< Яков 3 >

1 Братя мои, не ставайте мнозина учители, като знаете, че ще приемем по-тежко осъждане.
Ndugu zangu, msiwe walimu wengi, kwa maana mnafahamu kwamba sisi tufundishao tutahukumiwa vikali zaidi.
2 Защото всички ние в много неща грешим; а който не греши в говорене, той е съвършен мъж, способен да обуздае и цялото тяло.
Sisi sote tunajikwaa katika mambo mengi. Ikiwa mtu yeyote hakosei kamwe katika yale anayosema, yeye ni mkamilifu, naye anaweza kuuzuia pia na mwili wake wote.
3 Ето, ние туряме юздите в устата на конете, за да ни се покоряват, и обръщаме цялото им тяло.
Tunapotia lijamu kwenye vinywa vya farasi ili kuwafanya watutii, tunaweza kuigeuza miili yao yote.
4 Ето, и корабите, ако да са толкова големи, и се тласкат от силни ветрове, пак с твърде малко кормило се обръщат на където желае кормчията.
Au angalia pia meli, ingawa ni kubwa sana, nazo huchukuliwa na upepo mkali, lakini hugeuzwa kwa usukani mdogo sana, kokote anakotaka nahodha.
5 Така и езикът е малка част от тялото, но много се хвали. Ето, съвсем малко огън, колко много вещество запалва!
Vivyo hivyo ulimi ni kiungo kidogo sana katika mwili, lakini hujivuna majivuno makuu. Fikirini jinsi moto mdogo unavyoweza kuteketeza msitu mkubwa!
6 И езикът, тоя цял свят от нечестие, е огън. Между нашите телесни части езикът е, който заразява цялото тяло и запалва колелото на живота, ни, а сам той се запалва от пъкъла. (Geenna g1067)
Ulimi pia ni moto, ndio ulimwengu wa uovu kati ya viungo vya mwili. Ulimi huutia mwili wote wa mtu unajisi na kuuwasha moto mfumo mzima wa maisha yake, nao wenyewe huchomwa moto wa jehanamu. (Geenna g1067)
7 Защото всякакъв вид зверове, птици, гадини, и морски животни се укротяват и укротени са били от човечеството;
Kwa maana kila aina ya wanyama, ndege, wanyama watambaao na viumbe vya baharini vinafugika na vimefugwa na binadamu,
8 но езикът никой човек не може да укроти; буйно зло е, пълен е със смъртоносна отрова.
lakini hakuna mtu awezaye kuufuga ulimi. Ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti.
9 С него благославяме Господа и Отца, и с него кълнем човеците създадени по Божие подобие!
Kwa ulimi tunamhimidi Bwana, yaani Baba yetu, na kwa huo twawalaani watu walioumbwa kwa mfano wa Mungu.
10 От същите уста излизат благословения и проклятия! Братя мои, не трябва това така да бъде.
Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haistahili kuwa hivyo.
11 Изворът пуща ли от същото отверстие сладка и горчива вода?
Je, chemchemi yaweza kutoa katika tundu moja maji matamu na maji ya chumvi?
12 Възможно ли е, братя мои смоковницата да роди маслини, или лозата смокини? Така също не може солената вода да дава сладка.
Je, ndugu zangu, mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Wala chemchemi ya maji ya chumvi haiwezi kutoa maji matamu.
13 Кой от вас е мъдър и разумен? Нека показва своите дела чрез добрият си живот, с кротостта на мъдростта.
Ni nani aliye na hekima na ufahamu miongoni mwenu? Basi na aionyeshe hiyo kwa maisha yake mema na kwa matendo yake yaliyotendwa kwa unyenyekevu utokanao na hekima.
14 Но ако в сърцето си имате горчива завист и крамолничество, не се хвалете и не лъжете против истината.
Lakini ikiwa mna wivu na ni wenye chuki na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu kwa ajili ya hayo wala msiikatae kweli.
15 Това не е мъдрост, която слиза отгоре, но е земна, животинска, бесовска;
Hekima ya namna hiyo haishuki kutoka mbinguni, bali ni ya kidunia, isiyo ya kiroho, na ya kishetani.
16 защото, гдето има завист и крамолничество, там има бъркотия и всякакво лошо нещо.
Kwa maana panapokuwa na wivu na ubinafsi, ndipo penye machafuko na uovu wa kila namna.
17 Но мъдростта, която е отгоре, е преди всичко чиста, после миролюбива, кротко умолима, пълна с милост и добри плодове, примирителна, нелицемерна.
Lakini hekima itokayo mbinguni kwanza ni safi, kisha inapenda amani, tena ni ya upole, iliyo tayari kusikiliza wengine kwa unyenyekevu, iliyojaa huruma na matunda mema, isiyopendelea mtu, tena isiyokuwa na unafiki.
18 А плодът на правдата се сее с мир от миротворците.
Mavuno ya haki hupandwa katika amani na wale wafanyao amani.

< Яков 3 >