< Kalatih 4 >

1 Cunsepi, hin kba pyen be tü veng: a pa khawh mkhäm khaia ahmäi cun capa a ka vai kyase pi a nghmaw ham üng cun m'ya mäiha ni ngaih khawi.
Ninasema kwamba maadamu mrithi ni mtoto, hana tofauti na mtumwa, hata ingawa ni mmiliki wa mali yote.
2 A nghmaw ham üng a pa naw a mhnütnaka kcün am a pha ham üng msumcei khaia khyang he awmki he.
Badala yake, yuko chini ya waangalizi na wadhamini mpaka wakati uliowekwa na baba yake.
3 Acukba mimi pi ngmüimkhya lama am mi xüxam ham üng cun khawmdek ukia ngmüimkhya he keha m'ya mi kyaki.
Kadhalika pia na sisi, tulipokuwa watoto, tulishikiliwa katika utumwa wa kanuni za kwanza za ulimwengu.
4 Cunsepi akcüna pha law üng Pamhnam naw amäta Capa a tüih law. Nghngicim nghnumia capa mäiha law lü Judah he Thuma keha xüngseiki,
Lakini wakati sahihi ulipofika, Mungu alimtuma mwanawe, mzaliwa wa mwanamke, mzaliwa chini ya sheria.
5 Thuma keha awmki he jah thawng se, Pamhnama ca he mi kya lawnak vaia kyaki.
Alifanya hivi ili kuwakomboa wale waliokuwa chini ya sheria, ili kwamba tupokee hali ya kuwa kama wana.
6 A ca he nami kyanak mdanak vaia Pamhnam naw a Capaa Ngmüimkhya cun nami mlung k’uma a tüih law. Acuna Ngmüimkhya naw, “Ka Pa, ka Pa” tia ngpyangki.
Kwa sababu ninyi ni wana, Mungu alimtuma Roho wa mwanawe ndani ya mioyo yetu, Roho aitaye, “Abba, Baba.”
7 Acunakyase m'yaa am kya ti u lü capa nami kyaki. A capa nami kya pängkia kyase Pamhnam naw a capaa phäh vai a tak avan ning jah pe khai.
Kwa sababu hii wewe si mtumwa tena bali mwana. Kama ni mwana, basi wewe pia ni mrithi kupitia Mungu.
8 Tuhkbäih Pamhnam nami ksingki am acunüng Pamhnam naw ning jah ksingki ti veng. Ise a ktha kcek lü m'yenei phyakia ngmüimkhya veia nami nglat be vai nami ngaihki ni.
Hata kabla, wakati hamkumjua Mungu, mlikuwa watumwa kwa wale ambao kwa asili si miungu kabisa.
9 Mhnam nami ksing kän la Mhnam naw a ning jah ksing käna, Ise am ktha mah lü m'yenei phyakia ngmüimkhya veia nami nghlat be vai nami ngaihki ni ti pyen hlü veng? Ise acun hea m'ya nami kya vai cun nami ngaih beki ni?
Lakini sasa kwamba mnamjua Mungu, au kwamba mnajulikana na Mungu, kwa nini mnarudi tena kwenye kanuni dhaifu za kwanza na zisizo za thamani? Je mnataka kuwa watumwa tena?
10 Khawmhmüp he, nghngi khya he, akcün he la khawkum he, nami jah künaki.
Mnashika kwa uangalifu siku maalumu, miandamo ya miezi, majira, na miaka. Ninaogopa kwa ajili yenu.
11 Ning jah cäi na veng! Nami phäha ka kthanak avan amdanga kya khai aw?
Ninaogopa kwamba kwa namna fulani nimejitaabisha bure.
12 Ka püi he aw, “Keia mäiha awm u” tia ning jah nghui na veng. Nangmia mäih ka lawki. Akse ka khana nami bi am ve.
Ninawasihi, ndugu, muwe kama nilivyo, kwa kuwa pia nimekuwa kama mlivyo. Hamkunikosea.
13 Akcüka nami veia ivai thangkdaw ka pyen ni ti cen süm ua; am ka phetyaia phäha kyaki ni.
Bali mnajua kwamba ilikuwa ni kwa sababu ya ugonjwa wa mwili kwamba nilihubiri injili kwenu kwa mara ya kwanza.
14 Ka pumsa üng am ka phetyainak cen nami hama khameinaka kyase pi am na hmumsit u lü, am nami na yawkinki. Khankhaw üngka khankhawngsä mata mäiha nami na dokhamki. Jesuh Khritawa mäiha nami na dokhamki.
Ingawa hali yangu ya mwili iliwaweka katika jaribu, hamkunidharau au kunikataa. Badala yake mlinipokea kama malaika wa Mungu, kana kwamba nilikuwa Kristo Yesu mwenyewe.
15 Aktäa nami jekyaiki! Ise ni? Akya thei vai sü ta nami mik pi lo u lü nami na pe khai sü ti kamät naw pyen thei veng.
Kwa hiyo, iko wapi sasa furaha yenu? kwa kuwa ninashuhudia kwenu kwamba, ikiwezekana, mungelin'goa macho yenu na kunipa mimi.
16 Ngthungtak ka ning jah mtheha phäha nami yea ka kya lawki aw?
Hivyo sasa, je nimekuwa adui yenu kwa sababu ninawaambia ukweli?
17 Khyang kce he naw ning jah kü na leng lengkia mäiha awmki he, cunsepi ami ning jah künak am daw. Ami ning jah künaka kba nami jah künak be vaia phäha kei üngka ning jah mtai hlü ve u.
Wanawatafuta kwa shauku, bali si kwa mema. Wanataka kuwatenganisha ninyi na mimi ili muwafuate.
18 Bünak a daw üng ta künak hin dawki ni. Nami hlawnga ka awma kcün däng üng am kyakia nami hlawnga am ka awm üng pi.
Ni vyema daima kuwa na shauku kwa sababu zilizo njema, na si tu wakati ninapokuwa pamoja nanyi.
19 Ka cana he aw, Khritawa ngneiksak nangmi üng am a awm hama küt üng ta nghnumi naw a ca law vai üng a huieia kba nami hama na huiei ve.
Wanangu wadogo, ninaumwa uchungu kwa ajili yenu tena mpaka Kristo aumbike ndani yenu.
20 Atuh nami hlawnga ka ve vai ngaih veng. Ahin kba am ka ning jah tinak vai sü. Aktäa ning jah cäi na veng.
Ningependa kuwepo pale pamoja nanyi sasa na kugeuza sauti yangu, kwa sababu ninamashaka juu yenu.
21 Thuma keha awm hlüki he ning jah kthäh vang: Thum naw i a pyen am nami ngjaki aw?
Niambieni, ninyi ambao mnatamani kuwa chini ya sheria, hamsikii sheria isemavyo?
22 Abraham naw cangpyang nghngih ca naki. Mat m'yanua ca kya lü mat cun m'yanu am nikia ca kyaki.
Kwa kuwa imeandikwa kwamba Abrahamu alikuwa na wana wa kiume wawili, mmoja kwa yule mwanamke mtumwa na mwingine kwa mwanamke huru.
23 M'yanu am ani ca cun pumsa thuma hmi lü, m'yanu am niki am ani ca cun khyütama thuma hmi lawkia kyaki tia pyenki.
Hata hivyo, yule wa mtumwa alizaliwa kwa mwili tu, bali yule wa mwanamke huru alizaliwa kwa ahadi.
24 Acuna ngthu cun msuimcäpnaka kyaki ti ksing theia kyaki; acuna nghnuminu xawi cun ngthumkhän nghngiha kyaki xawi. M'ya jah ca nakia nghnumi Hakarah cun Sinai mcung üng pawha ngthumkhäna kyaki.
Mambo haya yanaweza kuelezwa kwa kutumia mfano, kwa kuwa wanawake hawa wanafanana na maagano mawili. Mojawapo kutoka katika mlima Sinai. Huzaa watoto ambao ni watumwa. huyu ni Hajiri.
25 Arab khawa Sinai mcunga nghnün üng ngdüikia Hakarah cun, tuhkbäih Jerusalem a khyang he mah mah am m'yaa kyaki msuimcäpnaka kyaki.
Sasa Hajiri ni mlima Sinai ulioko Arabuni. Hufananishwa na Yerusalem ya sasa, kwa kuwa ni mtumwa pamoja na watoto wake.
26 Cunsepi khankhaw Jerusalem cun m'ya am kyakia kyase, acun cun mi nua kyaki.
Bali Yerusalemu ambayo iko juu ni huru, na hii ndiyo mama yetu.
27 “Na cingkia nghnumi jekyaia! Na am pawi na khawi lü na hmia natnak am na khamei khawiki je lü ngpyanga! A cei naw am a yawk khawia nghnumia kthaka a cei naw am a ktä naw hnasen da na bawk khai” tia cangcim naw pyenki.
Kwa kuwa imeandikwa, “Furahi, wewe mwanamke uliye tasa, wewe usiye zaa. Paza sauti na upige kelele kwa furaha, wewe ambaye huna uzoefu wa kuzaa. kwa maana wengi ni watoto wa aliye tasa, zaidi ya wale wa yule ambaye ana mume.”
28 Acunakyase ka püi he aw, nangmi cun Isaka mäiha khyütama phäha Pamhnama ca hea nami kyaki.
Sasa ndugu, kama Isaka, ninyi ni watoto wa ahadi.
29 Acuna kcün üng pumsa thuma hmi lawki naw Pamhnama Ngmüimkhya thuma hmi lawki a mkhuimkha khawia kba; tuhkbäih pi acuna mäih lawki.
Kwa wakati ule ambao mtu ambaye alizaliwa kwa mujibu wa mwili alimtesa yule aliyezaliwa kwa mujibu wa Roho. Kwa sasa ni vilevile.
30 Cunsepi, cangcim naw, “M'yanu cun a capa am jah ksäta; m'yanua capa naw ä m'yanua capa khawh ä mkhämpüi khai” tia a pyen.
Maandiko husemaje? “Muondoe mwanamke mtumwa pamoja na mwanawe wa kiume. Kwa kuwa mtoto wa mwanamke mtumwa hatarithi pamoja na mtoto wa mwanamke huru.”
31 Acunakyase ka püi he aw, mimi cun m'yanua ca am mi kya u lü ä m'yanua ca hea mi kyaki.
Kwa hiyo, ndugu, sisi si watoto wa mwanamke mtumwa, bali ni wa mwanamke huru.

< Kalatih 4 >