< 2 Khokhuen 32 >

1 He oltak olka hnukah tah Assyria manghai Sennacherib tah cet tih Judah la pawk. Te vaengah khopuei vong cak rhoek te a rhaeh thil tih amah hut la ka muk eh a ti.
Baada ya yale yote aliyokuwa amefanya Hezekia kwa uaminifu mkubwa, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaja na kuvamia Yuda. Akaizunguka miji yenye ngome kwa jeshi, akifikiri kuiteka iwe yake.
2 A mikhmuh ah caemtloek ham Jerusalem la Sennacherib a pawk te Hezekiah loh a hmuh.
Hezekia alipoona kuwa Senakeribu amekuja na kwamba alikusudia kufanya vita juu ya Yerusalemu,
3 Te dongah a mangpa rhoek neh a hlangrhalh rhoek taengah khopuei rhamvoel kah tuiphuet tui te mak hamla a uen tih a bom uh.
akafanya shauri na maafisa wake na mashujaa wake juu ya kuzuia maji kutoka chemchemi zilizo nje ya mji, nao wakamsaidia.
4 Te dongah pilnam te muep tingtun tih tuisih boeih neh khohmuen khui la aka long soklong khaw a mak uh. Te vaengah, “Balae tih Assyria manghai rhoek ha pawk uh vetih tui muep a hmuh uh mai eh?” a ti uh.
Umati mkubwa wa watu ukakusanyika na kuzuia chemchemi zote na vijito vilivyotiririka katika nchi yote, wakisema: “Kwa nini wafalme wa Ashuru waje na kukuta maji tele?”
5 Te phoeiah thaa a huel uh tih vongtung aka puut boeih te a biing uh. Rhaltoengim so neh a tloe vongtung rhamvoel hil a hil tih David khopuei kah vaikhap te a moem. Pumcumnah neh photling khaw a cungkuem la a saii.
Hezekia akafanya kazi kwa bidii kukarabati sehemu zote zilizokuwa zimebomoka za ukuta na kujenga minara juu yake. Akajenga ukuta mwingine nje ya ule uliokuwepo na kuimarisha Milo katika Mji wa Daudi. Akatengeneza pia silaha nyingi na ngao.
6 Pilnam soah caemtloek mangpa rhoek a khueh tih amih te khopuei vongka toltung ah amah taengla a coi. Te vaengah amih thinko ah a thui pah tih,
Akaweka maafisa wa jeshi juu ya watu, wakawakutanisha mbele yake katika uwanja kwenye lango la mji, naye akawatia moyo kwa maneno haya:
7 Thaahuel uh lamtah namning uh, Assyria manghai mikhmuh ah rhih uh boeh, rhihyawp uh boeh. Te lamloh anih taengah hlangping loh cungkuem mai cakhaw anih taengkah lakah mamih taengkah he ping ngai.
“Kuweni hodari na wenye moyo mkuu. Msiogope, msifadhaike wala msikate tamaa kwa sababu ya mfalme wa Ashuru na hili jeshi kubwa lililo pamoja naye, kwa kuwa aliye pamoja nasi ni mkuu kuliko aliye pamoja naye.
8 Anih taengah pumsa kah bantha ni a om. Mamih taengah tah mamih kah Pathen BOEIPA he mamih aka bom ham neh mamih kah caemtloeknah te aka vathoh puei la om coeng,” a ti nah. Te dongah Judah manghai Hezekiah ol lamloh pilnam khaw duel uh thae.
Kwake uko mkono wa mwili tu, bali kwetu yuko Bwana Mungu wetu kutusaidia na kutupigania vita vyetu.” Nao watu wakatiwa moyo kutokana na maneno aliyowaambia Hezekia mfalme wa Yuda.
9 A hnukah tah Assyria manghai Sennacherib loh a sal rhoek te Jerusalem la a tueih. Te vaengah anih te amah taengkah a khohung boeih neh Lakhish imdan ah Judah manghai Hezekiah neh Jerusalem kah Judah boeih te a pai thil.
Hatimaye Senakeribu mfalme wa Ashuru na majeshi yake yote walipokuwa wameuzunguka Lakishi, akawatuma maafisa wake kwenda Yerusalemu wakiwa na ujumbe huu kwa Hezekia mfalme wa Yuda, na kwa watu wote wa Yuda waliokuwako humo, kusema:
10 Te vaengah, “Assyria manghai Sennacherib loh he ni a thui. Me dongah nim na pangtung uh tih Jerusalem kah vongup ah kho na sak uh?
“Hili ndilo asemalo Senakeribu mfalme wa Ashuru: Je, mmeweka tumaini lenu wapi, hata mnaendelea kukaa katika Yerusalemu, hali mmezungukwa na jeshi?
11 Hezekiah loh nangmih te m'vueh moenih a? Khokha neh tuihalh ah duek sak hamla nangmih m'voeih tih, 'Mamih kah Pathen BOEIPA loh, mamih he Assyria manghai kut lamkah n'huul bitni,’ a ti.
Hezekia asemapo, ‘Bwana Mungu wetu atatuokoa kutokana na mkono wa mfalme wa Ashuru,’ anawapotosha ninyi, naye atawaacha mfe kwa njaa na kiu.
12 A hmuensang neh a hmueihtuk aka khoe khaw Hezekiah amah moenih a? Te vaengah Judah taeng neh Jerusalem taengah a uen tih, 'Hmueihtuk pakhat hmai bueng ah ni na bakop uh vetih te soah ni na phum eh?,’ a ti.
Je, si Hezekia mwenyewe aliyeondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake, akiwaambia Yuda wa Yerusalemu, ‘Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu moja na kuteketeza dhabihu juu yake’?
13 Kai neh a pa loh khohmuen pilnam boeih taengah ka saii te na ming pawt nim? Khohmuen namtom pathen rhoek loh, a khohmuen te kai kut lamloh a huul ham coeng rhoe coeng ve nim?
“Je, hamjui yale mimi na baba zangu tuliyoyafanya kwa mataifa yote ya nchi zingine? Je, miungu ya mataifa hayo iliweza kuokoa nchi zao kutoka mkononi mwangu?
14 Kai napa rhoek loh a thup namtom pathen rhoek boeih soah unim aka om? A pilnam te ka kut lamloh huul hamla unim aka coeng thai eh? Kai kut lamloh nangmih huul hamla nangmih kah Pathen te coeng thai aya?
Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya mataifa haya ambayo baba zangu waliyaangamiza ameweza kuwaokoa watu wake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Mungu wenu kuwaokoa mkononi mwangu?
15 Tahae ah nangmih te Hezekiah loh n'rhaithi boel saeh lamtah he tlam he nangmih te m'vuet boel saeh. Anih te tangnah uh boeh. Namtom neh ram boeih pathen boeih long pataeng ka kut lamkah neh a pa rhoek kut lamloh a pilnam a huul ham a noeng moenih. Nangmih kah Pathen loh nangmih te ka kut lamloh n'huul mahpawh,” a ti nah.
Sasa basi, msikubali Hezekia awadanganye na kuwapotosha namna hii. Msimwamini, kwa kuwa hakuna mungu wa taifa lolote wala wa ufalme wowote aliyeweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu au mkononi mwa baba zangu. Sembuse huyo mungu wenu atawaokoaje kutoka mkononi mwangu!”
16 A sal rhoek khaw Pathen BOEIPA taeng neh BOEIPA kah sal Hezekiah taengah cal uh pueng.
Maafisa wa Senakeribu wakaendelea kunena dhidi ya Bwana aliye Mungu na dhidi ya mtumishi wake Hezekia.
17 Israel Pathen BOEIPA te veet hamla cabu a daek uh tih a taengah cal uh. Diklai namtom kah pathen rhoek loh ka kut lamkah a pilnam a huul pawt bangla, Hezekiah kah Pathen loh a pilnam te ka kut lamkah huul mahpawh,” a ti uh.
Mfalme pia aliandika barua akimtukana Bwana, Mungu wa Israeli na kusema haya dhidi yake: “Kama vile miungu ya mataifa ya nchi nyingine ilivyoshindwa kuwaokoa watu wao mkononi mwangu, vivyo hivyo Mungu wa Hezekia hataweza kuwaokoa watu wake kutoka mkononi mwangu.”
18 Amih hih ham neh amih te let sak ham, khopuei te duep hamla vongtung sokah Jerusalem pilnam te Judah ol neh a len la a doek uh.
Kisha wakawaita kwa Kiebrania watu wa Yerusalemu waliokuwa juu ya ukuta ili kuwatisha na kuwatia hofu ili waweze kuuteka mji.
19 Jerusalem kah Pathen te hlang kut dongkah bisai, diklai pilnam kah pathen kawng bangla a thui uh.
Wakanena juu ya Mungu wa Yerusalemu kama vile walivyonena juu ya miungu ya mataifa mengine ya dunia ambayo ni kazi ya mikono ya wanadamu.
20 He kongah manghai Hezekiah neh tonghma Amoz capa Isaiah tah thangthui tih vaan a khue rhoi.
Mfalme Hezekia na nabii Isaya mwana wa Amozi wakalilia mbingu katika maombi kuhusu jambo hili.
21 Te dongah BOEIPA loh puencawn a tueih tih Assyria manghai rhaehhmuen kah tatthai hlangrhalh boeih neh mangpa rhaengsang rhoek te a thup pah. Te dongah amah khohmuen la maelhmai yahpohnah neh mael tih amah pathen im la pawk. Te vaengah a cakhueh neh a ko khui lamkah a cakhueh loh anih te cunghang dongah hnap cungku uh.
Naye Bwana akamtuma malaika ambaye aliangamiza wanajeshi wote, na viongozi na maafisa katika kambi ya mfalme wa Ashuru. Kwa hiyo, mfalme wa Ashuru akarudi nchini mwake kwa aibu. Naye alipokwenda katika hekalu la mungu wake, baadhi ya watoto wake wakamuua kwa upanga.
22 BOEIPA loh Hezekiah neh Jerusalem khosa rhoek te Assyria manghai Sennacherib kut lamkah khaw, a cungkuem kut lamkah khaw a khang tangloeng tih a kaepvai ah amih te a khool.
Hivyo Bwana akamwokoa Hezekia na watu wa Yerusalemu kutoka mkononi mwa Senakeribu mfalme wa Ashuru na kutoka mikononi mwa wengine wote. Bwana akawastarehesha kila upande.
23 Te dongah BOEIPA ham khocang neh Judah manghai Hezekiah ham kawnthen khaw Jerusalem la muep a pawk pah. Te dongah a hnuk lamloh namtom cungkuem kah mikhmuh ah a phueih.
Watu wengi wakaleta sadaka Yerusalemu kwa ajili ya Bwana na zawadi za thamani kwa ajili ya Hezekia mfalme wa Yuda. Tangu hapo na kuendelea, Hezekia aliheshimiwa sana na mataifa yote.
24 Te vaeng tue ah Hezekiah te a duek ham duela tlo. Te dongah BOEIPA taengah a thangthui hatah anih te a doo tih a taengah kopoekrhai pakhat a paek.
Katika siku hizo, Hezekia akaugua, naye akawa karibu kufa. Akamwomba Bwana, ambaye alimjibu na kumpa ishara.
25 Tedae a sokah a tiing la Hezekiah loh a thuung pawt dongah a lungbuei a sang sak. Te dongah anih so neh Judah, Jerusalem soah thinhulnah om.
Lakini moyo wa Hezekia ukajaa majivuno na hakuonyesha itikio kwa wema aliotendewa, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana ikawa juu yake na juu ya Yuda na Yerusalemu.
26 Te phoeiah tah a lungbuei a sang khui lamloh Hezekiah amah neh Jerusalem khosa rhoek khaw kunyun tih Hezekiah tue vaengah tah BOEIPA kah thinhulnah loh amih thoeng thil pawh.
Ndipo Hezekia akatubu kwa ajili ya kiburi cha moyo wake, kama walivyofanya watu wa Yerusalemu, kwa hiyo ghadhabu ya Bwana haikuja juu yao katika siku za Hezekia.
27 Hezekiah taengah khuehtawn khaw om tih thangpomnah neh muep rhoeng. Te dongah amah loh cak ham neh sui ham khaw, lung vang ham neh botui ham khaw, photling ham neh sahnaih hnopai cungkuem ham khaw thakvoh a saii.
Hezekia alikuwa na utajiri mwingi sana na heshima, naye akajifanyia hazina kwa ajili ya fedha yake na dhahabu na kwa ajili ya vito vyake vya thamani, vikolezi, ngao na aina zote za vyombo vya thamani.
28 Canghum cangpai, misur thai neh situi ham rhuengim khaw, rhamsa saelhung boeih neh tuvong khuikah tuping ham khaw im a sak.
Akajenga pia maghala ya kuhifadhi mavuno ya nafaka, divai mpya na mafuta. Akatengeneza mabanda kwa ajili ya aina mbalimbali za mifugo, na mazizi kwa ajili ya kondoo na mbuzi.
29 Pathen loh anih te khuehtawn muep a paek khungdaeng dongah amah ham khopuei a saii tih saelrhoi boiva neh saelhung khaw a cungkuem la a det.
Akajenga vijiji na kujipatia idadi kubwa ya kondoo na mbuzi, pamoja na ngʼombe kwa kuwa Mungu alikuwa amempa utajiri mwingi sana.
30 Hezekiah amah loh Gihon tui hnun te a soah a ueng tih David khopuei kah khotlak hil a dang la a hlawn. Hezekiah tah a cungkuem dongah a bibi khaw a thaihtak pah.
Ilikuwa ni Hezekia aliyeziba njia za kutolea maji za chemchemi za juu za Gihoni na kuyaelekeza maji kutiririkia upande wa magharibi wa Mji wa Daudi. Akafanikiwa katika kila kitu alichofanya.
31 Tedae khohmuen ah aka thoeng kopoekrhai kawng dawt ham te Babylon mangpa rhoek loh a taengla hmuiyoi a tueih vaengah tah anih te noemcai ham neh, a thinko khuikah boeih te ming hamla Pathen loh anih te a hnoo.
Lakini wakati wajumbe walipotumwa na watawala wa Babeli kumuuliza juu ya ishara ambayo ilitokea katika nchi, Mungu alimwacha ili kumjaribu na kujua kila kitu kilichokuwa moyoni mwake.
32 Hezekiah kah ol noi neh a sitlohnah te tonghma Amoz capa Isaiah kah mangthui khuiah khaw, Judah neh Israel manghai rhoek kah cabu khuiah khaw a daek uh.
Matukio mengine ya utawala wa Hezekia na matendo yake ya kujitoa kwa moyo yameandikwa katika maono ya nabii Isaya mwana wa Amozi kwenye kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
33 Hezekiah te a napa rhoek taengla a khoem uh vaengah tah anih te David koca rhoek kah phuel tangkham ah a up uh. A dueknah hnin ah anih te Judah pum neh Jerusalem khosa rhoek loh thangpomnah a saii uh. Te phoeiah tah a capa Manasseh te anih yueng la manghai.
Hezekia akalala na baba zake na akazikwa kwenye kilima mahali yalipo makaburi ya wazao wa Daudi. Yuda wote na watu wa Yerusalemu wakamheshimu alipofariki. Naye Manase mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Khokhuen 32 >