< Съдии 3 >

1 А ето народите, които Господ остави, за да изпита чрез тях Израиля, всички от тях, които не знаеха всичките ханаански богове:
Sasa Bwana aliyaacha mataifa haya yaijaribu Israeli, yaani kila mtu katika Israeli ambaye hakushiriki vita yoyote huko Kanaani.
2 само за да знаят и да се научат на бой поне тия от поколенията на израилтяните, които най-напред не са знаели; именно:
(Alifanya hivyo ili kuwafundisha vita kizazi kipya cha Waisraeli ambao hawakujua kabla).
3 петте началници на филистимците, и всичките ханаанци, сидонци и евейци, които живеят в Ливанската планина, от планината Ваалермон до прохода на Емат.
Haya ndio mataifa: wafalme watano kutoka kwa Wafilisti, Wakanaani wote, Wasidoni, na Wahivi waliokaa milima ya Lebanoni, kutoka Mlima Baali Hermoni hadi Hamathi.
4 Те служеха, за да се изпита Израил чрез тях та да се знае, ще слушат ли заповедите, които Господ заповяда на бащите им чрез Моисея.
Mataifa haya yaliachwa kama njia ambayo Bwana angeijaribu Israeli, kuthibitisha kama watazitii amri alizowapa babu zao kupitia Musa.
5 Така също израилтяните се заселиха между ханаанците, хетейците, аморейците, ферезейците, евейците и евусейците;
Basi wana wa Israeli wakakaa kati ya Wakanaani, na Wahiti, na Waamori, na Waperizi, na Wahivi, na Wayebusi.
6 и вземаха си дъщерите им за жени, и даваха дъщерите си на синовете им, и служеха на боговете им.
Waliwachukua binti zao kuwa wake zao, nao wakawapa wana wao binti zao, nao wakaitumikia miungu yao.
7 И израилтяните сториха зло пред Господа, като забравиха Господа своя Бог и служеха на ваалимите и на ашерите.
Wana wa Israeli walifanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, wakamsahau Bwana, Mungu wao. Waliabudu Baali na Asherah.
8 Затова гневът на Господа пламна против Израиля, и Той ги предаде в ръката на месопотамския цар Хусанрисатаима; и израилтяните бяха подчинени на Хусанрисатаима осем години.
Basi, hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawauza mkononi mwa Kushan-rishathaimu mfalme wa Aram Naharaimu. Watu wa Israeli walitumikia Kushan Rishathaimu kwa miaka nane.
9 А когато израилтяните извикаха към Господа, Господ въздигна избавител на израилтяните, който ги спаси, Готониила син на Кенеза, по-младият брат на Халева.
Watu wa Israeli walipomwomba Bwana, Bwana akamuinua mtu atakayewasaidia wana wa Israeli, na mtu atakayewaokoa: Othnieli mwana wa Kenazi (ndugu mdogo wa Kalebu).
10 Дух Господен дойде върху него, и той съди Израиля. Излезе и на бой, и Господ предаде в ръката му месопотамския цар Хусанрисатаима; и ръката му преодоля против Хусанрисатаима.
Roho wa Bwana akamtia nguvu, naye akahukumu Israeli na akatoka kwenda vitani. Bwana akampa kuishinda Kush-rishataimu mfalme wa Aramu. Mkono wa Othnieli alishinda Kushan Rishathaimu.
11 Тогава земята имаше спокойствие четиридесет години. И Готониил Кенезовият син умря.
Nchi ilikuwa na amani kwa miaka arobaini. Ndipo Otinieli mwana wa Kenazi akafa.
12 Пак израилтяните сториха зло пред Господа; и Господ укрепи моавския цар Еглон против Израиля, по причина, че сториха зло пред Господа.
Baada ya hayo, Waisraeli wakafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana; Bwana akampa Egloni mfalme wa Moabu nguvu, kuwashinda Waisraeli.
13 И той събра при себе си амонците и амаличаните и отиде та порази Израиля, и завладя Града на палмите.
Eglon alijiunga na wana wa Amoni na Waamaleki wakaenda na kuwashinda Israeli, na walichukua mji wa Mitende.
14 И израилтяните бяха подчинени на моавския цар Еглон осемнадесет години.
Watu wa Israeli walimtumikia Eglon mfalme wa Moabu kwa miaka kumi na nane.
15 А когато израилтяните извикаха към Господа, Господ им въздигна избавител, Аода син на вениаминеца Гира, мъж левак. Чрез него израилтяните пратиха подарък на моавския цар Еглон;
Wana wa Israeli walipomwomba Bwana, Bwana akamwinua mtu aliyewasaidia, Ehudi mwana wa Gera, Mbenjamini, mtu shoto. Wana wa Israeli wakamtuma kwa Egloni, mfalme wa Moabu, kwa malipo yao ya kodi.
16 но Аод си направи меч остър и от двете страни, дълъг един лакът, и опаса го под горната си дреха на дясното си бедро.
Ehudi akajifanyia upanga uliokuwa na makali kuwili, urefu wa dhiraa moja; aliufunga chini ya nguo zake juu ya mguu wake wa kulia.
17 Той, прочее, принесе подаръка на моавския цар Еглон. А Еглон беше човек твърде тлъст.
Akampa Egloni Mfalme wa Moabu malipo ya kodi. (Egloni alikuwa mtu mnene sana.)
18 И като свърши да принесе подаръка, и изпрати човеците, които носеха подаръка,
Baada ya Ehudi kulipa malipo ya kodi, aliondoka na wale waliokuwa wameibeba.
19 той се върна от пограничните камъни които са при Галгал, и каза: Имам тайна дума за тебе, царю. А той му рече: Мълчи. И излязоха от него всичките, които стояха при него.
Hata hivyo Ehudi mwenyewe, alipofikia mahali ambapo sanamu za kuchonga zilitengenezwa karibu na Gilgali, akageuka na kurudi, akasema, 'Nina ujumbe wa siri kwako, mfalme wangu.' Eglon akasema, 'Nyamazeni kimya!' Kwa hiyo wote waliomtumikia wakatoka kwenye chumba.
20 Тогава Аод дойде при него; и той седеше сам в лятната си горна стая. И рече Аод: Имам дума от Бога за тебе. Тогава той стана от стола си.
Ehudi akaja kwake. Mfalme alikuwa amekaa peke yake, peke yake katika chumba cha juu cha baridi. Ehudi akasema, 'Nina ujumbe kutoka kwa Mungu kwa ajili yeko.' Mfalme akasimama kutoka katika kiti chake.
21 А Аод простря лявата си ръка и, като измъкна меча от дясното си бедро, заби го в корема му
Ehudi akanyoosha mkono wake wa kushoto na akachukua upanga kutoka mguu wake wa kulia, na akautia ndani ya mwili wa mfalme.
22 толкоз, щото и дръжката влезе след желязото; и тлъстината до там стисна желязото, щото не можеше да изтръгне из корема му меча, който излезе отзад.
Na kipini cha upanga kikaingia ndani yake baada ya upanga, nao ukatokea nyuma yake, na mafuta yakashikamana juu ya upanga, kwa kuwa Ehudi hakuutoa upanga nje ya mwili wake.
23 Тогава Аод излезе през трема и затвори след себе си вратата на горната стоя, и я заключи.
Kisha Ehudi akatoka kwenye ukumbi na akafunga milango ya chumba cha juu nyuma yake na akawafungia.
24 А когато излезе той, дойдоха слугите на Еглона, и, като видяха, че, ето, вратата на горната стая беше заключена, рекоха: Без съмнение по нуждата си е в лятната стая.
Baada ya Ehudi kuondoka, watumishi wa mfalme wakaja; wakaona milango ya chumba cha juu imefungwa, kwa hiyo wakafikiri, 'Hakika atakuwa anajitoa mwenyewe katika hali ya baridi ya chumba cha juu.'
25 Но макар че чакаха догде ги хвана срам, ето, той не отваряше вратата на горната стая, затова, взеха ключа та отвориха, и, ето, господарят им лежеше мъртъв на земята.
Walizidi kuwa na wasiwasi hata walipoanza kuhisi kuwa walikuwa wakipuuza wajibu wao wakati mfalme bado hakufungua milango ya chumba cha juu. Kwa hiyo walichukua ufunguo wakawafungua, tazama bwana wao, ameanguka chini, amekufa.
26 А докато те се бавеха, Аод избяга; и премина пограничните камъни, та се отърва в Сеирота.
Wakati watumishi wakisubiri, wakijiuliza nini wanapaswa kufanya, Ehudi alikimbia na kupita mahali ambako kulikuwa na sanamu za kuchonga, na hivyo akakimbia kwenda Seira.
27 И когато дойде, засвири с тръба в Ефремовата хълмиста земя, та израилтяните слязоха с него от хълмистата земя, и той бе на чело.
Alipofika, alipiga tarumbeta katika nchi ya mlima wa Efraimu. Kisha wana wa Israeli wakashuka pamoja naye kutoka milimani, naye akawaongoza.
28 И рече им: Вървете подир мене, защото Господ предаде неприятелите ви моавците в ръката ви. И те слязоха подир него, и като превзеха бродовете на Иордан към моавската страна, не оставиха да премине ни един човек.
Akawaambia, Nifuate, kwa kuwa Bwana atawashinda adui zenu, Wamoabu. Wakamfuata, wakakamata vivuko vya Bonde la Yordani, toka kwa Wamoabi, wala hawakuruhusu mtu yeyote kuvuka mto.
29 И в онова време поразиха от моавците около десет хиляди мъже, всички едри и всички яки; не се избави ни един човек.
Wakati huo waliwaua watu elfu kumi wa Moabu, na wote walikuwa watu wenye nguvu na wenye uwezo. Hakuna aliyekimbia.
30 Така в онова време Моав се покори под ръката на Израиля. Тогава земята имаше спокойствие осемдесет години.
Kwa hiyo siku hiyo Moabu ilishindwa na nguvu ya Israeli. Na nchi ilikuwa na amani kwa miaka thelathini.
31 След него настана времето на Самегар Анатовият син, който с един волски остен порази шестстотин мъже от филистимците; също и той избави Израиля.
Baada ya Ehudi, mwamuzi aliyefuata alikuwa Shamgari mwana wa Anathi ambaye aliwaua Wafilisti 600 kwa konzo la ng'ombe. Pia aliwaokoa Israeli kutoka kwenye hatari.

< Съдии 3 >