< 2 Khokhuen 27 >
1 Jotham te kum kul kum nga a lo ca vaengah manghai tih Jerusalem ah kum hlai rhuk manghai. A manu ming tah Zadok canu Jerusha ni.
Yothamu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
2 A napa Uzziah kah a saii bang boeih la BOEIPA mikhmuh ah a thuem saii cakhaw BOEIPA bawkim la a kun pawt dongah pilnam koep poci.
Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya, lakini tofauti na yeye, hakuingilia huduma za hekaluni mwa Bwana. Lakini hata hivyo, watu wakaendelea na desturi zao mbaya.
3 Anih loh a so BOEIPA im kah vongka te a thoh tih Ophel vongtung dongah a cungkuem la a sak.
Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana na kufanya kazi kubwa kwenye ukuta katika kilima cha Ofeli.
4 Judah tlang ah khopuei a suen tih thingkho ah rhalmah im neh rhaltoengim a sak.
Akajenga miji katika vilima vya Yuda pamoja na ngome na minara mwituni.
5 Anih loh Ammon koca kah manghai te a vathoh thil tih amih te a buem. Te dongah anih te Ammon koca loh kum khat ah cak talent yakhat, cang kore thawng rha, cangtun thawng rha a paek. Te tlam te Ammon ca rhoek loh anih te kum bae ah khaw, a kum thum dongah khaw a sah uh.
Yothamu akafanya vita na mfalme wa Waamoni na kumshinda. Mwaka ule Waamoni wakamlipa talanta 100 za fedha, kori 10,000 za ngano na kori 10,000 za shayiri. Waamoni wakamletea kiasi hicho hicho mwaka wa pili na wa tatu.
6 A Pathen BOEIPA mikhmuh ah a longpuei a cikngae sak dongah Jotham khaw a thaa caang.
Yothamu akaendelea kuwa na nguvu kwa sababu alienenda kwa ukamilifu mbele za Bwana Mungu wake.
7 Te dongah kah ol noi khaw, a caemtloek boeih neh a longpuei khaw, Israel neh Judah manghai rhoek kah cabu dongah a daek uh coeng ke.
Matukio mengine ya utawala wa Yothamu, pamoja na vita vyake vyote na vitu vingine alivyofanya, vimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
8 A manghai vaengah kum kul neh kum nga lo ca tih Jerusalem ah kum hlai rhuk manghai.
Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita.
9 Te dongah te a napa rhoek taengla a khoem uh vaengah anih te David khopuei ah a up uh. Te phoeiah a capa Ahaz te anih yueng la manghai.
Yothamu akalala na baba zake na akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.