< Битие 24 >

1 А когато Авраам беше стар, напреднал във възраст, и Господ беше благословил Авраама във всичко,
Wakati huu Abrahamu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, naye Bwana alikuwa amembariki katika kila njia.
2 рече Авраам на най-стария слуга в дома си, който беше настоятел на всичкия му имот: Тури, моля, ръката си под бедрото ми;
Akamwambia mtumishi wake mkuu wa vitu vyote katika nyumba yake, yule aliyekuwa msimamizi wa vitu vyote alivyokuwa navyo, “Weka mkono wako chini ya paja langu,
3 и ще те закълна в Господа, Бог на небето и Бог на земята, че няма да вземеш жена за сина ми от дъщерите на ханаанците, между които живея;
Ninataka uape kwa Bwana, Mungu wa mbingu na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke kutoka binti za Wakanaani, ambao ninaishi miongoni mwao,
4 но да отидеш в отечеството ми, при рода ми, и от там да вземеш жена за сина ми Исаака.
bali utakwenda katika nchi yangu na jamaa zangu umpatie Isaki mwanangu mke.”
5 А слугата му рече: Може да не иска жената да дойде след мене в тая земя; трябва ли да заведа сина ти в оная земя, отгдето си излязъл?
Yule mtumishi akamuuliza, “Je, kama huyo mwanamke atakataa kuja nami katika nchi hii? Je, nimpeleke mwanao katika hiyo nchi uliyotoka?”
6 Но Авраам му каза: Пази се да не върнеш сина ми там.
Abrahamu akasema, “Hakikisha kwamba hutamrudisha mwanangu huko.
7 Господ, небесният Бог, Който ме изведе из бащиния ми дом и от родната ми земя, и Който ми говори, и Който ми се закле, казвайки: На твоето потомство ще дам тая земя; Той ще изпрати ангела си пред тебе и ще вземеш жена за сина ми оттам.
Bwana, Mungu wa mbingu, aliyenitoa nyumbani kwa baba yangu na nchi yangu niliyozaliwa na aliyesema nami na akaniahidi kwa kiapo, akisema, ‘Nitawapa watoto wako nchi hii,’ atatuma malaika wake akutangulie ili umpatie mwanangu mke kutoka huko.
8 Но, ако жената не иска да дойде след тебе, тогава ти ще бъдеш свободен от това мое заклеване; само да не върнеш сина ми там.
Kama huyo mwanamke asipokubali kufuatana nawe, basi utafunguliwa kutoka kiapo nilichokuapisha. Ila usimrudishe mwanangu huko.”
9 Тогава слугата тури ръката си под бедрото на господаря си Авраама и му се закле за това нещо.
Basi yule mtumishi akaweka mkono wake chini ya paja la bwana wake Abrahamu akamwapia kuhusu shauri hili.
10 И тъй, слугата взе десет от камилите на господаря си и тръгна, като носеше в ръцете си от всички богатства на господаря си; стана и отиде в Месопотамия, в Нахоровия град.
Ndipo huyo mtumishi akachukua ngamia kumi miongoni mwa ngamia za bwana wake, akaondoka, akiwa amechukua aina zote za vitu vizuri kutoka kwa bwana wake. Akaelekea Aramu-Naharaimu na kushika njia kwenda mji wa Nahori.
11 И надвечер, когато жените излизат да си наливат вода, той накара камилите да коленичат вън от града при водния кладенец.
Akawapigisha ngamia magoti karibu na kisima cha maji nje ya mji, ilikuwa inaelekea jioni, wakati ambapo wanawake wanakuja kuteka maji.
12 Тогава каза: Господи, Боже на господаря ми Авраама, дай ми, моля, добър успех днес и покажи благост към господаря ми Авраама.
Kisha akaomba, “Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, nipatie ushindi leo, uonyeshe huruma kwa bwana wangu Abrahamu.
13 Ето, аз стоя при извора на водата, и дъщерите на града излизат да си наливат вода.
Tazama, nimesimama karibu na kisima hiki cha maji, nao binti za watu wa mji huu wanakuja kuteka maji.
14 Нека момата, на която река: Я наведи водоноса си да пия; и тя рече: Пий, и ще напоя и камилите ти; -тя нека е оная, която си отредил за слугата си Исаака; от това ще позная, че си показал милост към господаря ми.
Basi na iwe hivi, nitakapomwambia binti mmojawapo, ‘Tafadhali tua mtungi wako nipate kunywa maji,’ naye akisema, ‘Kunywa, nitawanywesha na ngamia wako pia.’ Basi na awe ndiye uliyemchagua kwa ajili ya mtumishi wako Isaki. Kwa hili nitajua umemhurumia bwana wangu.”
15 Докато той още говореше, ето Ревека излизаше с водоноса си на рамото си; тя бе се родила на Ватуила, син на Мелха, жената на Авраамовия брат Нахор.
Ikawa kabla hajamaliza kuomba, Rebeka akatokea akiwa na mtungi begani mwake. Alikuwa binti wa Bethueli. Bethueli alikuwa mwana wa Milka aliyekuwa mke wa Nahori ndugu wa Abrahamu.
16 Момата беше твърде красива на глед, девица, която никой мъж не беше познал; тя, като слезе на извора, напълни водоноса си и се изкачи.
Huyu msichana alikuwa mzuri sana wa sura, bikira, ambaye hakuna mtu aliyekuwa amekutana naye kimwili. Aliteremka kisimani, akajaza mtungi wake akapanda juu.
17 А слугата се завтече да я посрещне и рече: Я дай ми да пия малко вода от водоноса ти.
Ndipo yule mtumishi akaharakisha kukutana naye akamwambia, “Tafadhali nipe maji kidogo katika mtungi wako.”
18 А тя рече: Пий, господарю; и бърже сне водоноса си на ръката си, и му даде да пие.
Yule msichana akasema, “Kunywa, bwana wangu.” Akashusha kwa haraka mtungi mkononi mwake na akampa, akanywa.
19 И като му даде доволно да пие, рече: И за камилите ти ще налея догде се напоят.
Baada ya kumpa yule mtumishi yale maji, akamwambia, “Nitateka maji kwa ajili ya ngamia zako pia mpaka wote watosheke.”
20 И като изля бърже водоноса си в поилото, завтече се на кладенеца да налее още и наля за всичките му камили.
Akafanya haraka kumimina maji kwenye birika ya kunyweshea wanyama, akakimbia kisimani kuteka maji mengine na akateka ya kuwatosha ngamia wake wote.
21 А човекът я наблюдаваше внимателно и мълчеше, за да узнае дали Господ бе направил пътуването му успешно или не.
Pasipo kusema neno, yule mtumishi akamtazama kwa makini aone kama Bwana ameifanikisha safari yake, au la.
22 Като напоиха камилите, човекът взе една златна обица, тежка половин сикъл, и две гривни за ръцете й, тежки десет сикли злато, и рече:
Ikawa ngamia walipokwisha kunywa wote, yule mtumishi akampa huyo msichana pete ya puani ya dhahabu yenye uzito wa beka moja na bangili mbili za dhahabu zenye uzito wa shekeli kumi.
23 Чия си дъщеря? - я ми кажи. Има ли в къщата на баща ти място за нас да пренощуваме?
Kisha akamuuliza, “Wewe ni binti wa nani? Tafadhali uniambie, je, kuna nafasi katika nyumba ya baba yako tutakapoweza kulala?”
24 А тя му рече: Аз съм дъщеря на Ватуила, син на Мелха, когото тя е родила на Нахора.
Yule msichana akamjibu, “Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Milka aliyemzalia Nahori.”
25 Рече му още: Има у нас и слама, и храна доволно, и място за пренощуване.
Akaendelea kusema, “Kwetu kuna majani mengi na malisho, tena kuna nafasi kwa ajili yenu kulala.”
26 Тогава човекът се наведе, та се поклони на Господа.
Yule mtumishi akasujudu na kumwabudu Bwana,
27 И рече: Благословен да бъде Господ, Бог на господаря ми Авраама, Който не лиши господаря ми от милостта си и верността си, като отправи Господ пътя ми в дома на братята на господаря ми.
akisema, “Atukuzwe Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hakuondoa wema na uaminifu wake kwa bwana wangu. Mimi nami, Bwana ameniongoza safarini akanifikisha nyumbani kwa jamaa za bwana wangu.”
28 А момата се завтече, та разказа тия неща на майка си.
Yule msichana akakimbia akawaeleza watu wa nyumbani mwa mama yake kuhusu mambo haya.
29 И Ревека имаше брат на име Лаван; и Лаван се завтече вън при човека на извора.
Rebeka alikuwa na kaka aliyeitwa Labani, huyo akaharakisha kukutana na yule mtumishi kule kisimani.
30 Защото, като видя обицата и гривните на ръцете на сестра си и чу думите на сестра си Ревека, която казваше: Така ми говори човекът; той отиде при човека; и, ето, той стоеше при камилите до извора.
Mara alipoiona ile pete puani, na bangili mikononi mwa dada yake na kusikia yale maneno Rebeka aliyoambiwa na huyo mtumishi, alimwendea huyo mtumishi, akamkuta amesimama karibu na ngamia wake pale karibu na kisima.
31 И рече му: Влез, ти, благословен от Господа; защо стоиш вън? Защото приготвих къщата и място за камилите.
Akamwambia, “Karibu nyumbani wewe uliyebarikiwa na Bwana, kwa nini unasimama huko nje? Mimi nimekuandalia nyumba na mahali kwa ajili ya ngamia.”
32 И тъй, човекът влезе вкъщи; а Лаван разтовари камилите му и даде слама и храна за камилите, и вода за умиване неговите нозе и нозете на хората, които бяха с него.
Hivyo yule mtumishi akaenda nyumbani, mizigo ikaondolewa juu ya ngamia. Majani na malisho yakaletwa kwa ajili ya ngamia na maji kwa ajili yake na watu wake ili kunawa miguu.
33 И сложиха пред него да яде; но той рече: Не искам да ям, догде не кажа думата си. А Лаван рече: Казвай.
Ndipo chakula kikaandaliwa kwa ajili yake, lakini akasema, “Sitakula mpaka niwe nimewaambia yale niliyo nayo ya kusema.” Labani akasema, “Basi tuambie.”
34 Тогава той каза: Аз съм слуга на Авраама.
Hivyo akasema, “Mimi ni mtumishi wa Abrahamu.
35 Господ е благословил господаря ми премного, та стана велик; дал му е овци и говеда, сребро и злато, слуги и слугини, камили и осли.
Bwana amembariki sana bwana wangu, amekuwa tajiri. Amempa kondoo na ngʼombe, fedha na dhahabu, watumishi wa kiume na wa kike, ngamia na punda.
36 И Сара, жената на господаря ми, роди син на господаря ми, когато беше вече остаряла; и на него той даде всичко, що има.
Sara mkewe bwana wangu amemzalia mwana katika uzee wake, naye amempa kila kitu alichokuwa nacho.
37 И господарят ми, като ме закле, рече: Да не вземеш за сина ми жена от дъщерите на ханаанците, в чиято земя живея.
Naye bwana wangu ameniapisha na akasema, ‘Kamwe usimtwalie mwanangu mke katika binti za Wakanaani, ambao ninaishi katika nchi yao,
38 Но да отидеш в бащиния ми дом и в рода ми, и от там да вземеш жена за сина ми.
ila uende mpaka kwa jamaa ya baba yangu na ukoo wangu mwenyewe, ukamtwalie mwanangu mke huko.’
39 И рекох на господаря ми: Може да не иска жената да дойде след мене.
“Kisha nikamuuliza bwana wangu, ‘Je, kama huyo mwanamke hatakubali kurudi nami?’
40 Но той ми каза: Господ, пред Когото ходя, ще изпрати ангела си с тебе и ще направи пътуването ти успешно; и ще вземеш жена за сина ми от рода ми и от бащиния ми дом.
“Akanijibu, ‘Bwana ambaye nimetembea mbele zake, atatuma malaika wake pamoja nawe, na kuifanikisha safari yako, ili uweze kupata mke kwa ajili ya mwanangu katika ukoo wangu na kutoka jamaa ya baba yangu.
41 Само тогава ще бъдеш свободен от заклеването ми, когато отидеш при рода ми; и, ако не ти я дадат, тогава ще бъдеш свободен от заклеването ми.
Kisha, utakapokwenda kwenye ukoo wangu, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu hata kama wakikataa kukupa huyo binti, utakuwa umefunguliwa kutoka kiapo changu.’
42 И като пристигнах днес на извора, рекох: Господи, Боже на господаря ми Авраама, моля, ако правиш пътуването ми, по което ходя, успешно,
“Nilipokuja kisimani leo nilisema, ‘Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ikikupendeza, naomba uifanikishe safari niliyoijia.
43 ето, аз стоя при водния извор; момата, която излезе да налее вода, и аз й река: Я ми дай да пия малко вода от водоноса ти,
Tazama, ninasimama kando ya kisima hiki, kama mwanamwali akija kuteka maji nami nikimwambia, tafadhali niruhusu ninywe maji kidogo kutoka kwenye mtungi wako,
44 и тя ми рече: И ти пий, и ще налея и за камилите ти, - тя нека е жената, която Господ е отредил за сина на господаря ми.
naye kama akiniambia, “Kunywa, nami nitateka maji kwa ajili ya ngamia wako pia,” basi huyo awe ndiye mke ambaye Bwana amemchagulia mwana wa bwana wangu.’
45 Докато още говорех в сърцето си, ето, Ревека излезе с водоноса на рамото си. И като слезе на извора и наля, рекох й: Я ми дай да пия.
“Kabla sijamaliza kuomba moyoni mwangu, Rebeka akatokea, amebeba mtungi begani mwake. Akashuka kisimani akateka maji, nami nikamwambia, ‘Tafadhali nipe maji ninywe.’
46 И тя бързо сне водоноса от рамото си и рече: Пий и ще напоя и камилите ти. И тъй, аз пих, а тя напои и камилите.
“Akafanya haraka kushusha mtungi wake begani na kusema, ‘Kunywa na nitawanywesha ngamia wako pia,’ basi nikanywa, akawanywesha na ngamia pia.
47 Тогава я попитах, казвайки: Чия си дъщеря? А тя рече: Аз съм дъщеря на Ватуила, Нахоровия син, когото му роди Мелха. Тогава турих обицата на лицето й и гривните на ръцете й.
“Nikamuuliza, ‘Wewe ni binti wa nani?’ “Akasema, ‘Mimi ni binti wa Bethueli, mwana wa Nahori, Milka aliyemzalia.’ “Ndipo nilipotia pete puani mwake na bangili mikononi mwake,
48 И наведох се, та се поклоних на Господа и благослових Господа, Бога на господаря ми Авраама, Който ме доведе по правия път, за да взема за сина на господаря ми братовата му дъщеря.
nikasujudu na nikamwabudu Bwana. Nikamtukuza Bwana, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, aliyeniongoza katika njia sahihi ili nimtwalie mwana na bwana wangu mke katika jamaa zake.
49 Сега, прочее, ако искате да постъпите любезно и верно спрямо господаря ми, кажете ми; и, ако не, пак ми кажете, за да се обърна надясно или наляво.
Ikiwa mtaonyesha wema na uaminifu kwa bwana wangu, mniambie, la sivyo, mniambie, ili niweze kujua njia ya kugeukia.”
50 А Лаван и Ватуил в отговор рекоха: От Господа стана това; ние не можем да ти речем ни зло, ни добро.
Labani na Bethueli wakajibu, “Jambo hili limetoka kwa Bwana, hatuwezi kukuambia jambo lolote baya au jema.
51 Ето Ревека пред тебе; вземи я и си иди; нека бъде жена на сина на господаря ти, както Господ е говорил.
Rebeka yuko hapa, mchukue na uende, awe mke wa mwana wa bwana wako, sawasawa na Bwana alivyoongoza.”
52 Като чу думите им, Авраамовият слуга се поклони на Господа до земята.
Ikawa huyo mtumishi wa Abrahamu aliposikia waliyosema, alisujudu mpaka nchi mbele za Bwana.
53 И слугата извади сребърни и златни накити и облекла, та ги даде на Ревека; така също даде скъпи дарове на брат й и на майка й.
Ndipo huyo mtumishi akatoa vitu vilivyotengenezwa kwa dhahabu na kwa fedha pamoja na mavazi, akampa Rebeka, pia akawapa zawadi za thamani kubwa nduguye na mamaye.
54 Подир това, той и хората, които бяха с него, ядоха, пиха и пренощуваха; и като станаха сутринта, слугата рече: Изпратете ме при господаря ми.
Kisha yeye na wale watu waliokuwa pamoja naye wakala, wakanywa na kulala palepale. Walipoamka asubuhi, yule mtumishi, akasema, “Nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”
55 А брат й и майка й казаха: Нека поседи момата с нас известно време, най-малко десетина дни, после нека иде.
Lakini ndugu yake Rebeka pamoja na mama yake wakajibu, “Acha binti akae kwetu siku kumi au zaidi, ndipo mwondoke.”
56 Но той им каза: Не ме спирайте, тъй като Господ е направил пътуването ми успешно; изпратете ме да ида при господаря си.
Lakini yule mtumishi akawaambia, “Msinicheleweshe, kwa kuwa Bwana amefanikisha safari yangu, nipeni ruhusa nirudi kwa bwana wangu.”
57 А те рекоха: Да повикаме момата и да я попитаме, какво ще каже.
Ndipo wakasema, “Acha tumwite huyo binti tumuulize, tusikie atakavyosema.”
58 И тъй, повикаха Ревека и рекоха й: Отиваш ли с тоя човек? А тя рече: Отивам.
Kwa hiyo wakamwita Rebeka na kumuuliza, “Je, utakwenda na mtu huyu?” Akasema, “Nitakwenda.”
59 И така, изпратиха сестра си Ревека с бавачката й и Авраамовия слуга с хората му.
Hivyo wakamwaga ndugu yao Rebeka aondoke, pamoja na mjakazi wake, mtumishi wa Abrahamu na watu wake.
60 И благословиха Ревека, като й рекоха: Сестро наша, да се родят от тебе хиляди по десет хиляди и потомството ти да завладее портата на ненавистниците си.
Wakambariki Rebeka, wakamwambia, “Ndugu yetu, uwe wewe kumi elfu, mara elfu nyingi, nao wazao wako wamiliki malango ya adui zao.”
61 И Ревека и слугите й станаха, възседнаха камилите и отидоха след човека. Така, слугата взе Ревека и си замина.
Rebeka na vijakazi wake wakajiandaa, wakapanda ngamia zao wakafuatana na yule mtu. Hivyo yule mtumishi akamchukua Rebeka akaondoka.
62 А Исаак идеше от Вир-лахайрои, защото живееше в южната земя.
Basi Isaki alikuwa ametoka Beer-Lahai-Roi, kwa kuwa alikuwa anaishi nchi ya Negebu.
63 И като излезе Исаак, за да размишлява на полето привечер, повдигна очи и видя; и, ето камили се приближаваха.
Isaki akatoka kwenda shambani kutafakari wakati wa jioni, alipoinua macho yake, akaona ngamia wanakuja.
64 Също и Ревека повдигна очи и видя Исаака; и слезна от камилата.
Rebeka pia akainua macho akamwona Isaki. Akashuka kutoka kwenye ngamia wake
65 Защото беше рекла на слугата: Кой е оня човек, който иде през полето насреща ни? И слугата беше казал: Това е господарят ми. Затова тя взе покривалото си и се покри.
na akamuuliza yule mtumishi, “Ni nani mtu yule aliye kule shambani anayekuja kutulaki?” Yule mtumishi akajibu, “Huyu ndiye bwana wangu.” Hivyo Rebeka akachukua shela yake akajifunika.
66 И слугата разказа на Исаака всичко, което бе извършил.
Kisha yule mtumishi akamweleza Isaki mambo yote aliyoyatenda.
67 Тогава Исаак въведе Ревека в шатъра на майка си Сара и я взе, и тя му стана жена, и той я обикна. Така Исаак се утеши след смъртта на майка си.
Ndipo Isaki akamwingiza Rebeka katika hema la Sara mama yake, Isaki akamchukua Rebeka, hivyo akawa mke wake. Isaki akampenda, akafarijika baada ya kifo cha mama yake.

< Битие 24 >