, hiche chunga chun chamna thilto leh thangvah na thilto abollin ahi, aman Judah mipi techu Israel Pathen Pakai chu nahou diu ahitin thu apen ahi
Kisha akarudisha madhabahu ya Bwana na kutolea juu yake dhabihu za sadaka za amani pamoja na sadaka za shukrani, naye akawaamuru Yuda wamtumikie Bwana, Mungu wa Israeli.
17 Ahin lah mipi hochun munsang dunga pumgo thilto chu achepi jing nalaijun ahi, ahivangin Pakai Pathen komma bou abol taovin ahi
Lakini hata hivyo watu wakaendelea kutoa dhabihu mahali pa juu pa kuabudia miungu, lakini wakimtolea Bwana Mungu wao peke yake.
18 Manasseh in anabol jouse, Pathen henga ataona, themgao hon Pathen minna akom ma thu aseihou abonchan Israel lengte thusim bua abonchan akijhlut sohkei jin ahi
Matukio mengine ya utawala wa Manase, maombi yake kwa Mungu wake na maneno aliyoambiwa na waonaji walionena naye kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli, yameandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli.
19 Lengpa taonaleh Pathennin adonbutna alung ahin hei masanga achonset na ho jouse le thilse abolho, namdnag pathen houna le adoihou munchom chomma atundoh ho jouse chu themgao ho thusim bua akijih lut nin ahi
Maombi yake, pamoja na jinsi Mungu alivyoguswa na kusihi kwake, pia dhambi zake zote na kukosa kwake uaminifu pamoja na sehemu alizojenga mahali pa juu pa kuabudia miungu, kule kusimamisha nguzo za Ashera na sanamu kabla ya kujinyenyekeza kwake, yote yameandikwa katika kumbukumbu za waonaji.
20 Manasseh athiphat nin khopi sungah avuijun achapa Amon nin lengmun alotan ahi
Manase akalala pamoja na baba zake akazikwa katika jumba lake la kifalme. Naye Amoni mwanawe akawa mfalme baada yake.
21 Amon chu Juda gamma leng ahung chanchun kum 22 alhingtan ahi, amahin Jerusalema kum ni aleng chang ngin ahi
Amoni alikuwa na miaka ishirini na miwili, alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka miwili.
22 Ama apa Manasseh bangin Pakai dounan achonse tan ahi aman apan anahou doiho chu ana houvin ahi
Akatenda maovu machoni mwa Bwana, kama baba yake Manase alivyofanya. Amoni akaabudu na kutoa dhabihu kwa sanamu zote alizokuwa ametengeneza Manase.
23 Ahinlah apa banhgin Pakai anga kisuhnem na anabol pon apa sangin chonset ana ha boljon ahi
Lakini tofauti na Manase baba yake, hakujinyenyekeza mbele za Bwana, badala yake Amoni aliongeza hatia zaidi na zaidi.
24 Amon noija natong lamkai ho chu ana kihoutoh un leng inpi sunga chun ana that taovin ahi
Watumishi wa Amoni wakafanya fitina juu yake, nao wakamuulia kwake nyumbani.
25 Judah mipiten Amon that hochu ana thatdoh un achapa Josiah chu leng anachan sah un ahi
Kisha watu wa nchi wakawaua wale wote waliokuwa wamefanya hila dhidi ya Mfalme Amoni. Wakamfanya Yosia mwanawe kuwa mfalme mahali pake.