< Данаил 12 >
1 И в онова време великият княз Михаил, който се застъпва за твоите люде, ще се повдигне; и ще настане време на страдание, каквото никога не е бивало, откакто народ съществува до онова време; и в онова време твоите люде ще се отърват, - всеки, който се намери записан в книгата.
Katika kipindi hicho, Mikaeli, jemedari mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwa na wakati wa mateso ambao haujawahi kutokea tangu mwanzo wa taifa lolote mpaka kipindi hicho. Katika muda huo watu wako wataokolewa, yeyote ambaye jina lake litapatikana katika kitabu.
2 И множеството от спящите в пръстта на земята ще се събудят, едни за вечен живот, а едни за срам и вечно презрение.
Na wengi wa wale waliolala katika mavumbi ya dunia watainuka. baadhi kwa uzima wa milele na baadhi kwa ajili ya fedheha na matwezo ya milele.
3 Разумните ще сияят със светлостта на простора, и ония, които обръщат мнозина в правда като звездите до вечни векове.
Wale wenye hekima watang'ara kama mng'ao wa anga la juu, na wale wenye kuwaelekeza wengine katika haki, watakuwa kama nyota milele na milele.
4 А ти, Данииле, затвори думите и запечатай книгата до края на времето, когато мнозина ще я изследват, и знанието за нея ще се умножава.
Lakini wewe, Danieli, yafunge maneno haya; kihifadhi kitabu kikiwa kimetiwa chapa mpaka nyakati za mwisho. Watu wengi watakimbia huku na kule, na maarifa yataongezeka.
5 Тогава, като погледнах аз Даниил, ето, стояха двама други, един на брега отсам реката, и един на брега оттам реката.
Kisha mimi, Danieli, nilitazama, na kulikuwa na malaika wengine wawili wamesimama. Mmoja alisimama katika upande huu wa ukingo wa mto, na mwingine alisimama katika ukingo wa upande mwingine wa mto.
6 И единият рече на облечения в ленени дрехи човек, който бе над водата на реката: Докога ще се чака за края на тия чудеса?
Mmoja wao alimwambia mtu aliyevaa nguo za kitani, yeye aliyekuwa juu ya mkondo wa mto, “Je itachukua muda gani mpaka mwisho wa matukio haya ya kushangaza?”
7 И чух облечения в ленени дрехи човек, който бе над водата на реката, когато издигна десницата си и левицата си към небето и се закле в Оня, който живее до века, че това ще бъде след време, времена, и половина време, и че всичко това ще се изпълни, когато ще са свършили да смажат силата на светите люде.
Nilimsikia mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu katika mkondo wa mto, aliinua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni na kuapa kwa yeye aishiye milele kwamba itakuwa kwa wakati, nyakati, na nusu wakati. Na wakati nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimeshaharibiwa, mambo haya yote yatakuwa yamemalizika.
8 И аз чух, но не разбрах. Тогава рекох: Господарю, мой, каква ще бъде сетнината на това?
Nilisikia, lakini sikufahamu. Basi nikamwuliza, “Bwana wangu, mambo haya yote yatakuwa na matokeo gani?”
9 А той рече: Иди си, Данииле; защото думите са затворени и запечатани до края на времето.
Alisema, “Nenda zako Danieli, kwa kuwa maneno yamefungwa na kutiwa chapa mpaka wakati wa mwisho.
10 Мнозина ще се чистят и избелят и ще бъдат опитани; а нечестивите ще вършат нечестие, и никой от нечестивите не ще разбере; но разумните ще разберат.
Watu wengi watakuwa wametakaswa, wameoshwa, na kusafishwa, lakini waovu wataenenda katika uovu.
11 И от времето, когато се премахне всегдашната жертва, и се постави мерзостта, която докарва запустение; ще има хиляда и двеста и деветдесет дена.
Katika muda ule ambapo sadaka ya kawaida ya kuteketezwa itakapokuwa imeondolewa na chukizo la uharibifu liliosababisha ukiwa limesimamishwa, kutakuwa na siku zipatazo 1, 290.
12 Блажен, който изтърпи и стигне до хиляда и триста и тридесет и петте дена.
Ana heri mtu yule anayengojea mpaka mwisho wa siku 1, 335.
13 Но ти си иди, додето настане краят; и ще се успокоиш, и в края на дните ще застанеш в дела си.
Unapaswa uondoke uende njia yako hata mwisho, na kisha utapumzika. Utainuka katika sehemu uliyopewa, mwishoni mwa siku.”