< Thothuengnah 25 >

1 Sinai tlang ah BOEIPA loh Moses a voek tih,
Bwana akamwambia Mose katika Mlima Sinai,
2 Israel ca rhoek te voek lamtah thui pah. Kai loh nangmih taengah kam paek khohmuen te na kun thil uh vaengah khohmuen loh BOEIPA ham Sabbath te yaeh saeh.
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapa ninyi, nchi yenyewe ni lazima ishike Sabato kwa ajili ya Bwana.
3 Na khohmuen te kum rhuk tawn lamtah na misur khaw kum rhuk na hloe khuiah a thaih te bit.
Kwa miaka sita mtapanda mazao katika mashamba yenu, nanyi kwa miaka sita mtaikata mizabibu yenu matawi na kuvuna mazao yake.
4 Tedae a kum rhih dongah tah khohmuen ham koiyaeh Sabbath la om saeh. BOEIPA kah Sabbath ah na khohmuen te tawn boeh. Na misur khaw hloe boeh.
Lakini mwaka wa saba nchi lazima iwe na Sabato ya mapumziko, Sabato kwa Bwana. Msipande mbegu katika mashamba yenu, wala msikate mizabibu yenu matawi.
5 Na cang pong te at boeh. Na khohai misur khaw bit boeh. Khohmuen kah koiyaeh kum la om saeh.
Msivune na kuweka akiba kinachoota chenyewe, wala kuvuna na kusindika zabibu ambayo hamkuhudumia mashamba yake. Nchi lazima iwe na mwaka wa mapumziko.
6 Na Khohmuen kah Sabbath vaengah tah cakok te namah ham neh na salpa ham khaw, na salnu ham khaw, na kutloh ham khaw, na taengah aka bakuep na lampah ham khaw om bitni.
Chochote nchi itoacho katika mwaka wa Sabato kitakuwa chakula chenu wenyewe, watumishi wenu wa kiume na wa kike, mfanyakazi aliyeajiriwa, na mkazi wa muda anayeishi miongoni mwenu,
7 Na khohmuen kah na rhamsa neh mulhing loh a caak ham khaw a thaih boeih om ni.
vilevile malisho ya mifugo yenu na wanyama pori katika nchi yenu. Chochote nchi itakachozalisha kinaweza kuliwa.
8 Te dongah kum rhih kum rhih kah Sabbath voei rhih tae lamtah voei rhih a cup phoeikah kum sawmli pako vaengah Sabbath kum la om saeh.
“‘Hesabu Sabato saba za miaka, yaani miaka saba mara saba, ili Sabato saba za miaka utakuwa muda wa miaka arobaini na tisa.
9 Hla rhih dongkah hlasae hnin rha vaengah tamlung neh tuki na ueng ni. Tholh dawthnah khohnin ah khaw na khohmuen boeih ah tuki na ueng ni.
Ndipo tarumbeta itapigwa kila mahali katika siku ya kumi ya mwezi wa saba. Katika Siku ya Upatanisho, piga tarumbeta katika nchi yako yote.
10 Kum sawmnga kum te ciim uh lamtah kho khuikah khosa rhoek boeih ham sayalhnah hoe uh. Te te nangmih ham jubilee la om saeh. Hlang kah a khohut te mael lamtah hlang boeih te a huiko taengla mael uh.
Mwaka wa hamsini mtauweka wakfu na kutangaza uhuru katika nchi kwa wakazi wake wote. Itakuwa ni yubile kwenu; kila mmoja wenu atairudia mali ya jamaa yake, na kila mmoja kurudi kwenye ukoo wake.
11 A sawmnga kum te nangmih ham jubilee kum la om saeh lamtah, lo tawn uh boeh. Te dongah amah aka pong khaw at uh boeh. Khohai kah khaw bit uh boeh.
Mwaka wa hamsini utakuwa yubile kwenu, msipande wala msivune kile kiotacho chenyewe, au kuvuna zabibu zisizohudumiwa.
12 Tekah jubilee tah nangmih ham a cim la a om dongah khohmuen kah a thaih te na caak uh ni.
Kwa kuwa ni yubile, nayo itakuwa takatifu kwenu; mtakula tu kile kilichotoka moja kwa moja mashambani.
13 Tekah jubilee kum vaengah hlang kah a khohut te mael uh.
“‘Katika huu Mwaka wa Yubile, kila mmoja atarudi kwenye mali yake mwenyewe.
14 Hnoyoih te na imben taengah na yoih uh tih, na imben kut lamkah na lai atah manuca te khat neh khat vuelvaek uh thae boeh.
“‘Ikiwa utauza ardhi kwa mmoja wa wazawa wa nchi yako, au ukinunua ardhi kutoka kwake, mmoja asimpunje mwingine.
15 Jubilee phoeikah kum na tae soah na imben kah khohmuen te na lai uh neh a vuei a thaih kum na tae soah yoi saeh.
Utanunua ardhi kwa mzawa wa nchi yako kwa misingi ya hesabu ya miaka baada ya Yubile. Naye ataiuza kwako kwa misingi ya hesabu ya miaka iliyobaki kwa kuvuna mavuno.
16 A cangvuei kah a tarhing te namah taengah han yoih coeng dongah a kum loh amah tarhing ah yet tih a lainah loh rhoeng cakhaw kum kah a tarhing te hnah pah lamtah a lainah te hnah pah.
Miaka inapokuwa mingi, utaongeza bei, nayo miaka ikiwa michache, utapunguza bei, kwa sababu kile anachokuuzia kwa hakika ni hesabu ya mazao.
17 Hlang pakhat long he a imben te vuelvaek boel saeh. Tedae kai tah nangmih kah BOEIPA Pathen la ka om dongah na Pathen te rhih lah.
Mmoja asimpunje mwingine, bali utamcha Mungu wako. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.
18 Te dongah ka khosing te vai uh lamtah ka laitloeknah te ngaithuen uh. Te te na saii uh daengah ni diklai ah ngaikhuek la kho na sak uh eh.
“‘Fuateni amri zangu, mwe waangalifu kutii amri zangu, nanyi mtaishi salama katika nchi.
19 Diklai long khaw a thaih a paek vetih kodam la na caak ni. A khuiah khaw ngaikhuek la kho na sak uh ni.
Kisha nchi itazaa matunda yake, nanyi mtakula na kushiba na kuishi humo kwa salama.
20 Tedae, “Kum rhih dongah lo ka tawn uh pawt tih ka cangvuei khaw ka khoem uh pawt koinih balae ka caak uh eh,” na ti uh oeh cakhaw,
Mwaweza kuuliza, “Tutakula nini katika mwaka wa saba ikiwa hatutapanda wala kuvuna mazao yetu?”
21 kai kah yoethennah he kum rhuk khuiah nangmih ham kang uen vetih kum thum ham a vuei a thaih om bitni.
Nitawapelekeeni baraka ya pekee katika mwaka wa sita, kwamba nchi itazalisha mazao ya kutosha kwa miaka mitatu.
22 Kum rhet dongah tawn uh lamtah cang rhuem te kum ko hil ca uh. Cangah a pha duela cang rhuem te ca uh.
Mnapopanda mwaka wa nane, mtakula mavuno ya miaka iliyopita. Pia mtaendelea kuyala mazao hayo hadi mvune mavuno ya mwaka wa tisa.
23 Nangmih tah kai taengah yinlai neh na lampah uh dae khohmuen tah kamah taengah a ti ham dongah khohmuen te khaw yoi boeh.
“‘Kamwe ardhi isiuzwe kwa mkataba wa kudumu, kwa sababu nchi ni mali yangu, nanyi ni wageni na wapangaji wangu.
24 Te dongah na khohut khohmuen boeih dongah khohmuen ham tlannah khueh uh.
Katika nchi yote mtakayoshika kuwa milki yenu, ni lazima mtoe ukombozi wa ardhi.
25 Na manuca te daeng tih a khohut te a yoih atah khohmuen aka tlan ham anih neh aka yoei uh loh ham paan saeh lamtah a manuca kah hnoyoih te koep tlan saeh.
“‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini na akauza baadhi ya mali yake, ndugu yake wa karibu atakuja na kukomboa kile ndugu yako alichokiuza.
26 Aka tlan ham hlang ni a om pawt tih khohmuen a tlannah rhoeh te a kut loh pha pawh, a dang pawt bal atah,
Iwapo mtu huyo hana jamaa wa karibu wa kukomboa mali hiyo kwa ajili yake, lakini yeye mwenyewe akafanikiwa na kupata mali itoshayo kuikomboa,
27 a hnoyoih kah kum te tae saeh lamtah a hoei te koe a yoih thil hlang taengah thuung saeh. Te phoeiah amah khohut te lat saeh.
ataamua tena thamani yake kwa miaka tangu alipoiuza, na kurudisha kiasi kilichobaki cha thamani kwa mtu ambaye alikuwa amemuuzia mali hiyo, naye ataweza kuirudia mali yake.
28 Tedae anih taengah a mael rhoeh te a kut loh a dang pawt atah a hnoyoih te aka lai kut dongah jubilee kum duela om dae saeh. Tedae jubilee vaengah hlah pah saeh lamtah amah khohut taengla mael saeh.
Lakini kama hatapata njia ya kumlipa mnunuzi, ile mali aliyouza itabaki kumilikiwa na mnunuzi mpaka Mwaka wa Yubile. Mali hiyo itarudishwa mwaka wa Yubile, naye ataweza kuirudia mali yake.
29 Hlang loh tolrhum khopuei vongtung khuikah im te a yoih mai ni. Tedae a yoihnah kum a thok hil a tlannah om saeh lamtah a tlannah tue te khueh saeh.
“‘Ikiwa mtu atauza nyumba iliyo ndani ya mji uliozungukwa kwa ukuta, yeye anayo haki ya kuikomboa mwaka mzima baada ya mauzo ya hiyo nyumba. Wakati huo anaweza kuikomboa.
30 Kum loh cup tih a thok duela a tlan pawt atah khopuei vongtung khuikah im te im aka lai neh anih kah cadilcahma taengah a ti la pai saeh lamtah jubilee vaengah khaw hlah boel saeh.
Ikiwa haikukombolewa kabla ya mwaka mmoja kamili kupita, nyumba iliyo ndani ya mji uliozungukwa kwa ukuta itakuwa mali ya kudumu ya mnunuzi na wazao wake. Haitarudishwa mwaka wa Yubile.
31 Vongup kah im mai cakhaw a kaepvai ah vongtung a om pawt atah khohmuen lohma bangla poek uh saeh. Anih ham tlannah om saeh lamtah jubilee vaengah hlah pah saeh.
Lakini nyumba zilizo vijijini bila ya kuwa na kuta zilizozizunguka zitahesabiwa kama mashamba. Zinaweza kukombolewa, nazo zirudishwe katika mwaka wa Yubile.
32 Levi khopuei kah khopuei im tah amih kah khohut ni. Levi ham tah kumhal ah tlannah om saeh.
“‘Walawi siku zote wana haki ya kukomboa nyumba zao katika miji ya Walawi wanayoimiliki.
33 Israel ca rhoek khuiah Levi rhoek long tah a khopuei neh a im bueng he amih kah a khohut la a khueh uh dongah Levi rhoek long tah tlan saeh. A khohut khopuei kah im a yoih tangtae khaw jubilee vaengah koep lat saeh.
Kwa hiyo mali ya Mlawi inaweza kukombolewa, yaani nyumba iliyouzwa katika mji wowote wanaoushikilia itarudishwa mwaka wa Yubile, kwa sababu nyumba zilizo katika miji ya Walawi ni mali yao miongoni mwa Waisraeli.
34 Tedae amih Levi khopuei kah khohmuen khocaak te tah amamih kah kumhal a khohut la a om coeng dongah yoi uh boel saeh.
Lakini nchi ya malisho iliyo mali ya miji yao kamwe isiuzwe, ni milki yao ya kudumu.
35 Na manuca te daeng tih nang taengah a kut a hmawn oeh atah anih te yinlai neh lampah banghui lam khaw talong lamtah namah taengah hing sak.
“‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini, naye akashindwa kujitegemeza mwenyewe katikati yako, msaidie kama vile ambavyo ungelimsaidia mgeni au kama mkazi wa muda, ili aweze kuendelea kuishi katikati yako.
36 Anih taeng lamkah a casai neh a pueh a kan khaw lo boeh. Na Pathen te na rhih daengah ni na manuca loh nang taengah a hing eh.
Usichukue riba wala faida yoyote kutoka kwake, bali utamwogopa Mungu wako, ili mzawa wa nchi yako aweze kuendelea kuishi katikati yako.
37 Anih te a casai la tangka pu boeh. Na cang khaw a pueh a kan la yoi boeh.
Usimkopeshe fedha ili alipe na riba, wala usimuuzie chakula kwa faida.
38 Kai tah nangmih taengah Pathen la om ham neh nang taengah Kanaan khohmuen paek ham Egypt khohmuen lamkah nangmih aka doek na Pathen BOEIPA ni.
Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekuleta kutoka nchi ya Misri nikupe nchi ya Kanaani, nami niwe Mungu wako.
39 Na taengkah na manuca te daeng tih nang taengla amah a yoih uh atah sal kah thohtatnah bangla anih te thohtat sak boeh.
“‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini katikati yako, naye akajiuza kwako, usimfanye atumike kama mtumwa.
40 Namah taengah kutloh neh lampah bangla om saeh lamtah Jubilee kum hil nang taengah thotat saeh.
Atatendewa kama mfanyakazi aliyeajiriwa, au kama mkazi wa muda katikati yako, naye atatumika mpaka Mwaka wa Yubile.
41 Te phoeiah amah neh a ca rhoek te nang taeng lamkah nong saeh lamtah a huiko taengla mael saeh. Te vaengah a napa kah khohut la mael saeh.
Ndipo yeye na watoto wake wataachiwa, naye atarudi kwa watu wa ukoo wake, na kwenye mali ya baba zake.
42 Kamah kah sal la om ham amih te Egypt kho lamkah ka loh. Amih te sal yoih la yoi uh boel saeh.
Kwa sababu Waisraeli ni watumishi wangu niliowaleta kutoka nchi ya Misri, kamwe wasiuzwe kama watumwa.
43 Anih te mangkhak la taemrhai boeh. Na Pathen te rhih lah.
Usiwatawale kwa ukatili, lakini utamcha Mungu wako.
44 Na kaepvai namtom taeng lamkah sal, salnu na lai te tah namah taengah namah kah salnu salpa la om uh saeh.
“‘Watumwa wako wa kiume na wa kike watatoka katika mataifa yanayokuzunguka; kutoka kwao waweza kununua watumwa.
45 Nangmih loh na lai uh tih nangmih taengah aka bakuep lampah ca rhoek neh nangmih taengkah a huiko lamloh na kho kah nangmih lakliah a cun uh te khaw khohut bangla nangmih taengah om uh saeh.
Pia waweza kununua baadhi ya wakazi wa muda wanaoishi katikati yako, na jamaa ya koo zao waliozaliwa katika nchi yako, nao watakuwa mali yako.
46 Te dongah amih te namah phoeikah na ca rhoek taengah kumhal kah a pang khohut la pang sak lamtah thohtat sak. Tedae na manuca Israel ca rhoek khat khat neh anih kah a manuca soah mangkhak la taemrhai boeh.
Hao waweza kuwarithisha watoto wako kuwa urithi wao, na wanaweza kuwafanya watumwa maisha yao yote, lakini usiwatawale ndugu zako Waisraeli kwa ukatili.
47 Nang taengkah yinlai neh lampah kut long pataeng a kae vaengah a taengkah na manuca tah daeng tih na taengkah yinlai lampah taengah khaw, yinlai huiko kah a mii taengah khaw, amah a yoi uh khaming,
“‘Ikiwa mgeni au mkazi wa muda katikati yako atakuwa tajiri, na mmoja wa wazawa wa nchi yako akawa maskini, naye akajiuza kwa yule mgeni anayeishi katikati yako, au kwa mmoja wa jamaa wa koo za wageni,
48 a yoih uh phoeiah khaw a manuca khui lamkah khat khat long ni tlannah a khueh atah tlan saeh.
anayo haki ya kukombolewa baada ya kujiuza. Mmoja wa jamaa zake aweza kumkomboa:
49 A nupu long khaw, a nupu capa long khaw tlan saeh. A pumsa saa lamkah, amah huiko long khaw tlan saeh. A kut loh a na mak atah amah khaw tlan uh saeh.
Mjomba wake, au binamu yake, au yeyote aliye ndugu wa damu katika ukoo wake aweza kumkomboa. Au ikiwa atafanikiwa, anaweza kujikomboa mwenyewe.
50 Anih a yoih lamkah a lai kum te jubilee kum duela tae pah saeh. Te phoeiah a kum tarhing dongkah a khohnin vanbangla a yoih tangka te om saeh lamtah anih te kutloh bangla om saeh.
Yeye na huyo aliyemnunua watahesabu muda kuanzia mwaka aliojiuza hadi Mwaka wa Yubile. Mahali pa kuanzia bei ya kuachiwa kwake itakadiriwa kwa ujira unaolipwa mfanyakazi aliyeajiriwa kwa idadi ya hiyo miaka.
51 Kum muep a ngaih pueng atah a yet tarhing la a lainah tangka dong lamkah te tlannah la pae saeh.
Ikiwa imebaki miaka mingi, ni lazima atalipia ukombozi wake fungu kubwa la bei iliyolipwa kumnunua yeye.
52 Tedae jubilee kum duela kum cavilcavel ni a ngaih coeng atah a kum tarhing te poek pah saeh lamtah a tlannah te pae van saeh.
Ikiwa miaka iliyobaki ni michache kufikia Mwaka wa Yubile, atafanya hesabu yake, naye atalipa malipo yanayostahili kwa ajili ya ukombozi wake.
53 Kum at phoeiah kum at kutloh bangla om saeh. Anih te na mikhmuh ah mangkhak la taemrhai boeh.
Atatendewa kama mtu wa kuajiriwa mwaka hadi mwaka; lazima uone kwamba yule aliyemnunua hamtawali kwa ukatili.
54 Te tlam pataeng a tlan thai pawt atah Jubilee kum vaengah anih te a ca rhoek neh rhenten hlah saeh.
“‘Hata ikiwa hakukombolewa kwa njia mojawapo ya hizi, yeye na watoto wake wataachiwa katika Mwaka wa Yubile,
55 Israel ca rhoek he kamah taengah ka sal rhoek kah sal la om ham ni Egypt kho lamkah ka loh. Kai tah nangmih kah BOEIPA Pathen ni, a ti nah.
kwa maana Waisraeli ni mali yangu kama watumishi. Wao ni watumishi wangu, niliowatoa kutoka nchi ya Misri. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.

< Thothuengnah 25 >