< Битие 38 >

1 По онова време Юда се отдели от братята си и свърна при един одоламец на име Ира.
Wakati ule, Yuda akawaacha ndugu zake, akaenda kuishi na Hira Mwadulami.
2 И Юда като видя там дъщерята на един ханаанец, на име Суя, взе я и влезе при нея.
Huko Yuda akakutana na binti wa Kikanaani aitwaye Shua, akamwoa na akakutana naye kimwili,
3 И тя зачна и роди син; и той го наименува Ир.
akapata mimba, akamzaa mwana, ambaye alimwita Eri.
4 И зачна пак и роди син; и тя го наименува Онан.
Akapata mimba tena, akamzaa mwana na kumwita Onani.
5 Пак роди и друг син и го наименува Шела. А Юда беше в Ахдив, когато тя го роди.
Akamzaa mwana mwingine tena, akamwita Shela. Huyu alimzalia mahali paitwapo Kezibu.
6 След време Юда взе жена за първородния си Ир, на име Тамар.
Yuda akampatia Eri, mzaliwa wake wa kwanza, mke aitwaye Tamari.
7 А Ир, Юдовият първороден, беше нечестив пред Господа; и Господ го уби.
Lakini Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu machoni pa Bwana, kwa hiyo Bwana akamuua.
8 Тогава рече Юда на Онана: Влез при братовата си жена и извърши към нея длъжността на девер и въздигни потомството на брата си.
Kisha Yuda akamwambia Onani, “Kutana kimwili na mke wa ndugu yako, na utimize wajibu wako kwake kama mke wa ndugu yako, ili umpatie ndugu yako uzao.”
9 Но Онан знаеше, че потомството нямаше да бъде негово; затова, когато влизаше при братовата си жена, изливаше семето си на земята, за да не въздигне потомство на брата си.
Lakini Onani alijua kwamba uzao haungekuwa wake, kwa hiyo kila alipokutana kimwili na mke wa ndugu yake, alimwaga chini mbegu za kiume ili asimpatie ndugu yake uzao.
10 А това, което правеше, бе зло пред Господа; затова и него уби.
Alichofanya kilikuwa kiovu machoni pa Bwana, hivyo, pia Bwana akamuua Onani.
11 Тогава, Юда, рече на снаха си Тамар: Живей, като вдовица в бащиния си дом, догде отрасне син ми Шела; защото си думаше: Да не би и той да умре като братята си. И така, Тамар отиде и живя в бащиния си дом.
Kisha Yuda akamwambia Tamari mkwewe, “Ishi kama mjane nyumbani mwa baba yako mpaka mwanangu Shela atakapokua.” Kwa maana alifikiri, “Angeweza kufa pia kama ndugu zake.” Kwa hiyo Tamari alikwenda kuishi nyumbani kwa baba yake.
12 След дълго време, Юдовата жена, дъщеря на Суя, умря; и като се утеши Юда, отиде, той и приятелят му, одоламецът Ира, при стригачите на овците си в Тамна.
Baada ya muda mrefu mke wa Yuda binti wa Shua akafariki. Baada ya msiba, Yuda alikwenda Timna, kwa watu waliokuwa wakikata kondoo wake manyoya, naye alifuatana na rafiki yake Hira Mwadulami.
13 И известиха на Тамар, казвайки: Ето, свекърът ти отива в Тамна, за да стриже овците си.
Tamari alipoambiwa, “Baba mkwe wako yuko njiani kwenda Timna kukata kondoo wake manyoya,”
14 Тогава тя съблече вдовишките си дрехи, покри се с покривалото си, обви се и седна при кръстопътя на Енаим, който е по пътя за Тамна; защото видя, че порасна Шела, а тя не му бе дадена за жена.
alivua mavazi yake ya ujane, akajifunika kwa shela ili asifahamike, akaketi kwenye mlango wa Enaimu, ambao upo njiani kuelekea Timna. Akafanya hivyo kwa sababu aliona kwamba, ingawa Shela amekua, lakini alikuwa hajakabidhiwa kwake kuwa mkewe.
15 А Юда, като я видя, помисли, че е блудница: защото беше покрила лицето си.
Yuda alipomwona alifikiri ni kahaba, kwa sababu alikuwa amefunika uso wake.
16 Той, прочее, свърна към нея на пътя и рече: Остави ме, моля, да вляза при тебе; ( защото не позна, че беше снаха му ). И тя рече: Какво ще ми дадеш, за да влезеш при мене?
Pasipo kutambua kwamba alikuwa mkwe wake, akamwendea kando ya njia na kumwambia, “Njoo sasa, nikutane na wewe kimwili.” Yule mkwewe akamuuliza, “Utanipa nini nikikutana nawe kimwili?”
17 А той рече: Ще ти изпратя яре от стадото. И тя отвърна: Даваш ли ми залог, догде го изпратиш?
Akamwambia, “Nitakutumia mwana-mbuzi kutoka kundi langu.” Akamuuliza, “Utanipa kitu chochote kama amana mpaka utakapompeleka?”
18 Рече той: Какъв залог да ти дам? И тя каза: Печата си, ширита си и тоягата си, която е в ръката ти. И той й ги даде. И влезе при нея, и тя зачна от него.
Akamuuliza, “Nikupe amana gani?” Akamjibu, “Pete yako na kamba yake pamoja na fimbo iliyo mkononi mwako.” Kwa hiyo akampa vitu hivyo kisha akakutana naye kimwili, naye akapata mimba yake.
19 После тя стана та си отиде, свали покривалото си и облече вдовишките си дрехи.
Tamari akaondoka, akavua shela yake akavaa tena nguo zake za ujane.
20 А Юда изпрати ярето, чрез ръката на приятеля си одоламеца, за да вземе залога от ръката на жената; но той не я намери.
Wakati ule ule, Yuda akamtuma rafiki yake Mwadulami apeleke yule mwana-mbuzi ili arudishiwe amana yake kutoka kwa yule mwanamke, lakini yule rafiki yake hakumkuta yule mwanamke.
21 Затова попита хората от онова място, казвайки: Где е блудницата, която беше на пътя при Енаим? А те рекоха: Тука не е имало блудница.
Akawauliza watu wanaoishi mahali pale, “Yuko wapi yule kahaba wa mahali pa kuabudia miungu aliyekuwa kando ya barabara hapa Enaimu?” Wakamjibu, “Hajawahi kuwepo mwanamke yeyote kahaba wa mahali pa kuabudia miungu hapa.”
22 И той се върна при Юда и рече: Не я намерих; още и хората от онова място рекоха: Тук не е имало блудница.
Kwa hiyo akamrudia Yuda na kumwambia, “Sikumpata. Zaidi ya hayo, watu wanaoishi mahali pale walisema ‘Hapakuwahi kuwepo mwanamke yeyote kahaba wa mahali pa kuabudia miungu hapa.’”
23 И рече Юда: Нека си държи нещата, да не станем за присмех; ето, аз пратих това яре, но ти не я намери.
Kisha Yuda akasema, “Mwache avichukue vitu hivyo, ama sivyo tutakuwa kichekesho. Hata hivyo, nilimpelekea mwana-mbuzi, lakini hukumkuta.”
24 Около три месеца подир това, известиха на Юда, казвайки: Снаха ти Тамар блудствува; а още, ето, непразна е от блудството. А Юда рече: Изведете я да се изгори.
Baada ya miezi mitatu Yuda akaambiwa, “Tamari mkweo ana hatia ya kuwa kahaba, na matokeo yake ana mimba.” Yuda akasema, “Mtoeni nje na achomwe moto hadi afe!”
25 А когато я извеждаха, тя изпрати до свекъра си да му кажат: От човека, чиито са тия неща, съм непразна. Рече още: Познай, моля, чии са тия неща - печатът, ширитът и тоягата.
Alipokuwa akitolewa nje, akatuma ujumbe kwa baba mkwe wake kusema, “Nina mimba ya mtu mwenye vitu hivi.” Akaongeza kusema, “Angalia kama utatambua kwamba pete hii na kamba yake pamoja na fimbo hii ni vya nani.”
26 И Юда ги позна и рече: Тя е по-права от мене, тъй като не я дадох на сина си Шела. И не я позна вече.
Yuda akavitambua na kusema, “Yeye ana haki kuliko mimi, kwa kuwa sikumkabidhi kwa mwanangu Shela ili awe mkewe.” Tangu hapo hakukutana naye kimwili tena.
27 И когато дойде времето й да роди, ето, имаше близнета в утробата й.
Wakati ulipofika wa kujifungua, kukawa na wana mapacha tumboni mwake.
28 И като раждаше, едното простря ръка: и бабата взе та върза червен конец на ръката му и каза: Тоя пръв излезе.
Alipokuwa akijifungua, mmoja akatoa mkono wake nje, kwa hiyo mkunga akachukua uzi mwekundu na kuufunga mkononi mwa yule mtoto, akasema, “Huyu ametoka kwanza.”
29 А като дръпна надире ръката си, ето, брат му излезе; и тя рече: Какъв пролом си направи ти? Затова го наименуваха Фарес.
Lakini alipourudisha mkono wake ndugu yake akaanza kutoka, naye akasema, “Hivi ndivyo ulivyotoka kwa nguvu!” Akaitwa Peresi.
30 После излезе брат му, който имаше червения конец на ръката си, и него наименуваха Зара.
Kisha ndugu yake, aliyekuwa na uzi mwekundu mkononi, akatoka, naye akaitwa Zera.

< Битие 38 >