< Tingtoeng 63 >

1 [Judah khosoek ah a om vaengkah David tingtoenglung] Pathen namah tah ka Pathen ni. Namah ni kan toem coeng. Namah te ka hinglu loh halthi tih, ka pumsa loh namah te a hue, Diklai ah he rhamrhae neh buhmueh rhathih, tui mueh la om.
Zaburi ya Daudi. Wakati alipokuwa katika Jangwa la Yuda. Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, nakutafuta kwa moyo wote; nafsi yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakuonea wewe shauku, katika nchi kame na iliyochoka mahali ambapo hapana maji.
2 Tedae na sarhi neh na thangpomnah hmuh ham hmuencim ah nang kan dan.
Nimekuona katika mahali patakatifu na kuuona uwezo wako na utukufu wako.
3 Na sitlohnah he hingnah lakah then tih ka hmuilai he nang taengah domyok ti uh saeh.
Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakuadhimisha.
4 Te dongah ka hingnah neh nang kan uem vetih, na ming neh ka kut ka thueng ni.
Nitakusifu siku zote za maisha yangu, na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
5 A tha neh maehhloi bangla ka hinglu hah vetih ka ka loh omngaih laa kah hmuilai neh a thangthen ni.
Nafsi yangu itatoshelezwa kama kwa wingi wa vyakula; kwa midomo iimbayo kinywa changu kitakusifu wewe.
6 Ka rhaenghmuen lamkah loh nang kan poek vaengah nang te hlaempang pakhat puet kan mangtuk.
Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe, ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.
7 Kai ham bomnah la na om dongah na phae hlip ah ka tamhoe.
Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu, chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.
8 Nang dongah ka hinglu pangnal tih kai he na bantang kut loh n'duel.
Nafsi yangu inaambatana nawe, mkono wako wa kuume hunishika.
9 Amih loh ka hinglu pocinah ham a mae uh dae diklai hmui la kun uh bitni.
Wale wanaotafuta uhai wangu wataharibiwa, watakwenda chini kwenye vilindi vya dunia.
10 cunghang kut ah pat uh vetih maetang buham la om uh ni.
Watatolewa wafe kwa upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 Tedae, manghai tah Pathen rhang neh a kohoe ni. Amah dongah ol aka caeng boeih te a thangthen vaengah laithae aka thui kah a ka te a biing pah ni.
Bali mfalme atafurahi katika Mungu, wale wote waapao kwa jina la Mungu watamsifu, bali vinywa vya waongo vitanyamazishwa.

< Tingtoeng 63 >