< 2 Thusimbu 23 >
1 kum sagi channa a chun Jehoiada in adinmun akisuhdet nin sepai jakhat toh lamkai hochutoh akinoptouvin amahochu Jehoram chapa Azariah, Jehohanan chapa Ishmael, Obed chapa Azariah, Adaizah chapa Maaseiah chuleh Zikri chapa Elishaphat ahiove
Katika mwaka wa saba, Yehoyada akaonyesha nguvu zake. Alifanya agano na wakuu wa vikosi vya mamia: yaani Azaria mwana wa Yerohamu, Ishmaeli mwana wa Yehohanani, Azaria mwana wa Obedi, Maaseya mwana wa Adaya, na Elishafati mwana wa Zikri.
2 Amahohi Judah khopi ho jousea acheovin Levite phung nga phung upacheh Jerusalemma ahin puilutnun ahi
Wakazunguka katika Yuda yote na kukusanya Walawi na viongozi wa jamaa za Israeli kutoka miji yote. Walipofika Yerusalemu,
3 Amaho houin nachun akikhom mun lengpa chapa Joash chutoh kitepna ana semmun ahi. Jehoiada chun amaho kommah anaseijin: “Ilahuva hin lengpan athingel chapa chu aummin ahi! amahi Pakai thutep dung jui'a David chilhah ahi dung jui'a leng ichan sah diu ahi.
kusanyiko lote likafanya agano na mfalme katika Hekalu la Mungu. Yehoyada akawaambia, “Mwana wa mfalme atatawala, kama Bwana alivyoahidi kuhusu wazao wa Daudi.
4 Hitia hi iboldiu ahi, thempu holeh Levi techu choldonia akinnu tonga ahung tenguleh hopthumma hopkhatnin houin kelkot ho angadiu ahi,
Basi hivi ndivyo iwapasavyo kufanya: Theluthi yenu makuhani na Walawi ambao mnaingia zamu siku ya Sabato mtalinda milangoni,
5 Adang hopthumma hopkhat chun leng inpi angading, chuleh hopthumma hopkhatman kulpi bul kelkot phung nangadiu, chutengleh mipi abonchaova Pakai houin mai hong cha –a chu kikhom ding ahiove
theluthi yenu mtalinda jumba la kifalme, na theluthi nyingine mtalinda Lango la Msingi. Walinzi wengine wote mwe ndani ya nyua za Hekalu la Bwana.
6 Ahinlah Pathen insunga chu Pakai kinbol Levite toh thempu akiseiho tailou adang hunglut thei louding ahi, amahochu houinsung nga luttheidiu ahi ajeh chu ama hochu atheng ahiove, ahinla adanghose chun Pathen thupeh ngah a apamma dingdiu ahiove
Hakuna mtu yeyote ataingia katika Hekalu la Bwana isipokuwa makuhani na Walawi walioko kwenye zamu. Wao wanaweza kuingia kwa sababu ni watakatifu, lakini watu wengine wote itawapasa kulinda kile walichoamriwa na Bwana.
7 Chuleh Levitechun lengpa chu aum kimveldiu akhutnuvah manchah akichoi chehdiu ahin insung hunglut jouse chu athadiu ahi. nanghon lengpa ahung lut hihen apotdoh hijongleh nakilhon pidingu ahi
Walawi watajipanga kumzunguka mfalme, kila mtu akiwa na silaha zake mkononi. Mtu mwingine yeyote aingiaye Hekaluni lazima auawe. Kaeni karibu na mfalme popote aendapo.”
8 Hitichun Levite leh Juda ten thempupa Jehoiada thupeh bang bang chun achontaovin ahi. Lamkai khatcheh chun anoija hochu akipuijun cholngah nileh akinnuva akimanchah petnu hihenlang aonpetnu hijongleh aumpi jingun ahi, ajeh chu thempupa Jehoiada in sepai hochu alha ongpon ahi.
Walawi na watu wote wa Yuda wakafanya kama vile kuhani Yehoyada aliagiza. Kila mmoja akawachukua watu wake, wale waliokuwa wakiingia zamu siku ya Sabato na wale waliokuwa wakienda mapumziko, kwa sababu kuhani Yehoyada hakuruhusu kikosi chochote kiondoke.
9 Chuleh Jehoiada thempupa chun sepai aja ajalah a lamkai hochu Pathen houinna um ompho holeh tengcha hochu ahop pehin ahi
Kisha akawapa wakuu wa vikosi vya mamia mikuki na ngao kubwa na ndogo zilizokuwa za Mfalme Daudi, zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu.
10 Hitichun aman sepai hochu Houin kotmai vella chun chemjam dodohsan akichoisah in lengpa hoibitna dinga chun phasademmin pan alahsahin ahi
Akawapanga walinzi wote kumzunguka mfalme, kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi mwake, karibu na madhabahu na Hekalu, kuanzia upande wa kusini hadi upande wa kaskazini mwa Hekalu.
11 Hijou chun Jehoiada in Joash chu ahin puidoh in aluchung nga lallukhuh akhuhpeh in lengte kivaihom na danbuchu apen hiti chun leng achansahtan ahi. Thempupa Jehoiada leh achaten Joash chu thao anu vin chuleh mijouse chun “Lengpa hingsothen” tin asammun ahi
Yehoyada na wanawe wakamtoa Yoashi mwana wa mfalme nje na kumvika taji. Wakampa nakala ya agano na kumtangaza kuwa mfalme. Wakamtia mafuta na kupaza sauti, wakisema, “Mfalme aishi maisha marefu!”
12 Athaliah chun lengpa thangvahna a kisam mipi Ogin husan chu ajah phatnin mipi dimsetna akikhopnao houinna chun ahung lhailutnin ahi.
Athalia aliposikia kelele za watu wakikimbia na kumsifu mfalme, akawaendea watu katika Hekalu la Bwana.
13 Amanun agahven ahileh lengthah pachu Houin lutna khombul panga sepai lamkai holeh sumkon muthon ana umkimvel chu amun ahi. Ama lengchanna –a alopnaoleh akipapinao ogin chuleh semjang saipumma lasaholeh sumkon mutho ogin chu akithong jeju jengin ahi, hichun amanun asangkhol abot eh jengin, hiche hi “Lengmun chuna ahi, Lengmun chuna ahi” tin asamtaan ahi
Athalia akaangalia, tazama alikuwepo mfalme akiwa amesimama karibu na nguzo yake kwenye ingilio. Maafisa na wapiga tarumbeta walikuwa kando ya mfalme, nao watu wote wa nchi walikuwa wanashangilia na kupiga tarumbeta na waimbaji wakiwa na vyombo vya uimbaji, walikuwa wakiongoza nyimbo za sifa. Ndipo Athalia akararua mavazi yake na kupiga kelele, akisema, “Uhaini! Uhaini!”
14 Hichun Jehoiada thempupan amanuchu Houin sunga akitha ding chu adeipon hijeh chun sepai lamkai hochu aseipeh in “Amanu chu polanga kaidoh unlang koi hijongleh ama chu huhdoh go a umleh that jengun ati”
Kuhani Yehoyada akawatuma majemadari wa vikosi vya mamia, waliokuwa viongozi wa jeshi, na kuwaambia: “Mleteni nje kati ya safu, na mkamuue kwa upanga yeyote anayemfuata.” Kwa kuwa kuhani alikuwa amesema, “Msimuulie ndani ya Hekalu la Bwana.”
15 Amahon amanuchu aman nun leng inpia apuijun sakol kelkot komma chun athat taovin ahi
Kwa hiyo wakamkamata alipofika kwenye ingilio la Lango la Farasi katika viwanja vya jumba la mfalme wakamuulia hapo.
16 Jehoiada thempupan Joash lengpa leh mipite chu akoukhomin Pakai mite ahijing nadiuvin kitepnakhat anei pitaan ahi
Kisha Yehoyada akafanya agano kwamba yeye na watu wote na mfalme watakuwa watu wa Bwana.
17 Hijouchun Baal houinnah acheovin ajeplhu gamtaovin ahi. Amahon semthu Pathen holeh amaichamho jong avochip gamun Baal thempupa Mattan jong amaicham maijachun athat taovin ahi
Kisha watu wote wakaenda kwenye hekalu la Baali na kulibomoa. Wakavunjavunja madhabahu pamoja na sanamu na kumuua Matani kuhani wa Baali mbele ya hayo madhabahu.
18 Jehoiada in thempu holeh Levi techu Pakai houin na natoh na –a mopohna apen ahi. Amahohin Leng David nin angansenao kinhochu atohdiu Mose daan semtoh kitoh a Pakaiyin pumgo thilto gimnamtwi halnamna kin jong atohdiu ahi. amahohin tumging tothon golnop bolnajong mopohna alahdiu ahi
Kisha Yehoyada akaweka uangalizi wa Hekalu la Bwana mikononi mwa makuhani, waliokuwa Walawi, ambao Mfalme Daudi alikuwa amewagawa ili wahudumu hekaluni kwa ajili ya kutoa sadaka za kuteketezwa za Bwana kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose, kwa kushangilia na kuimba kama Daudi alivyokuwa ameagiza.
19 Jehoiada in houin sunga hi miboh ho ahung lut louna ding avesuidingin houin kelkotna angahding akoiyin ahi
Pia akawaweka mabawabu kwenye malango ya Hekalu la Bwana ili kwamba kwa vyovyote asije akaingia mtu yeyote aliye najisi.
20 Hitichun Jehoiada in sepai lamkaiho leh gamsunga mithupiho, gamvaipoholeh mihonpi ahinpuijin, chuin houinna kon in lengpachu ahinpuidohin kelkkot sahlang pa achun alut un leng in chu ajonlutnin, lengpa chu aleng gam laltouna a atousah taovin ahi
Akawachukua majemadari wa mamia, watu waheshimiwa, viongozi wa watu pamoja na watu wote wa nchi na kumteremsha mfalme kutoka Hekalu la Bwana. Wakaingia kwenye jumba la mfalme kupitia Lango la Juu na kumkalisha mfalme kwenye kiti cha enzi,
21 Hichun gamsung mipite chu kipana leh thanop na – a adimsetnun chuleh khopi jong alung mong mongtaan ahi
nao watu wote wa nchi wakafurahi. Mji ukatulia kwa sababu Athalia alikuwa ameuawa kwa upanga.