< 2 Thusimbu 26 >
1 Judah mipiten Amaziah chapa Uzziah chu kum 16 alhin kummin apakhellin leng achan sahtaovin ahi
Kisha watu wote wa Yuda wakamtwaa Uzia, aliyekuwa na umri wa miaka kumi na sita, nao wakamfanya mfalme mahali pa Amazia baba yake.
2 Apa Amaziah athijou chun Uzziah in Elath anung lahpeh kitnin akhopi chu asempha kitnin ahi
Ndiye alijenga upya Elathi kuirudisha kwa Yuda baada ya Amazia kulala pamoja na baba zake.
3 Uzziah leng ahung chanchun kum 16 alhingtan ahi chuleh aman Jerusalem machun kum 52 sungin vai anahommin ahi. Anuchu Jerusalemma konna Jecoliah kitinu chu ahi
Uzia alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka hamsini na miwili. Mama yake aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.
4 Apa umdaan chu anachepi in Pathen deilam jong ana bollin ahi
Akatenda yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Amazia baba yake alivyofanya.
5 Houlanga ana puihoijah Zechariah anahin leisen Pakai chu kitahna neitah in anajuijin ahileh Pathenin jong phatthei ana bohin ahi
Akamtafuta Mungu katika siku za Zekaria, aliyemwelekeza kumcha Mungu. Wakati wote alipomtafuta Bwana, Mungu alimfanikisha.
6 Uzziah in Philistine te dounan gal anasatnin ahi. Aman Gath, Jemniah leh Ashdod khopi kulpi hochu ana volhun hijouchun
Alipigana vita dhidi ya Wafilisti na kubomoa kuta za Gathi, Yabne na Ashdodi. Kisha akajenga upya miji karibu na Ashdodi na mahali pengine katikati ya Wafilisti.
7 Pathen panpi najallin Philistine te Gur – Baal a cheng Arabians Mehunins mite ana jouvin ahi
Mungu akamsaidia dhidi ya Wafilisti na dhidi ya Waarabu walioishi Gur-Baali na dhidi ya Wameuni.
8 Amon miten jong Uzziah kommah kai anapeovin hitichun amahi ahung hatdoh lheh jengtaan ahileh Egypt gamsung geijin ana minthang pehin ahi
Waamoni wakamletea Uzia ushuru, umaarufu wake ukaenea hadi kwenye mpaka wa Misri, kwa sababu alikuwa amekuwa na nguvu sana.
9 Uzziah in Jerusalem ninglang kelkot leh phaicham lang kelkot chuleh kulpi pal kihei konna munho jouse chunga chun insang asadohin hitihin khopi kulpi chu anasudet soh keijin ahi
Uzia akajenga minara huko Yerusalemu katika Lango la Pembeni, katika Lango la Bondeni na katika pembe, mahali kuta zikutanapo, kisha akaijengea ngome.
10 Aman gam ong lah a jenga jong kulpi dingin insang ho anasan chuleh twiputna dingin mun tamtah analaijin, lhumlam molpang holeh phaicham mah gancha tamtah ana vah'in ahi. aman mipi hojong lengpilei boldingin atilkhouvin thinglhang louphat na hoa jong lou abolsah in ahi
Akajenga pia minara jangwani na kuchimba visima vingi vya maji, kwa sababu alikuwa na mifugo mingi chini ya vilimani na kwenye nchi tambarare. Alikuwa na watu wanaofanya kazi katika mashamba yake na kwenye mashamba yake ya mizabibu huko vilimani na katika ardhi zenye rutuba, kwa kuwa aliupenda udongo.
11 Aman galmi tamtah galsat dinga kigosadem ho aneiyin, ama ho record chu leng insungmi sepai lamkai Hananiah vetsui nanoija thuching teni Jeiel leh Maaseiah in ajihlut lhonin ahi
Zaidi ya hayo, Uzia alikuwa na jeshi lililofunzwa vizuri, lililokuwa tayari kwenda vitani kwa vikosi kufuatana na idadi yao kama walivyokusanywa na Yeieli mwandishi na Maaseya msimamizi chini ya maelekezo ya Hanania, mmojawapo wa maafisa wa mfalme.
12 A sepai techu sepai lamkai 2600 (Sangni le jagup) ho thupeh nanoija um ahiove
Idadi yote ya viongozi wa jamaa waliowaongoza hawa wapiganaji walikuwa 2,600.
13 Amaho noija lengpa huhna dinga thanei tah a galsat thei sepai 307500 (Lakh thumle sang sagi le ja nga) aneiyin ahi
Chini ya uongozi wao kulikuwa na jeshi la askari 307,500 watu waliofundishwa kwa ajili ya vita, jeshi lenye nguvu la kumsaidia mfalme dhidi ya adui zake.
14 Uzziah sepai hijat dingin ompho, tengcha thihlukhuh asempeh in, thalpi jong asempeh in song sena bomjong asem peh in achang ding jong alokhom peh in ahi
Uzia akalipatia jeshi lote ngao, mikuki, chapeo, dirii, pinde na mawe ya kombeo.
15 Jerusalem khopiah khopi pal chunga konna songlentah tah sedoh thei nading leh thal kapdoh theinading manchah semthemho agoijin ahi. Aman Pathenna konna panpina amujeh in athahat na akijesallin gamtinnah amin thang lheh jengtaan ahi
Huko Yerusalemu watu wenye utaalamu mkubwa wakatengeneza mitambo iliyotumika katika minara na kwenye pembe za ulinzi ili kurusha mishale na kuvurumisha mawe makubwa. Sifa zake zikaenea mbali sana kwa sababu alisaidiwa mno mpaka akawa na nguvu sana.
16 Uzziah lengpa hi ahung hatdoh phatnin ahung kiletsah taan hiche hin a lhuhnading lampi ahin gongdoh taan ahi. Aman a Pakai a Pathen dou na in houin nah alutnin maicham muntheng ngachun gimnamtwi ahal gotaan ahi
Lakini baada ya Uzia kuwa na nguvu sana, majivuno yake yakamsababishia kuanguka. Alikosa uaminifu kwa Bwana Mungu wake, naye akaingia hekaluni mwa Bwana ili afukize uvumba kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba.
17 Thempupa Azariah chu mithahat lehmihang san cheh thempu hotoh akilhon nin lengpa chu ajui taovin
Azaria kuhani akiwa pamoja na makuhani wengine themanini wa Bwana wenye ujasiri wakamfuata huko ndani.
18 Ama suhtang nading chun hitin aphoh un ahi “Uzziah! nangin Pakai dinga gimnam twi nahal nading tha nanei poi, Aaron chilhah hitobang boldinga kisutheng thempu honbou abol diu ahi hiche munthenga konhin potdoh'in nangin Pakai Pathen doumah nabol jeh a hi a malsomna nachan jou louding ahitai” atiovin ahi.
Wakamkabili na kumwambia, “Siyo sawa kwako, Uzia, kumfukizia Bwana uvumba. Hiyo ni kazi ya makuhani, wazao wa Aroni, ambao wamewekwa wakfu ili kufukiza uvumba. Ondoka mahali patakatifu, kwa kuwa umekosa uaminifu nawe hutaheshimiwa na Bwana.”
19 Uzziah chun gimnamtwi halnachu achoijin houin sunga maicham panga chun adingin ahi. Ama thempu ho chunga ahung lunghang jahjeng phat chun tiphah khohtah chu adeh panga ahung chutaan ahi
Uzia, ambaye alikuwa na chetezo mkononi mwake tayari kufukiza uvumba, akakasirika. Alipokuwa anawaghadhibikia makuhani mbele ya madhabahu ya kufukizia uvumba katika Hekalu la Bwana, ukoma ukamtokea penye kipaji chake cha uso.
20 Azariah leh thempu dang hochun lengpa dehpang chu tijatah'in aveovin ahi, hijouchun amachu houinna kon in anodoh tho taovin ahi, ajeh chu Pakaiyin ama chu ajep ahi tai
Azaria kuhani mkuu pamoja na makuhani wengine wote walipomtazama wakaona kwamba alikuwa na ukoma penye kipaji chake cha uso wakaharakisha kumtoa nje. Naam, hata yeye mwenyewe alikuwa anatamani kuondoka kwa sababu Bwana alikuwa amempiga.
21 Uzziah lengpachu hiche phahna jehhin ahinkho lhung keijin dandung juiyin thenglou vin aumtaan ahi. Houin sung lelut kit thei louvin aleng hi na a akin tongthei talouvin a in'ah achuti umtaan achapa Jotham min ama khellin agam sunga vai ahomtaan ahi
Mfalme Uzia alikuwa na ukoma mpaka siku ya kufa kwake. Akatengwa katika nyumba ya pekee akiwa mwenye ukoma, naye akawa ametengwa kutoka Hekalu la Bwana. Yothamu mwanawe akawa msimamizi wa jumba la mfalme, pia akawaongoza watu wa nchi.
22 Uzziah avaihom sunga atoh ho jouse chu Amoz chapa themgao Isaiah in ajihlut soh keijin ahi
Matukio mengine ya utawala wa Uzia, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, yameandikwa na nabii Isaya mwana wa Amozi.
23 Uzziah athi phatnin lengte kivuina gamsunga avuijun ahinlah aphah jeh chun lengte kivui na lhan navang avui tapouve. Achapa Jotham min aleng mun chu alo taan ahi
Uzia akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa karibu nao katika shamba la kuzikia lililokuwa mali ya wafalme, kwa kuwa watu walisema, “Alikuwa na ukoma.” Yothamu mwanawe akawa mfalme baada yake.