< 4 Царе 18 >

1 В третата година на Израилевия цар Осия, Иловия син, се възцари Езекия, син на Юдовия цар, Ахаз.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Hoshea mwana wa Ela mfalme wa Israeli, Hezekia mwana wa Ahazi mfalme wa Yuda alianza kutawala.
2 Той беше двадесет и пет години на възраст, когато се възцари, и царува двадесет и девет години в Ерусалим; а името на майка му беше Авия, Захариева дъщеря.
Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka ishirini na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti Zekaria.
3 Той върши това, което бе право пред Господа, напълно както извърши баща му Давид;
Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, kama Daudi baba yake alivyofanya.
4 събори високите места, изпотроши кумирите, изсече ашерите и сломи медната змия, която Моисей беше направил, защото дори до онова време израилтяните й кадяха; и нарече я Нехущан.
Akapaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu, akazivunja sanamu, akakatakata nguzo za Ashera. Akavunja vipande vipande ile nyoka ya shaba Mose aliyotengeneza, kwa kuwa hadi siku hizo wana wa Israeli walikuwa wanaifukizia uvumba (ilikuwa ikiitwa Nehushtani).
5 На Господа Израилевия Бог упова. Нямаше подобен нему между всичките Юдови царе, ни между ония, които бяха подир него, нито преди него;
Hezekia aliweka tumaini lake kwa Bwana, Mungu wa Israeli. Hapakuwepo na mfalme mwingine wa kufanana naye miongoni mwa wafalme wa Yuda, kabla yake au baada yake.
6 защото се прилепи към Господа, не престана да Го следва, но опази заповедите, които Господ даде на Моисея.
Alishikamana na Bwana kwa bidii wala hakuacha kumfuata; alishika amri ambazo Bwana alikuwa amempa Mose.
7 И Господ бе с него; където и да излизаше, той благоуспяваше; и въстана против асирийския цар, и не му слугуваше вече.
Naye Bwana alikuwa pamoja naye, akafanikiwa katika kila alichokifanya. Aliasi dhidi ya mfalme wa Ashuru, wala hakumtumikia.
8 Той порази филистимците до Газа и до околностите й, от стражарска кула до укрепен град.
Kuanzia mnara wa ulinzi hadi kwenye mji wenye ngome, aliwashinda Wafilisti, hadi kufikia Gaza na himaya yake yote.
9 А в четвъртата година на цар Езекия, която бе седмата година на Израилевия цар Осия, син на Ила, асирийският цар Салманасар възлезе против Самария и я обсаждаше.
Mwaka wa nne wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa saba wa Hoshea mwana wa Ela kutawala Israeli, Shalmanesa mfalme wa Ashuru alikwenda kuishambulia Samaria na kuuzunguka kwa majeshi.
10 След три години я превзе; в шестата година на Езекия, която бе деветата година на Израилевия цар Осия, Самария бе превзета.
Baada ya miaka mitatu Waashuru wakautwaa. Kwa hiyo Samaria ulitekwa katika mwaka wa sita wa utawala wa Mfalme Hezekia, ambao ulikuwa mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea mfalme wa Israeli.
11 И асирийският цар отведе Израиля в плен в Асирия, и ги настани в Ала и в Авор при реката Гозан и в Мидските градове;
Mfalme wa Ashuru akawahamishia Waisraeli huko Ashuru na akawaweka Hala, na Gozani karibu na Mto Habori, na katika miji ya Wamedi.
12 защото не послушаха гласа на Господа своя Бог, но престъпиха завета Му, - всичко, което Господният слуга Моисей заповяда, - и не послушаха, и нито го извършиха.
Hili lilitokea kwa sababu hawakumtii Bwana Mungu wao, lakini walikuwa wamevunja agano lake, yale yote ambayo Mose mtumishi wa Bwana aliwaamuru. Hawakuzisikiliza amri wala kuzitimiza.
13 А в четиренадесетата година на цар Езекия, асирийският цар Сенахирим възлезе против всичките укрепени Юдови градове и ги превзе.
Katika mwaka wa kumi na nne wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru akaishambulia miji yote ya Yuda yenye ngome na kuiteka.
14 Тогава Юдовият цар Езекия прати до асирийския цар в Лахис да кажат: Съгрешихме; върни се от мене; каквото ми наложиш ще го нося. И тъй, асирийският цар наложи на Юдовия цар Езекия триста таланта сребро и тридесет таланта злато.
Basi Hezekia mfalme wa Yuda akamtumia ujumbe mfalme wa Ashuru huko Lakishi akisema: “Nimefanya makosa. Ondoka katika nchi yangu, nami nitakulipa chochote unachokitaka kwangu.” Mfalme wa Ashuru akamtoza Hezekia mfalme wa Yuda talanta 300 za fedha, na talanta thelathini za dhahabu.
15 И Езекия му даде всичкото сребро, което се намери в Господния дом и в съкровищницата на царската къща.
Basi Hezekia akampa fedha yote iliyopatikana ndani ya Hekalu la Bwana na katika hazina ya jumba la mfalme.
16 В това време Езекия откова златото от вратите на Господния храм и от стълбовете, които той, Юдовият цар Езекия, бе обковал със злато, и го даде на есирийския цар.
Wakati huu Hezekia mfalme wa Yuda akabandua dhahabu yote iliyokuwa imefunika milango na miimo ya Hekalu la Bwana, akampa mfalme wa Ashuru.
17 Но асирийския цар прати от Лахис Тартана, Рапсариса и Рапсака с голява мойске при цар Езекия в Ерусалим. А те възлязоха и дойдоха в Ерусалим. И когато стигнаха, дойдоха та застанаха при водопровода на горния водоем, който е по друма към тепавичарската нива.
Mfalme wa Ashuru akamtuma jemadari wake mkuu, na afisa wake mkuu, na jemadari wa jeshi, pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi hadi kwa Mfalme Hezekia huko Yerusalemu. Wakaja Yerusalemu na kusimama kwenye mfereji wa Bwawa la Juu, lililojengwa katika barabara iendayo kwenye Uwanja wa Dobi.
18 И когато извикаха към царя, излязоха при тях управителят на двореца Елиаким, Хелкиевият син и секретарят Шевна, и летописецът Иоах, Асафовият син.
Wakaagiza mfalme aitwe. Eliakimu mwana wa Hilkia aliyekuwa msimamizi wa jumba la mfalme, Shebna aliyekuwa katibu, na Yoa mwana wa Asafu mwandishi wakawaendea.
19 Тогава Рапсак им рече: Кажете сага на Езекия: Така казва великият цар, асирийският цар, каква е тая увереност, на която уповаваш?
Yule jemadari wa jeshi akawaambia, “Mwambieni Hezekia: “‘Hili ndilo asemalo mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru: Ni wapi unapoweka hili tumaini lako?
20 Ти казваш: Имам благоразумие и сила за воюване. Но това са само лицемерни думи. На кого, прочее, се надяваш та си въстанал против мене?
Unasema mnayo mikakati na nguvu za kijeshi, lakini unasema maneno matupu tu. Je, wewe unamtegemea nani, hata ukaniasi mimi?
21 Виж, ти се надяваш, като че ли на тояга, на оная строшена тръстика на Египет, на която, ако се опре някой, ще се забучи в ръката му та ще я промуши. Такъв е египетския цар Фараон за всички, които се надяват на него.
Tazama sasa, unaitegemea Misri, fimbo ile ya mwanzi uliopasuka, ambayo huuchoma na kuujeruhi mkono wa mtu akiiegemea! Hivyo ndivyo alivyo Farao mfalme wa Misri, kwa wote wanaomtegemea.
22 Но ако би речете: На Господа нашия Бог, поваваме, то Той не е ли Оня, Чиито високи местаи жертвеници премахна Езекия, като рече на Юда и на Ерусалим: Пред тоя олтар в Ерусалим се покланяйте?
Nawe kama ukiniambia, “Tunamtumainia Bwana Mungu wetu”: je, siyo yeye ambaye Hezekia aliondoa mahali pake pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu zake, akiwaambia Yuda na Yerusalemu, “Ni lazima mwabudu mbele ya madhabahu haya katika Yerusalemu”?
23 Сега, прочее, дай човеци в залог на господаря ми асирийския цар; а аз ще ти дам две хиляди коне, ако можеш от своя страна да поставиш на тях ездачи.
“‘Njooni sasa, fanyeni mapatano na bwana wangu, mfalme wa Ashuru: Nitakupa farasi elfu mbili, kama unaweza kuwapandisha waendesha farasi juu yao!
24 Как тогава ще отблъснеш един военачалник измежду най-ниските слуги на господаря ми? Но пак уповаваш на Египет за колесници и за конници!
Utawezaje kumzuia hata afisa mmoja aliye mdogo kati ya maafisa wa bwana wangu, ijapo unategemea Misri kwa magari ya vita na wapanda farasi?
25 Без волята на Господа ли възлязох сега на това място за да го съсипя? Господ ми рече: Възлез против тая земя та я съсипи.
Zaidi ya hayo, je, nimekuja kushambulia na kuangamiza mahali hapa pasipo neno kutoka kwa Bwana? Bwana mwenyewe ndiye aliniambia niishambulie nchi hii na kuiangamiza.’”
26 Тогава Елиаким, Хелкиевият син, Шевна и Иоах рекоха на Рапсака: Говори, молим, на слугите си на сирийски, защото го разбираме: недей ни говори на юдейски, та да чуят людете, които са на стената.
Ndipo Eliakimu mwana wa Hilkia, Shebna na Yoa wakamwambia yule jemadari wa jeshi, “Tafadhali zungumza na watumishi wako kwa lugha ya Kiaramu, kwa kuwa tunaifahamu. Usiseme nasi kwa Kiebrania watu walioko juu ya ukuta wakiwa wanasikia.”
27 Но Рапсак им рече: Да ли ме е пратил господарят ми само при твоя господар и при тебе да говоря тия думи? не ме ли е изпратил при мъжете, които седят на стената, за да ядат с вас заедно изпражненията си и да пият пикочта си?
Lakini yule jemadari wa jeshi akajibu, “Je, bwana wangu amenituma kutoa ujumbe huu kwa bwana wenu na kwenu tu? Je, hakunituma pia kwa watu walioketi ukutani, ambao, kama ninyi, itawabidi kula mavi yao na kunywa mikojo yao wenyewe?”
28 Тогава Рапсак застана та извика на юдейски със силен глас, като говори, казвайки: Слушайте думата на великия цар, асирийския цар:
Kisha yule jemadari wa jeshi akasimama na kuita kwa lugha ya Kiebrania, akasema: “Sikieni neno la mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru!
29 така казва царят: Да ви не мами Езекия. Защото той не ще може да ви избави от ръката ми.
Hili ndilo asemalo mfalme: Msikubali Hezekia awadanganye. Hawezi kuwaokoa mkononi mwangu.
30 И да ви не прави Езекия да уповавате на Господа, като казва: Господ непременно ще ни избеви, и тоя град няма да бъде предаден в ръката на асирийския цар.
Msikubali Hezekia awashawishi kumtumaini Bwana kwa kuwaambia, ‘Hakika Bwana atatuokoa. Mji huu hautaangukia mikononi mwa mfalme wa Ashuru.’
31 Не слушайте Езекия, защото така казва асирийският цар: Направете спогодбе с мене и излезте при мене, и яжте всеки от лозето си, и всеки от смокината си, и пийте всеки от водата на щерната си
“Msimsikilize Hezekia. Hili ndilo mfalme wa Ashuru asemalo: Fanyeni amani nami na mje kwangu. Kisha kila mmoja wenu atakula kutoka kwa mzabibu wake na mtini wake mwenyewe, na kunywa maji kutoka kisima chake mwenyewe,
32 докле дойда и ви заведа в земя подобна на вашата земя, зимя изобилваща с жито и вино, земя изобилваща с хляб и лозя, земя изобилваща с дървено масло и мед, за да живеете и да не умрете; и не слушайте Езекия, когато би ви убеждавал, като казва: Господ ще ни избави.
mpaka nije nikawapeleke katika nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na mashamba ya mizabibu, nchi ya mizeituni na asali. Chagueni uzima, sio mauti! “Msimsikilize Hezekia, kwa kuwa anawapotosha asemapo, ‘Bwana atatuokoa.’
33 Някой от боговете на народите избавил ли е земята си от ръката на асирийския цар?
Je, yuko mungu wa taifa lolote aliyewahi kuokoa nchi yake kutoka mkononi mwa mfalme wa Ashuru?
34 Где са боговете на Емат и Аршад? Где са боговете на Сефаруим, на Ена и на Ава? Избавиха ли те Самария от ръката ми?
Iko wapi miungu ya Hamathi na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu, Hena na Iva? Je, imeokoa Samaria kutoka mkononi mwangu?
35 Кой измежду всичките богове на разните страни са избавили земята си от моята ръка, та да избави Иеова Ерусалим от ръката ми?
Ni yupi miongoni mwa miungu yote ya nchi hizi ameweza kuokoa nchi yake mkononi mwangu? Inawezekanaje basi Bwana aiokoe Yerusalemu mkononi mwangu?”
36 А людете мълчаха, и не му отговориха ни дума, защото царят беше заповядал, казвайки: Да му не отговаряте.
Lakini wale watu wakakaa kimya, wala hawakujibu lolote, kwa kuwa mfalme alikuwa amewaamuru, “Msimjibu lolote.”
37 Тогава управителят на двореца Елиаким, Хелкиевият син, и секретарят Шевна, и летописецат Иоах, Асафовият син, дойдоха при Езекия с раздрани дрехи та му известиха Рпсаковите деми.
Kisha Eliakimu mwana wa Hilkia msimamizi wa jumba la kifalme, Shebna katibu, na Yoa mwana wa Asafu, mwandishi wakamwendea Hezekia, nguo zao zikiwa zimeraruliwa, na kumwambia yale jemadari wa jeshi aliyoyasema.

< 4 Царе 18 >