< Joshua 14 >
1 Kanaan kho ah Israel ca rhoek loh a pang uh he khaw khosoih Eleazar, Nun capa Joshua neh Israel ca rhoek kah cako khuiah a lu la aka om a napa rhoek long ni a phaeng.
Basi haya ndiyo maeneo Waisraeli waliyopokea kama urithi katika nchi ya Kanaani, ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliwagawia.
2 Koca pako neh hlangvang ham rho he BOEIPA loh a uen vanbangla hmulung neh Moses kut loh a yueh pah.
Urithi wao uligawanywa kwa kura kwa yale makabila tisa na nusu, kama Bwana alivyoamuru Mose.
3 Koca panit neh hlangvang te Jordan rhalvangan ah Moses loh rho a paek coeng. Tedae amih khui ah Levi te tah rho a paek moenih.
Mose alikuwa amewapa yale makabila mawili na nusu urithi wao upande wa mashariki mwa Yordani, lakini Walawi hawakupewa urithi miongoni mwa hao wengine,
4 Joseph ca rhoi te Manasseh neh Ephraim koca la om uh. Levi te khohmuen khuikah khoyo pae uh pawt dae khosak nah ham khopuei neh a boiva, a hnopai ham bueng ni a khocaak a khueh pah.
kwa kuwa wana wa Yosefu walikuwa makabila mawili; Manase na Efraimu. Walawi hawakupata mgawo wa ardhi, bali walipewa miji tu kwa ajili ya kuishi, pamoja na maeneo ya malisho kwa ajili ya makundi yao ya kondoo, mbuzi na ngʼombe wao.
5 BOEIPA loh Moses a uen vanbangla Israel ca rhoek loh a saii uh tih khohmuen a tael uh.
Kwa hiyo Waisraeli wakagawana ile nchi, kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
6 Te vaengah Gilgal kah Joshua taengah Judah koca rhoek te thoeih uh. Te dongah Kenizzi Jephunneh capa Kaleb loh, “Kadeshbarnea ah Pathen kah hlang Moses taengah BOEIPA loh kai kawng neh nang kawng a thui vanbangla olka khaw namah loh na ming.
Kisha watu wa Yuda wakamwendea Yoshua huko Gilgali, naye Kalebu mwana wa Yefune yule Mkenizi, akamwambia, “Unajua jambo ambalo Bwana alimwambia Mose mtu wa Mungu huko Kadesh-Barnea kukuhusu wewe na mimi.
7 Kum sawmli ka lo ca vaengah BOEIPA kah sal Moses loh khohmuen hip hamla Kadeshbarnea lamloh kai n'tueih tih ka thinko kah aka om vanbangla olka khaw ka bal puei.
Nilikuwa na umri wa miaka arobaini, wakati Mose mtumishi wa Bwana, aliponituma kutoka Kadesh-Barnea kuipeleleza hiyo nchi. Nami nikamletea taarifa kama kulingana na nilivyosadiki moyoni.
8 Te vaengah kamah neh ka cet hmaih ka manuca rhoek loh pilnam kah lungbuei a yut sak. Tedae kai tah BOEIPA ka Pathen hnukah ni ka tukkoei.
Lakini ndugu zangu tuliopanda nao waliifanya mioyo ya watu iyeyuke kwa hofu. Bali mimi, nilimfuata Bwana Mungu wangu kwa moyo wote.
9 Te dongah Moses loh amah khohnin ah a toemngam tih, “Na kho loh a til khohmuen te tah namah kah rho la om saeh lamtah BOEIPA ka Pathen hnukah na tukkoei van dongah kumhal duela na ca rhoek ham om laeh saeh,” a ti.
Hivyo katika siku ile, Mose akaniapia, ‘Nchi ambayo umeikanyaga kwa miguu yako itakuwa urithi wako na wa watoto wako milele, kwa sababu umemfuata Bwana Mungu wangu kwa moyo wote.’
10 Kum sawmli kumnga vaengah a thui vanbangla BOEIPA loh kai tahae due n'hlun coeng he. BOEIPA loh Moses taengah hekah olka a thui vaengah Israel he khosoek ah ni a pongpa. Te dongah kai khaw tihnin ah kum sawmrhet kum nga ka lo ca coeng he.
“Sasa basi, kama vile Bwana alivyoahidi, ameniweka hai kwa miaka arobaini na mitano tangu wakati alipomwambia Mose jambo hili, wakati Waisraeli wakiwa wanazunguka jangwani. Hivyo mimi hapa leo, nina umri wa miaka themanini na mitano!
11 Moses loh kai n'tueih hnin vaengkah bangla tihnin ah ka tlungluen pueng ta. Ka thadueng khaw ka thadueng nah pueng dongah caemtloek ham pataeng ka caeh rhoe ka caeh ham om.
Bado ninazo nguvu kama siku ile Mose aliponituma. Bado ninazo nguvu za kwenda vitani sasa kama vile nilivyokuwa wakati ule.
12 Te dongah he kah tlang he kai taengah m'pae laeh. Te khohnin ah BOEIPA loh a thui te na yaak coeng. Te khohnin ah Anakim neh khopuei tanglue khaw cakrhuet dae, kai taengah BOEIPA a om khaming. Te dongah BOEIPA kah a thui bangla amih te ka haek bitni,” a ti nah.
Basi nipe nchi hii ya vilima, ambayo Bwana aliniahidi siku ile. Wewe mwenyewe ulisikia wakati ule kwamba Waanaki walikuwako huko na miji yao ilikuwa mikubwa na yenye maboma, lakini, kwa msaada wa Bwana, nitawafukuza watoke huko kama vile alivyonena.”
13 Te dongah Joshua loh yoethen a paek tih Hebron he Jephunneh capa Kaleb taengah rho la a paek.
Ndipo Yoshua akambariki Kalebu mwana wa Yefune, na akampa Hebroni kama urithi wake.
14 Israel Pathen BOEIPA hnukah a tukkoei dongah Hebron tah tihnin duela Kenizzi Jephunneh capa Kaleb kah rho la om.
Hivyo Hebroni imekuwa mali ya Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi tangu wakati ule, kwa sababu alimwandama Bwana, Mungu wa Israeli, kwa moyo wote.
15 Hebron ming he khaw hlamat vaengah tah Anakim khuikah hlang len Kiriatharba tila om tih a khohmuen te caemrhal lamloh mong.
(Hebroni uliitwa Kiriath-Arba hapo mwanzo, kutokana na huyo Arba ambaye alikuwa mtu mkuu kupita wote miongoni mwa Waanaki.) Kisha nchi ikawa na amani bila vita.