< 2 Khokhuen 12 >
1 Rehoboam kah ram neh a thadueng he cikngae bangla om, amah neh Israel boeih long khaw BOEIPA kah olkhueng te a hnawt.
Baada ya nafasi ya Rehoboamu kuimarika na kuwa na nguvu, yeye na Israeli yote waliiacha sheria ya Bwana Mungu.
2 Rehoboam manghai kah a kum nga dongah tah BOEIPA taengah boe a koek uh dongah Egypt manghai Shishak loh Jerusalem te a muk.
Kwa sababu hawakuwa waaminifu kwa Bwana, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu.
3 Te vaengah leng thawngkhat yahnih, marhang caem thawng sawmrhuk lo. Egypt, Lubim, Sukkiim neh Kushi lamloh anih taengla aka pawk he pilnam hlangmi naa moenih.
Akiwa na magari ya vita 1,200 na wapanda farasi 60,000 na idadi isiyohesabika ya majeshi ya Walibia, Wasukii na Wakushi yaliyokuja pamoja naye kutoka Misri.
4 Judah kah kasam khopuei rhoek te a loh tih Jerusalem la pawk.
Akateka miji ya Yuda yenye ngome akaendelea mpaka Yerusalemu.
5 Te vaengah tonghma Shemaiah te Jerusalem kah Shishak maelhmai kongah aka tingtun Rehoboam neh Judah mangpa rhoek taengla pawk tih amih te, “Nangmih kah BOEIPA loh he ni a thui. Kai nan hnawt uh coeng dongah ni kai loh nangmih te Shishak kut ah kam voeih,” a ti nah.
Ndipo nabii Shemaya akaja kwa Rehoboamu na kwa viongozi wa Yuda waliokuwa wamekusanyika huko Yerusalemu kwa ajili ya hofu ya Shishaki naye akawaambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, ‘Ninyi mmeniacha mimi, kwa hiyo, mimi nami sasa ninawaacha ninyi mkononi mwa Shishaki.’”
6 Te daengah Israel mangpa rhoek neh manghai khaw kunyun tih, “BOEIPA tah dueng pai,” a ti uh.
Viongozi wa Israeli na mfalme wakajinyenyekeza na kusema, “Bwana Mungu ni mwenye haki.”
7 Te dongah a kunyun uh te BOEIPA loh a hmuh vaengah BOEIPA ol Shemaiah taengla pawk tih, “A kunyun coeng dongah amih te ka phae mahpawh. Tedae amih te loeihnah ka paek pawn ni. Ka kosi Shishak kut lamloh Jerusalem ah bo mahpawh.
Bwana Mungu alipoona kwamba wamejinyenyekeza, neno hili la Bwana likamjia Shemaya: “Maadamu wamejinyenyekeza, sitawaangamiza bali hivi karibuni nitawapatia wokovu. Ghadhabu yangu haitamwagwa juu ya Yerusalemu kwa kupitia Shishaki.
8 Tedae anih taengah sal la a om uh daengah nikai kah thothuengnah neh diklai ram kah thothuengnah te a ming uh eh,” a ti nah.
Hata hivyo, watamtumikia Shishaki ili wapate kujifunza tofauti kati ya kunitumikia mimi na kuwatumikia wafalme wa nchi nyingine.”
9 Egypt manghai Shishak loh Jerusalem te a paan vaengah BOEIPA im thakvoh neh manghai im kah thakvoh te a loh. A cungkuem te a loh tih Solomon loh a saii sui photling khaw a khuen.
Shishaki mfalme wa Misri alipoishambulia Yerusalemu, alichukua hazina za Hekalu la Bwana na hazina za jumba la kifalme. Akachukua kila kitu, pamoja na zile ngao za dhahabu ambazo Solomoni alikuwa amezitengeneza.
10 Te dongah te rhoek yueng la manghai Rehoboam loh rhohum photling a saii tih manghai im kah thohka aka tawt, imtawt mangpa kut ah a khueh.
Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba badala ya zile za dhahabu na kuzikabidhi kwa majemadari wa ulinzi wa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme.
11 Manghai te BOEIPA im la a caeh dingdoeng vaengah imtawt rhoek khaw cet uh tih photling te a bai uh. Te phoeiah imtawt kah tanhnaem la a thak uh.
Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu la Bwana walinzi walikwenda pamoja naye wakiwa wamebeba hizo ngao na baadaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.
12 Amah a kunyun van dongah BOEIPA kah thintoek khaw anih lamloh mael tih a bawtnah hil phae pawh. Tedae Judah ah khaw ol then om pueng.
Kwa sababu Rehoboamu alijinyenyekeza, hasira ya Bwana ikageukia mbali naye, hakuangamizwa kabisa. Kukawa na hali nzuri katika Yuda.
13 Manghai Rehoboam tah Jerusalem ah cak tih sawmli kum khat a lo ca hil manghai. Rehoboam a manghai van neh Jerusalem khopuei ah kum hlai rhih manghai. Te tah Israel koca boeih lamloh amah ming pahoi khueh ham ni BOEIPA loh a coelh. Rehoboam manu ming tah Ammoni Naamah ni.
Mfalme Rehoboamu akajiweka imara katika Yerusalemu na akaendelea kuwa mfalme. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na saba, mji ambao Bwana alikuwa ameuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli ili aliweke Jina lake humo. Mama yake aliitwa Naama, alikuwa Mwamoni.
14 Tedae BOEIPA te toem hamla a lungbuei a cikngae pawt dongah boethae a saii.
Rehoboamu akatenda maovu kwa sababu hakuuelekeza moyo wake katika kumtafuta Bwana Mungu.
15 Rehoboam kah olka a kung neh a doong te tonghma Shemaiah olka, khohmu Iddo kah a khuui dongah Rehoboam kah caemtloek neh Jeroboam kah a tue boeih neh a daek uh moenih a?
Kwa habari ya matukio katika utawala wa Rehoboamu, tangu mwanzo mpaka mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Shemaya na mwonaji Ido zinazohusiana na vizazi? Kulikuwako na vita mara kwa mara kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
16 Rehoboam khaw a napa rhoek taengla a khoem uh vaengah tah David khopuei ah a up uh. Te phoeiah a capa Abijah te anih yueng la manghai.
Rehoboamu akalala na baba zake, akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Abiya mwanawe akawa mfalme baada yake.