< 1 Samuel 17 >

1 Judah gamsung Socoh muna chun Philistine mite galsat dingin akikhom’un, chule Socoh le Azekah kikah’a Ephes-dammim’a chun ngahmun asem tauvin ahi.
Wakati huu Wafilisti wakakusanya majeshi yao kwa ajili ya vita, nao wakakusanyika huko Soko katika Yuda. Wakapiga kambi huko Efes-Damimu, kati ya Soko na Azeka.
2 Chuin Saul le Israelte jong akikhom’un, Philistine te dounan Elah phaicham panga ngahmun akisem’un ahi.
Sauli na Waisraeli wakakusanyika na kupiga kambi katika Bonde la Ela na kupanga jeshi ili kupigana vita na Wafilisti.
3 Philistine techu lhangkhat ah akigol’un chule Israel te jong chu lhangkhat ah akigol’un chule akikah uva phaicham khat in akhentan un ahi.
Wafilisti wakawa katika kilima kimoja na Waisraeli katika kilima kingine, hilo bonde likiwa kati yao.
4 Chule Philistine te mihat tah Gath khopia akona hungkon, amin Goliath kitipa chun Israelte satding in Philistine te ngahmun akonin ahung potdoh'in ahi. Amachu tong gup le khap khat jen in asangin ahi.
Shujaa aliyeitwa Goliathi, aliyetoka Gathi, akajitokeza kutoka kambi ya Wafilisti. Alikuwa na urefu dhiraa sita na shibiri moja.
5 Chule aman sum-eng lukhuh akhuh in, sum-eng a kisem ompho shekel sang nga jen agih aki-ah in ahi.
Alikuwa na chapeo ya shaba kichwani mwake, na alivaa dirii ya shaba kifuani mwake yenye uzito wa shekeli elfu tano.
6 Akengte ni jong sum-eng’a kitomjol ahin, chule alengkouva ama sum-eng tengcha akipoh chu kitungdoh peh ahi.
Miguuni mwake alivaa mabamba ya shaba, na alikuwa na mkuki wa shaba mgongoni mwake.
7 Atengcha lung tumbi tejen ahin, atengpeh jong thih jeng, gihdan chu shekel jagup’a gih ahin, apho chu mikhat poh ahi.
Mpini wa huo mkuki ulikuwa kama mti wa mfumaji, na ncha ya chuma yake ilikuwa na uzito wa shekeli mia sita. Mbeba ngao wake alitangulia mbele yake.
8 Goliath ading in Israel galsat miho jah’a ahin samin, “Ipi dinga galsat dinga hung kigola nahiuvem, keima Philistine mihatpa kahin, nangho Saul sohte mai mai nahiuve, ei kisatpi ding mikhat hung kilheng doh un,” atin ahi.
Goliathi alisimama na kuwapigia kelele majeshi ya Israeli, akisema, “Kwa nini mmetoka kupanga vita? Je, mimi si Mfilisti, na ninyi ni watumishi wa Sauli? Chagueni mtu na anishukie mimi.
9 “Aman keima eitha le nasoh’u kahi diu, ken ama katha le keiho soh nahi diu ahi,” ati.
Kama anaweza kupigana nami na kuniua, tutakuwa chini yenu; lakini kama nikimshinda na kumuua, ninyi mtakuwa chini yetu na mtatutumikia.”
10 “Tunia hi Israel galsatho kachou nahiuve, kakisatpi ding pachu hin soldoh’un,” ati.
Kisha yule Mfilisti akasema, “Siku hii ya leo nayatukana majeshi ya Israeli! Nipeni mtu tupigane.”
11 Chuin Saul le Israel mite jousen Plilistine mipa thusei ajah phat’un, akichalheh jeng tauvin ahi.
Kwa kusikia maneno ya Wafilisti, Sauli na Waisraeli wote wakafadhaika na kuogopa.
12 David kitipa chu Judah gam Bethlehem khopia Ephrah mi Jesse chapa ahin, hiche lai chun Jesse chu ateh lheh jeng tan chule aman chapa get jen aneiyin ahi.
Basi Daudi alikuwa mwana wa Mwefrathi jina lake Yese aliyekuwa ametoka Bethlehemu ya Yuda. Yese alikuwa na wana wanane, naye wakati wa Sauli alikuwa mzee tena wa umri mkubwa.
13 Jesse chapa alen thumho, chu Eliab, Abindab, chule Shimea hochu Philistine te sat dia Saul lengpa sepai a pang ahiuve.
Wana wakubwa watatu wa Yese walikuwa wamefuatana na Sauli vitani: Mzaliwa wa kwanza alikuwa Eliabu, wa pili Abinadabu, na wa tatu Shama.
14 David chu achate lah’a aneopen ahi. David ute thum hochu Saul sepaiho toh khom’a ahiuve.
Daudi ndiye alikuwa mdogo wa wote. Hao wakubwa watatu wakamfuata Sauli,
15 Ahin David chu Saul inpia kona apa kelngoi chin kithopi dia Bethlehem ah hung kile kitji jia ahi.
lakini Daudi alikuwa akienda kwa Sauli na kurudi ili kuchunga kondoo wa baba yake huko Bethlehemu.
16 Ni somli sungin jingkah, nilhah seh leh Philitine mihatpan Israel sepai ho ahin naiyin achou jing in ahi.
Kwa siku arobaini huyo Mfilisti alikuwa akija mbele kila siku asubuhi na jioni na kujionyesha.
17 Nikhat Jesse in David jah’ah, “Hiche pucha-a chang kanpoh hile changlhah lhon som hi choijin lang gangtah in naute gapen.
Wakati huo Yese akamwambia mwanawe Daudi, “Chukua hii efa ya bisi na hii mikate kumi kwa ajili ya ndugu zako uwapelekee upesi kambini mwao.
18 Chule hiche bongnoiha-a kisem lhon som hi sepaiho lamkaipa pen. Na-ute iti nauvem gavenlang, thu nahin nungpoh kit ding ahi,” tin anasollin ahi.
Chukua pamoja na hizi jibini kumi kwa jemadari wa kikosi chao. Ujue hali ya ndugu zako na uniletee taarifa za uhakika kutoka kwao.
19 David uteho chu Saul to umkhom'a ahiuvin, Israel sepaiho chu Elah phaichama gal mun’ah um ahiuve.
Wao wako pamoja na Sauli na watu wote wa Israeli huko kwenye Bonde la Ela, wakipigana na Wafilisti.”
20 Chuin David in akelngoiho chu avetup din mi khat angansen, jingkah matah in apan athupeh bang in thilho chu apon, achen ahile sepaiho galsat dinga ngahmun dalha dinga akigotuva a-ao laitah’un ngahmun chu agalhungin ahi.
Asubuhi na mapema Daudi akaondoka, akaliacha kundi la kondoo pamoja na mchungaji, akapakia vitu vile na kuondoka, kama vile Yese alivyokuwa amemwagiza. Akafika kambini wakati jeshi lilikuwa likitoka kwenda kwenye sehemu yake ya kupigania, huku wakipiga kelele za vita.
21 Israelte le Philistine sepaiho galkisat dia kidinte-a kimaitoa akigol laitah’un,
Israeli na Wafilisti walikuwa wakipanga safu zao wakitazamana.
22 David in thilkeo chingtup pa henga athilpoh ho chu adalhan, gangtah’in a-ute ho chibai agaboltai.
Daudi akaacha vile vitu vyake kwa mtunza vifaa, akakimbilia katika safu za vita na kuwasalimu ndugu zake.
23 Aman a-uteho akihoulimpi laitah in, Gath mi Philistine mihatpa chu Philistine sepai ho lah’a kon in ahung potdoh'in ana seingaiji bang in asamin, Israel mite chu ahin choukit tan ahile, hichu David in ajatan ahi.
Alipokuwa akisema nao, Goliathi, yule Mfilisti shujaa kutoka Gathi, akajitokeza mbele ya safu zake na kupiga ile kelele yake ya kawaida ya matukano, naye Daudi akayasikia.
24 Chuin Israel sepaiten hiche mipa chu amu phat’un akicha behseh jengun ajam tauvin ahi.
Waisraeli walipomwona yule mtu, wote wakamkimbia kwa woga mkuu.
25 Hichun alah uva mikhat in David jah’a, “Hiche mihatpa chu namu em? Aniseh leh hitia khu hung potdoh’a Israel sepaite achou chou jin ahi, koihile ama thatpen pen khu lengpan kipaman lentah apeh ding, achanu khat jong aji ding’a apeh ding, chule Israel ten kai peh dingdol a kon in jong onthol sah ding ahi,” ati.
Basi Waisraeli walikuwa wakisema, “Je, mnaona jinsi mtu huyu anavyoendelea kujitokeza. Hujitokeza ili kutukana Israeli. Mfalme atatoa utajiri mwingi kwa yule mtu atakayemuua. Pia atamwoza binti yake na atasamehe jamaa ya baba yake kulipa kodi katika Israeli.”
26 David in akimvella ding Israel sepai ho jah’ah, “Hiche cheptanlou Philistine mahatpa that’a, Israel mite avettomna kona huhdoh mi chu ipi amu ding ham? Ipi hile iti hiche cheptanlou Philistine pan hingjing Pathen sepaite ajumso ding ham?” ati.
Daudi akauliza watu waliokuwa wamesimama karibu naye, “Je, atafanyiwa nini mtu atakayemuua huyu Mfilisti na kuondoa aibu hii katika Israeli? Ni nani huyu Mfilisti asiyetahiriwa hata atukane majeshi ya Mungu aliye hai?”
27 Chuin miho chun adonbut un, “Henge hiche mipa that pen pen chu kipaman akisei chu peh ding ahi,” atiuve.
Wakarudia yale yaliyokuwa yamesemwa na kumwambia kuwa, “Hili ndilo atakalotendewa mtu yule atakayemuua.”
28 Ahinlah David uteho lah’a alenpen Eliab chun David thusei ajahdoh phat’in alung ahang in, “Hichea hi ipi nahung bolle ham? Na kelngoi hon hochu ipi itihen nati ham? Nakiletsahna le na jonchih na chu kahe nai, hichea kidounaho venom mai maija hunga nahibouve,” ati.
Eliabu nduguye mkubwa Daudi alipomsikia akizungumza na watu hasira ikawaka juu yake akamuuliza, “Kwa nini umeteremka kuja hapa? Nao wale kondoo wachache kule nyikani umewaacha na nani? Ninajua jinsi ulivyo na kiburi na jinsi moyo wako ulivyo mwovu; umekuja hapa kutazama vita tu.”
29 Hichun David in, “Ken ipi kabol em? Thudoh kagah nei mai mai ahi,” tin adonbut in ahi.
Daudi akasema, “Sasa nimefanya nini? Je, siwezi hata kuongea.”
30 Chuin amahoa konin adangho langah akihei kit in athudoh mama adoh’a ahile, amahon jong aseima ma asei kit un ahi.
Daudi akamgeukia mtu mwingine na kumuuliza jambo lilo hilo, nao watu wakamjibu vilevile kama mwanzo.
31 David thudoh chu Saul lengpa kom agalhut un ahile Saul lengpan jong aheng’a ahin pui diuvin thu ape tan ahi.
Lile Daudi alilosema likasikiwa na kuelezwa kwa Sauli, naye Sauli akatuma aitwe.
32 “Hiche Philistine mipa chunga khun boi tahih’un, kache ding kaga kimaitopi ding ahi,” tin David in Saul jah’a aseiyin ahi.
Daudi akamwambia Sauli, “Mtu yeyote asife moyo kwa habari ya huyu Mfilisti; mtumishi wako atakwenda kupigana naye.”
33 Saul in, “Angol nahim! nangman hiche Philistine mihatpa nasatna najo nading lampi aum theipoi, nangma chapang chabou nahin, ama akhangdon laiya kipatna galsat mi ahi,” ati.
Sauli akamjibu Daudi, “Wewe hutaweza kwenda kupigana dhidi ya huyu Mfilisti; wewe ni kijana tu, naye amekuwa mtu wa vita tangu ujana wake.”
34 Ahinlah David in, “Kapa kelngoi hole kelcha ho jong kana vetkol ahin, nasohpa hin apa kelngoi anachin na’a chun keipi bahkai le vompi ahunga kelnou ho ahung lhohmang ding agot tengle,
Lakini Daudi akamwambia Sauli, “Mtumishi wako amekuwa akichunga kondoo wa baba yake. Wakati simba au dubu alikuja na kuchukua kondoo kutoka kundi,
35 Anung kadellin, kakidalpin, akamsung’a konin kahuhdohjin ahi, chule keima thadia eigot tengleh, akha ah kaman in kathat jitai.
nilifuatia, nikampiga na nikampokonya kondoo kwenye kinywa chake. Aliponigeukia, nilimkamata nywele zake, nikampiga na kumuua.
36 Keipi le vompi ani nia hitia chu kabolji ahin chule tua jong Philistine cheptan loupa jong chutia chu kabol ding ahi, ajeh chu aman hing jing Pathen sepai ho ajumso jeh’a hitia chu bolding ahi.
Mtumishi wako ameshaua simba na dubu pia; huyu Mfilisti asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wa hao, kwa sababu ameyatukana majeshi ya Mungu aliye hai.
37 Pakaiyin keipi bahkai le vompi khutphanga kona eihuhdoh pa chun tunia jong hiche Philistine mihatpa a kona eihuhdoh tei ding ahi,” atin boltei agoi. Hichun Saul in achaina a lunggel lhahna aneiyin, “Aphai nakigot bang chun boltan chule Pakaiyin naumpi jingta hen,” ati.
Bwana ambaye aliniokoa toka katika makucha ya simba na makucha ya dubu ataniokoa kutoka mikono ya huyu Mfilisti.” Sauli akamwambia Daudi, “Nenda, naye Bwana na awe pamoja nawe.”
38 Chuin Saul in David agalvon apen, alukhuh sum-eng a kisem akhuhpeh in, thih sangkhol a-ahpeh tan ahi.
Ndipo Sauli akamvika Daudi silaha zake mwenyewe za vita. Akamvika dirii na chapeo ya shaba kichwani mwake.
39 Hichun David in agalvon chunga chun achemjam ako’in, kal khat kal agah son le galvon ho akivon khahlou jeh in, achethei tapon ahi. Hijeh chun aman Saul jah’a, “Hicheho pumin chethei ponge, ajeh chu hicheho hi kamang theipoi,” atin, asut lhatai.
Daudi akajifunga upanga juu ya hayo mavazi na kujaribu kutembea kwa sababu alikuwa hana uzoefu navyo. Daudi akamwambia Sauli, “Siwezi kwenda nikiwa nimevaa hivi, kwa sababu sina uzoefu navyo.” Hivyo akavivua.
40 Hichun David in vadung songchang jolsel chang nga akilopan, akelngoi chinna sakhao neovah akikon, chuin akelngoi chinna tenggol le sailungchang kapna gophel akichoijin, Philistine mihatpa umna phaicham ajontai.
Kisha akachukua fimbo yake mkononi, akachagua mawe laini matano kutoka kwenye kijito, akayaweka kwenye kifuko ndani ya mfuko wake wa kichungaji, akiwa na kombeo yake mkononi mwake, akamkaribia yule Mfilisti.
41 Goliath jong ahung potdoh'in David lam ahin jontai chule agalvon popa chu ahung masan ahi.
Wakati ule ule, yule Mfilisti, akiwa na mbeba ngao wake mbele yake, akaendelea kujongea karibu na Daudi.
42 Goliath in David chu phatah a avettoh phat’in, chapang melhoi cha bou ahinah laijeh in, asit behseh jeh in alung ahang tai.
Mfilisti akamwangalia Daudi kote na kumwona kuwa ni kijana tu, mwekundu na mzuri wa kupendeza, naye akamdharau.
43 David jah’a lunghang tah in, “Keima uicha kahim? Mol kichoija kahenga hung nahim?” ati. Hichun Philistine mipa chun, apathen ho min pan in David chu agaosap tai.
Akamwambia Daudi, “Je, mimi ni mbwa, hata unanijia na fimbo?” Yule Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake.
44 Goliath in David chu achouvin, “Hilam ah hungin, keiman natahsa chu vachate le gamsa te kapeh ding ahi,” ati ahi.
Tena Mfilisti akamwambia, “Njoo hapa, nami nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni nyama yako.”
45 David in Philistine mipa chu adonbut in, “Nangma chemjamle tengcha choiya hung nahin, Ahinlah keima vang van gam sepai galsatte Pakai mina hung kahi.
Daudi akamwambia yule Mfilisti. “Wewe unanijia na upanga, mkuki na fumo, lakini mimi ninakujia kwa jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa majeshi ya Israeli, ambaye wewe umemtukana.
46 Tunia hi Pakaiyin najoding, keiman nang katha-a nalu katan ding, natahsa thisa chu vachate le gamsate kapeh ding chule leiset pumpin Israel Pathen khat aume ti ahet diu ahi,” ati.
Siku hii leo Bwana atakutia mkononi mwangu, nami nitakupiga na kukukata kichwa chako. Leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya jeshi la Wafilisti, nayo dunia yote itajua kuwa yuko Mungu katika Israeli.
47 “Chule hichea hung kikhom jousen Pakaiyin chemjam le tengchan ahuhhingpoi ti ahet dingu ahi. Ajeh chu galsat hi Pakaiya ahin, aman nangho kakhutna eipeh doh diu ahitai,” ati.
Wale wote waliokusanyika hapa watajua kuwa Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; kwa kuwa vita ni vya Bwana, naye atawatia wote mikononi mwetu.”
48 Goliath ahung kipatdoh a David henglam ahin jot phat in, David chu kintah in Philistine mihatpa toh kisuto ding in alhaisuh tan ahi.
Yule Mfilisti aliposogea karibu ili kumshambulia, Daudi akaenda mbio kuelekea safu ya vita kukutana naye.
49 David in akhut in asakhao sung asoh in, song chang khat aladoh in, ah-songse’a chu asea ahile, Philistine mipa chalpang ah achun, songchang chu alut in, Goliath tol-lhang ah alhutan ahi.
Daudi akatia mkono wake mfukoni na kuchukua jiwe, akalirusha kwa kombeo, nalo likampiga yule Mfilisti kwenye paji la uso. Lile jiwe likaingia kipajini mwa uso, akaanguka chini kifudifudi.
50 Chuti chun David in chemjam pang louhellin, songchang khatseh le ah-songse in Goliath ajoutan ahi.
Basi Daudi akamshinda huyo Mfilisti kwa kombeo na jiwe; bila kuwa na upanga mikononi mwake akampiga huyo Mfilisti na kumuua.
51 Chuin David in adel lut paiyin, Goliath chemjam chu asatdoh in, ama chemjam ma ma chun alol atantan ahi. Chuin Philistine mipiten ami hatpa’u athi amu phat un, akinung heijun ajam tauvin ahi.
Daudi akakimbia na kusimama juu yake. Akaushika upanga wa huyo Mfilisti na kuuvuta toka kwenye ala yake. Baada ya kumuua, akakata kichwa chake kwa ule upanga. Wafilisti walipoona kuwa shujaa wao amekufa, wakageuka na kukimbia.
52 Chuin Israelte le Judah miho akipat’un, a-aovun, phaicham le Ekron kotpi aphah kah seuvin Philistine mite nung adel’un ahi. Chule Philistine mipi ho chu Shaariam lam lhon lhungin thilong akijam thang’un, Gath le Ekron changeijin athilong u chu alum thang sohkei jenginn ahi.
Ndipo watu wa Israeli na Yuda wakainuka kwenda mbele wakipiga kelele na kufuatia Wafilisti mpaka kwenye ingilio la Gathi kwenye malango ya Ekroni. Maiti zao zilitawanyika kando ya barabara ya Shaaraimu hadi Gathi na Ekroni.
53 Chuin Israel chaten Philistine mite anungdel uva kon in ahung kinung leuvin, angahun hou chu asumang’un achom tauvin ahi.
Waisraeli waliporudi kutoka kuwafukuza Wafilisti, waliteka nyara kutoka kambi yao.
54 Chuin David in Philistine mihatpa luchang chu alan Jerusalem ah ahin potai; ahin galvon vang apon in’ah akoitai.
Daudi akachukua kichwa cha yule Mfilisti na kukileta Yerusalemu, naye akaweka silaha za huyo Mfilisti katika hema lake mwenyewe.
55 David Philistine pa satdinga akon doh chun Saul in agalvon popa Abner jah’ah, “Hiche gollhang pa khu koicha ham? tin adongin ahile Abner in jong, “Atahbah in kahepoi,” tin anadonbut e.
Sauli alipomwona Daudi anakwenda kukabiliana na huyo Mfilisti, alimwambia Abneri, jemadari wa jeshi, “Abneri, yule kijana ni mwana wa nani?” Abneri akajibu, “Hakika kama uishivyo, ee mfalme, mimi sifahamu.”
56 Hichun lengpan jong, “Aphai, koiham hinkhol chen’in,” ati.
Mfalme akasema, “Uliza huyu kijana ni mwana wa nani.”
57 David in Goliath ahintha jouva ahung lhun in, Abner in Philistine mihatpa luchang chu Saul komah ahin lhuttan ahi.
Mara Daudi aliporudi kutoka kumuua huyo Mfilisti, Abneri akamchukua na kumleta mbele ya Sauli. Daudi alikuwa bado anakishikilia kichwa cha yule Mfilisti.
58 Hichun Saul in, “Gollhang, napa koiham neisei peh in,” atin ahile David in adonbut in, “Kapa min Jesse ahin, Bethlehem a um kahiuve,” ati.
Sauli akamuuliza, “Kijana, wewe ni mwana wa nani?” Daudi akasema, “Mimi ni mwana wa mtumishi wako Yese wa Bethlehemu.”

< 1 Samuel 17 >