< 2 Manghai 19 >
1 Manghai Hezekiah loh a yaak van neh a himbai te a phen. Tlamhni te a bai tih BOEIPA im la cet.
Mfalme Hezekia aliposikia haya, akararua nguo zake na kuvaa nguo ya gunia, naye akaenda katika Hekalu la Bwana.
2 Te phoeiah im aka hung Eliakim, cadaek Shebna, tlamhni aka bai khosoih ham rhoek te Amoz capa tonghma Isaiah taengla a tueih.
Akawatuma Eliakimu msimamizi wa nyumba ya mfalme, Shebna mwandishi, na viongozi wa makuhani, wote wakiwa wamevaa nguo za magunia, waende kwa nabii Isaya mwana wa Amozi.
3 Te phoeiah Isaiah te, “Hezekiah loh he ni a. thui. Tahae khohnin he tah citcai neh, toelthamnah neh kokhahnah khohnin coeng ni. Camoe om ham a pha coeng dae a cun ham thadueng om pawh.
Wakamwambia, “Hili ndilo asemalo Hezekia: Siku hii ni siku ya dhiki, ya kukaripiwa na ya aibu, kama wakati watoto wanapofikia karibu kuzaliwa na kumbe hakuna nguvu ya kuwazaa.
4 Rabshakeh kah ol cungkuem te na Pathen BOEIPA loh a yaak khaming. Anih te a boei Assyria manghai loh aka hing Pathen veet hamla a tueih. Na Pathen BOEIPA loh a yaak bangla a ol soah a tluung bitni. Te dongah a meet la a hmuh rhoek ham mah thangthuinah khueh mai laeh,” a ti uh.
Yamkini Bwana, Mungu wako atayasikia maneno ya jemadari wa jeshi, ambaye bwana wake, mfalme wa Ashuru, amemtuma kumdhihaki Mungu aliye hai, tena kwamba atamkemea kwa maneno ambayo Bwana, Mungu wako ameyasikia. Kwa hiyo omba kwa ajili ya mabaki ambao bado wako.”
5 Manghai Hezekiah kah sal rhoek te khaw Isaiah taengla pawk uh tangloeng.
Maafisa wa Mfalme Hezekia walipofika kwa Isaya,
6 Te vaengah amih te Isaiah loh, “Na boei rhoek te thui pah. BOEIPA loh he ni a. thui. Ol na yaak soah rhih uh boeh. Assyria manghai kah tueihyoeih rhoek loh kai n'hliphen uh.
Isaya akawaambia, “Mwambieni bwana wenu, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Usiogope kwa hayo uliyoyasikia, yale maneno ambayo watumishi wa mfalme wa Ashuru wamenitukana nayo.
7 Kai loh a khuiah mueihla ka paek tih olthang a yaak coeng ke. Te dongah amah kho la mael bitni. Anih te amah kho ah cunghang dongla ka cungku sak ni,” a ti nah.
Sikiliza! Nitatia roho fulani ndani yake ili atakaposikia taarifa fulani, atarudi nchi yake mwenyewe, nami huko nitafanya auawe kwa upanga.’”
8 Lakhish lamkah a caeh te a yaak vaengah Rabshakeh khaw nong tih Assyria manghai loh Libnah a vathoh thil te a hmuh.
Jemadari wa jeshi aliposikia kwamba mfalme wa Ashuru ameondoka Lakishi, alirudi, akamkuta mfalme akipigana na Libna.
9 Kusah manghai Tirhakah kawng a yaak vaengah khaw, “Nang vathoh thil ham ha pawk coeng ke,” a ti nah. Te dongah mael tih Hezekiah taengla puencawn a tueih.
Basi Senakeribu akapata taarifa kwamba Tirhaka, Mkushi mfalme wa Misri, alikuwa anaenda kupigana naye. Basi akatuma tena wajumbe kwa Hezekia na neno hili:
10 Te vaengah, “Judah manghai Hezekiah te thui pah lamtah, 'A soah na pangtung thil na Pathen loh nang n'rhaithi boel saeh. Jerusalem te Assyria manghai kut ah tloeng mahpawh na ti.
“Mwambieni Hezekia mfalme wa Yuda: Usikubali huyo Mungu unayemtumainia akudanganye wakati anaposema, ‘Yerusalemu haitatiwa mkononi mwa mfalme wa Ashuru.’
11 Assyria manghai rhoek loh diklai tom ah a saii te na yaak coeng he. ‘Amih te a thup ham coeng dongah na loeih uh hatko.
Hakika umesikia yale ambayo wafalme wa Ashuru wametenda kwa nchi zote, wakiwaangamiza kabisa. Je, wewe utaokolewa?
12 Kai napa rhoek aka phae namtom pathen loh amih Gozan neh Haran, Rezeph neh Telassar kah Eden ca rhoek te a huul aya?
Je, miungu ya mataifa ambayo yaliangamizwa na baba zangu iliweza kuwaokoa, hiyo miungu ya Gozani, Harani, Resefu, na ya watu wa Edeni waliokuwa Telasari?
13 Khamath manghai neh Arpad manghai, Hena Sepharvaim neh Ivvah khopuei manghai te ta?” na ti,” a ti nah.
Yuko wapi mfalme wa Hamathi, mfalme wa Arpadi, mfalme wa mji wa Sefarvaimu, au wa Hena au wa Iva?”
14 Hezekiah loh puencawn kut lamkah capat te a doe tih a tae. Te phoeiah BOEIPA im la cet tih Hezekiah loh BOEIPA mikhmuh ah a kut a phuel.
Hezekia akapokea barua kutoka kwa wale wajumbe, naye akaisoma. Kisha akapanda katika Hekalu la Bwana, akaikunjua mbele za Bwana.
15 Hezekiah te BOEIPA mikhmuh ah thangthui tih, “Cherubim ah aka ngol Israel Pathen BOEIPA aw, nang namah bueng ni diklai ram boeih soah Pathen la na om. Namah loh vaan neh diklai na saii.
Naye Hezekia akamwomba Bwana akisema: “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, uketiye juu ya kiti cha enzi kati ya makerubi, wewe peke yako ndiwe Mungu juu ya falme zote za dunia. Wewe umeumba mbingu na nchi.
16 BOEIPA aw na hna kaeng lamtah ya lah, BOEIPA aw na mik dai lamtah hmu laeh. A hing Pathen veet hamla Sennacherib loh ol a pat te hnatun nawn.
Tega sikio, Ee Bwana, usikie; fungua macho yako, Ee Bwana, uone; sikiliza maneno ambayo Senakeribu ametuma kumtukana Mungu aliye hai.
17 BOEIPA aw Assyria manghai rhoek loh namtom rhoek neh a khohmuen te khaw a khah coeng.
“Ni kweli, Ee Bwana, kwamba wafalme wa Ashuru wameyaangamiza mataifa haya na nchi zao.
18 Amih kah pathen rhoek te hmai khuila a pup coeng. Te rhoek te pathen pawt tih hlang kut dongkah bibi, thing neh lungto la a om dongah milh uh coeng.
Wameitupa miungu yao kwenye moto na kuiangamiza, kwa kuwa haikuwa miungu, bali miti na mawe tu iliyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
19 Kaimih kah Pathen BOEIPA aw tahae ah kaimih he anih kut lamloh n'khang laeh. Te daengah ni diklai ram pum loh nang namah bueng te Pathen BOEIPA la m'ming eh?,” a ti.
Sasa basi, Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe kutoka mkononi mwake, ili falme zote duniani zipate kujua kwamba wewe peke yako, Ee Bwana, ndiwe Mungu.”
20 Te dongah Amoz capa Isaiah loh Hezekiah taengla ol atah tih, “Israel Pathen BOEIPA loh he ni a. thui. Assyria manghai Sennacherib kongah kai taengla na thangthui te ka yaak coeng.
Kisha Isaya mwana wa Amozi akapeleka ujumbe kwa Hezekia, akasema: “Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Nimesikia maombi yako kuhusu Senakeribu mfalme wa Ashuru.
21 Ol he BOEIPA loh anih a thui thil coeng. Zion nu, oila nang te n hnoelrhoeng thil uh tih nang te n'tamdaeng coeng. Na hnuk ah Jerusalem nu loh lu a hinghuen.
Hili ndilo neno ambalo Bwana amelisema dhidi yake: “‘Bikira Binti Sayuni anakudharau na kukudhihaki. Binti Yerusalemu anatikisa kichwa chake unapokimbia.
22 Unim na veet tih na hliphen? U taengah nim ol na huel? Israel kah a cim la na maelhmai kah koevoeinah na phueih thil.
Ni nani uliyemtukana na kumkufuru? Ni nani uliyeinua sauti yako dhidi yake, na kumwinulia macho yako kwa kiburi? Ni dhidi ya yule Aliye Mtakatifu wa Israeli!
23 Na puencawn rhoek kah kut lamloh ka Boeipa te na veet tih, “Leng khaw kamah kah leng muep om, kai tah Lebanon hlaep kah tlang sang la ka luei, a lamphai thing sang neh hmaical a hloe khaw ka top. A cangphil cangngol duup a bawtnah kah rhaehim khaw ka pha.
Kupitia kwa wajumbe wako umelundika matukano juu ya Bwana. Nawe umesema, “Kwa magari yangu mengi ya vita, nimepanda juu ya vilele vya milima, vilele vya juu sana katika Lebanoni. Nami nimeiangusha mierezi yake mirefu, misunobari yake iliyo bora sana. Nimefikia sehemu zake zilizo mbali sana, misitu yake iliyo mizuri sana.
24 Kamah loh ka rhawt dae kholong tui ni ka ok. Ka kho dongkah khopha loh Egypt sokko khaw boeih ka kak sak,’ na ti.
Nimechimba visima katika nchi za kigeni na kunywa maji yake. Kwa nyayo za miguu yangu nimekausha vijito vyote vya Misri.”
25 Hlamat tue lamloh ka saii te na ya daengrhae pawt nim? Te te ka hlinsai tih ka thoeng sak coeng. Te dongah vong cak khopuei aka hnuei tih lungkuk aka pong sak la na om coeng.
“‘Je, hujasikia? Zamani sana niliamuru hili. Siku za kale nilipanga hili; sasa nimelifanya litokee, kwamba umegeuza miji yenye ngome kuwa malundo ya mawe.
26 A khuikah khosa rhoek khaw a kut toi uh coeng. Rhihyawp uh tih yak uh coeng. Lohma kah baelhing neh imphu kah baeldaih sulnoe khopol bangla om uh tih canghli kah mawn bangla om.
Watu wa miji hiyo wameishiwa nguvu, wanavunjika mioyo na kuaibishwa. Wao ni kama mimea katika shamba, kama machipukizi mororo ya kijani, kama majani yachipuayo juu ya paa la nyumba, ambayo hukauka kabla ya kukua.
27 Tedae na ngol khaw, na vuenva neh na kunael khaw, kai nan tlai thil te khaw ka ming.
“‘Lakini ninajua mahali ukaapo, kutoka kwako na kuingia kwako, na jinsi unavyoghadhibika dhidi yangu.
28 Kai nan tlai thil tih nan lawn khaw kai hna la ha pawk coeng. Te dongah ka thisum neh na hnarhong ah kan toeh vetih ka kamrhui he na hmuilai ah kam bang ni. Te lamkah na pawk vanbangla nang te tekah longpuei lamloh kam mael sak ni.
Kwa sababu unaghadhibika dhidi yangu, na ufidhuli wako umefika masikioni mwangu, nitaweka ndoana yangu puani mwako na hatamu yangu kinywani mwako, nami nitakufanya urudi kwa njia ile uliyoijia.’
29 He tah nang ham miknoek la om saeh. Kum khat pong vetih kum bae dongah anboe te ca. Kum thum dongah tawn uh lamtah at uh. Misur khaw phung uh lamtah a thaih te ca uh.
“Hii ndiyo itakuwa ishara kwako, ee Hezekia: “Mwaka huu utakula kile kiotacho chenyewe, na mwaka wa pili utakula kutoka machipukizi yake. Lakini katika mwaka wa tatu, panda na uvune, panda mashamba ya mizabibu na ule matunda yake.
30 A dang ah a yung aka sueng Judah imkhui kah rhalyong te a koei vetih a soah a thaih thai ni.
Mara nyingine tena mabaki ya nyumba ya Yuda wataeneza mizizi chini na kuzaa matunda juu.
31 Jerusalem lamkah a meet neh Zion tlang lamkah rhalyong loh a pawk vaengah, caempuei BOEIPA kah thatlainah khaw cung bitni.
Kwa kuwa kutoka Yerusalemu watakuja mabaki, na kutoka Mlima Sayuni kundi la walionusurika. Wivu wa Bwana Mwenye Nguvu Zote ndio utatimiza jambo hili.
32 Te dongah BOEIPA loh Assyria manghai kongah he ni a. thui. Anih te he khopuei la ha pawk mahpawh. Heah he thaltang khaw nuen mahpawh. photling te khaw dan pawt vetih tanglung khaw lun thil mahpawh.
“Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana kuhusu mfalme wa Ashuru: “Hataingia katika mji huu wala hatapiga mshale hapa. Hatakuja mbele yake akiwa na ngao, wala kupanga majeshi kuuzingira.
33 Tekah longpuei lamloh ha pawk vanbangla te lamlong ni a. mael eh. He khopuei khuila kun mahpawh. He tah BOEIPA kah olphong coeng ni.
Kwa njia ile aliyoijia, ndiyo atakayorudi; hataingia katika mji huu, asema Bwana.
34 Kamah ham neh ka sal David kongah khopuei he daem sak ham ka tungaep ni,” a ti nah.
Nitaulinda mji huu na kuuokoa, kwa ajili yangu mwenyewe, na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.”
35 Te khoyin ah tah BOEIPA kah puencawn te cet tangloeng tih Assyria caem khuikah te thawng yakhat sawmrhet thawng nga a ngawn. Te dongah mincang kah a thoh uh vaengah tah amih te a rhok la boeih ana duek.
Usiku ule, malaika wa Bwana akaenda, akawaua wanajeshi 185,000 katika kambi ya Waashuru. Wenzao walipoamka asubuhi yake, walikuta maiti kila mahali!
36 Te dongah puen uh tih a nong phoeiah tah Assyria manghai Sennacherib khaw mael tih Nineveh ah kho a sak.
Basi Senakeribu mfalme wa Ashuru akavunja kambi na kuondoka. Akarudi Ninawi na kukaa huko.
37 Te phoeiah om tih anih te a pathen Nisrock im ah tho a thueng dae a capa Adrammelech neh Sharezer loh cunghang neh a ngawn. Amih rhoi te Ararat kho la a poeng rhoi dongah a capa Esarhaddon te anih yueng la manghai.
Siku moja, alipokuwa akiabudu katika hekalu la mungu wake Nisroki, wanawe Adrameleki na Shareza wakamuua kwa upanga, nao wakakimbilia nchi ya Ararati. Naye Esar-Hadoni mwanawe akawa mfalme badala yake.