< Данаил 4 >
1 Цар Навуходоносор към всичките племена, народи и езици, които живеят по цял свят - Мир да ви се умножи!
Mfalme Nebukadneza, Kwa kabila za watu, mataifa na watu wa kila lugha, wanaoishi katika ulimwengu wote: Mafanikio yawe kwenu sana!
2 Видя ми се за добре да оповестя знаменията и чудесата, които ми направи всевишният Бог.
Ni furaha yangu kuwaambia kuhusu ishara za miujiza na maajabu ambayo Mungu Aliye Juu Sana amenifanyia.
3 Колко са велики Неговите знамения! И колко могъщи са чудесата му! Неговото царство е вечно царство, и Неговото владичество из род в род.
Ishara zake ni kuu aje, na maajabu yake yana nguvu aje! Ufalme wake ni ufalme wa milele; enzi yake hudumu kutoka kizazi hadi kizazi.
4 Аз Навуходоносор, като бях спокоен у дома си и благополучен в палата си,
Mimi, Nebukadneza, nilikuwa nyumbani katika jumba langu la kifalme, nikiwa ninaishi kwa raha na hali ya kufanikiwa.
5 видях сън, който ме уплаши; и размишленията ми на леглото ми и виденията на главата ми ме смутиха.
Niliota ndoto iliyoniogopesha. Nilipokuwa nimelala kitandani mwangu, njozi na maono yaliyopita mawazoni mwangu vilinitisha.
6 За това, издадох указ да се въведат пред мене всичките вавилонски мъдреци, за да ми явят значението на съня.
Hivyo nikaagiza kwamba watu wote wenye hekima wa Babeli waletwe mbele yangu kunifasiria ndoto yangu.
7 Тогава влязоха врачовете, вражарите, халдейците, и астролозите, и аз разказах съня си пред тях; но не можаха да ми явят значението му.
Walipokuja waganga, wasihiri, wanajimu na waaguzi, niliwaambia ndoto yangu, lakini hawakuweza kunifasiria.
8 А най- после дойде пред мене Даниил, чието име бе Валтасасар по името на моя бог, и в когото е духът на светите богове; и аз разказах съня пред него, като рекох:
Mwishoni, Danieli alikuja mbele yangu nikamweleza hiyo ndoto. (Danieli anaitwa Belteshaza, kwa jina la mungu wangu, nayo roho ya miungu mitakatifu inakaa ndani yake.)
9 Валтасасаре, началниче на врачовете, понеже узнах, че духът на светите богове е в тебе, и че никаква тайна не е мъчна за тебе, обясни ми виденията на съня, който видях, и кажи ми значението му.
Nilisema, “Belteshaza, mkuu wa waganga, ninajua kuwa roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, wala hakuna siri iliyo ngumu kwako. Hii ndiyo ndoto yangu, nifasirie.
10 Ето какви бяха виденията на главата ми и на леглото ми: Гледах, и ето дърво всред света, на което височината бе голяма.
Haya ndiyo maono niliyoona nilipokuwa nimelala kitandani mwangu: Nilitazama, na mbele yangu ulisimama mti katikati ya nchi. Ulikuwa mrefu sana.
11 Това дърво стана голямо и яко, височината му стигаше до небето, и то се виждаше до краищата на целия свят.
Mti ule ulikua, ukawa mkubwa na wenye nguvu, nayo ncha yake ikagusa anga; ulionekana mpaka miisho ya dunia.
12 Листата му бяха хубави, плодът му изобилен, и в него имаше храна за всички; под сянката му почиваха полските животни, и на клоновете му обитаваха небесните птици, и от него се хранеше всяка твар.
Majani yake yalikuwa ya kupendeza, matunda yake yalikuwa mengi, na juu yake kulikuwa na chakula kwa ajili ya wote. Chini ya kivuli chake wanyama wa kondeni walipata hifadhi, na ndege wa angani waliishi katika matawi yake. Kila kiumbe kililishwa kutokana na mti huo.
13 Видях във виденията на главата си на леглото си, и ето, един свет страж слезе от небето,
“Katika maono niliyoyaona nikiwa nimelala kitandani mwangu, nilitazama, na mbele yangu alikuwepo mlinzi, aliye mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni.
14 и извика със силен глас, казвайки така: Отсечете дървото и изсечете клоновете му; отърсете листата му и разпръснете плода му; нека бягат животните изпод него, и птиците от клоновете му;
Akaita kwa sauti kubwa: ‘Kateni mti huu, myafyeke matawi yake; yaondoeni majani yake na kuyatawanya matunda yake. Wanyama na wakimbie kutoka chini yake na ndege waondoke kutoka matawi yake.
15 обаче оставете в земята пъна с корените му всред полската трева, и то с железен и меден обръч наоколо, и нека се мокри с небесна роса, и участта му нека бъде с животните в тревата на земята;
Lakini acheni kisiki chake na mizizi, kikiwa kimefungwa kwa chuma na shaba, kibaki ardhini, kwenye majani ya kondeni. “‘Mwacheni aloweshwe na umande wa mbinguni, naye aachwe aishi pamoja na wanyama miongoni mwa mimea ya dunia.
16 нека се измени човешкото му сърце, и нека му се даде животинско сърце; и така нека минат над него седем времена.
Akili yake na ibadilishwe kutoka ile ya mwanadamu na apewe akili ya mnyama, mpaka nyakati saba zipite juu yake.
17 Тая присъда е по заповед от стражите, и делото на думата на светите, за да знаят живите, че Всевишният владее над царството на човеците, дава го комуто ще, и поставя над него най-нищожният измежду човеците.
“‘Uamuzi huu umetangazwa na walinzi, hukumu imetangazwa na watakatifu, ili walio hai wajue kuwa Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme zote za wanadamu, naye humpa yeyote amtakaye na kumtawaza juu yake hata yeye aliye mnyonge sana miongoni mwa wanadamu.’
18 Тоя сън видях аз цар Навуходоносор, и ти, Валтасасаре, кажи значението му; защото ни един от мъдреците на царството ми не може да ми яви значението; а ти можеш, защото духът на светите богове е в тебе.
“Hii ndiyo ndoto niliyoipata mimi, Mfalme Nebukadneza. Sasa Belteshaza, niambie maana yake, kwa maana hakuna hata mmoja wa wenye hekima katika ufalme wangu anayeweza kunifasiria. Bali wewe waweza, kwa sababu roho ya miungu mitakatifu imo ndani yako.”
19 Тогава Даниил, чието име бе Валтасасар, остана смаян за малко, и размишленията му го смущаваха. Царят продумайки, рече: Валтасасаре, да те не смущава сънят или значението му. Валтасасар рече в отговор: Господарю мой, сънят нека бъде върху ония, които те мразят, и това, което означава, върху неприятелите ти!
Ndipo Danieli (aliyeitwa pia Belteshaza) alipofadhaika sana kwa muda, nayo mawazo yake yakamtia hofu. Basi mfalme akasema, “Belteshaza, usiruhusu ndoto wala maana yake kukutia hofu.” Belteshaza akamjibu, “Bwana wangu, laiti ndoto hii ingehusu adui zako, na maana yake iwahusu watesi wako!
20 Дървото, което си видял, че станало голямо и яко, чиято височина стигала до небето, и което се виждало от целия свят,
Mti uliouona, uliokua ukawa mkubwa na wenye nguvu, nayo ncha yake ikagusa anga na kuonekana duniani kote,
21 чиито листа били хубави и плодът му изобилен, дори достатъчна храна за всички, под което живеели полските животни, и по клоновете на което се подсланяли небесните птици,
ukiwa na majani ya kupendeza na matunda mengi, ukitoa chakula kwa wote, na ukiwapa hifadhi wanyama wa kondeni na kuwa mahali pa viota katika matawi yake kwa ajili ya ndege wa angani.
22 това дърво си ти, царю, който си станал голям и як; защото величието ти нарасна и стигна до небето, и владичеството ти до края на света.
Ee mfalme, wewe ndiwe ule mti! Umekuwa mkubwa na mwenye nguvu, nao ukuu wako umekua mpaka kufika juu angani, nayo mamlaka yako yameenea mpaka miisho ya dunia.
23 А дето царят е видял един свет страж да слиза от небето и да казва: Отсечете дървото и го съборете, но оставете в земята, в полската трева, пъна с корените му, и то със железен и меден обръч наоколо, и нека се мокри от небесната роса, и нека бъде участта му с полските животни, докато така минат над него седем времена,
“Ee mfalme, wewe ulimwona mlinzi, aliye mtakatifu, akishuka kutoka mbinguni na kusema, ‘Ukateni mti na kuuangamiza, lakini kiacheni kisiki kikiwa kimefungwa kwa chuma na kwa shaba, kwenye majani ya kondeni, wakati mizizi yake inabaki ardhini. Mwacheni aloweshwe na umande wa mbinguni, mwacheni aishi kama wanyama pori mpaka nyakati saba zipite juu yake.’
24 ето значението му, царю: Решението на Всевишния, което постигна господаря ми царя, е
“Ee mfalme, hii ndiyo tafsiri, na hii ni amri ya Aliye Juu Sana aliyoitoa dhidi ya bwana wangu mfalme:
25 да бъдеш изгонен измежду човеците, жилището ти да бъде с полските животни, да ядеш трева като говедата, и да те мокри небесната роса, и да минат над тебе седем времена, догдето познаеш, че Всевишният владее в царството на човеците, и го дава комуто ще.
Wewe utafukuzwa mbali na wanadamu, nawe utaishi pamoja na wanyama pori; utakula manyasi kama ngʼombe, na kuloana kwa umande wa mbinguni. Nyakati saba zitapita juu yako, mpaka utakapokubali kuwa Yeye Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye humtawaza yeyote amtakaye.
26 А дето се заповядало да оставят пъна с корените на дървото, значи, че царството ти ще бъде обезпечено щом признаеш, че небесата владеят.
Amri ya kuacha kisiki pamoja na mizizi yake inamaanisha kwamba ufalme wako utarejezwa kwako utakapokubali kwamba Mbingu ndizo zitawalazo.
27 Затова, царю, нека ти бъде угоден моят съвет да напуснеш греховете си чрез вършене на правда, и беззаконията си чрез правене благодеяния на бедните, негли се продължи благоденствието ти.(Или: се прости престъплението ти)
Kwa hiyo, ee mfalme, uwe radhi kupokea shauri langu: Acha dhambi zako kwa kutenda yaliyo haki, ukaache uovu wako, na uwe na huruma kwa walioonewa. Hivyo itawezekana baada ya hayo, mafanikio yako yakaendelea.”
28 Всичко това постигна цар Навуходоносора.
Haya yote yalimpata Mfalme Nebukadneza.
29 В края на дванадесет месеца, като ходеше по царския палат у Вавилон,
Miezi kumi na miwili baadaye, mfalme alipokuwa akitembea juu ya paa la jumba la kifalme la Babeli,
30 царят проговори, казвайки: Не е ли велик тоя Вавилон, който аз съградих с мощната си сила за царското жилище и за славата на величието си!
alisema, “Je, huu si Babeli mji mkuu nilioujenga kama makao ya kifalme, kwa uwezo wangu mkubwa, na kwa ajili ya utukufu wa enzi yangu?”
31 Думата бе още в устата на царя, и глас дойде от небесата, който рече: На тебе се известява, царю Навуходоносоре, че царството премина от тебе;
Maneno hayo yalikuwa bado katika midomo yake wakati sauti ilipokuja kutoka mbinguni, ikisema, “Mfalme Nebukadneza, hiki ndicho kilichoamriwa kwa ajili yako: Mamlaka yako ya ufalme yameondolewa kutoka kwako.
32 и ще бъдеш изгонен измежду човеците, между полските животни ще бъде жилището ти, и ще те хранят с трева като говедата; и седем времена ще минат над тебе, додето признаеш, че Всевишният владее над царството на човеците, и го дава комуто ще.
Utafukuzwa mbali na wanadamu, ukaishi pamoja na wanyama pori, na utakula manyasi kama ngʼombe. Nyakati saba zitapita juu yako, mpaka utakapokubali kuwa Yeye Aliye Juu Sana ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye humtawaza yeyote amtakaye.”
33 В същия час това нещо се изпълни над Навуходоносора; той бе изгонен измежду човеците, ядеше трева като говедата, и тялото му се мокреше от небесната роса, додето космите му пораснаха като пера на орли, и ноктите му като на птици.
Papo hapo yale yaliyokuwa yamesemwa kuhusu Nebukadneza yakatimia. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akala majani kama ngʼombe. Mwili wake uliloweshwa kwa umande wa mbinguni mpaka nywele zake zikakua kama manyoya ya tai na kucha zake kama makucha ya ndege.
34 А в края на тия дни аз Навуходоносор повдигнах очите си към небесата; и разумът ми се възвърна като благослових Всевишния и похвалих и прославих Оногова, който живее до века, понеже владичеството Му е вечно владичество, и царството Му из род в род;
Mwisho wa huo wakati, mimi Nebukadneza, niliinua macho yangu kuelekea mbinguni, nazo fahamu zangu zikanirudia. Ndipo nikamsifu Yeye Aliye Juu Sana, nikamheshimu na kumhimidi yeye aishiye milele. Utawala wake ni utawala wa milele; ufalme wake hudumu kutoka kizazi na kizazi.
35 пред Него всичките земни жители се считат като нищо; по волята Си Той действа между небесната войска и между земните жители; и никой не може да спре ръката Му, или да Му каже - Що правиш Ти?
Mataifa yote ya dunia yanahesabiwa kuwa si kitu. Hufanya kama atakavyo kwa majeshi ya mbinguni, na kwa mataifa ya dunia. Hakuna anayeweza kuuzuia mkono wake au kumwambia, “Umefanya nini wewe?”
36 И в същото време, когато разумът ми се възвърна, възвърнаха ми се, за славата на царството ми, и величието и светлостта ми; защото съветниците ми и големците ми ме търсеха, закрепих се на царството си, и ми се притури превъзходно величие.
Wakati huo huo fahamu zangu ziliponirudia, nikarudishiwa heshima yangu na fahari yangu kwa ajili ya utukufu wa ufalme wangu. Washauri wangu na wakuu wangu walikuja kunitafuta, nami nikarudishwa kwenye kiti changu cha ufalme hata nikawa mkuu kuliko mwanzoni.
37 Сега аз Навуходоносор хваля, превъзнасям, и славя небесния Цар; защото всичко, що върши е с вярност, и пътищата му са справедливи; а Той може да смири ония, които ходят горделиво.
Basi mimi, Nebukadneza, humhimidi, na humtukuza na kumsifu Mfalme wa mbinguni, kwa sababu kila kitu afanyacho ni haki, na njia zake zote ni adili. Nao waendao kwa kiburi anaweza kuwashusha.