< 1 Samuel 27 >

1 David loh a lungbuei ah, “Hnin at atah Saul kut neh ka khoengvoep uh pawn ni. Kai ham a then pawt lakah tah Philisti kho la ka poeng ka hal mai eh. Te daengah ni Israel khorhi khui boeih atah kai tlap ham akhaw Saul loh kai taeng lamkah vi uh vetih a kut te ka poeng ka hal eh,” a ti.
Daudi akasema moyoni mwake, “Katika mojawapo ya siku hizi nitaangamizwa kwa mkono wa Sauli. Jambo lililo bora ni kutorokea kwenye nchi ya Wafilisti. Hivyo Sauli atakata tamaa ya kunisaka popote katika Israeli, nami nitakuwa nimeponyoka mkononi mwake.”
2 Te phoeiah David te thoo tih, a taengkah hlang ya rhuk neh Gath manghai Maoch capa Akhish te a paan.
Hivyo Daudi akaondoka na hao watu mia sita waliokuwa pamoja naye na kwenda kwa Akishi mwana wa Maoki mfalme wa Gathi.
3 David amah neh a hlang rhoek khaw, a hlang kah a imkhui khaw, David neh a yuu rhoi Jezreel nu Ahinoam, Karmel Nabal yuu Abigail khaw, Gath kah Akhish taengah kho a sak.
Daudi na watu wake wakakaa huko Gathi pamoja na Akishi. Kila mtu alikuwa pamoja na jamaa yake, naye Daudi pamoja na wakeze wawili: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili wa Karmeli, mjane wa Nabali.
4 Gath la David a yong te Saul taengla a puen pah ngawn dae David tlap koep ham te khoep rhoe khoep voel pawh.
Sauli alipokuwa ameambiwa kwamba Daudi alikuwa amekimbilia Gathi, hakuendelea kumsaka tena.
5 Te vaengah David loh Akhish taengah, “Na mikhmuh ah mikdaithen ni ka dang atah, khohmuen kah khopuei pakhat ah kai he hmuen m'pae mai lamtah pahoi ka om mai eh. Ram kah khopuei khuiah na sal loh namah taengah kho a sak te ba ham lae?” a ti nah.
Ndipo Daudi akamwambia Akishi, “Kama nimepata kibali machoni pako, unipe sehemu katika mojawapo ya miji katika nchi nikae huko. Kwa nini mtumwa wako akae pamoja nawe katika mji huu wa kifalme?”
6 Tekah khohnin ah anih te Akhish loh Ziklag kho te a paek. Te dongah Ziklag he tihnin hil Judah manghai rhoek kah la om.
Hivyo siku hiyo Akishi akampa Daudi mji wa Siklagi, nao Siklagi umekuwa mali ya wafalme wa Yuda tangu wakati huo.
7 David loh Philisti khohmuen ah kho a sak te a khohnin khaw amah tarhing atah kum at neh hla li lo coeng.
Daudi akaishi katika nchi ya Wafilisti muda wa mwaka mmoja na miezi minne.
8 Te vaengah David neh a hlang rhoek loh cet uh tih Geshuri neh Gezari te a cuuk thil uh. Tedae te khohmuen kah khosa rhoek Gezari neh Amalek rhoek tah khosuen lamloh Shur neh Egypt kho duela na paan tangtae ni.
Basi Daudi na watu wake wakapanda na kuwashambulia Wageshuri, Wagirizi na Waamaleki. (Tangu zamani haya mataifa yalikuwa yameishi kwenye eneo lililotanda kuanzia Telemu katika njia iteremkayo Shuri hadi kufikia nchi ya Misri.)
9 Khohmuen te David loh a ngawn tih huta khaw tongpa khaw hing sak pawh. Tedae boiva, saelhung, laak, kalauk neh himbai te a loh tih a mael daengah Akhish te a paan.
Kila mara Daudi aliposhambulia eneo, hakubakiza hai mwanaume wala mwanamke, lakini alichukua kondoo na ngʼombe, punda na ngamia, na nguo. Kisha akarudi kwa Akishi.
10 Te vaengah Akhish loh, “Tihnin atah na muk mahpawt a?” a ti nah hatah David loh, “Judah tuithim neh Jerahmeli tuithim, Keni tuithim a?” a ti nah.
Akishi alipomuuliza, “Je leo umeshambulia wapi?” Daudi humjibu, “Dhidi ya Negebu ya Yuda,” au wakati mwingine husema, “Dhidi ya Negebu ya Yerameeli,” au “Dhidi ya Negebu ya Wakeni.”
11 Tedae David kah a saii neh a thui soah, “Kaimih kawng he Gath la a khuen vetih puen ve,” a ti dongah David loh huta khaw tongpa khaw hlun pawh. Tekah khosing nen ni Philisti kho kah a om tue khuiah kho a sak.
Daudi hakumwacha hai mwanaume au mwanamke ili apate kuletwa Gathi, kwa maana Daudi aliwaza, “Wanaweza kujulisha habari zetu na kusema, ‘Hivi ndivyo alivyofanya Daudi.’” Hii ndiyo ilikuwa desturi yake wakati wote aliishi katika nchi ya Wafilisti.
12 Te vaengah Akhish loh David te a tangnah tih, “A pilnam Israel taengah a bo rhim la rhim coeng tih kamah taengah kumhal sal la om saeh,” a ti.
Akishi akamsadiki Daudi na kuwaza moyoni mwake, akasema, “Daudi amekuwa kitu cha kuchukiza kabisa kwa watu wake, Waisraeli, hivi kwamba atakuwa mtumishi wangu milele.”

< 1 Samuel 27 >